YAI LA MWANAMKE NA MBEGU YA MWANAUMEAfyaclass Bongo Social •

 Yai la mwanamke(ovum) linapotoka kwenye vifuko vyake(ovaries) ambapo kitendo hicho kitaalam huitwa "OVULATION" na kuingia kwenye mirija ya uzazi yaani Fallopian tubes,Ndipo huanza kukutana na mbegu za kiume(Sperms) na hatua ya kwanza ya kutengeneza mtoto huanzia hapo(FERTILIZATION).

Siku ambapo yai linatoka kwenye vifuko vyake,ndyo tunaita SIKU YA HATARI-Tukiwa na maana kwamba ni siku ambayo mwanamke anaweza kupata MIMBA.

JE UNAZIJUA SIKU ZA HATARI KWAKO?

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Karibu Sana..!!!



0 Comment

JE KUVUJA DAMU MAPEMA KATIKA UJAUZITO NI NINI?Afyaclass Bongo Social •

 Je, kuvuja damu mapema katika ujauzito ni nini?


Kuvuja damu kabla ya wiki 28 za ujauzito hudhaniwa kuwa ni kuvuja damu mapema katika ujauzito. Ikitokea baada ya wiki 28, huitwa utokaji wa damu wa baadaye katika ujauzito. 

.

Mgawanyo huu wa wiki 28 umezingatia uwezekano wa kuishi ikiwa mtoto atazaliwa kabla ya tarehe iliyotarajiwa katika wiki 28. Matumaini ya kuishi kabla ya wiki 28 ni madogo sana katika nchi nyingi zinazoendelea maana kuna upungufu wa vifaa vya afya vya utunzaji maalum kwa watoto wanaozaliwa kabla ya wakati.

.

 Siku hizi nchi zingine zimepunguza mgawanyo huu hadi wiki 20 kwa sababu ya utunzaji ulioimarishwa na teknolojia inayotolewa na mfumo wao wa afya.


Visababishi vikuu vya kuvuja damu mapema katika ujauzito ni 

-utokaji wa mimba au mimba kutishia kutoka.

 -mimba iliyotungwa nje ya kizazi au uterasi (hapa mtoto hujishikiza na kukua nje ya kizazi au uterasi),

-Uvimbe kwenye kizazi

-Kondo la nyuma au placenta kuachia ambapo kitaalamu huitwa (placenta abruption)

-Kondo la nyuma kushuka chini hali inayojulikana kama Placenta previa

-Mama mjamzito kupigwa au kuanguka na kupelekea mshtuko kwny tumbo la uzazi n.k

#kuvujadamu

#Mjamzito 

#ombenimkumbwa

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Karibu Sana..!!!



0 Comment

TATIZO LA MIMBA ZA UTOTONIAfyaclass Bongo Social •

 Mimba za Utotoni(Teenage Pregnancy). Kwa Tanzania tunaweza tukasema ukipata mimba chini ya Miaka 18 upo kwenye kundi hili la mimba za utotoni.

.

Point yangu ni kwamba,mimba za utotoni zina madhara kila kona katika maisha ya mhusika,Lakini pia jamii yake.

.

Madhara ni pamoja na mtoto kufukuzwa shule, kupoteza Dira ya maisha, Lakini pia kupatwa na madhara makubwa ya kiafya kama kujifungua kwa Upasuaji,Kupoteza maisha wakati wa kujifungua n.k.

.

Takwimu zinaonyesha kuwa asilimia kubwa ya wanawake waliopata mimba au ujauzito katika umri mdogo hujifungua kwa UPASUAJI.

.

Maisha ya kuwa mama Yanahitaji maandalizi, Swala la Mimba za utotoni huchangiwa na sababu nyingi,ikiwemo hali ya kiuchumi,vishawishi, Mambo ya mila pia kama swala la NDOA ZA UTOTONI.

@Naomba utambue mimba za utotoni huharibu maisha ya mwanamke,

#mimbazautotoni 

#ombenimkumbwa

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Karibu Sana..!!!



0 Comment

DALILI ZA MSONGO WA MAWAZO KWA MAMA BAADA YA KUJIFUNGUAAfyaclass Bongo Social •

 📸Msongo wa mawazo baada ya mama Kujifungua ambao huambatana na tabia za kutaka kujiua"Severe depression accompanied with suicidal behavior".🤔

.

DALILI ZA MSONGO WA MAWAZO KWA MAMA BAADA YA KUJIFUNGUA.😘

Utajuaje kuwa mama yupo kwenye msongo wa mawazo,ili umsaidie kumpeleka kupata ushaur wa kutosha au Deep conseling.#####

.

1-Mama kupoteza mood na tumain "hopeless" kabsa la kuishi hapa huonyesha tabia kama kutaka kujiua au kumuua mtoto.

Ukiona hali hii mama anahitaji msaada wa haraka

2-Mama kulia sana pasipo sababu zinazoeleweka

3-Difficulty bonding with baby(Mama kuwa mbali na mtoto) 

4-Mama kuona aibu kwa watu na kujiona mkosaji kila mda na kwa kila anachokifanya

5-Mama kujiona kapoteza mvuto baada ya kujifungua na kila mda anaonekana kujihurumia

6-Mama kuwa na hofu kuu"severe anxiety"

@Zipo sababu ambazo zinachangia hali hii,see you next lesson

#msongowamawazo

#Severedepression

#ombenimkumbwa


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Karibu Sana..!!!



0 Comment

MATOKEO YA MUINGILIANO WA RHESUS FACTOR KWA UJAUZITO(KWA MAMA MWENYE BLOOD GROUP NEGATIVE NA BABA POSITIVE) HASA KATIKA UJAUZITO WA PILIAfyaclass Bongo Social •

 MATOKEO YA MUINGILIANO WA RHESUS FACTOR KWA UJAUZITO(KWA MAMA MWENYE BLOOD GROUP NEGATIVE NA BABA POSITIVE) HASA KATIKA UJAUZITO WA PILI


1) Mtoto alieo tumboni kupungukiwa damu (Fetal anemia)


2) Mtoto kuvimba akiwa tumboni (oedema)


3) Mtoto kuvimba tumbo akiwa tumboni (ascitis)


4) Moyo wa mtoto kujaa maji akiwa tumboni (pericardial effusion)


5) Mapafu ya mtoto kujaa maji (pleural effusion)


6) Mtoto kufia tumboni (IUFD)


7) Mimba kuharibika (misacariage)


JE HALI HII HUTAMBULIWAJE?

Kutambua kama kuna muingiliano wa rhesus kwa ujauzito Fulani vipo vipimo vya kuangalia kama mtoto ana shida yeyote au la;vilevile vipo vipimo vya kuangalia kama mama ametengeneza kingamwili kwa ajili ya kumshambulia mtoto au la. Vipimo hivo ni kama ultrasounds,kupima maji ya mtoto(amniotic fluid analysis),kupima damu ya mama na mtoto aliepo tumboni na aliezaliwa.

Vipimo hivi hufanyika ili kubaini kama kuna madhara makubwa kwa mtoto ili kusaidia katika kumtibu,mfano kwa walioendelea hua wakikuta mtoto aliepo tumboni ana upungufu mkubwa wa damu basi huongezewa damu na kupata dawa zingine akiwa humo humo tumboni na hivo kuokoa maisha yake.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Karibu Sana..!!!



0 Comment

FANGASI WA MDOMONI NA MAENEO MENGINEAfyaclass Bongo Social •

 FANGASI WA MDOMONI NA MAENEO MENGINE

FANGASI inaweza kushambulia maeneo mbali mbali ya mwili wako mfano; mdomoni,miguuni au sehem za siri. 

Kwa asilimia kubwa WANAWAKE wanateswa sana na FANGASI wa ukeni, na moja ya dalili mbali mbali za ugonjwa huu ni pamoja na kuwashwa mara kwa mara sehem za siri,pamoja na kutokwa na uchafu wenye rangi tofauti tofauti kama maziwa n.k

KAMA UNA TATIZO HILO TUWASILIANE UPATE MSAADA +255758286584.


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Karibu Sana..!!!




0 Comment

MAUMIVU MAKALI YA KICHWAAfyaclass Bongo Social •

 MAUMIVU MAKALI YA KICHWA

. Kipandauso (Migrain)

Aina hii ya maumivu ya kichwa ya awali ndiyo iliyoenea sana na watu wengi wanaosumbuliwa na maumivu ya kichwa ya mara kwa mara huwa na tatizo hili. Maumivu haya yanaweza kuwa ya upande mmoja; lakini yanaweza kuwa katika paji la uso pia na kusikika katika eneo lote la paji la uso, na shingo.


