Afyaclass AFYA BORA KWA MTOTO

 Afya bora kwa mtoto ipo mikononi mwako.Kuna mambo muhimu lazima uyafanye kwa mtoto kuanzia tu pale anapozaliwa.

.

Jambo la kwanza kabsa ni kuhakikisha unaanza kumnyonyesha ndani ya lisaa la kwanza mara tu baada ya kujifungua

.

Unyonyeshaji huo unaenda mpaka miez sita pasipo kumchanganyia kitu kingine chochote,Baada ya miezi sita anza kumchanganyia mtoto vyakula pamoja na maziwa ya mama

.

Hiyo nayo inaenda mpaka mtoto akifika miaka miwili,hapo utakuwa umezingatia unyonyeshaji bora kwa mtoto wako,na kumbuka maziwa ya mama ndo kinga kubwa kwa mtoto dhidi ya magonjwa

.

Jambo lingine ni kuhakikisha mtoto anapata chanjo zote muhimu kuanzia anapozaliwa mpaka anapofikisha umri wa miaka mitano

.

Usafi kwa mtoto ni jambo la muhimu kwa mtoto pia, na kuzingatia swala la kutokuweka kitu chochote kwenye kitovu cha mtoto mpaka kidongoke chenyewe

.

Pia zingatia dalili zote za hatari kwa mtoto ili uzionapo tu uhakikishe mtoto anapata msaada wa kitaam,mfano mtoto kugeuka rangi na kuwa manjano,mtoto kupatwa na degedege,mtoto kutokunyonya kabsa,n.k

#mtoto 

#afya 

#ombenimkumbwa

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Karibu Sana..!!!



You, Mehreen and others

WEKA MAONI HAPA(Reply)

Notification
My blog is in the process of editing and perfecting the new template, so there are still some functions to click but not yet used. Note which blogs associated with your side please read this lesson to update the blog logo.
UNDERSTOOD