Kupata Damu Ya Hedhi Nyeusi inaashiria nini?
Kupata damu ya hedhi nyeusi mara nyingi si tatizo kubwa, bali inaashiria damu ya zamani iliyokaa muda mrefu ndani ya mji wa mimba (uterasi) kabla ya kutoka. Damu inapokaa muda, hukosa hewa (oxidation) na kuwa rangi ya kahawia au nyeusi.
Tuangalie nini huashiria Damu ya Hedhi ikitoka Nyeusi,Hapa kuna maana mbalimbali:
1. Damu ya zamani kutoka
Hii Huonekana mwanzoni au mwishoni mwa hedhi,na inakuwa;
- Kiasi kidogo
- Na Haina harufu kali
Hii huwa ni kawaida.
2. Mzunguko wa hedhi kuchelewa
Kama hedhi ilichelewa, damu inaweza kuwa nzito na nyeusi
Huambatana na maumivu kidogo ya tumbo
3. Mabaki ya mimba (kama Mimba iliwahi kuharibika)
Kama Mimba iliharibika na kukuwa na mabaki ndani,Damu nyeusi inaweza kutoka kwa siku kadhaa,Na Huambatana na maumivu makali au damu nyingi.
4. Maambukizi ya Kwenye Via vya Uzazi (kama PID au UTI kali)
Ikiwa tatizo ni maambukizi haya,Damu nyeusi yenye na harufu mbaya sana inaweza kutoka,Lakini pia unaweza kupata dalili Zingine kama vile;
- Maumivu wakati wa tendo la ndoa
- Maumivu ya tumbo la chini au Chini ya Kitovu
Hapa inahitaji kuonana na daktari au Kuongea na Wataalam wa afya kwa Ushauri wa haraka.
5. Dalili za mimba changa (implantation bleeding)
Damu kidogo sana, rangi kahawia au nyeusi huweza kutokea kabla ya tarehe ya hedhi, hii ikiwa inaashiria Mimba changa inapojishikiza kwenye mji wa Mimba,Damu hii kitaalamu hujulikana kama Implantation bleeding.
Kumbuka: Hakikisha Unaongea na daktari kama damu inatoka nyeusi na Inaambatana na Dalili hizi;
- Kuna harufu kali sana
- Unapata Maumivu makali ya tumbo
- Damu nyingi isiyo ya kawaida
- Hali inaendelea miezi kadhaa
Je,Una tatizo hili na hujapata Tiba bado?
KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.





.jpeg)



image quote pre code