Showing posts with label afyatips. Show all posts
Showing posts with label afyatips. Show all posts

Fahamu Vitu ambavyo Vinaharibu FIGO zako polepole bila kujuaAfyaclass Forum •

Fahamu Vitu ambavyo Vinaharibu FIGO zako polepole bila kujua

“Je, unajua kuna kitu unatumia kila siku ambacho kinaweza kuharibu figo zako polepole bila wewe kujua? Leo nakwambia ukweli ambao watu wengi hawajui!”

Baadhi ya Vitu ambavyo usipotumia kwa uangalifu huharibu kabsa Figo zako;

1.Kula chumvi nyingi kupita kiasi

Matumizi ya chumvi nyingi ni hatari kwa afya ya Figo kwani huweza kuongeza presha ya damu(Shinikizo la Damu)

Presha ya juu huharibu figo taratibu

2.Vinywaji vyenye sukari nyingi

Vinywaji kama Soda na juice za viwandani usipotumia kwa kiasi huweza kuleta madhara makubwa kwa figo zako, kwani vina kiwango kikubwa cha Sukari

3.Dawa za kienyeji zisizo na kipimo

Baadhi zina kemikali nzito (toxins),ambapo huumiza figo moja kwa moja

4.Matumizi mabaya ya dawa za maumivu

Fahamu kwamba Dawa zikitumika mara kwa mara bila ushauri wa daktari ikiwemo dawa za maumivu,pia huweza kusababisha matatizo ya Figo.

Huathiri mtiririko wa damu kwenye figo n.k.

5.Kunywa maji kidogo

Figo zinahitaji maji kusafisha sumu mwilini,

Upungufu wa maji huongeza hatari ya mawe kwenye figo na kupata matatizo mengine ya Figo.

6. Kula Vitu vyenye protein nyingi kupita kiasi

(hasa nyama nyekundu nyingi sana kila siku),Huongeza mzigo kwa figo kufanya kazi kupita kiasi.

 7. Kuvuta sigara

Hupunguza mtiririko wa damu kwenye figo,huongeza hatari ya magonjwa ya figo n.k

8. Pombe kupita kiasi

Huathiri uwezo wa figo kusafisha damu,Pia huongeza presha ya damu, vyote hivi huweza kuleta shida kwa Figo

Bonus Point;

 9. Maambukizi yasiyotibiwa mapema

Kama UTI (maambukizi ya njia ya mkojo),Yanaweza kuenea hadi figo na kuharibu figo zako

10. Magonjwa sugu kama kisukari na Shinikizo la Damu

Haya ndiyo visababishi vikubwa vya uharibifu wa figo duniani

Dalili za tahadhari (usizipuuze)

  • Miguu na uso kuvimba
  • Mkojo kuwa na povu au kubadilika rangi
  • Uchovu wa kupita kiasi
  • Maumivu ya chini ya mgongo n.k.

JE, UNA TATIZO HILI NA HUJAPATA TIBA BADO? Tuwasiliane kwa namba hizi: Call,Sms,Whatsapp +255758286584.

0 Comment

Unasikiliza Muziki mpaka ngozi inabadilika hivi? Una FrissonAfyaclass Forum •

Baadhi ya watu hupata baridi kali ya ghafla, mwili kutetemeka, mapigo ya moyo kwenda mbio pamoja na hisia kali kupita maelezo wanaposikiliza muziki wenye nguvu. Wataalam wa afya huita jambo hili kama Frisson, mwitikio wa kihisia na kisaikolojia unaosababishwa na sauti, melodi, au nyakati fulani za muziki.

Utafiti unaonyesha kwamba takriban 50–60% ya watu hupata frisson. Hutokea wakati ubongo unashughulikia sauti na hisia kwa nguvu iliyoongezeka, haswa katika maeneo yanayohusiana na zawadi na uchakataji wa kihisia(reward and emotional processing). Wakati wa nyakati hizi, ubongo hutoa Dopamine, kemikali ile ile inayohusiana na raha na motisha.

Mabadiliko madogo ya kimuziki—kama vile mabadiliko ya ghafla katika mdundo, noti yenye nguvu ya sauti, au mkusanyiko wa drama—yanaweza kusababisha mwitikio huu. Ubongo huunganisha kwa nguvu maana ya kihisia ya muziki na ishara za kusikia, na kuunda uzoefu wenye nguvu wa hisia.

Kwa kifupi, muziki unapokupa baridi, sio tu kuhusu wimbo wenyewe—ni kuhusu jinsi ubongo wako unavyoitikia sauti na hisia kwa njia ya kipekee.

0 Comment

Minyoo husababishwa na nini,Minyoo huingiaje mwiliniAfyaclass Forum •

Minyoo husababishwa na nini,Minyoo huingiaje mwilini

Njia ambazo minyoo huweza kuingia mwilini na kukushambulia ni Zipi?

