Afyaclass Bongo Social Boti ya Kifahari Yazama Dakika 15 Baada ya Uzinduzi

Boti ya Kifahari Yazama Dakika 15 Baada ya Uzinduzi



BOTI mpya ya kifahari (yacht) yenye thamani ya Dola za Kimarekani 940,000 (sawa na takribani Shilingi Bilioni 2.3 za Kitanzania) imezama dakika 15 pekee baada ya kuzinduliwa rasmi majini, tukio lililoacha wengi midomo wazi.

Ajali hiyo imetokea takribani mita 200 kutoka ufukweni katika wilaya ya Eregli, mkoa wa Zonguldak, kaskazini mwa Uturuki, siku ya Jumanne.

Mashuhuda walisema yacht hiyo ilianza kupoteza mlingano mara tu baada ya kushushwa majini, na hatimaye kuzama kwa haraka. Mmiliki wa meli hiyo, ambaye alikuwemo ndani, alilazimika kuogelea mwenyewe kuelekea ufukweni. Hakuna taarifa za majeruhi wengine zilizoripotiwa.

Tukio hili limezua mjadala mkali mitandaoni, wengi wakishangazwa na jinsi chombo cha kifahari chenye thamani kubwa kiasi hicho kilivyoshindwa kudumu hata robo saa baharini. Wengine wameeleza masikitiko yao kwa hasara kubwa iliyompata mmiliki, huku baadhi wakigeuza tukio hilo kuwa utani mitandaoni.

You, Mehreen and others

WEKA MAONI HAPA(Reply)

Notification
Karibu Afyaclass Bongo Social Jukwaa linalojadili mambo mbali mbali ikiwemo afya,Magonjwa na Updates Zote,Tembelea hapa kila Siku,Pia Share Maoni yako kwenye jukwaa hili Afyaclass Bongo Social ASANTE.
UNDERSTOOD