Fahamu Vitu ambavyo Vinaharibu FIGO zako polepole bila kujua
“Je, unajua kuna kitu unatumia kila siku ambacho kinaweza kuharibu figo zako polepole bila wewe kujua? Leo nakwambia ukweli ambao watu wengi hawajui!”
Baadhi ya Vitu ambavyo usipotumia kwa uangalifu huharibu kabsa Figo zako;
1.Kula chumvi nyingi kupita kiasi
Matumizi ya chumvi nyingi ni hatari kwa afya ya Figo kwani huweza kuongeza presha ya damu(Shinikizo la Damu)
Presha ya juu huharibu figo taratibu
2.Vinywaji vyenye sukari nyingi
Vinywaji kama Soda na juice za viwandani usipotumia kwa kiasi huweza kuleta madhara makubwa kwa figo zako, kwani vina kiwango kikubwa cha Sukari
3.Dawa za kienyeji zisizo na kipimo
Baadhi zina kemikali nzito (toxins),ambapo huumiza figo moja kwa moja
4.Matumizi mabaya ya dawa za maumivu
Fahamu kwamba Dawa zikitumika mara kwa mara bila ushauri wa daktari ikiwemo dawa za maumivu,pia huweza kusababisha matatizo ya Figo.
Huathiri mtiririko wa damu kwenye figo n.k.
5.Kunywa maji kidogo
Figo zinahitaji maji kusafisha sumu mwilini,
Upungufu wa maji huongeza hatari ya mawe kwenye figo na kupata matatizo mengine ya Figo.
6. Kula Vitu vyenye protein nyingi kupita kiasi
(hasa nyama nyekundu nyingi sana kila siku),Huongeza mzigo kwa figo kufanya kazi kupita kiasi.
7. Kuvuta sigara
Hupunguza mtiririko wa damu kwenye figo,huongeza hatari ya magonjwa ya figo n.k
8. Pombe kupita kiasi
Huathiri uwezo wa figo kusafisha damu,Pia huongeza presha ya damu, vyote hivi huweza kuleta shida kwa Figo
Bonus Point;
9. Maambukizi yasiyotibiwa mapema
Kama UTI (maambukizi ya njia ya mkojo),Yanaweza kuenea hadi figo na kuharibu figo zako
10. Magonjwa sugu kama kisukari na Shinikizo la Damu
Haya ndiyo visababishi vikubwa vya uharibifu wa figo duniani
Dalili za tahadhari (usizipuuze)
- Miguu na uso kuvimba
- Mkojo kuwa na povu au kubadilika rangi
- Uchovu wa kupita kiasi
- Maumivu ya chini ya mgongo n.k.
JE, UNA TATIZO HILI NA HUJAPATA TIBA BADO? Tuwasiliane kwa namba hizi: Call,Sms,Whatsapp +255758286584.





