Showing posts with label hali ya hewa. Show all posts
Showing posts with label hali ya hewa. Show all posts

TMA yatoa tahadhari ya hali Mbaya ya Hewa kwa siku 5Afyaclass Forum •

TMA yatoa tahadhari ya hali Mbaya ya Hewa kwa siku 5

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari ya hali mbaya ya hewa kwa siku tano zijazo, kuanzia leo Jumatatu, Oktoba 27, 2025.

Aidha katika taarifa yake kwa umma imeonya wakazi wa mikoa kadhaa ya pwani na maeneo ya Kaskazini-Mashariki mwa nchi kujiandaa kwa mvua kubwa, upepo mkali, na mawimbi makubwa baharini.

Taarifa iliyotolewa na Mamlaka hiyo jana Jumapili imebainisha kuwa hali mbaya zaidi inatarajiwa kuanza leo Jumatatu na Jumanne katika maeneo yaliyotajwa.

Aidha TMA katika taarifa yake iuliyotolewa jana Jumapili imesema kwamba leo Jumatatu, Oktoba 27, 2025, TMA mvua kubwa inatarajiwa kunyesha kwa baadhi ya maeneo ya Mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani (ikijumuisha visiwa vya Mafia) na Morogoro. Pia tahadhari hiyo imetolewa kwa visiwa Visiwa vya Unguja na Pemba.

“Kiwango cha athari zinazoweza kutokea ni kubwa… tunatarajia baadhi ya makazi kuzungukwa na maji, pamoja na kuathirika kwa baadhi ya shughuli za kiuchumi, uvuvi na usafirishaji baharini,” ilisema sehemu ya taarifa hiyo.

Wakati huo huo, angalizo la upepo mkali unaofikia kilomita 40 kwa saa na mawimbi makubwa yanayofikia mita 2 limetolewa kwa ajili ya ukanda wote wa pwani ya Bahari ya Hindi, ikijumuisha mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani (Mafia), Lindi, Mtwara na visiwa vya Unguja na Pemba.

Imeelezwa kuwa hali inatarajiwa kupungua kidogo Jumanne, Oktoba 28, 2025,japo kuna angalizo la mvua kubwa kwa maeneo machache ya mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Tanga, Dar es Salaam, Pwani (Mafia) na Morogoro.

Mamlaka hiyo imewashauri wananchi wanaoishi katika maeneo ya hatari kuchukua tahadhari za kutosha, huku ikiwakumbusha wadau wa bahari, hasa wavuvi, kuwa makini katika kipindi chote cha tahadhari hiyo.

0 Comment

Tsunami yaipiga Urusi pamoja na JapanAfyaclass Forum •

Madhara na uhamishwaji wa watu umeripotiwa kwenye mikoa ya Urusi iliyo karibu na kitovu cha tetemeko hilo katika Rasi ya Kamchatka.



Tetemeko hilo ni kubwa kabisa kuwahi kulipiga eneo hilo tangu mwaka 1952, kwa mujibu wa Mamlaka ya Jiolojia ya Urusi.

Tsunami iliyopelekea mawimbi ya bahari yenye ukubwa wa hadi mita 30 imeripotiwa katika visiwa vya Hokkaido vya Japan na visiwa vya Kuril vinavyomilikiwa na Urusi, na yanakhofiwa kuelekea pia Ufilipino, Chile na Visiwa vya Solomon.

Tayari Ufilipino nayo imetangaza tahadhari ya kiwango cha juu ya tsunami.

Athari za tetemeko hilo zinatazamiwa kuonekana hadi nchini Marekani kwenye miji ya Carlifornia na Washington. 

0 Comment

Ripoti Mpya;Ongezeko la Joto Duniani lisilolakawaidaAfyaclass Forum •

Kulingana na ripoti mpya iliyotolewa na Huduma ya Mabadiliko ya Tabia nchi ya Muungano wa Ulaya ya Copernicus, wastani wa hali joto duniani umekuwa juu ya nyuzi joto 1.5 za Selsiasi kwa miezi 12 mfululizo jambo ambalo si la kawaida na mara ya mwisho kushuhudia hali kama hii ilikuwa mwaka 2015/2018.

Data za Huduma ya Mabadiliko ya Tabia nchi ya Muungano wa Ulaya, Copernicus ERA5, zinaonesha kwamba mwezi juni ulikuwa na nyuzi joto 1.50 za Selsiasi juu ya makadirio ya awali ya Mwezi Juni kwa mwaka 1850 – 1900 wakati wa mapinduzi ya viwanda ikiwa huu ni mwezi wa 12 mfululizo hali joto kuvuka nyuzi joto 1.5.

“Takwimu hizi za hivi karibuni  kutoka kwa Huduma ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa ya Copernicus kwa bahati mbaya zinaangazia kwamba tutakuwa tukizidi kiwango cha nyuzijoto 1.5 za selsiasi kwa muda na kuongezeka kwa marudio, kila mwezi. Hata hivyo, ni muhimu kusisitiza kwamba ukiukaji wa muda mfupi haumaanishi kuwa lengo la 1.5 °C litapotea kabisa kwa sababu hii inahusu ongezeko la joto la muda mrefu kwa angalau miongo miwili,” Anasema Katibu Mkuu wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) Celeste Saulo.