Aina hii ya maumivu ya kichwa huwa ni ya “kichwa kugonga” (throbbing pain) na huambatana na dalili kama vile kichefuchefu na/au kutapika, kizunguzungu, macho kushindwa kuona vizuri, macho kuuma yanapoangalia mwanga. Aina hii ya maumivu ya kichwa huzidishwa na kutembea au kujisogeza kwa namna yoyote, na mgonjwa hujisikia nafuu akipumzika/kulala; kwa kawaida, maumivu haya huwa makali kwa muda wa masaa 1-2, na yanaweza kuchukua kati ya saa 4 hadi 72. Vitu ambavyo huweza kusababisha mtu mwenye tatizo la migraine kuanza kuumwa kichwa (triggers) ni kama vile vinywaji vyenye kemikali ya caffeine au pombe/sigara, mawazo, uchovu/usingizi, hasira, kwa kinadada kama akiwa anakaribia siku zake, au kwenye siku zake, mwanga mkali/sauti.


Aina hii ya maumivu ya kichwa pia huwasumbua zaidi wanawake ambao wako katika umri wa kuweza kushika mimba ambao ndio wameanza kupata hedhi zao kipindi cha karibuni. Pia, migraine huweza kurithiwa kutoka kwa wazazi kwa sababu mara nyingine husababishwa na vitu ambavyo viko kwenye vinasaba (genetics) za uzao husika.


Pia, aina hii ya maumivu ya kichwa mara nyingi hutanguliwa na ‘dalili za kabla’ (aura), ambazo hutokea kwa kati ya dakika 5-20, na hudumu si zaidi ya dakika 60; dalili hizi za kabla zinaweza kuwa kizunguzungu, kichefuchefu,mwili kukosa nguvu, n.k.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Karibu Sana..!!!



0 Comment

MAUMIVU YA KIUNO, NYONGA, NA TUMBO LA CHINI KWA WANAWAKEAfyaclass Bongo Social •

 JE, WAJUA VYANZO VYA MAUMIVU YA KIUNO, NYONGA, NA TUMBO LA CHINI KWA WANAWAKE?


(@kwa ushauri,elimu,au msaada juu ya afya yako MWANAMKE +255758286584)


Maumivu ya kiuno,nyonga,au tumbo chini ya kitovu, yanaweza kusababishwa na tatizo moja au zaidi kama ifuatavyo;


Matatizo kwenye mfumo wa uzazi


Vivimbe kwenye kuta za tumbo la uzazi


Hali ya tishu zinazoota ndani ya ukuta wa uzazi(endometriosis) au kuota nje ya ukuta wa mji wa uzazi.


Maumivu wakati wa hedhi ambayo hutokana na vivimbe katika kuta za tumbo la uzazi


Mimba kutunga nje kizazi(ectopic pregnancy)


Maumivu yanayotokea upande mmoja chini ya kitovu katikati ya mzunguko wa hedhi yaani siku ya 14


Saratani kwenye mifuko ya mayai


Maambukizi kwenye mfumo wa uzazi ambayo hutokana na bakteria wanaosababisha kisonono, na klamidia,UTI,PID au Fangasi. Watu wengi wamekuwa wakipatwa na magonjwa haya pale wanapojaribu kupata ujauzito bila mafanikio(ugumba) au wanaposumbuliwa kwa muda mrefu na Maumivu ya kiuno na nyonga.


Vivimbe kwenye kuta za kizazi(uterine fibroids) ambavyo hutokana na mvugiko wa homoni ama kurithi kwa vinasaba.


Maumivu kwenye via vya uzazi ambayo husababisha kushindwa kushiriki tendo la ndoa kwa muda mrefu ama kushindwa kukaa kwa muda mrefu


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Karibu Sana..!!!




0 Comment

KUTOKWA NA UCHAFU SEHEMU ZA SIRIAfyaclass Bongo Social •

 KUTOKWA NA UCHAFU SEHEMU ZA SIRI.

➡️ (imeandikwa na Ombeni Mkumbwa)

WANAWAKE wengi husumbuliwa na tatizo la kutokwa na uchafu sehemu za siri, lakini hawajui sababu ni nini! na wala hawajui cha kufanya.


Vitu muhimu vya kuangalia katika uchafu huo ni pamoja na; aina ya uchafu unaotoka,mwepesi au mzito,una rangi gani?,una harufu n.k

KWA ASILIMIA KUBWA UCHAFU KUTOKA SEHEM ZA SIRI HUCHANGIWA NA MAAMBUKIZI(INFECTION) YA MAGONJWA MBALI MBALI KAMA FANGASI,PID,

LAKINI PIA MATATIZO KAMA KUZIBA MIRIJA YA UZAZI.

Uchafu huo unaweza kuwa na rangi nyingi tofauti kulingana na aina ya ugonjwa au maambukizi.Mfano;cream,maziwa,njano,n.k NA kwa wakati mwingine huambatana na miwasho sehem za Siri.

.

JUKUMU LANGU NI KUKUELIMISHA,KUKUSHAURI NA KUKUSAIDIA KATIKA TATIZO LAKO, 

@Mawasiliano +255758286584.


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Karibu Sana..!!!



0 Comment

TABIA ZA UJAUZITO KATI YA MWANAMKE NA MWANAMKEAfyaclass Bongo Social •

 TABIA ZA UJAUZITO KATI YA MWANAMKE NA MWANAMKE.

Kuna wengine baada ya kuwa na Ujauzito hutokea sana kuwapenda waume zao, kuwapenda baadhi ya watoto walio nao,au baadhi ya watu flani hata kama hawana undugu.

Kuna wengine baada ya kupata mimba,huanza kuwachukia sana baadhi ya watu mfano MUME,baadhi ya WATOTO,au hata baadhi ya watu flani kwenye JAMII.


UJAUZITO UNAWEZA KUKUFANYA UPENDE BAADHI YA HARUFU ZA VITU FLANI NA KUCHUKIA HARUFU ZA VITU FLANI.MFANO KWA BAADHI YA WATU HUCHUKIA PERFUME FLAN,N.K.

Wengine hupenda harufu flani hata za vitu vichafu.MFANO HARUFU YA MKOJO.


Ujauzito unaweza kubadilisha kabsa LIFESTYLE yako nakuanza kuchagua baadhi ya vyakula. 

LAKINI PIA HATA STAYLE YA UVAAJI INABIDI IBADILIKE KULINGANA NA HALI YA UJAUZITO,IKIANZIWA NA;


1-kutokuvaa viatu virefu

2-Kutokuvaa nguo zinazobana,mikanda n.k.


PIA KUWA MWANGALIFU HATA KATIKA MATUMIZI YA DAWA,MAANA BAADHI YA DAWA ZINA MADHARA MAKUBWA KWA MJAMZITO. *Jukumu langu ni kukuelimisha,kukushauri na kukupa msaada wa kafya pale inapohitajika.Karibu tuijenge afya Bora.*

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Karibu Sana..!!!



0 Comment

KUTOKWA NA DAMU NYINGI SANA WAKATI WA HEDHIAfyaclass Bongo Social •

 KUTOKWA NA DAMU NYINGI SANA WAKATI WA HEDHI.


Hali hii imekuwa ikitokea kwa wanawake wengi siku hizi.Mfano MWANAMKE aliyekuwa anabadilisha pedi mara tatu kwa siku sasa anabadilisha mara 8.n.k na mwanamke ambaye alikuwa anablid kwa siku tatu anablid kwa WIKI 2. 



VIPO VISABABISHI MBALIMBALI VYA HALI HII IKIWEMO;


1-Mvurugiko wa vichocheo mwilini(hormone imbalance)


2- Uvimbe kwenye kizazi


3- Matumizi ya baadhi ya njia za UZAZI WA MPANGO


HIVO NI BAADHI TU LAKINI KUNA MAGONJWA KAMA YA INI AU FIGO, NA HALI YA DAMU YA MWANAMKE KUSHINDWA KUGANDA.

 

Njia rahisi ya kugundua kuwa una tatizo la kuvuja damu kupita kiasi wakati wa Hedhi ni ubadlishaji wa PEDI ya MWANAMKE KWA SIKU.


