Madhara na uhamishwaji wa watu umeripotiwa kwenye mikoa ya Urusi iliyo karibu na kitovu cha tetemeko hilo katika Rasi ya Kamchatka.
Tetemeko hilo ni kubwa kabisa kuwahi kulipiga eneo hilo tangu mwaka 1952, kwa mujibu wa Mamlaka ya Jiolojia ya Urusi.
Tsunami iliyopelekea mawimbi ya bahari yenye ukubwa wa hadi mita 30 imeripotiwa katika visiwa vya Hokkaido vya Japan na visiwa vya Kuril vinavyomilikiwa na Urusi, na yanakhofiwa kuelekea pia Ufilipino, Chile na Visiwa vya Solomon.
Tayari Ufilipino nayo imetangaza tahadhari ya kiwango cha juu ya tsunami.
Athari za tetemeko hilo zinatazamiwa kuonekana hadi nchini Marekani kwenye miji ya Carlifornia na Washington.
image quote pre code