Katika mkataba wa Paris, nchi zilikubaliana kuweka wastani wa halijoto wa muda mrefu  kuwa ni chini ya nyuzi joto 2 kabla ya kuanza kwa viwanda na baadae wakaweka kikomo hadi nyuzi joto 1.5 kufikia mwisho wa karne hii, huku wanasayansi wameonya mara kwa mara kwamba ongezeko la joto la zaidi ya nyuzi joto 1.5 linasababisha athari mbaya zaidi za mabadiliko ya tabianchi.

Hata, Katika viwango vya sasa vya ongezeko la joto duniani, tayari kuna athari mbaya za hali ya hewa ambazo ni Pamoja na joto kali, mvua kali na ukame, barafu ya bahari, kuongeza kasi ya kupanda kwa kina cha bahari na joto la bahari.

“Juni ilishuhudiwa kuenea na kuongezeka kwa joto kwa muda mrefu katika nchi nyingi, na athari kubwa katika nyanja zote za maisha ya watu. Hii ilikuwa hata kabla ya kilele cha jadi cha majira ya joto ya kaskazini mwa ulimwengu, ambayo bila shaka itaona joto kali zaidi. Halijoto iliyorekodiwa kwenye uso wa bahari inatia wasiwasi mkubwa kwa mifumo ya ikolojia ya baharini na pia inatoa nishati kwa vimbunga vya kitropiki vinavyoshangaza zaidi – kama tulivyoona kwenye Kimbunga Beryl,” Amesema Celeste Saulo.

WMO hutumia hifadhi data sita za kimataifa, ikiwa ni pamoja na ERA5, kwa hali yake ya ufuatiliaji wa tabianchi. Ni muhimu kutambua kwamba hifadhi data nyingine huenda zisithibitishe mfululizo wa miezi 12 ulioangaziwa na Huduma ya Mabadiliko ya Tabianchi ya Copernicus, kutokana na ukingo mdogo zaidi ya nyuzi joto 1.5 ya viwango vya joto duniani ERA5 kwa Julai na Agosti 2023 na Mei na Juni 2024.

Mkurugenzi wa Huduma ya Mabadiliko ya Tabianchi ya Copernicus, Carlo Buontempo anatoa tahadhari kwamba hata kama hali hii ya kuongeza kwa hali joto itaisha kwa wakati Fulani, lakini kuna uwezekano mkubwa wa jambo hili kujirudia tena, hivyo dunia inapaswa kuangalia namna ya kuacha kuongeza hewa chafu kwenye ang ana bahari ili kuepukana na athari za baadae endapo jambo hili litajirudia tena.

Ripoti Mpya;Ongezeko la Joto Duniani lisilolakawaida
0 Comment

TMA yataja chanzo cha mvua zinazonyesha kwa Sasa,baadhi ya maeneoAfyaclass Forum •

TMA yataja chanzo cha mvua zinazonyesha kwa Sasa,baadhi ya maeneo

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imesema, mvua zinazoendelea kunyesha tangu jana katika baadhi ya mikoa nchini zimetokana na kuongezeka kwa joto la bahari magharimbi mwa Bahari ya Hindi katika mwambao wa pwani wa nchi.

Mvua hizo ziliibua sintofahamu kutokana na majira ya Juni kuwa ya kipupwe, huku TMA ikitaja mikoa ambayo inapata mvua hizo.

Mikoa hiyo ni yote  ya ukanda wa Pwani,ukanda wa ziwa Victoria kwenye mikoa ya Kagera, Simiyu, Geita na Mara na maeneo ya Nyanda za juu Kaskazini Mashariki katika mikoa ya Kilimanjaro, Arusha na Manyara na Kaskazini mwa mkoa wa Kigoma.

Meneja wa Utabiri wa TMA, Dk Mafuru Kantamla leo Jumatano Juni 19, 2024 ameiambia Mwananchi Digital kwamba mvua hizo hazina madhara.

“Ni mvua za kawaida, kama itatokea mifumo ikasoma zitakuwa na madhara pia tutasema, watu waendelee kufuatilia utabiri kwa kuwa mifumo inapoimarika zaidi ndipo kunasababisha mvua kuwa nyingi kidogo, kwa sasa mifumo inaonyesha mvua hizi hazina madhara,” amesema.

Amesema, kwenye ukanda wa pwani mvua zitayesha leo Juni 19 na kesho Juni 20 kisha itapungua na vipindi vya jua vitaendelea kama kawaida baada ya siku hizo mbili.

“Hata mikoa mingine, si kama zitakuwa na muendelezo, mifumo inaonyesha ni za kutafuta na ilionekana katika msimu huu wa kipupwe pamoja na kuwa na vipindi vya ukavu na upepo mkali, kutakuwa na mvua kutokana na kuongezeka kwa joto Magharibi mwa Bahari ya Hindi.” amesema.

TMA yataja chanzo cha mvua zinazonyesha kwa Sasa,baadhi ya maeneo
0 Comment
Notification
My blog is in the process of editing and perfecting the new template, so there are still some functions to click but not yet used. Note which blogs associated with your side please read this lesson to update the blog logo.
UNDERSTOOD