Showing posts with label habari mpya. Show all posts
Showing posts with label habari mpya. Show all posts

Upendo Nkone akabidhiwa Gari Rasmi kutoka kwa Mashabiki ZakeAfyaclass Forum •

Upendo Nkone akabidhiwa Gari Rasmi kutoka kwa Mashabiki Zake

Ni Hafla iliyofanyika Aprili 23,Mlimani City jijini Dar es Salaam ambapo Msanii wa nyimbo za Injili Upendo Nkone alikabidhiwa Gari na Mashabiki Zake,

Kwa Furaha na Machozi,Upendo Nkone alitoa shukurani za Dhati na Kuwatamkia Baraka Wote waliotoa wazo hilo,na Wote Waliomchangia katika Changizo hilo,

Kwa kuthamini mchango wake mkubwa katika muziki wa injili na Huduma yake ya Uimbaji ambayo imebadilisha wengi,Mashabiki wa Upendo Nkone Waliamua Kumnunulia Gari.

Upendo Nkone aliwashukuru Kipekee Sana Resty Bulla pamoja na Lillian Mwasha ambao walisimamia Zoezi zima kwa Uwazi wa hali ya Juu ili kuhakikisha Zoezi hilo Linatimia.

Na Hatimaye Nkone akanunuliwa Gari na Wadau Mbali mbali ambao Walihusika katika Zoezi hilo.

Shukurani za Kipekee na Baraka Tele kutoka kwa Upendo Nkone aliziachilia kwa Kila aliyehusika kwa namna yoyote,ikiwemo kuchanga Pesa,Kutoa mawazo,au hata kuhudhuria tu kwenye hafla hiyo.

0 Comment

Mahakama ya Afrika Kusini yaamuru Zambia irudishe mwili wa rais wa zamani Edgar LunguAfyaclass Forum •

Mahakama ya Afrika Kusini yaamuru Zambia irudishe mwili wa rais wa zamani Edgar Lungu

Edgar Lungu alisema hakutaka mrithi wake kuwepo kwenye mazishi yake au "mahali popote karibu" na mwili wake

Saa chache tu baada ya serikali ya Zambia kusema imechukua mwili wa Rais wa zamani Edgar Lungu, mahakama nchini Afrika Kusini -imeamuru mwili huo urudishwe.

Ni mabadiliko ya hivi punde katika sakata ya miezi 10 kuhusu kile kinachopaswa kutokea kwa mabaki yake kufuatia ugomvi wa muda mrefu kati ya Lungu na mrithi wake, Rais Hakainde Hichilema.

Serikali imesisitiza kwa muda mrefu kwamba, kama mkuu wa zamani wa nchi, Lungu anapaswa kuheshimiwa nchini na kuzikwa pamoja na watangulizi wake katika eneo maalum la mazishi ya rais katika mji mkuu, Lusaka.

Lakini familia ya Lungu ilitaka mazishi ya faragha baada ya mazungumzo na serikali kuhusu mipango ya mazishi kuvunjika.

Agosti iliyopita, mahakama kuu ya Afrika Kusini huko Pretoria ilitoa uamuzi kwamba serikali ya Zambia inaweza kurudisha mwili huo na kumpa mazishi ya kitaifa - matokeo ambayo yaliwaacha jamaa za Lungu wakiwa wamechanganyikiwa waziwazi mahakamani.

0 Comment

Ripoti ya Tume ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu Amani Oktoba, 2025Afyaclass Forum •

Ripoti ya Tume ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu Amani Oktoba, 2025

Tume ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu Amani Oktoba, 2025 imesema baadhi ya wanasiasa na wanaharakati walitumia changamoto za wananchi kuwashawi na kuwachochoea kushiriki ghasia kabla na wakati wa uchaguzi mkuu.

Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Othman Chande ameeleza hayo leo Jumatano Aprili 23, 2026 akitoa matokea ya ripoti ya Tume ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu Amani wakati na baada ya uchaguzi mkuu wa Oktoba 29,2025 mbele ya Rais Samia Suluhu Hassan, Ikulu Dar es Salaam

Tume hiyo imefafanua kuwa baadhi ya wanaharakati hao na wanasiasa walitumia kauli mbiu na matamko mbalimbali.

“Ushahidi taarifa umeonyesha baadhi ya wanaharakati na wanasiasa walitumia changamoto za wananchi zilizotokana na vyanzo mbalimbali kama fursa ya kuhamasisha wananchi kushiriki katika ghasia hizo,”

“Tathimini yha Tume imebaini kulikowapo na vichocheo mahsusi vilivyohamasisha ari ya kufanya ghasia kabla na baada ya uchaguzi mkuu,” amesema Jaji Chande.