Kwa ushauri zaidi,elimu au msaada juu ya tatizo lako tufahamishane


*Jukumu langu kubwa ni kukushauri,kukuelimisha na kukupa msaada wa kiafya pale unapohitajika.Karibu tuijenge afya Bora*


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Karibu Sana..!!!






0 Comment

KUZAA WATOTO WATATU KWA MARA MOJA(TRIPLETS)Afyaclass Bongo Social •

 KUZAA WATOTO WATATU KWA MARA MOJA(TRIPLETS).


Watu wengi hawafaham kwamba ukizaa watoto watatu hawaitwi TWINS bali kitaalam huitwa TRIPLETS.


Watoto hawa huzaliwa watatu,japo kwa asilimia kubwa watu wamezoea kuzaa watoto Mapacha ambao ni Wawili.


Mama akiwa mjamzito(MULTIPLE PREGANCY)    watoto hawa huanza kuonekana kwa kipimo cha ULTRASOUND,....

Ambapo kwa kutumia Ultrasound tutajua idadi ya watoto waliopo katika tumbo la mama.

JAPO VIPO VIASHIRIA MBALIMBALI AMBAVYO VINAWEZA KUONEKANA KWA NJE KAMA MAMA KUWA NA TUMBO KUBWA KULIKO KAWAIDA N.K


Je unapenda watoto mapacha?,Je unapenda TRIPLETS?


KWA MAONI KUHUSU UNACHOPENDA KUFAHAM ZAIDI KUHUSU AFYA YAKO MWANAMKE AU MTOTO,USISITE NIANDIKIE KWENYE COMMENT HAPO CHINI ILI TWENDE SAWA...


KUMBUKA;Jukumu langu ni kukuelemisha,kukushauri na kukupa msaada wa kiafya paleinapohitajika...!!!!! karibu

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Karibu Sana..!!!



0 Comment

KUPATA BLID PASIPO KUTARAJIAAfyaclass Bongo Social •

 KUPATA BLID PASIPO KUTARAJIA.

Zipo sababu mbali mbali ambazo huweza kuchangia hali hii kwa MWANAMKE...

1-Unaweza kupata blid pasipo kutarajia kutokana na Mzunguko wako wa hedhi kutoeleweka au kitaalam tunaita "IRREGULAR MENSTRUAL CYCLE"


2-Kuwa katika hali ya STRESS AU MSONGO WA MAWAZO, HASIRA KALI, WOGA AU HOFU JUU YA KITU FLANI unaweza kupata blid pasipo wewe kutarajia.


3- Dalili za maambukizi ya magonjwa mbali mbali kama SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI.


4-Matumizi ya baadhi ya njia za UZAZI WA MPANGO.


HALI HII INAWEZA KUWA YA HATARI AU SIO YA HATARI KUTOKANA NA CHANZO CHA KUPATA HIYO BLID..


kwa wale pia wanaopata blid mara mbili au tatu kwa mwezi,wanaopata  blid inayochukua mdamrefu mfano wiki mbili,au mwezi,  na wale wanaopata blid yenye mabonge na nyeusi pia tuwasiliane +255758286584 kwa msaada zaidi.


KUMBUKA; JUKUMU LANGU NI KUKUSHAURI,KUKUELIMISHA NA KUKUPA MSAADA WA KIAFYA PALE INAPOHITAJIKA.....

Karibu Sana..!!!



0 Comment

TATIZO LA KUWASHWA KWENYE NGOZIAfyaclass Bongo Social •

 🔻KUWASHWA KWENYE NGOZI.

Ugonjwa huu umekuwa ukiwasumbua watu wengi siku hizi,bila kujali umri au jinsia.


ZIPO SABABU MBALI MBALI KITAALAM AMBAZO HUCHANGIA HALI HII IKIWEMO; 


-Swala la allergy ambayo hutokana na vitu mbali mbali kama Maji(ya kisima,mvua n.k), baadhi ya mafuta ya kula,vyakula kama aina ya flani ya nyama mfano ya mbuzi,ng'ombe,kuku n.k. KUNA WATU WANA ALLERGY KUTOKANA NA VITU HIVI.


-Swala lingine ni Magonjwa kama FANGASI YA NGOZI, AU DAMU.ambayo hii matokeo yake huonekana moja kwa moja kwenyengozi na hali ya miwasho isiyoisha hujitokeza.


KAMA UNAPATA MUWASHO WA NGOZI AU SEHEM ZA SIRI PIA,TUWASILIANE +255758286584 UPATE MSAADA.

Karibu Sana..!!!



0 Comment

MATOKEO YA MVURUGIKO WA VICHOCHEO VINGI MWILINI KWA MWANAMKEAfyaclass Bongo Social •

 MATOKEO YA MVURUGIKO WA VICHOCHEO VINGI MWILINI KWA MWANAMKE

➡️ Ombeni Mkumbwa

Zipo dalili mbalimbali ambazo huonyesha vichocheo vingi katika mwili wa MWANAMKE havipo sawa,ikiwemo vile vichocheo vinavyohusiana na ukuaji wa mwili kwa Mwanamke.


DALILI HIZO NI KAMA IFUATAVYO;

(1) MWANAMKE KUOTA NYWELE NYINGI KATIKA MAENEO MBALI MBALI YA MWILI WAKE,IKIWEMO NDEVU KAMA MWANAUME


(2)MWANAMKE KUWA NA KIPARA


(3)MWANAMKE KUPATWA NA HALI YA KUWA NA CHUNUSI NYINGI USONI AMBAZO HAZIISHI


(4) MWANAMKE KUWA NA MZUNGUKO WA HEDHI USIYOELEWEKA


(5) MWANAMKE KUSHINDWA KUSHIKA MIMBA(INFERTILITY) AU MIMBA KUTOKA KILA AKISHIKA UJAUZITO N.K


KUMBUKA; JUKUMU LANGU NI KUKUSHAURI,KUKUELIMISHA NA KUKUPA MSAADA WA KIAFYA PALE INAPOHITAJIKA..+255758286584(PHONE NUMBER)

Karibu Sana..!!!



0 Comment

SABABU AMBAZO ZINAWEZA KUWA CHANZO CHA KICHEFUCHEFU NA KUTAPIKAAfyaclass Bongo Social •

 SABABU AMBAZO ZINAWEZA KUWA CHANZO CHA KICHEFUCHEFU NA KUTAPIKA.

✓ Dalili za mimba

✓ Magonjwa kama Malaria,UTI

✓Matumizi ya baadhi ya Dawa

✓Matumizi ya baadhi ya vyakula

✓ Allergy inayotokana na vyakula flani kama nyama n.k
✓ Matumiz ya baadhi ya Njia za Uzazi wa Mpango n.k

✓ Mabadiliko ya Gafla ya vichocheo vya mwili

✓ Harufu ya Baadhi ya Vitu kama pafume n.k

JE USHAWAHI KUPATWA NA HALI HII? COMMENT NDYO AU HAPANA KWENYE COMMENT HAPO 👇

KUMBUKA: KWA USHAURI,ELIMU AU MSAADA WA KIAFYA NAMBA NI 0758286584 ,TUMA MESEGI UTAJIBIWA KWA HARAKA ZAIDI.

Karibu Sana..!!!




0 Comment

MAMBO MUHIMU KWA MTOTO BAADA YA KUZALIWA MPAKA ATAKAPOFIKISHA UMRI WA MIAKA MITANOAfyaclass Bongo Social •

 MAMBO MUHIMU KWA MTOTO BAADA YA KUZALIWA MPAKA ATAKAPOFIKISHA UMRI WA MIAKA MITANO.

➡️ Ombeni Mkumbwa

Katika hali ya kuhakikisha afya ya mtoto inaimarika kuna vitu vya muhim vya kuzingatia sana,Leo nitagusia baadhi ya vitu hivo;


(1)KUPATA CHANJO ZOTE MUHIMU mfano; kuna chanjo ya kuzuia kifua kikuu BCG,chanjo ya kuzuia ugonjwa wa kupooza POLIO, chanjo za kuzuia mtoto kuharisha ROTAX, vitamin A, DAWA za MINYOO n.k.


(2)LISHE KWA MTOTO,hapa nazungumzia swala nzima la unyonyeshaji kwa MIEZ 6,ambao unahusisha maziwa ya mama peke yake ili kuzidi kuimarisha kinga ya mwili kwa mtoto, KWANI Kinga ya mwili kwa mtoto dhidi ya magonjwa hutokana zaidi na maziwa ya mama katika kipindi hiki.


