Colombia:Mgombea Uraisi apigwa risasi kichwani akiwa kwenye mkutano
Mgombea urais wa Colombia yuko katika hali mbaya baada ya kupigwa risasi tatu, ikiripotiwa mara mbili kichwani, katika hafla ya kampeni katika mji mkuu, Bogotá.
Miguel Uribe Turbay, seneta mwenye umri wa miaka 39, alishambuliwa alipokuwa akiwahutubia wafuasi wake kwenye bustani siku ya Jumamosi.
Polisi walimkamata mshukiwa mwenye umri wa miaka 15 katika eneo la tukio, ofisi ya mwanasheria mkuu ilisema.
Mkewe Uribe, Maria Claudia Tarazona, alitoa wito kwa taifa kumuombea apone.
“Miguel kwa sasa anapigania maisha yake, tumuombe Mungu aongoze mikono ya madaktari wanaomhudumia,” alisema.
Chama cha Uribe Centro Democratico kimelaani shambulio hilo, na kulitaja kuwa tishio kwa "demokrasia na uhuru nchini Colombia".
REPLY HAPA
image quote pre code