Amesema vichocheo hivyo vimewekwa katika makundi matatu likiwemo ya mitandao ya kijamii, akisema kwa mujibu wa mashahidi waliofika mbele ya Tume walieleza kuwa mitandao yao ilitumika kabla na baada ya uchauguzi mkuu kuwa mitandao yao ilitumika kwa kiwango kikubwa.

“Aidha waliibuka wabuni mada kwenye mitandao ‘content creator’ ikiwemo kuhamasisha wananchi wasishiriki uchaguzi mkuu au kuhakikisha haufanyiki,” amesema. Via Global Publishers

0 Comment

Mtoto azaliwa akiwa ameshika KitanziAfyaclass Forum •

Mtoto azaliwa akiwa ameshika Kitanzi ambacho kilishindwa kuzuia ujauzito kwa mama yake

Mtoto mchanga aligonga vichwa vya habari baada ya kuzaliwa akiwa ameshika kifaa cha ndani ya uterasi (IUD) au Kitanzi au Lupu ambacho kilikusudiwa kuzuia ujauzito.

Madaktari waliripotiwa kushangazwa kuona kifaa hicho bado kipo mahali pake wakati wa kuzaliwa, na kuifanya kuwa tukio la nadra na lisilo la kawaida kimatibabu.

Ingawa IUD ni miongoni mwa aina bora za njia ya uzazi wa mpango—ujauzito bado unaweza kutokea ikiwa kifaa kitabadilika au kushindwa kufanya kazi kama ilivyokusudiwa. Ingawa ni nadra sana, kesi hii inaonyesha uwezekano mdogo wa IUD kushindwa kufanya kazi na imezua mjadala mkubwa katika duru za kimatibabu na kijamii.

#IUD #Udhibiti wa Kuzaliwa #Kesi ya Kimatibabu nadra #Ukweli wa Mtoto Mchanga #Uzazi wa Mpango.....

0 Comment

Jinsi Wanaanga wa NASA Walioenda Mwezini Walivyorejea Salama DunianiAfyaclass Forum •

Wanaanga wanne wa shirika la anga za juu la NASA waliokuwa kwenye misheni ya Artemis II wamerejea salama duniani baada ya kukamilisha safari ya kihistoria ya kuuzunguka Mwezi kwa mara ya kwanza baada ya miaka 50.

Chombo cha anga cha Orion kiliwabeba wanaanga hao na kutua baharini (splashdown) katika Bahari ya Pasifiki karibu na pwani ya California Aprili 10, 2026, baada ya safari ya takriban siku 10 angani.

Wanaanga hao—Reid Wiseman, Victor Glover, Christina Koch na Jeremy Hansen, walifanikiwa kuzunguka upande wa mbali wa Mwezi kabla ya kurejea duniani, wakivunja rekodi ya umbali mkubwa zaidi kuwahi kufikiwa na binadamu kutoka Dunia.

Katika hatua ya kurejea, chombo hicho kiliingia katika anga ya Dunia kwa kasi ya takribani maili 23,000 kwa saa, kikikumbana na joto kali na kukatika kwa mawasiliano kwa dakika kadhaa kutokana na msuguano wa hewa (plasma), hali ambayo ni ya kawaida katika misheni za aina hii.

Baada ya kutua, wanaanga walipokelewa na kikosi cha Jeshi la Wanamaji la Marekani na kufikishwa kwenye meli kwa uchunguzi wa afya kabla ya kurejeshwa katika kituo cha anga cha Johnson Space Center.

Misheni ya Artemis II ni hatua muhimu kuelekea malengo ya NASA ya kurejesha binadamu Mwezini katika miaka ijayo, ikiwa ni pamoja na mipango ya kutua rasmi juu ya uso wa Mwezi na baadaye safari za kwenda sayari ya Mirihi (Mars).

Safari hiyo pia imeweka historia kwa kuwa na mchanganyiko wa wanaanga wa jinsia na mataifa tofauti, ikiashiria ushirikiano wa kimataifa katika utafiti wa anga za juu.

0 Comment
Notification
Karibu Afyaclass Forum Jukwaa linalojadili mambo mbali mbali ikiwemo afya,Magonjwa na Updates Zote,Tembelea hapa kila Siku,Pia Share Maoni yako kwenye jukwaa hili Afyaclass Forum ASANTE.
UNDERSTOOD