Showing posts with label Mvua kubwa. Show all posts
Showing posts with label Mvua kubwa. Show all posts

TMA yatoa tahadhari mvua kubwa mikoa 19 LeoAfyaclass Forum •

Mvua hizo zinatarajiwa kunyesha Leo Jumapili, Desemba 28, 2025.

Zinaweza kusababisha mafuriko, maporomoko ya udongo na usumbufu wa shughuli za kiuchumi na kijamii. 

Dar es Salaam. Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imewataka wananchi kuchukua tahadhari ya kujikinga na madhara ya mvua kubwa inayotarajia kunyesha katika mikoa 19 nchini ikiwemo Dar es Salaam. 

TMA imesema mvua hizo zinatarajiwa kunyesha kesho Jumapili, Desemba 28, 2025, na huenda zikasababisha madhara mbalimbali ikiwamo mafuriko, maporomoko ya udongo na usumbufu wa shughuli za kiuchumi na kijamii. 

Taarifa ya TMA iliyotolewa leo Desemba 27, 2025 imeeleza kuwa mvua hiyo itanyesha katika mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Manyara, Kigoma, Katavi, Singida, Dodoma, Rukwa, Songwe, Mbeya na Iringa.

Mikoa mingine ni Njombe, Morogoro, Ruvuma, Tanga, Dar es Salaam, Lindi, Mtwara na Pwani ikijumuisha visiwa vya Mafia.

Wananchi wanaoishi katika maeneo tajwa, hususan walioko mabondeni na maeneo hatarishi, kuchukua tahadhari za mapema ili kuepuka athari zinazoweza kujitokeza kutokana na mvua hizo.

TMA imewasisitiza wananchi kuendelea kufuatilia taarifa na utabiri wa hali ya hewa unaotolewa mara kwa mara ili kupata taarifa sahihi na za wakati.

0 Comment

Tukio:Kufuatia Mvua kubwa,Watu 90 wafariki kwa mafuriko IndonesiaAfyaclass Forum •

Mafuriko makubwa na maporomoko ya ardhi yamesababisha vifo vya takriban watu 90 nchini Indonesia wiki hii huku mvua kubwa isiyo ya kawaida ikinyesha katika kisiwa cha Sumatra.

Kanda za video zinaonyesha mafuriko yakivunja kingo za mito, wakaazi wakiingia kwenye maji hadi kifuani, na magari na nyumba zikikaribia kuzama kabisa katika mitaa iliyofurika - huku sehemu za paa zao zikiwa zimesalia tu kuonekana.

Waokoaji wanakimbia kuwaleta watu zaidi kwenye maeneo salama, lakini kukatika kwa umeme na maporomoko ya matope kumetatiza juhudi zao za kutafuta.

Wakati huo huo, Sri Lanka pia inakabiliwa na maafa mabaya zaidi ya hali ya hewa katika miaka ya hivi karibuni, na takriban watu 56 wamekufa na 21 hawajulikani walipo baada ya mafuriko na maporomoko ya ardhi katika maeneo kadhaa ya nchi.

Watu 21 waliuawa katika wilaya ya kati inayolima chai ya Badulla wakati maporomoko ya ardhi yalipoanguka kwenye nyumba zao usiku kucha, Kituo cha Kudhibiti Maafa (DMC) kilisema katika taarifa.

Video zinazoonekana kwenye mitandao ya kijamii zinaonyesha nyumba zikisombwa na maji huku mafuriko yakipita mijini na huduma nyingi za treni zikifutwa kote nchini.

Sri Lanka sasa inajizatiti kukabili hali mbaya ya hewa siku ya Ijumaa huku Kimbunga Ditwah kikisonga kando ya pwani yake ya mashariki.

0 Comment

Tukio,Kimbunga Kalmaegi chasababisha maafa makubwa VietnamAfyaclass Forum •

Kimbunga Kalmaegi kimesababisha upepo mkali na mvua kubwa huko Vietnam. Watu watano wameuwawa wakati kimbunga hicho kilipopiga eneo hilo, kutokea Ufulipino ambako huko idadi ya waliouwawa wamefikia 188.

Nchini Ufilipino katika eneo la Cebu watu 188 waliuawa wengi wao kutokana na mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa iliyotokana na kimbunga Kalmaegi. Watu katika eneo hilo walikusanyika kutoa heshima zao za mwisho kwa waliouawa.

Eneo kubwa la kufanyia mazoezi, ndilo lililogeuzwa sehemu ya kuiaga miili ya walioangamia. Vilio vilisikika huko wakati masanduku meupe ya kubebea maiti, yaliyokuwa na picha za walioaga, yakibebwa na kuanza safari ya kuzikwa. Dharura ya Kitaifa iliyotangazwa na rais Ferdinand Marcos Jr. bado ilikuwa inaendelea Ufilipino wakati nchi hiyo ikijitayarisha kwa kimbunga kingine kinachopewa jina la Uwan.