(3)BAADA YA MTOTO KUZALIWA,USIWEKE KITU CHOCHOTE KWENYE KITOVU CHA MTOTO,kuna baadhi ya watu wenye iman potofu,hadi wengine hufikia hatua ya kupaka MAVI ya Ng'ombe kwenye kitovu cha mtoto.Hii ni hatari sana kwa afya ya Mtoto,Usiweke ktu chochote mpka kitovu kidondoke chenyewe.


(4)USAFI WA MWILI,Hakikisha mtoto unamsafisha vizuri


(5)NGUO ZA KUZUIA BARIDI,mvalishe mtoto au mfunike ili kuepuka hali ya baridi kwa mtoto;Kwani baridi kwa mtoto huweza kumsababishia kuumwa.


KUMBUKA;JUKUMU LANGU NI KUKUSHAURI,KUKUELIMISHA NA KUKUPA MSAADA WA KIAFYA PALE INAPOHITAJIKA. MAWASILIANO +255758286584.

Karibu Sana..!!!



0 Comment

UVIMBE KWENYE MIDOMO YA UKEAfyaclass Bongo Social •

 TATIZO LA KUWA NA UVIMBE KWENYE MASHAVU AU MIDOMO YA UKE

Tezi za Bartholin huwa ki kawaida zinapatikana katika pande za mashavu/midomo ya uke. Huwa ni ndogo mno na hufanya kazi ya kutengeneza uteute/majimaji ili kufanya uke kuwa na unyevunyevu na kuepusha ukavu


Uteute huu husambazwa ukeni kupitia vimirija vidogo (ducts). Inapotokea kuna kizuizi (blockage), uteute huu hujaa na kusababisha tezi kuvimba, na ndio huitwa BARTHOLIN CYST


CHANZO

Wataalamu mpaka sasa hawana jibu la uhakika kwa nini kizuizi hutokea na kusababisha uvimbe. Lakini huhusishwa na maambukizi ya Magonjwa ya Zinaa kama Kisonono na Pangusa


NANI YUPO KATIKA HATARI?

Wanawake kati ya umri wa miaka 20 mpaka 30, japo huweza kutokea pia katika umri mwingine. Uwezekano wa kupata tatizo hupungua kadri umri unavyo ongezeka. Wanawake 2 kati ya 10 hupatwa na tatizo hili


DALILI

Unaweza usiwe na dalili zozote mpaka uvimbe unapokuwa mkubwa zaidi ama unapopata maambukizi (infection)ya bakteria •Maumivu makali katika uvimbe

•Maumivu katika tendo la ndoa

•Maumivu wakati wa kutembea

•Uvimbe ukiwa mkubwa hushusha zaidi shavu la uke katika pande husika

•Homa (kutokana na maambukizi)

•Kutokwa na uchafu (discharge)


Soma: Tatizo la uke Kujamba,chanzo na Tiba yake


MATIBABU

1•Kama una umri chini ya miaka 40 na uvimbe haukupi shida, Fanya "Sitz Bath"- Weka maji ya vuguvugu katika beseni kisha kalia maji kwa dakika 15-20, hakikisha maji yanafunika eneo lote la uke. Fanya hivi mara 3 kila siku kwa siku 4. Uvimbe utatoweka wote na utarudi kama zamani

.

.

2•Kama uvimbe unaleta shida, daktari ataamua kati ya Tiba zifuatazo

》Upasuaji na kutumbua (Surgical Drainage)

》Marsupialization (Kutumbua na kushona nje ndani) hii kuzuia tatizo kujirudiarudia

》Upasuaji wa kuondoa tezi yote •Kama Vipimo vitaonesha una maambukizi ya Magonjwa ya Zinaa utapata pia Tiba husika

(NA @afyabongo)

#Afyaclass


Soma: Tatizo la uke Kujamba,chanzo na Tiba yake


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Karibu Sana..!!!



0 Comment

FAIDA ZA KUTUMIA MICHAICHAI MWILINIAfyaclass Bongo Social •

FAIDA ZA MICHAICHAI MWILINI

➡️ Michaichai

Ukitaka kuwafukuza Mbu wanaoleta ugonjwa wa Malaria nyumbani kwako panda Mmea wa Mchaichai au weka huo Mmea ndani ya nyumba yako kama pambo basi Mbu hawata sogea nyumbani kwako utakuwa umewaweza Mbu wana uchukia huo Mmea wa Mchaichai. Haya nimewapeni Dawa ya bure hiyo kazi kwenu.


FAIDA YA KUTUMIA MCHAICHAI KAMA TIBA NA CHAKULA


Faida za mchachai zipo nyingi sana wengi wetu hudhani mchaichai ni kiungo cha kuweka kwenye chai pekee, au ni dawa kwa ajili ya kuua mbu pekee, ila mchaichai huwa na faida lukuki zaidi ya hizo tu. Naomba uweze kusoma makala haya ili uone faida nyinginezo za mchaichai.


Zifuatazo ni faida za kutumia mchaichai kiafya.


1. Mchaichai ni kinga dhidi ya saratani.

Tafiti mbalimbali zimeonyesha kuwa kwenye kila gram 100 ya mchaichai, kuna viondosha

sumu ambavyo vina uwezo wa kuukinda mwili dhidi ya ugonjwa wa saratani. Mwaka 2006, timu ya watafiti kutoka Chuo kikuu cha Gurion, Israel waligundua mchaichai una uwezo wa kuua seli zinaweza kusababisha saratani.


2. Hutibu magonjwa ya kuhara.

Husaidia umeng’enyaji wa chakula Chai ya mchaichai hurahisisha utaratibu wa mmeng’enyo wa chakula na pia hutibu magonjwa ya kuhara na maumivu ya tumbo ikiwamo kujaa gesi.


Hurahisisha utaratibu wa kuondoa uchafu mwilini Katika matibabu, unatibu magonjwa mengi ikiwemo kushusha joto, hasa kwa wagonjwa wanaosumbuliwa na malaria kali.


3. Husaidia kusafisha figo na mkojo.

Mchaichai pia una kazi ya kusafisha figo ambayo kazi yake kubwa ni kusafisha damu mwilini, kuondoa mafuta mabaya mwilini ambayo mengi yanatengenezwa na kemikali kiwandani na hivyo mwili kushindwa kuziondoa na baadaye kusasababisha magonjwa mbalimbali ikiwemo saratani.


Figo inapokuwa safi na imara, hata kazi nyingine kama kusafisha mkojo zinafanyika kirahisi kwani mkojo unapozidi kuwa mchafu mtu hujikuta akivimba mwili na wakati mwingine kufikia hata hatua ya kupoteza maisha.


4. Hupunguza maumivu wakati wa hedhi.

Mchaichai pia huwasaidia kina mama ambao wanaumwa na tumbo kipindi cha hedhi, ambao wengi wao huchukulia kama chango.


“Unapokunywa mchaichai, unawezesha kusafisha mirija ya uzazi na hivyo kuwezesha damu kupita kwa urahisi,”

Cc:afyasolution #afyaclass

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Karibu Sana..!!!



0 Comment

TATIZO LA KUPATA CHOO KIGUMU,UKOSEFU WA CHOO PAMOJA NA TIBA YAKEAfyaclass Bongo Social •

🔻TATIZO LA KUPATA CHOO KIGUMU PAMOJA NA UKOSEFU WA CHOO

Watu wengi sana siku hizi hupatwa na tatizo hili la Choo Kigumu Pamoja na kukosa choo kabsa,hata kupelekea kupata Maumivu,michubuko na kutokeza kinyama sehemu za Haja kubwa ambapo kwa Kitaalam huitwa Bawasiri wakati wa Kujisaidia. Tuangalie chanzo cha Tatizo hili la Choo Kigumu,ukosefu wa choo kabsa na jinsi ya Kupata Tiba.

➡️ SABABU ZA KUTOKEA KWA TATIZO LA KUPATA CHOO KIGUMU?

Tatizo la kupata choo kigumu pamoja na ukosefu wa choo husababishwa zaidi na ulaji mbaya wa vyakula,mabadiliko ya vichocheo mwilini hasa hasa kwa Mjamzito, kuacha kula matunda na mboga na staili mbaya ya maisha ikiwa ni pamoja na kutokunywa maji ya kutosha kwa siku.


