Israel yazindua Satelaiti mpya ya kijasusi

Israel yazindua Satelaiti mpya ya kijasusi

#1

Israel yazindua Satelaiti mpya ya kijasusi

Israel imesema imefanikiwa kurusha satelaiti mpya ya kijasusi angani, hatua ambayo itaimarisha kwa kiwango kikubwa uwezo wake wa upelelezi katika eneno la Mashariki ya Kati. Kwa mujibu wa maafisa wa Israel, satelaiti hii inaweza kupiga picha za vitu vidogo hadi ukubwa wa sentimita 50, mchana na usiku.

Waziri wa Ulinzi wa Israel, Israel Katz, alisema uzinduzi wa satelaiti hiyo, iliyopewa jina la "Horizon 19," ni ujumbe wa moja kwa moja kwa maadui kwamba "tunawaangalia kila wakati na katika hali zote."

Bw. Katz alielezea urushaji huo kuwa ni "mafanikio ya hali ya juu kabisa" ambayo ni mataifa machache pekee duniani yanaweza kuyafikia.

Kwa mujibu wa taarifa ya Wizara ya Ulinzi ya Israel, satelaiti hiyo ilirushwa angani usiku wa Jumanne, Septemba 2, kwa msaada wa roketi cha Shavit, na kufika kwenye obiti ya dunia kwa mafanikio.

Urushwaji wa satelaiti hii mpya unafuatia miezi miwili baada ya vita vya siku 12 kati ya Israel na Iran, ambapo Israel ilishambulia vituo vya kijeshi na vile vya nyuklia vya Iran pamoja na baadhi ya maeneo ya makazi vilivyoko zaidi ya umbali wa kilomita 1,000.

Changia Mada hapa(Reply)


image quote pre code