Kulingana na mamlaka ya hali ya hewa ya Vietnam, kimbunga Kalmaegi kilichoambatana na upepo mkali kimeyang'oa mapaa ya nyumba na kimesomba miti na kuangusha minara ya mawasiliano.

Viwanja vya ndege vimefungwa 

Kutokana na janga hilo viwanja sita vya ndege vimefungwa wakati serikali ikisema watu 260,000 wamehamishwa kutoka mkoani Gia Lai na kupelekwa maeneo salama. Serikali imeongeza kuwa wanajeshi 268,000 wamewekwa tayaei kwa ajili ya operesheni za uokoaji na kuwatafuta waathiriwa wa kimbunga hicho.

Baada ya kimbunga Kalmaegi, kupiga maeneo hayo mawili, kazi ya uokoaji ilianza katika miji na vijiji vilivyoathiriwa katika nchi zote mbili Ufilipino na Vietnam barabi Asia. Watu walianza polepole kuondoa vifusi vya majengo yaliyoanguka na na kurekebisha paa za nyumba zao.

Jimmy Abatayo, aliye na miaka 53 na aliyempoteza mke wake na jamaa tisa wa karibu baada ya kimbunga kusababisha mafuriko katika jimbo la kati la Ufilipino la Cebu, alizidiwa na huzuni alipokuwa anapitisha mikono yake katika jeneza la mke wake.

"Nilifanikiwa kuogelea na kujiokoa, niliiambia familia yangu pia wajaribu kuogelea, kwamba waendelee kuogelea na wataokolewa, lakini hawakunisikiliza, kwahiyo sitowaona tena," alisema kwa majonzi makubwa huku akibubujikwa na machozi.

0 Comment

Watu 26 wafariki Kenya kufuatia maporomoko ya matope yaliyosababishwa na mvua kubwaAfyaclass Forum •

Maporomoko hayo ya matope yamechangiwa na kuendelea kunyesha kwa mvua kubwa

Waziri wa Mambo ya Ndani wa Kenya, Kipchumba Murkomen, ametoa wito kwa wakaazi katika eneo hilo kuwa waangalifu hasa wale wanaoishi sehemu za milima na kuwagiza mamlaka katika eneo hilo kuwahamisha watu walio hatarini hadi maeneo ya juu.

Kwa sasa polisi na shirika la msalaba mwekundu wanapiga doria katika eneo hilo kwa kutumia ndege aina ya helikopta ili kuweza kuwatambua waathiriwa waliohai walipo.

Waziri wa usalama wa ndani Kipchumba Murkomen amesema kwamba vikosi vya kitengo maalum cha uokoaji kutoka jeshi la Kenya KDF linashirikiana na polisi , wahudumu wengine wa dharura kusaidia kuwatafuta waliopotea na pia kutafuta ikiw akuna miiili iliyozikwa ardhini na tope.

Mvua kubwa inaripotiwa kunyesha usiku wa kuamkia Jumamosi Novemba 1 na kusababisha maji kujaa katika maeno yaliyo chini yam ilima katika bondo hilo la Kerio.

Usafiri katika eneo la tukio umesimamishwa kwa muda kwa sababu ya maji yaliyojaa kote na mapormoko ya ardhi. Wakazi wameombwa kutopanga safari ambazo zio za dharura kwa sasa hadi hali iwe nzuri. Maji wa mafuriko na maporomoko ya usiku wa kuamkia Jumamosi hii yalisomba baadhi ya nyumba katika eneo hilo.

Familia zilizoathirika zinapokea misaada ya mahali pa kulala, maji safi, dawa na chakula.

Idara ya utabiri wa hali ya hewa ya Kenya imesema kwamba maporomoko ya ardhi huenda yakatokea katika kaunti angalau 30 ambazo zinashuhudiwa viwango vya juu vya mvuwa.

Ajali hii inatokea siku chache tu baada ya ajali inyine kutokea nchini Uganda ambapo watu tisa walifariki, wakiwemo Watoto waliokutwa na mauti walipozikwa na mapormoko ya ardhi yaliyotokea katika maeneo mawili yaliyipo mashariki mwa Uganda.

Mapormoko hayo yalitokea katika miji ya milimani ya Bukwo na Kween usiku wa Jumatano October 29 kutokana na mvua kubwa iliyonyesha magharibi mwa Kenya na Mashariki mwa Uganda

0 Comment
Notification
My blog is in the process of editing and perfecting the new template, so there are still some functions to click but not yet used. Note which blogs associated with your side please read this lesson to update the blog logo.
UNDERSTOOD