➡️ NINI KIFANYIKE ILI KUONDOA TATIZO HILI LA KUPATA CHOO KIGUMU NA KUKOSA CHOO KABSA?

Ili kuondoa tatizo kabla halijawa sugu, fanya moja miongoni mwa haya yafuatayo:

  •  Kunywa maji ya uvuguvugu asubuhi mapema, kisha tembea tembea, baada ya muda utasikia haja ya kwenda msalani. Ili usifanye haraka na upate muda wa kutosha kujiandaa kwenda kazini, amka mapema zaidi. 
  • Kula kiasi cha kutosha cha salad ya mboga mboga na juisi ya matunda halisi asubuhi kabla ya kula chochote,Kula matunda kama Mapapai,Na machungwa.
  • Kila siku kabla ya kwenda kulala, kunywa maji ya uvugu uvugu yaliyochanganywa na kijiko kimoja cha asali. Kunywa maji ya uvugu yaliyochanganywa na limau asubuhi na mapema kabla hujala kitu chochote. Kunywa castor Oil' muda mfupi kabla ya kwenda kulala.
  •  Ili kujiepusha kabisa na tatizo la ukosefu wa choo, jenga mazoea ya kunywa maji mengi, kula mboga na matunda kwa wingi kila siku na kuacha kabisa ulaji wa vyakula vilivyoondolewa virutubisho kama vile mikate myeupe, ugali wa unga mweupe, keki vyakula vyenye sukari nyingi na vyakula vingine vitamu. .

➡️ JINSI YA KUJIKINGA NA TATIZO HILI

  1. Epuka ulaji mbaya wa vyakula,
  2. pendelea kula matunda kama machungwa na Mapapai pamoja na mbogamboga au mboga za majani
  3. kunywa maji ya kutosha kwa siku angalau kuanzia lita 2.5-3 kwa Siku


                       "MWISHO"


#afyasolution #afyaclass


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Karibu Sana..!!!



0 Comment

ATHARI ZA KUNYONYA SEHEMU ZA SIRI(UKE) KWA KUTUMIA MDOMO WAKATI WA KUFANYA MAPENZIAfyaclass Bongo Social •

ATHARI ZA KUNYONYA SEHEMU ZA SIRI KWA KUTUMIA MDOMO WAKATI WA KUFANYA MAPENZI

➡️ Mdomo

Kuna utaratibu ambao siku hizi umeshamiri sana wa Wanaume kuwanyonya wanawake sehemu za Siri(uke) wakati wa kufanya mapenzi. Tabia hii kiafya ni hatari sana na inaweza kuleta madhara makubwa sana kwa Mhusika. 

Huwa unatumia vigezo gani kuchagua mtu wa kumlamba sehemu zake za siri? Una mwamini kiasi gani? Yupo salama?

- FAHAMU

Unaweza kupata maambukizi ya Herpes Simplex au hata kuhamisha Fangasi kutoka Sehemu za Siri kwenda Mdomoni,hivo kukuletea madhara makubwa kwenye Mdomo wako,Lips za Mdomo,Fizi za Meno na hata ulimi pia.



Hii ni picha ya mtu mwenye Herpes simplex,tatizo ambalo pamoja na sababu zingine husababishwa na kushiriki tendo la ndoa kwa kutumia midomo. Linaweza pia kutokea kwenye sehemu za siri za mhusika. Epuka kutumia midomo yako kulamba sehemu za siri za mtu usiye mwamini sana. Ni hatari sana,kwani unaweza kuamka siku moja kutoka usingizini ukakuta mdomo wako umevimba hivi

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Karibu Sana..!!!

0 Comment

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITIAfyaclass Bongo Social •

TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI

Tatizo hili la Mwanaume kuota matiti(Gynecomastia) huhusisha kuongezeka kwa tishu ndani ya tezi za matiti ya Mwanaume, Na Uwiano usio sawa wa vichocheo(imbalance of the hormones) vya estrogen pamoja na testosterone ndyo sababu kubwa ya tatizo hili.


Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama Mwanamke..

SABABU ZA TATIZO HILI

➖ Chanzo Kikubwa cha Tatizo hili Ni Mvurigiko wa vichocheo vya Mwili ambapo Kitaalam hujulikana kama Hormone Imbalance.

Mvurugiko wa vichocheo mwilini (Hormonal imbalance) hausumbui wanawake tu kama tulivyozoea kusikia. Tatizo hili huweza kuwapata Na Wanaume pia

 Tatizo hili huanza kuonekana kwa ukubwa wake kadri umri wa mwanamme unapozidi kuongezeka kwa kuwa vichocheo vya kiume (Testosterone) hupungua huku vile vya kike (Estrogen) vikianza kuongezeka. 

Ndipo hali hii husababisha baadhi ya tabia za kike kuonekana kwa mwanaume,Mfano mwanaume kuota matiti,kuwa na hips n.k

Kwa siku za hivi karibuni,mambo haya pia yameanza kutokea kwa vijana walio na umri mdogo

DALILI ZA TATIZO HILI

-Mojawapo ya dalili za uwepo wa tatizo hili ni kuongezeka kwa ukubwa wa matiti ambayo wakati mwingine huanza hadi kutoa majimaji,

-uchovu usio na sababu maalumu,

-kuongezeka sana kwa uzito wa mwili (unene uliopitiliza) 

-pamoja na kupungua sana kwa hamu ya tendo la ndoa au hata kushindwa kulishiriki kikamilifu.

 Ni vizuri ukazifuatilia dalili hizi kwa umakini ili ukiziona upate Msaada wa haraka

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Karibu Sana..!!!


TATIZO LA MWANAUME KUOTA MATITI(gynecomastia)

Tatizo hili linatokea kwa Baadhi ya wanaume,na hata kupelekea Wanaume hao kuwa na Matiti kama Mwanamke.

Tatizo hili la Mwanaume kuota matiti(Gynecomastia) huhusisha kuongezeka kwa tishu ndani ya tezi za matiti ya Mwanaume, Na Uwiano usio sawa wa vichocheo(imbalance of the hormones) vya estrogen pamoja na testosterone ndyo sababu kubwa ya tatizo hili.

Tatizo hili la Gynecomastia linaweza kuathiri titi moja au yote mawili, na wakati mwingine ukubwa wa matiti hutofautiana kati ya titi moja na jingine hata kama yote yanaongezeka.

Kumbuka: Sio kila matiti yakiongezeka ni tatizo la Gynecomastia, Inaweza kuwa hali inayojulikana kama Pseudogynecomastia,

Pseudogynecomastia: 

Hali hii huhusisha kuongezeka kwa mafuta na sio tishu ndani ya matiti ya Mwanaume.

Dalili za Tatizo la Matiti kuongezeka(Gynecomastia) ni pamoja na;

- Mwanaume kuanza kupata maumivu ya matiti

- Matiti kuanza kuongezeka ukubwa

- Kuhisi hali ya msisimko wa tofauti kwenye matiti baada ya kuyasugua,kugusa au kuguswa na nguo n.k

Hakikisha unapata Matibabu haraka ikiwa;

  • Matiti yako yanavimba zaidi
  • Unapata maumivu ya matiti
  • Matiti yanaanza kutoa maji,usaha au damu
  • Unahisi kitu kigumu kwenye titi au matiti
  • Chuchu kuingia ndani
  • Ngozi kujikunja Zaidi n.k

Sababu Zinazoongeza hatari Zaidi ya Mwanaume kuota Matiti

Hizi hapa ni baadhi ya Sababu zinazoongeza hatari Zaidi ya Mwanaume kupata tatizo hilo:

1. Mwanaume kufikia Umri wa balehe(Puberty).

2. Kuwa Mtu mzima Zaidi

3. Kuwa na tatizo la Uzito Mkubwa au Unene

4. Matumizi ya baadhi ya dawa jamii ya anabolic steroids hasa kwa Wanariadha

5. Kuwa na Matatizo mengine ya kiafya kama vile;

  • Magonjwa ya Ini
  • Magonjwa ya Figo
  • Magonjwa ya Tezi la Thyroid
  • Kuwa na Uvimbe(tumors)
  • Au matatizo mengine kama vile, Klinefelter syndromen.k
Chanzo cha Tatizo la Mwanaume kuota matiti

Kwa wanaume wakati wa kuzaliwa, mwili hutengeneza homoni ya kiume inayojulikana kama testosterone.  Pia hutengeneza kiasi kidogo cha homoni ya estrojeni.  Tatizo la Mwanaume kuota matiti au Gynecomastia Linaweza kutokea wakati kiasi cha testosterone katika mwili huwa kidogo ikilinganishwa na estrogen.  Kupungua huku kunaweza kusababishwa na hali ambazo hupunguza testosterone au kuzuia athari zake.  Au inaweza kusababishwa na hali zinazopandisha kiwango cha estrojeni.

