Wagonjwa kutoka nje ya nchi waliokuja kutibiwa nchini Tanzania ni 12,180
Waziri wa Afya, Jenista Mhagama amesema kutokana na uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali katika kuboresha huduma za ubigwa na ubingwa bobezi nchini,
uwekezaji huo umevutia wagonjwa mbalimbali kutoka nje ya nchi ambapo katika kipindi cha mwaka 2021 hadi March, 2025 idadi ya Wagonjwa kutoka nje ya nchi waliokuja kutibiwa nchini imeongezeka kutoka wagonjwa 5,705 mwaka 2021 hadi kufikia wagonjwa 12,180 Machi, 2025.
Akitoa hotuba kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026, Mhagama amesema “Wagonjwa hao ni kutoka katika nchi za Comoro, Malawi, Burundi, Zambia, Rwanda, Afrika Kusini, Msumbiji, Congo DRC, Sudan, Uganda, Zimbabwe, Ethipia, Somalia, Kenya, Egypt, na Mauritius”
“Wagonjwa hao walihudumiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, Taasisi ya Saratani Ocean Road, Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete, Taasisi ya Mifupa Muhimbili, Hospitali ya Aga khan na Hospitali ya Saifee”
REPLY HAPA
image quote pre code