Minyoo kwa binadamu hupatikana kutokana na vyanzo mbalimbali, hasa vinavyohusiana na usafi duni na mazingira.

Article author: Dr.Ombeni Mkumbwa
Reviewed: Afyaclass, MD's

Kwanini Unasikia Meza dawa za Minyoo Kila baada ya miezi 3, Miezi 6 na kuendelea hata kama huoni dalili zozote. Hii inatokana na Mazingira mengi tunayoishi yanakuwa na Kiwango kikubwa cha Minyoo hali ambayo hupelekea watu wengi kuipata bila wao kujua.

Katika Makala hii nmekuchambulia baadhi ya vyanzo vikuu vya kupata Minyoo,Soma hapa...

Hivi ndiyo vyanzo vikuu vya minyoo kwa mtu:

1. Kula Chakula kichafu

Kula mboga au matunda yasiyooshwa vizuri

Kula chakula kilichochafuliwa na mayai ya minyoo

Kula nyama au samaki wasioiva vizuri n.k

Vitu hivi huweza kuwa vyanzo vikuu vya wewe kuwa na Shida ya Minyoo

Ushauri: Hakikisha Mazingira ya kuandalia vyakula ikiwemo vyakula vyenyewe vinakuwa Safi

2. Kunywa Maji machafu

Kunywa maji yasiyochemshwa au yasiyotibiwa

Kutumia maji yaliyochafuliwa kupikia au kuosha vyombo

Ushauri: Kunywa maji Safi na Salama,maji yaliyochemshwa,kutibiwa n.k. Pamoja na vyombo vya kuhifadhia maji ya kunywa Viwe Visafi Sana.

3. Usafi binafsi duni

Kutokunawa mikono kabla ya kula au baada ya kutoka chooni huongeza hatari ya kuingiza minyoo kwenye mwili wako

Kucha ndefu zinazohifadhi uchafu na mayai ya minyoo, hii pia ni hatari kwa Watu wengi wanaofuga kucha bila wao kujua.

Ushauri: Hakikisha unanawa mikono kabla ya kula,baada ya kutoka chooni,Usafi wa kucha pia usisahau..

4. Kutembea peku au bila Viatu

Minyoo aina ya hookworm huingia mwilini kupitia ngozi ya mguu

Hutokea zaidi kwenye udongo wenye uchafu wa kinyesi

Ushauri: Usipende kutembea Peku,Vaa Viatu, hata kama ni Mkulima upo shambani usitembee peku kwenye Udongo hii ni hatari zaidi kushambuliwa na minyoo.

5. Vyoo visivyo salama

Kutumia vyoo vibovu au Vichafu sana hii huweza kuongeza hatari ya wewe kupata minyoo

Uchafu wa Vyoo huweza kuhusisha;

  • Mazingira yake kwa ujumla
  • Vyombo vya maji
  • Maji yenyewe yanayotumika n.k.
Pia kujisaidia eneo la wazi huweza kuongeza hatari ya minyoo kwani Huchafua udongo na maji pia.

Ushauri: Hakikisha vyoo vinakuwa Safi na Salama kwa matumizi muda wote

6. Kula Udongo

Wapo baadhi ya Watu hupenda kula Udongo ikiwemo watoto wadogo na wakina mama wajawazito, hii huweza kuwa chanzo kikubwa cha kupata Minyoo pia.

Ushauri: Acha Tabia ya kula Udongo,Lakini pia Mzuie mtoto wako kula Udongo

7. Kuambukizwa kutoka kwa mtu mwingine

Kugusana na mtu mwenye minyoo (hasa watoto)

Kushiriki vyombo, taulo au vitanda bila usafi

Vyote hivi huweza kuongeza hatari ya kupata Minyoo

Je,Una tatizo hilo na hujapata Msaada wa Tiba bado?

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU NA TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

➡️Dalili za Minyoo Soma hapa:https://www.afyaclass.com/2021/07/dalili-za-minyoo-jamii-ya-ascariasis.html

Rejea Sources:

  • https://www.cdc.gov/dpdx/hookworm/index.html
  • https://emedicine.medscape.com/article/218805-overview
  • https://australian.museum/learn/species-identification/ask-an-expert/what-are-worms/#:~:text=Many%20very%20different%20and%20unrelated,Flatworms%20are%20soft%2C%20unsegmented%20invertebrates.
  • https://www.who.int/news-room/fact-sheets/detail/soil-transmitted-helminth-infections

0 Comment

Je ni tatizo,Kwenda haja kubwa mara tu baada ya kula chakula?Afyaclass Forum •

Hitaji la kwenda chooni dakika chache tu baada ya kula ni tatizo ambalo watu wengi hukabiliana nalo kila siku.

Hili pia linaibua swali akilini, je, chakula tulichokula kimemeng'enywa ipasavyo?

Kulingana na wataalamu wa matibabu, moja ya sababu za haya ni kula kiasi kidogo wakati wa kazi na kula vitu vingi unavyopenda wakati wa likizo.