Hizi hapa ni baadhi ya Sababu ambazo huweza kuleta mabadiliko hayo kwa Mwanaume;

(1) Mabadiliko ya Vichocheo mwilini(Natural hormone changes)

Homoni za testosterone na estrojeni hudhibiti tabia zinazohusu jinsia ya mtu.  Testosterone hudhibiti sifa kama vile ujengaji wa misuli na nywele za mwili.  Estrojeni hudhibiti sifa zinazojumuisha ukuaji wa matiti.n.k

 Viwango vya estrojeni ambavyo viko juu sana au havina uwiano na viwango vya testosterone vinaweza kusababisha tatizo la Mwanaume kuota matiti au gynecomastia.

(2) Hali ya kuota Matiti toka utotoni(Gynecomastia in infants).

 Zaidi ya nusu ya watoto wa kiume huzaliwa na matiti yaliyoongezeka kutokana na athari za estrojeni wakati wa ujauzito.  Titi lililovimba kwa kawaida hupotea ndani ya wiki 2 hadi 3 baada ya kuzaliwa.

 (3) Hali ya kuota Matiti(Gynecomastia) wakati wa kubalehe.  

Gynecomastia inayosababishwa na mabadiliko ya homoni wakati wa kubalehe ni ya kawaida kwa kiasi fulani.  Mara nyingi, tishu za matiti zilizovimba hupotea bila matibabu ndani ya miezi 6 hadi miaka 2.

(4) Hali ya Kuota Matiti(Gynecomastia) kwa watu wazima.  

Takriban Asilimia 24% hadi 65% ya wanaume wenye umri wa miaka 50 hadi 80 hupata tatizo hili la kuota matiti yaani gynecomastia.  

Lakini watu wazima wengi walio na hali hiyo hawana dalili.

(5) Matumizi ya Dawa

Zipo baadhi ya Dawa ambazo huweza kuchangia uwepo wa tatizo la kuota matiti kwa Mwanaume yaani gynecomastia.  Mfano wa Dawa hizo ni pamoja na;

- Dawa jamii ya Anti-androgens ambazo hutumika kutibu matatizo kama Saratani ya Tezi dume(enlarged prostate and prostate cancer). Mfano wa dawa hizo ni pamoja na;
  • flutamide,
  •  finasteride (Proscar, Propecia)
  • spironolactone (Aldactone, Carospir).
- Dawa jamii ya Anabolic steroids na androgens

- Dawa kwa ajili ya maambukizi ya Virusi vya Ukimwi(Antiretroviral medicines). Mfano;
  •   efavirenz.
- Pamoja na dawa Zingine kama vile;
  •  Adderall.
  • Anti-anxiety medications, kama diazepam (Valium).
  • Dawa jamii ya Tricyclic antidepressants.
  • Dawa jamii ya Opioids,kutibu maumivu ya muda mrefu
  • Dawa kama omeprazole (Prilosec).
  • Matibabu ya Saratani,Chemotherapy n.k
  • Dawa za magonjwa ya moyo kama digoxin (Lanoxin) na calcium channel blockers.
  •  metoclopramide
(6) Unywaji wa Pombe 

Watu wengi hawafahamu kwamba,Unywaji wa Pombe kupita kiasi huongeza hatari ya Mwanaume kupata tatizo hili pia.

Recreational drugs, illegal drugs and alcohol
Substances that can cause gynecomastia include:

(7) Matumizi ya Dawa za Kulevyia

Hapa nazungumzia dawa mbali mbali za Kulevyia kama vile;
  • Marijuana.
  • Heroin.
  • Methadone (Methadose).
(8) Matatizo Mengine ya Kiafya;

Hali fulani za Kiafya zinazoathiri usawa wa homoni zinaweza kusababisha au kuhusishwa na tatizo la Mwanaume kuwa na matiti(gynecomastia).  Hali hizo ni pamoja na:

 • Tatizo la Hypogonadism

Matatizo ambayo hupunguza kiwango cha testosterone ambayo mwili huitengeneza yanaweza kuhusishwa na tatizo la Mwanaume kuota matiti gynecomastia.  Baadhi ya mifano ni ugonjwa wa Klinefelter na upungufu wa utendaji kazi wa tezi la pituitari.

Kuzeeka.  

Mabadiliko ya homoni yanayotokea wakati wa kuzeeka yanaweza kusababisha tatizo la Mwanaume kuota matiti , hasa kwa watu ambao ni overweight,Yaani wenye Uzito mkubwa kupita kiasi.

 • Uvimbe.  

Vivimbe vingine vinaweza kutengeneza homoni zinazobadilisha usawa wa homoni za mwili.  Hii ni pamoja na uvimbe unaohusisha korodani, tezi za adrenal au tezi ya pituitari.

 • Tatizo la Hyperthyroidism.  

Katika hali hii, tezi ya thyroid hutoa kiasi kikubwa cha homoni ya thyroxine. Hali hii huweza kuongeza hatari ya kupata tatizo la Mwanaume kuota matiti 

Kushindwa kwa figo. 

 Takribani nusu ya watu wanaopata matibabu ya dialysis hupata tatizo la gynecomastia kutokana na mabadiliko ya homoni.

Hivo hali hii huweza kuongeza hatari ya kupata tatizo la Mwanaume kuota matiti 

  Kushindwa Kufanya kazi kwa Ini na tatizo la cirrhosis. 

 Mabadiliko katika viwango vya homoni kuhusiana na matatizo ya ini na dawa za kutibu tatizo la cirrhosis, Na pia huhusishwa na tatizo la Mwanaume kuota matiti.

• Utapiamlo na njaa. 

Wakati mwili haupati lishe ya kutosha, viwango vya testosterone hupungua.  Lakini viwango vya estrojeni vinabaki sawa.  Hii husababisha kutokuwa na usawa wa homoni, Na matokeo yake huongeza hatari ya Kupata tatizo la Mwanaume kuota matiti 

 • Bidhaa za mitishamba
 Mafuta mengine ya mimea yaliyotumiwa katika shampoos, sabuni au lotions yamehusishwa na tatizo la Mwanaume kuota matiti . 

 Hizi ni pamoja na mti wa chai au mafuta ya lavender.  Uwezekano huu ni kutokana na misombo katika mafuta ambayo inaweza kuiga estrojeni au kuathiri testosterone.

 Sababu zinazoongeza hatari ya Kupata tatizo la Mwanaume kuota matiti 

Sababu za hatari kwa gynecomastia ni pamoja na:

  1.  Kubalehe.
  2.  Umri mkubwa.
  3.  Unene kupita kiasi.
  4.  Matumizi ya anabolic steroids
  5.  Hali fulani za kiafya.  Hizi ni pamoja na ugonjwa wa ini na figo, ugonjwa wa tezi, ugonjwa wa Klinefelter na baadhi ya uvimbe.
 Madhara ya tatizo la Mwanaume kuota matiti(Gynecomastia)

Gynecomastia ina matatizo machache ya kimwili.  Lakini inaweza kusababisha wasiwasi wa afya ya akili kutokana na mabadiliko ya jinsi kifua kinavyoonekana.

Jinsi ya  Kuzuia tatizo la Mwanaume kuota matiti 

Sababu kadhaa za tatizo hili zipo ndani ya udhibiti wako, Hivo ukizingatia unaweza kupunguza hatari ya kupata tatizo la Mwanaume kuota matiti :

 ✓ Usitumie madawa ya kulevya.  Mifano ni pamoja na anabolic steroids, amfetamini, heroini na bangi.

 ✓ Punguza au kaa mbali na pombe, Hii Inasaidia kutokunywa pombe.  Ikiwa unakunywa, fanya kwa kiasi.  Hiyo ina maana si zaidi ya vinywaji viwili kwa siku kwa wanaume.

✓ Fanya mazoezi ya mwili na dhibiti Uzito wako wa mwili

✓ Usitumie dawa hovio pasipo maelekzo ya kina kutoka kwa Wataalam wa afya.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Karibu Sana..!!!

