Zaidi ya watu milioni 21 wahitaji msaada wa kibinadamu Kongo

Zaidi ya watu milioni 21 wahitaji msaada wa kibinadamu Kongo

#1

Zaidi ya watu milioni 21 wanahitaji msaada wa kibinadamu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo,Haya ni kwa mujibu wa shirika la Oxfam nchini Ufaransa.

Shirika hilo limesema Kongo inakabiliwa na mojawapo ya majanga makubwa na yaliyosahaulika ya kibinadamu duniani na kwamba hali inaendelea kuwa mbaya zaidi.

Oxfam, pia imesema unyanyasaji wa kijinsia umefikia viwango vya kutisha, huku mwanamke mmoja akibakwa kila baada ya dakika nne.

Msaada wa kimataifa wapungua

Hata hivyo licha ya hali hiyo ya dharura, msaada wa kimataifa unapungua.

Oxfam, imesema katika muda wa mwaka mmoja, ufadhili wa misaada muhimu umepungua kwa thuluthi mbili nchini Kongo na imelihimiza kongamano la kimataifa kuhusu Kanda ya Afrika ya Maziwa Makuu, linaotarajiwa kufanyika nchini Ufaransa Oktoba 30, kuchukuwa hatua zaidi ya matamko ya nia. Via Dw.

Consultation ya Afya Moja kwa Moja

Mimi ni Dr. Ombeni Mkumbwa. Nakupa ushauri wa kitaalamu kuhusu tatizo lolote la kiafya kwa siri, haraka na uhakika.

WhatsApp

Changia Mada hapa(Reply)


image quote pre code