Showing posts with label Mungu. Show all posts
Showing posts with label Mungu. Show all posts

Mruhusu Mungu akuonyeshe Njia utakayoiendeaAfyaclass Forum •

Ujumbe wa Leo kwako,Unakukumbusha kwamba Mungu ni njia na jibu la kila Swali ulilonalo.

Mruhusu YEYE akuonyeshe njia utakayoiendea. "Zaburi 32:8- Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea; Nitakushauri, jicho langu likikutazama".

Weka tumaini lako lote kwake, weka Imani yako yote kwake nawe utapata jambo jema, faraja, au suluhisho la kila tatizo ulilonalo.

Tumia akili zako kwa kadri Mungu alivyokujalia, lakini kamwe tumaini lako lisiwe kwenye akili zako, Mtumaini Mungu Peke yake kwa moyo wako wote,Mtegemee yeye Peke yake, Nawe Utafanikiwa......

"Mithali 3:5 Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe".

Ukitegemea akili zako mwenyewe utakwama, Mtegemee Mungu.

Nimatumaini yangu kwamba, Tumaini lako sasa lipo kwa Mungu wako,wala hutegemei akili zako mwenyewe.

Mungu akubariki Sana, na Siku njema kwako......🙏🙏🙏🙏

0 Comment

Muangalie Mungu apate kukuokoa na Kila hatari iliyopo Mbele yakoAfyaclass Forum •

Muangalie Mungu apate kukuokoa na Kila hatari iliyopo Mbele yako

"Niangalieni mimi, mkaokolewe, enyi ncha zote za dunia; maana mimi ni Mungu; hapana mwingine".Isaya 45:22

Neno "Niangalieni" hapa lina maana ya kumgeukia Mungu kwa imani na kumtegemea. Ni mwaliko wa kuacha kutegemea sanamu, mali, au nguvu za kibinadamu na badala yake kumgeukia Mungu wa kweli kwa Imani na Kumtegemea kwa kila Kitu.

0 Comment
Notification
My blog is in the process of editing and perfecting the new template, so there are still some functions to click but not yet used. Note which blogs associated with your side please read this lesson to update the blog logo.
UNDERSTOOD