0 Comment

MAKOSA YANAYOFANYWA KATIKA KUCHAGUA AINA ZA PEDI PAMOJA NA MATUMIZI YAKEAfyaclass Bongo Social •

➖ MAKOSA YANAYOFANYWA KATIKA KUCHAGUA AINA ZA PEDI PAMOJA NA MATUMIZI YAKE

1. Kutonawa mikono kabla na baada ya kutumia pedi. Mikono hushika sehemu mbalimbali  hivyo kuna uwezekano ikawa na vimelea vinavyosababisha magonjwa kwa hiyo kushika pedi bila kunawa mikono kwa sabuni kunaweza kuhamisha vimelea hivyo kutoka mikononi na kwenda kwenye pedi inayotegemewa kuvaliwa.


2. Kutunza pedi bafuni au chooni. Wadada wengi hupendelea kutunza pedi zao chooni/bafuni.


3. Kutoangalia muda wa matumizi wa pedi kabla ya kutumia au baada ya kuzihifadhi kwa muda mrefu hali inayopunguza kiwango cha ufanisi.


4. Kununua pedi zinazouzwa kiholela kwa njia ya utangazaji na za bei rahisi (promotion) ambazo baadhi zimeonekana kutengenezwa kwa malighafi zilizo chini ya kiwango au kukaa kwa muda mrefu hivyo kuuzwa kwa bei rahisi ili zitoke na kutumika haraka kabla ya kuisha muda wake.


5. Kutumia pedi moja kwa muda mrefu


6. Kupendelea pedi zenye uwezo mkubwa wa kufyonza unyevunyevu ili ivaliwe muda mrefu pia ni tatizo sababu kwa kadri muda wa kuvaa pedi moja unapozidi kuongezeka na hatari za maambukizi ya magonjwa pia inazidi kuongozeka.


#afyabongo #drtareeq


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Karibu Sana..!!!



0 Comment

TATIZO LA KWIKWI( HICCUPS)Afyaclass Bongo Social •

➡️ TATIZO LA KWIKWI( HICCUPS)

Kwikwi takribani zote huwa ni za upande mmoja(one-sided). Hii ni kumaanisha kuwa ni upande mmoja tu wa diaphragm hujaa (diaphragm- ni misuli iliopo chini ya kifua ambayo hujaa na kusinyaa unapopumua)


VISABABISHI 

1. Kula kupita kiasi

2. Kunywa kupita kiasi

3. Kula haraka mno

4. Mida isiyoeleweka ya milo

5. Kunywa kwa wingi vinywaji baridi (carbonated drinks) kama soda n.k

6. Msongo wa mawazo 

7. Shauku iliyopitiliza (super excitement)

8. Kuoga maji ya baridi mno

9. Mabadiliko ya ghafla ya jotoridi (temperature)

10. Uvutaji sigara 

11. Unywaji pombe .

.

NINI CHA KUFANYA

1. Pumulia ndani ya bahasha. Vuta na achia pumzi mara 10 kwa nguvu na haraka

.

.

AU. Bana pumzi kisha meza mate/maji unapohisi kwikwi inakuja. Fanya hivyo mara 2-3 .

.

.

AU. Meza sukari- kijiko kimoja cha chai. Kwikwi itapotea baada ya dakika kadhaa. Sukari uliomeza hutuma taarifa-ishara (signals) katika njia za neva (nerve routes) hivyo kuingiliana na kwikwi

.

.

AU. Vuta pumzi kwa nguvu kisha kunywa mafundo 10 ya maji

.

.

AU. Kunywa maji mengi na kwa haraka

.

.

Watoto wakiwa wanakimbia na kucheza, mara mojamoja huishia kupata kwikwi. Inapotokea, kumtekenya (tickling) na kumuambia abane pumzi kidogo na ajikaze vilivyo asicheke. Itamfanya asahau kuhusu kwikwi na huweza kusaidia. .

.

MUHIMU:

Kama una kwikwi ya muda mrefu isiyokata Fika katika Kituo cha huduma za afya kwa matibabu zaidi.  (NA drtareeq)

#afyabongo #drtareeq #afyaclass


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Karibu Sana..!!!



0 Comment

UGONJWA WA GOITA,MAANA YAKE,CHANZO,DALILI NA TIBA YAKEAfyaclass Bongo Social •

FAHAMU UGONJWA WA GOITA


Goita (Goiter) ni hali ya kuvimba kwa tezi ya thyroid. Uvimbe huu hautokani na saratani (goita si saratani). Tezi ya thyroid ipo sehemu ya mbele ya shingo. Kazi kuu za tezi ya thyroid ni kuzalisha homoni mbalimbali ambazo husaidia mwili kuthibiti na kufanya kazi zake mbalimbali.


VIHATARISHI VYA GOITA

 

Kuna baadhi ya mambo yanayohusiana na kurithi yanayoweza kusababisha mtu kupata goita. Vihatarishi hivi ni pamoja na:


1. Kuwa na umri kuanzia miaka 40 na kuendelea


2. Historia ya ugonjwa wa goita miongoni mwa wanafamilia


3. Hali ya kuwa mwanamke


4. Na, kutopata iodine ya kutosha katika lishe. Iodine ni madini muhimu yanayohitajika katika utengenezaji wa homoni mbalimbali zinazozalishwa na tezi ya thyroid. Watu wanaoishi kwenye maeneo mbali kutoka pwani ya bahari au yaliyo katika nyanda za juu kutoka usawa wa bahari kama vile mikoa ya Mbeya, Iringa na Rukwa wapo katika hatari ya kupata goita kwa vile hawapati madini ya kutosha ya Iodine katika chakula chao.


•Soma: Ugonjwa wa Mgongo Wazi kwa Watoto,chanzo,Dalili na Tiba yake


DALILI ZA GOITA 


Dalili kuu ya goita ni kuvimba au kuongezeka ukubwa kwa tezi ya thyroid. Ukubwa wa tezi unaweza kuwa kijiuvimbe kidogo katika tezi au uvimbe mkubwa kama nundu sehemu ya mbele ya shingo. Kuvimba kwa tezi ya thyroid kunaweza kusababisha mgandamizo katika njia ya hewa na mrija wa chakula, hali ambayo inaweza kusababisha:


1. Shida katika kupumua


2. Kikohozi


3. Sauti kuwa ya mikwaruzo


4. Shida wakati wa kumeza chakula


5. Wakati mwingine, mishipa ya damu ya shingoni inaweza kuvimba pia na kusababisha mtu kujihisi kizunguzungu pindi anapoinua mikono juu


MADHARA YA GOITA 


1. Shida wakati wa kumeza au kupumua


2. Kiwango cha chini cha homoni za thyroid (Hypothyroidism)


3. Kiwango cha juu cha homoni za thyroid (Hyperthyroidism)


4. Saratani ya tezi ya thyroid (thyroid cancer)


5. Goita yenye vivimbe inayozalisha homoni kwa wingi (toxic nodular goiter)


#afyabongo #drtareeq #afyaclass


•Soma: Ugonjwa wa Mgongo Wazi kwa Watoto,chanzo,Dalili na Tiba yake


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Karibu Sana..!!!




0 Comment

UGONJWA WA TYPHOID(HOMA YA MATUMBOAfyaclass Bongo Social •

TYPHOID NI NINI?

Ni ugonjwa wa homa ya matumbo unaosababishwa na bakteria ajulikanae kama, Salmonella typhi. Homa hii huhusisha homa inayopanda juu taratibu mpaka kufikia joto la 40⁰C


HUAMBUKIZWAJE?

Bakteria hawa wa Salmonella typhi husambazwa kupitia kula vyakula/maji yaliyochafuliwa/kuingiwa na kinyesi/mkojo wa mgonjwa wa typhoid au carrier(mtu anayebeba ugonjwa anaweza kuambukiza wengine ila yeye haugui)

.

DALILI 

Typhoid huhusisha homa inayopanda taratibu mpaka kuweza kufikia joto la 40⁰C, kutokwa jasho jingi, maambukizi katika tumbo na utumbo(gastroenteritis) na kuhara kawaida ama damu


Mara chache mgonjwa anaweza kuwa na upele wa pink kwenye ngozi


Muda wa Utungishwaji(incubation period) wa typhoid hutofautiana kulingana na dozi ya maambukizi (yaani wadudu kiasi gani waliokuingia) na kipindi hiki huwa kati ya siku 10-20


Typhoid isiyotibiwa dalili zake hugawanyika katika wiki kama ifuatavyo


1. DALILI KATIKA WIKI YA KWANZA

Huwa hazieleweki zikijumuisha kichwa kuuma, uchovu, homa kali inayopanda, kukosa choo, kikohozi kikavu na mapigo ya moyo kwenda taratibu .

.

2. DALILI KATIKA WIKI YA PILI

Kama bado hujatibiwa, joto la mwili huzidi kupanda na zaidi ya nusu ya wagonjwa huanza kuharisha. Mgonjwa huonekana dhoofu na tumbo kuvimba upande wa kongosho(splenomegally), pia Mapigo ya moyo huwa hafifu .

.

3. DALILI KATIKA WIKI YA TATU

Mgonjwa huzidi kuwa hoi na kuanza kuchanganyikiwa, kutotulia na tatizo la akili la kusikia mambo yasiyokuwepo(hallucinations). Kuharisha uharo wenye harufu mbaya wenye rangi ya kijani/njano(kama supu ya njegere)


Mapigo ya moyo huwa legelege(feeble) na ya kasi(rapid), kupumua kwa kasi


KIFO huweza kutokea katika wiki hii kutokana na usumu kwenye damu(toxemia), maambukizi katika misuli ya moyo(myocarditis), utumbo kuvuja damu/kutoboka. Pia maambukizi ya ubongo(encephalitis) 

(NA afyabongo)

#afyaclass 

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Karibu Sana..!!!



0 Comment

UGONJWA WA MALARIA,CHANZO,DALILI,JINSI YA KUJIKINGA NA TIBA YAKEAfyaclass Bongo Social •

Ufahamu ugonjwa wa Malaria

Malaria ni ugonjwa unaosababishwa na vimelea vinavyojulikana kama Plasmodium.Vimelea hivi huenezwa na mbu jike aina ya anofelesi (anopheles). Lakini watu wengi huelewa kwamba malaria husababishwa na mbu. Mbu huyu husaidia katika usambazaji tuu wa vimelea husika.


Aina ya vimelea ambavyo humdhuru binadamu kati ya vimelea vingi vya Plasmodium ni:

• Plasmodium Vivax

• Plasmodium Falciparum

• Plasmodium Malariae

• Plasmodium Oval


Plasmodium Vivax: Vimelea hivi havina madhara makubwa ingawa vimesambaa sana kuliko vile vya Plasmodium Falciparum.

Plasmodium Falciparum: husababisha vifo vingi na kwa haraka zaidi.

Vimelea vingine kama Plasmodium Malariae na Plasmodium Oval husababisha pia malaria lakini sio kwa ukali na yenye uharibifu kama vile vya Plasmodium Falciparum. Ukurasa huu umejizatiti zaidi kuzungumzia malaria inayosababishwa na Plasmodium Falciparum, kwani ndio inayotushambulia zaidi ukanda huu wa Afrika Mashariki. (Cc @afyatrack.com)

DALILI ZA UGONJWA WA MALARIA

- Homa
- Kusikia kichefuchefu na Kutapika
- Uchovu wa hali ya juu wa mwili
- Maumivu ya Viungo
- Maumivu makali ya Kichwa
- Kuhisi Kizungu zungu n.k

Mwaka huu tunakwenda na kauli mbiu kuwa “KIWANGO SIFURI CHA MALARIA KINAANZA NA MIMI”

Chukua Hatua

Jinsi ya kuzuia maambukizi ya Malaria

1. Kuzuia mazalia ya mbu 

Fyeka vichaka na ondoa madimbwi ya maji katika  maeneo yanayokuzunguka.


2. Kuzuia kung’atwa na mbu kwa:

i. Matumizi ya vyandarua vyenye dawa ya kuua mbu

ii. Matumizi ya dawa za kupulizia za kuua mbu majumbani

iii. Matumizi ya dawa za kupaka za kuua mmbu


3. Dawa za kuzuia malaria kwa kina mama wajawazito (IPT)

Sulfadoxine Pyrimethamine (SP) hutolewa kwa kina mama katika wiki ya 20 na wiki ya 36 ya ujauzito.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Karibu Sana..!!!



0 Comment

MICHIRIZI YA NGOZI HUSABABISHWA NA NINI?(STRETCH MARKS)Afyaclass Bongo Social •

🔻MICHIRIZI YA NGOZI HUSABABISHWA NA NINI?(STRETCH MARKS)

Michirizi ya ngozi(stretch marks/striae) mara nyingi hutokea tumboni, juu ya matiti, mapajani, kwenye makalio na kwenye hips. Michirizi huwa ni kawaida kwa wanawake wajawazito, haswa katika miezi 3 ya mwisho ya ujauzito. Matibabu huweza kufifiza michirizi lakini sio kuiondoa kabisa


INA MADHARA YOYOTE?

Michirizi haisababishi maumivu na wala haina athari nyingine yoyote ILA TU baadhi ya wanawake hawapendezewi na muonekano wa maeneo yao ya mwili yenye michirizi .

.

HUSABABISHWA NA NINI?

Michirizi husababishwa na kuvutika kwa ngozi ya mwili. Uwingi wa michirizi hutokana na mambo mbalimbali ikiwemo hali za kurithi, mvutano wa ngozi na Homoni ya Cortisone. Hormone ya cortisone huhusika kufifisha nyuzinyuzi zinazoleta mvutano katika ngozi (elastic fibers)


VIHATARISHI 

1. Kuwa Mwanamke

2. Historia katika familia/kurithi

3. Ujamzito (haswa kwa wajawazito wenye umri mdogo/mimba ya kwanza)

4. Unene 

5. Kuongezeka/kupungua uzito kwa haraka 

6. Kutumia sana madawa ya jamii ya corticosteroids kama vile, prednisone

7. Upasuaji wa kuongeza makalio, matiti ama hips


NINI CHA KUFANYA KUIONDOA?

Kama unaona michirizi inakunyima raha unaweza kupaka mafuta katika maeneo yenye michirizi mara moja kwa siku. Mchanganyiko huo uwe na;

1. ½ kikombe cha mafuta ya zaituni (olive oil)

2. ½ kikombe cha ute wa aloe vera

3. Capsules 6 za vitamin E na Capsules 4 za Vitamin A. Pasua capsules hizo ungaunga wake uchanganye pamoja na olive oil na aloevera kisha upake. Kama utatengeneza mchanganyiko zaidi unaweza Kutunza katika jokofu. Mchanganyiko huu ni salama tofauti na cream nyingi zinazouzwa ambazo hazijathibitishwa na mamlaka husika

Cc:afyabongo #afyaclass

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Karibu Sana..!!!



0 Comment

MTOTO KUCHEUA BAADA YA KUNYONYA(Infant Reflux)Afyaclass Bongo Social •

➡️ SABABU ZA MTOTO KUCHEUA MARA TU BAADA YA KUNYONYA

Kwa kawaida mtoto hucheua baada ya kunyonya lakini mara nyingine kucheua kwa mtoto hutokana na


1. Allergic gastroenteritis- Mzio (Allergy) wa protini inayopatikana kwenye maziwa ya ng’ombe


2. Gastroesophageal reflux disease (GERD)-Huu ni ugonjwa unaosababishwa na kucheua kwa tindikali inayotoka tumboni ambayo pia huharibu kuta za mrija wa kupitisha chakula (oesophagus).Kitu chochote kile kinachoongeza presha (Intra-abdominal pressure) chini ya lower oesophageal sphincter kama uzito ulopitiliza (obesity), kutopata choo kwa muda (constipation), baadhi ya vyakula, vinywaji na baadhi ya dawa husababisha GERD.


3. Eosinophilic oesophagitis- Hali inayotokana na kukusanyika kwa wingi kwa chembechembe za damu aina ya eosinophils na hivyo kuharibu kuta za mrija wa kupitisha chakula.


4. Mrija wa chakula kuwa mwembamba/kuziba hali inayojulikana kitaalamu kama oesophageal stricture au sehemu ya misuli kati ya tumbo na mrija wa chakula kuwa nyembamba au kuziba nayo hujulikana kwa kitaalamu  kama pyloric stenosis

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Karibu Sana..!!!



0 Comment
Notification
Karibu Afyaclass Bongo Social Jukwaa linalojadili mambo mbali mbali ikiwemo afya,Magonjwa na Updates Zote,Tembelea hapa kila Siku,Pia Share Maoni yako kwenye jukwaa hili Afyaclass Bongo Social ASANTE.
UNDERSTOOD