Showing posts with label magonjwa ya watoto. Show all posts
Showing posts with label magonjwa ya watoto. Show all posts

Kitovu Cha Mtoto kikidondokea sehemu za siri – kinaathiri nguvu za kiume?Afyaclass Forum •

Kitovu Cha Mtoto kikidondokea sehemu za siri – kinaathiri nguvu za kiume?

Hii si kweli kabisa (ni imani tu).

Kitaalamu:

  • Kitovu ni mabaki ya kamba ya uzazi (umbilical cord)
  • Hakihusiani kwa namna yoyote na ukuaji wa uume, korodani au homoni za kiume
  • Nguvu za kiume zinategemea:
    • Homoni kama testosterone
    • Afya ya mishipa ya damu
    • Mfumo wa uzazi

Hivyo, kitovu kuangukia sehemu yoyote hakina uwezo wa kumfanya mtoto awe hanithi au apungukiwe nguvu za kiume.

Kitovu kinatakiwa kidondokee wapi?

Kitaalamu:

  • Hakuna sehemu maalum kinatakiwa kudondokea
  • Kinaweza kuanguka:
    • kwenye nguo
    • kitandani
    • ardhini
    • hata karibu na mwili wa mtoto

Muhimu si mahali kinapoangukia, bali:

  • Kianguke chenyewe (bila kung’olewa)
  • Hakina maambukizi
  • Eneo libaki safi na kavu

Kwa nini imani hizi zipo?

Katika jamii nyingi:

  • Kitovu huonekana kama sehemu muhimu ya uhai wa mtoto akiwa tumboni
  • Hivyo watu walihusisha na mambo ya nguvu au hatima ya mtoto
    Lakini hizi ni tafsiri za kitamaduni, si za kitabibu.

Hitimisho la kitaalamu

Kitovu hakina athari yoyote kwa nguvu za kiume, Hakina sehemu maalum ya kudondokea,Hakina uhusiano na uchawi kwa mtazamo wa sayansi ya tiba.

Rejea: Kitovu cha Mtoto hakikauki,Kinatoa damu,Usaha,Sababu zake>>>
0 Comment

Tatizo la KITOVU cha mtoto mchanga hakikauki,Kinatoa Usaha,DamuAfyaclass Forum •

KITOVU cha mtoto mchanga hakikauki,Kinatoa Usaha,Damu,Sababu ni nini?

Zipo dalili mbali mbali huweza kujitokeza kwenye Kitovu cha Mtoto wako,Ukiona Dalili hizi,hakikisha Mtoto anapata Msaada, Dalili hizi ni hatarishi sio nzuri wake:

  • Kitovu kinatoa usaha wenye harufu mbaya
  • Damu inatoka mara kwa mara
  • Ngozi kuzunguka kitovu kuwa nyekundu au kuvimba
  • Mtoto ana homa au analia sana
  • Kitovu hakikauki hata baada ya siku 7–14

Sababu zinazoweza kusababisha

1.Maambukizi ya bakteria (kutokana na uchafu au utunzaji mbaya)

2.Kitovu kubaki na unyevunyevu muda mrefu

3.Kitovu Kuguswa na vitu vichafu (mfano majivu, mafuta, dawa za asili zisizo salama) n.k

Nini cha kufanya

Hii ni hali ya muhimu—usichelewe:

Mpeleke mtoto hospitali au kituo cha afya mara moja Au Ongea na Mtaalam wa Afya au Kwa Ushauri Zaidi na Tiba tuwasiliane hapa hapa afyaclass,kupitia namba +255758286584(Call,Sms,Whatsapp).

-Usitumie dawa za kienyeji au kubonyeza kitovu bila Ushauri Sahihi.

-Acha kitovu kiwe kikavu (dry cord care) usiweke maji au Vitu vitakavyoongeza unyevu unyevu

-Epuka kukifunika kwa diaper

-Usikigusie mara kwa mara

Kwa mtoto mchanga, maambukizi ya kitovu yanaweza kuenea haraka mwilini, hivyo ni muhimu kuchukua hatua mapema.

YAPO BAADHI YA MAMBO MUHIMU SANA YA KUZINGATIA KUHUSU KITOVU CHA MTOTO

1-Mama hakikisha kitovu cha mtoto hakivuji damu baada ya kukatwa na kufungwa na mtaalam wa afya.

2-Kitovu hudondoka chenyewe,ambapo kwa asilimia kubwa kwa watoto wengi ndani ya wiki moja,kitovu huwa tayari kimeshadondoka.

3-Hakikisha kitovu cha mtoto hakitoi usaha,au kubalika rangi hasa ya manjano na kutoa harufu mbaya,hii sio dalili nzuri.

4-Usiweke kitu chochote kwenye kitovu cha mtoto mpka kidondoke chenyewe.

5-Epuka imani potofu kama zile za kuweka mavi ya Ng'ombe n.k,kwenye kitovu cha mtoto.

KWA USHAURI,ELIMU AU MSAADA WA KIAFYA MAWASILIANO NI +255758286584.

