Mruhusu Mungu akuonyeshe Njia utakayoiendea

Mruhusu Mungu akuonyeshe Njia utakayoiendea

#1

Ujumbe wa Leo kwako,Unakukumbusha kwamba Mungu ni njia na jibu la kila Swali ulilonalo.

Mruhusu YEYE akuonyeshe njia utakayoiendea. "Zaburi 32:8- Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea; Nitakushauri, jicho langu likikutazama".

Weka tumaini lako lote kwake, weka Imani yako yote kwake nawe utapata jambo jema, faraja, au suluhisho la kila tatizo ulilonalo.

Tumia akili zako kwa kadri Mungu alivyokujalia, lakini kamwe tumaini lako lisiwe kwenye akili zako, Mtumaini Mungu Peke yake kwa moyo wako wote,Mtegemee yeye Peke yake, Nawe Utafanikiwa......

"Mithali 3:5 Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe".

Ukitegemea akili zako mwenyewe utakwama, Mtegemee Mungu.

Nimatumaini yangu kwamba, Tumaini lako sasa lipo kwa Mungu wako,wala hutegemei akili zako mwenyewe.

Mungu akubariki Sana, na Siku njema kwako......🙏🙏🙏🙏

Changia Mada hapa(Reply)


image quote pre code