Wagonjwa wengi wanastahili huduma za KIBINGWA

#1

WAGONJWA WENGI WANASTAHILI HUDUMA ZA KIBINGWA

Na WAF, Ikungi-Singida

Wakati mahitaji ya huduma za afya zinazidi kuongezeka, wagonjwa wengi katika Wilaya ya Ikungi wanaonekana kustahili na kuhitaji huduma za kibingwa.

Hayo yamebainishwa na daktari bingwa wa magonjwa ya ndani Dkt. Antony Abraham ambapo ameeleza kuwa mahitaji ya huduma za kibingwa yanazidi kuongezeka katika jamii, huku akiwa amewaona wagonjwa zaid ya 70

Aidha, Dkt. Abraham ameelezea umuhimu wa kuwa na kampeni endelevu ya madaktari bingwa katika ngazi ya halmashauri na wilaya ili kukabiliana na mahitaji makubwa ya huduma za kibingwa.

Pia, amesema, hali hiyo itasaidia kuhakikisha kila mgonjwa anapata matibabu yanayostahili na yanayolingana na mahitaji yake.

Mwisho.

Consultation ya Afya Moja kwa Moja

Mimi ni Dr. Ombeni Mkumbwa. Nakupa ushauri wa kitaalamu kuhusu tatizo lolote la kiafya kwa siri, haraka na uhakika.

WhatsApp

Changia Mada hapa(Reply)


image quote pre code
مشاركة: