Uwezekano wa mafuriko zaidi waongezeka maeneo ya magharibi mwa Kenya

Uwezekano wa mafuriko zaidi waongezeka maeneo ya magharibi mwa Kenya

#1

Idara ya Hali ya Hewa ya Kenya (KMD) imetangaza kuwa mvua zitaendelea kunyesha nchini kote mwezi huu wa Novemba.

Katika mtazamo wake wa hali ya hewa, shirika hilo lilisema kuwa mvua zaidi ya wastani inatarajiwa kuendelea katika kaunti za Bonde la Ziwa Victoria, Nyanda za Juu Magharibi mwa Bonde la Ufa, na Kati na Kusini mwa Bonde la Ufa.

Vile vile, mvu ya chini ya wastani au kawaida inatarajiwa katika kaunti za Nyanda za Juu Mashariki mwa Bonde la Ufa (pamoja na Nairobi), nyanda za juu Kusini-mashariki, Pwani na sehemu kubwa ya Kaskazini-mashariki.

"Mvua itakayonyesha haitakuwa ya kiwango sawa, na vipindi vya ukame vya hapa na pale katika maeneo kadhaa ya nchi," mtaalamu wa hali ya hewa alibainisha.

Hata hivyo, halijoto inatarajiwa kusalia joto zaidi kuliko kawaida nchini kote huku kukiwa na uwezekano mkubwa wa mafuriko katika eneo la magharibi na vipindi virefu vya kiangazi katika maeneo ya mashariki mwa nchi.

Maeneo ya Nyanda za Juu Magharibi, Mashariki mwa Bonde la Ufa na Bonde la Ziwa yamebainishwa haswa kuwa yana uwezekano wa kupata mvua za wastani, hivyo kuhitaji tahadhari kutokana na udongo ambao tayari umejaa maji.

Changia Mada hapa(Reply)


image quote pre code
مشاركة: