Watu 115 wamefariki dunia kwa Mafuriko nchini Nigeria

Watu 115 wamefariki dunia kwa Mafuriko nchini Nigeria

#1

Watu 115 wamefariki dunia kwa Mafuriko nchini Nigeria



Watu 115 wamefariki dunia baada ya mafuriko kuukumba mji wa kibiashara wa Mokwa katika jimbo la Niger huko Nigeria.

Mkuu wa ofisi ya operesheni huko Minna, Husseini Isah, amesema watu wengi zaidi bado wako kwenye hatari huku juhudi za uokoaji zikiendelea Ijumaa.

Ripoti za awali zilikuwa zimesema kuwa watu 20 ndio waliofariki ila Isah amedai kuwa idadi inazidi kuongezeka.

Chanzo cha mafuriko hayo ni mvua kubwa iliyonyesha kwa masaa kadhaa na kulingana na ripoti, kuvunjika kwa bwawa moja katika eneo jirani ndiko kulikopelekea hali kuwa mbaya zaidi.

Mji wa Mokwa ni makutano ya wafanyabiashara kutoka kusini mwa Nigeria na wakulima wa kaskazini mwa nchi hiyo.

Mwaka 2024 kulikuwa na tukio kama hilo ambapo mvua kubwa na kuvunjika kwa bwawa kulisababisha vifo vya angalau watu 30 huko Maiduguri, kaskazini mashariki mwa Nigeria.

REPLY HAPA


image quote pre code