Lakini swali ni, je, ni kawaida kujisaidia haja kubwa mara baada ya kula au ni ishara ya ugonjwa?

Daktari bingwa wa magonjwa ya utumbo, Dkt. Mahadevan, anasema, "hitaji la kwenda chooni mara baada ya kula chakula inaitwa 'gastrocolic reflex'. Lakini watu wengi wana dhana potofu kwamba chakula kinacholiwa mara moja huwa kinyesi? Ilhali sivyo."

Je, chakula tunachokula hubadilika kuwa kinyesi kwa haraka?

Kuna matatizo kadhaa ambayo yanaweza kuhusishwa na ugonjwa wa utumbo

Kulingana na utafiti, kwa kawaida huchukua saa 10 hadi 73 kwa chakula kutoka mwilini kama kinyesi. Hii inaitwa 'muda wa kusafirisha chakula'.

Hata hivyo, wakati huu unategemea mambo mengi, kama vile umri wa mtu, jinsia, uzito na lishe.

0 Comment

Maji Kupita Kiasi Mwilini huweza Kusababisha Matatizo hayaAfyaclass Forum •

Maji ni muhimu sana kwa afya ya binadamu, lakini kama mwili ukiwa na maji mengi kuliko inavyohitajika, hali hii inaweza kusababisha matatizo makubwa kiafya. Hapa tunazungumzia hasara kuu zinazoweza kutokea kutokana na kuchukua au kushikilia maji mengi mwilini.

1. Kuongeza Uzito wa Mwili

Kushikilia maji mwilini, hali inayojulikana kama water retention, inaweza kuonekana haraka kwa kuongezeka kwa uzito. Hali hii inaweza kufanya mwili kuonekana kimebeba mafuta zaidi, ingawa siyo mafuta halisi, na pia inaweza kusababisha hisia ya kuvimba kwenye mikono, miguu, au tumbo.

2. Kuvimba kwa Viungo na Mishipa

Kama mwili unashikilia maji kupita kiasi, viungo kama mikono, miguu, vidole, na hata uso vinaweza kuvimba. Hali hii inajulikana kama edema. Edema inaweza kufanya kufanya kazi za kila siku kuwa ngumu, kwani mvuto wa maji unaongeza uchovu kwenye misuli na viungo.

3. Kuongeza Shinikizo la Damu

Maji mengi mwilini yanaweza kuongeza kiasi cha damu inayopita kwenye mishipa, hali inayosababisha shinikizo la damu kuongezeka. Shinikizo la damu lililo juu kwa muda mrefu linaweza kuongeza hatari ya magonjwa ya moyo, kiharusi, au kushindwa kwa figo.

4. Kuchangia Kazi Duni ya Figo

Figo linawajibika kusafirisha maji na chumvi mwilini. Wakati mwili unashikilia maji kupita kiasi, figo linaweza kuanza kushindwa kufanya kazi ipasavyo. Hii inaweza kusababisha maji kubaki mwilini na viwango vya chumvi kubadilika, hali inayosababisha matatizo ya kiafya kama kichefuchefu, kutapika, au uchovu.

5. Kuathiri Viwango vya Chumvi na Madini

Kuchukua maji kupita kiasi kunavuruga uwiano wa madini mwilini, hasa sodium na potassium. Hali hii inaweza kusababisha muscle cramps, udhaifu wa misuli, na matatizo ya moyo.

6. Kuongeza Hatari ya Magonjwa ya Moyo

Maji mengi mwilini yanaongeza mzigo kwa moyo na mishipa, jambo linaloweza kusababisha moyo kushindwa kufanya kazi ipasavyo. Watu wenye matatizo ya moyo wanapaswa kuwa makini sana na kumeza maji kupita kiasi.

7. Kudhuru Ubongo

Hali ya hyponatremia, ambayo hutokea pale mwili unashikilia maji kupita kiasi na kudhoofisha kiwango cha sodium katika damu, inaweza kuathiri ubongo. Dalili zake ni pamoja na kichefuchefu, kizunguzungu, mkazo wa kichwa, na hata kutoelewa hali. Katika hali mbaya, inaweza kusababisha fahamu kupotea au kifo.

Hitimisho

Kuwa na maji mwilini ni muhimu, lakini kuzidi kiasi kinachohitajika kunaweza kuwa hatari kiafya. Ili kuepuka matatizo haya, ni muhimu kunywa maji kwa kiasi kinachofaa na kufuata ushauri wa daktari, hasa ikiwa una hali zinazohusiana na moyo, figo, au mishipa. Mwili wenye maji sawa na mahitaji yake ni mwili wenye afya na nguvu zaidi.

0 Comment
Notification
My blog is in the process of editing and perfecting the new template, so there are still some functions to click but not yet used. Note which blogs associated with your side please read this lesson to update the blog logo.
UNDERSTOOD