Upendo Nkone akabidhiwa Gari Rasmi kutoka kwa Mashabiki Zake
Ni Hafla iliyofanyika Aprili 23,Mlimani City jijini Dar es Salaam ambapo Msanii wa nyimbo za Injili Upendo Nkone alikabidhiwa Gari na Mashabiki Zake,
Kwa Furaha na Machozi,Upendo Nkone alitoa shukurani za Dhati na Kuwatamkia Baraka Wote waliotoa wazo hilo,na Wote Waliomchangia katika Changizo hilo,
Kwa kuthamini mchango wake mkubwa katika muziki wa injili na Huduma yake ya Uimbaji ambayo imebadilisha wengi,Mashabiki wa Upendo Nkone Waliamua Kumnunulia Gari.
Upendo Nkone aliwashukuru Kipekee Sana Resty Bulla pamoja na Lillian Mwasha ambao walisimamia Zoezi zima kwa Uwazi wa hali ya Juu ili kuhakikisha Zoezi hilo Linatimia.
Na Hatimaye Nkone akanunuliwa Gari na Wadau Mbali mbali ambao Walihusika katika Zoezi hilo.
Shukurani za Kipekee na Baraka Tele kutoka kwa Upendo Nkone aliziachilia kwa Kila aliyehusika kwa namna yoyote,ikiwemo kuchanga Pesa,Kutoa mawazo,au hata kuhudhuria tu kwenye hafla hiyo.