0 Comment

Kuvimba kwa Uume wa Mtoto kwa Mbele sababu ni ipi?Afyaclass Forum •

Kuvimba kwa Uume wa Mtoto kwa Mbele sababu ni ipi?

Kuvimba kwa ngozi ya mbele ya uume (govi) kwa mtoto mara nyingi husababishwa na mambo haya:

1. Maambukizi (Balanitis au Balanoposthitis)

Hii ni kuvimba kwa kichwa cha uume na govi kunakosababishwa na maambukizi ya:

  • Bakteria
  • au Fangasi (kama Candida)

Dalili zake:
  • Uume kuwa mwekundu na kuvimba
  • Maumivu au mtoto kulia wakati wa kukojoa
  • Wakati mwingine usaha au harufu mbaya kutokea eneo hili

2. Kujikusanya kwa uchafu chini ya govi

Kwa watoto wadogo govi huwa halijafunguka kabisa (hali ya kawaida). Uchafu au mkojo ukibaki ndani unaweza kusababisha uvimbe.

3. Kuumia au msuguano

Inaweza kutokana na:

  • Diaper alizovaa kubana sana
  • Kuguswa au msuguano sana wakati wa kuoshwa n.k.

4. Hali inayoitwa Phimosis

Kwa watoto wadogo govi huwa halivutiki nyuma kabisa. Wakati mwingine linaweza kuvimba kidogo hasa likijaa mkojo kabla ya kutoka.

Mambo ya kufanya nyumbani:

  • Osha uume kwa maji safi ya uvuguvugu
  • Badilisha diaper mara kwa mara
  • Usivute govi kwa nguvu (kwa mtoto mdogo ni kawaida lisivutike)

Mwone daktari haraka kama:

  • Uvimbe ni mkubwa sana
  • Kuna usaha au harufu kali
  • Mtoto analia sana wakati wa kukojoa
  • Hatoi mkojo vizuri
  • Homa ipo

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU NA TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

0 Comment

Nyama za puani kwa Watoto,chanzo,dalili na TibaAfyaclass Forum •

Nyama za puani kwa Watoto,chanzo,dalili na Tiba

Tatizo la nyama za puani ni tatizo ambalo huweza kuwapata watoto pia, hali ambayo husababisha mtoto kupata shida mbali mbali ikiwemo ya Kupumua.

Dalili za Nyama za puani kwa Watoto

Ikiwa Mtoto wako ana shida ya nyama za puani huweza kuonyesha dalili mbali mbali ikiwemo;

– Kutoa Sauti wakati wa kupumua au mtoto kukoroma(Snoring)

– Kupata shida ya kupumua(kuvuta hewa na kutoa hewa)

– Mtoto kupumua kwa kutumia mdomo badala ya Pua

– Mtoto kuwa na mafua ambayo hayakatiki, ya mara kwa mara

– Mtoto kuvimba pua au kuwa na shida ya Runny nose

– Kupungua kwa uwezo wa kunusa na kusikia harufu ya vitu mbali mbali(Decreased sense of smell)

Mtoto wako anaweza kulalamika kwamba hawezi kunusa na kusikia harufu ya vitu au kuonja chakula na kupata ladha yake, ambayo hii ni athari ya kupungua kwa hisia ya kunusa.

– Pia mtoto anaweza kuonekana kama kuna kitu anajiribu kumeza mara kwa mara, kwa lengo la kusafisha koo na njia ya hewa kwa ujumla,

Na wakati mwingine mtoto anaweza kulalamika kuhisi hali ya muwasho kooni,vidonda n.k

Chanzo cha Nyama za puani kwa Watoto

Sababu halisi ya kusababisha nyama za puani kwa mtoto haijulikani;

“The exact cause of nasal polyps is not known”
Ingawa sababu hizi huongeza hatari ya kupata nyama za puani kwa mtoto;

–  Tatizo la mzio au Allergic rhinitis, ikiwa mtoto anapata shida ya mzio kwa baadhi ya vipindi huweza kupata shida ya nyama puani, kuvimba eneo la pua n.k

–  Tatizo la Cystic fibrosis, ambapo husababisha mucus kwenye mapafu pamoja na viungo vingine vya mwili kuwa nzito kupita kiasi hali ambayo huweza kupelekea maambukizi ya viini vya magonjwa kwa muda mrefu, kupumua kwa shida n.k,

na mara nyingi tatizo hili hugundulika kwa watoto kuanzia miaka 2

– Tatizo la pumu kwa watoto(Asthma), n.k

Matibabu ya Nyama za puani kwa Watoto

Baada ya kuona dalili zozote kama nilivyoorodhesha hapo awali, hakikisha mtoto wako anapata tiba ya tatizo hili la nyama za puani

– Soma Zaidi hapa kuhusu tatizo la Nyama za Puani

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.


0 Comment
Notification
My blog is in the process of editing and perfecting the new template, so there are still some functions to click but not yet used. Note which blogs associated with your side please read this lesson to update the blog logo.
UNDERSTOOD