Showing posts with label Jukwaa la ajira(jobs). Show all posts
Showing posts with label Jukwaa la ajira(jobs). Show all posts

Mwanamke ashare jinsi alivyopoteza ofa ya kazi baada ya kufichua kwamba ni mjamzitoAfyaclass Forum •

Mwanamke mmoja ashiriki(share) jinsi alivyopoteza ofa ya kazi ya kimataifa baada ya kufichua kwamba alikuwa mjamzito

Mwanamke mmoja wa Nigeria kwenye X amesambaa sana baada ya kusimulia jinsi alivyopoteza ofa ya kazi ya ndoto yake mara tu alipoifahamisha kampuni hiyo kwamba alikuwa na mimba ya miezi mitano.

Mazungumzo yalianza baada ya mtumiaji wa X kuwauliza watu "wamwambie jambo ambalo halimhusu." Kwenye majibu, mtumiaji mwingine wa X alishiriki uzoefu wake.

Kulingana naye, alikuwa amepitia mchakato wa mahojiano mtandaoni na kampuni ya kimataifa na kupata kazi hiyo. Kwa sababu ujauzito wake haukuonekana hadi miezi saba, kampuni hiyo haikuwa na wazo alilotarajia. Walimtumia barua ya ofa, na kila kitu kilionekana kuwa tayari.

Alisema aliamua kuwa mkweli na kuwapigia simu HR ili kufichua ujauzito wake - lakini wao wakamwomba "asubiri."

Siku nne baadaye, alipigiwa simu akimwambia kwamba kampuni hiyo haitaendelea tena na ofa yake. Kama hivyo tu.

0 Comment

Nafasi Kazi 10,026 Mpya – Fursa kwa Walimu, Wauguzi na Kada nyingineAfyaclass Forum •

Tangazo hilo ni rasmi la ajira serikalini lililotolewa na Ofisi ya Rais – Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma (TAMISEMI/PO-PSMGG) tarehe 18 Oktoba 2025 lenye Kumb. Na. JA.9/259/01/C/6.

Lengo lake ni kutangaza nafasi 10,026 za kazi kwa MDAs & LGAs (yaani Wizara, Idara, Wakala na Mamlaka za Serikali za Mitaa). Soma zaidi

TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI MDAs NA LGAs 

0 Comment

CCM yaahidi ajira mpya 5,000 sekta ya afya, ajira 7,000 sekta ya elimu.Afyaclass Forum •

CCM yaahidi ajira mpya 5,000 sekta ya afya, ajira 7,000 sekta ya elimu.



CHAMA Cha Mapinduzi ( CCM) kimejinasibu kuimarisha sekta ya elimu na afya, ambapo katika miaka mitano ijayo kimeahidi kutoa msukumo serikalini ili kutangazwa ajira mpya 5,000 sekta ya afya, ajira 7,000 sekta ya elimu.

Mgombea Mwenza wa Urais CCM, Dk. Emmanuel Nchimbi alieleza hayo jana wilayani Magu mkoani Mwanza, ikiwa ni mwendelezo wa kampeni za Uchaguzi Mkuu. Dk. Nchimbi alisema endapo CCM ikifanikiwa kushinda katika uchaguzi huo ajira 5,000 mpya zitatangazwa sekta ya afya na ajira 7,000 za walimu wa sayansi na hisabati.

Vilevile, alisema wanafunzi wa shule za msingi watapata mafunzo mazuri kwa lengo la kuwawezesha kujua kusoma, kuandika na kuhesabu.

0 Comment

Ajira 2,460 reli Dar – Makutopora kutolewa na TRCAfyaclass Forum •

Ajira 2,460 reli Dar – Makutopora kutolewa na TRC



DAR ES SALAAM: Ajira 2,460 zinatarajiwa kutolewa na Shirika la Reli Tanzania (TRC), katika utekelezaji wa mradi wa reli ya kiwango cha kimataifa (SGR) kwa vipande viwili vya Kutoka Dar es Salaam mpaka Makutopora.

Hayo yamebainishwa wakati wa ziara ya siku mbili ya Bodi ya Wakurugenzi TRC, kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa SGR na MGR, kati ya Kigoma – Tabora na Tabora Mwanza iliyoanza Agosti 19, 2025.

Katika ajira hizo 2,460 utekekezaji wake ni awamu, ambapo katika mwaka wa fedha 2024/25 zaidi ya watumishi 500 wameshaajiriwa na mwaka huu wa fedha 2025/26 marajio ni kuajiri watumishi 272 na TRC itaendelea kuajiri kufikia watumishi 2,460.

Wakati utekekezaji wa utoaji ajira rasmi za Shirika ukiendelea, jumla ya ajira 115,000 kutoka mkandarasi zimeshawanufaisha Watanzania 115,000 zikiwemo za vijana wa elimu ya darasa la saba na viwango vingine vya elimu katika fani mbalimbali.

Mchanganuo wa ajira hizo 115,000 kutoka kwa mkandarasi, ni kwamba ajira 35,000 ni za moja kwa moja na zaidi ya 80,000 ni zisizo za moja kwa moja zikijumuisha makundi mbalimbali kama baba na mama lishe, bodaboda, bajaji na watoa huduma za makampuni mbalimbali ya mawasiliano kama mocha, line za simu nk

0 Comment
Notification
Karibu Afyaclass Forum Jukwaa linalojadili mambo mbali mbali ikiwemo afya,Magonjwa na Updates Zote,Tembelea hapa kila Siku,Pia Share Maoni yako kwenye jukwaa hili Afyaclass Forum ASANTE.
UNDERSTOOD