Showing posts with label Dawa ya gono kwa mwanaume. Show all posts
Showing posts with label Dawa ya gono kwa mwanaume. Show all posts

Dawa ya gono kwa mwanaumeAfyaclass Forum •

Dawa ya gono kwa mwanaume

Je, ni ipi dawa sahihi ya kutibu ugonjwa wa Kisonono(gonorrhea)?

Dawa ya gono kwa Mwanaume; Baada ya kupata Maswali mengi kuhusu dawa sahihi ya Gono kwa Mwanaume,tumeambua kukuandalia Makala hii hapa;

Kisonono ni ugonjwa wa Zinaa ambao husabababishwa na maambukizi ya bacteria wanaojulikana kama Neisseria gonorrhoeae,

Ugonjwa huu wa kisonono ndyo hujulikana kama Gonorrhea au kwa kifupi wengi hupenda kuita “Gono”, Soma Zaidi hapa;

Dawa ya gono kwa mwanaume huweza kutibu kabsa tatizo hili ikiwa umepata tiba Sahihi,

Ni muhimu sana kupata Maelekezo kamili kutoka kwa Wataalam wa afya Wakati unapata au Kutumia Dawa ya Gono kwani badala ya kutibu gono unaweza kusababisha tatizo lingine linalojulikana kama “Usugu wa Dawa” ambapo vimelea hivi vya bacteria hutengeneza usugu kwenye dawa-Antimicrobial resistance”

Kwa hivi Sasa,Ukinzani wa viua vijidudu kwenye ugonjwa wa kisonono unazidi Kuongezeka, Hali ambayo hupelekea dawa ya Kutibu kwa mafanikio ugonjwa wa Gono au kisonono Kuzidi kuwa Mgumu.

Hivo ni muhimu sana baada ya kupata dalili za gono au kudundulika una ugonjwa wa gono, hakikisha unapata dawa ya Gono ambayo ni sahihi kwa tatizo lako, Usijaribu kila aina ya Dawa.

Hauhitaji Jaribio la kutibu ugonjwa wa Gono – ufuatiliaji wa dawa ya gono au matibabu Sahihi ili kuhakikisha kuwa maambukizi yametibiwa kwa ufanisi – Ni muhimu Zaidi.

Ikiwa dalili za mtu zinaendelea kwa zaidi ya siku chache baada ya kupokea matibabu, anapaswa kurudi kwa mtoa huduma wa afya ili kutathminiwa upya,

Kipimo cha tiba kinahitajika siku 7-14 baada ya matibabu kwa watu wanaotibiwa maambukizi ya koo. Kwa sababu kuambukizwa tena ni kawaida,

wanaume na wanawake walio na ugonjwa wa gono au kisonono wanapaswa kupimwa tena miezi mitatu baada ya matibabu ya maambukizi ya awali, bila kujali kama wanaamini kwamba wenzi wao walitibiwa kwa mafanikio.

Dawa ya gono kwa mwanaume

Dawa ya gono;

Kwa Mujibu wa vituo vya kudhibiti na Kuzuia magonjwa “The Centers for diseases control and Prevention- CDC”

Wanashauri kwenye matibabu ya Ugonjwa wa Kisonono au Gono; dawa ambapo huweza kutumika ni pamoja na;

  • Sindano
  • Na Vidonge

Ingawa dawa hizi Zitazuia maambukizi ya Gono hazitaweza kurudisha madhara yoyote yaliyosababishwa na Ugonjwa huu wa Kisonono au Gono.

NB: Hakikisha unaongea na Wataalam wa afya kwa kina kabla ya kutumia dawa yoyote ya Gono ili kupata maelekzo sahihi kulingana na hali yako.

NA KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Dawa ya gono kwa mwanaume
0 Comment

Dawa ya gono kwa mwanaumeAfyaclass Forum •

Dawa ya gono kwa mwanaume

Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa ambao husababishwa na Bacteria ambaye kwa kitaalam hujulikana kama Neisseria gonorrhoeae na kuambukizwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya kujamiiana.

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) NI PAMOJA NA;

Kumbuka; Ugonjwa huu wa kisonono kwa asilimia kubwa ni vigumu mwanamke kuonyesha dalili za moja kwa moja hata kama ameambukizwa. Lakini kama akionyesha dalili basi baadhi ya dalili kama hizi hapa chini huweza kutokea.

MIONGONI MWA DALILI AMBAZO HUWEZA KUJIONYESHA KWA MWANAMKE NI PAMOJA NA;

  1. Mwanamke kupatwa na tatizo la maumivu makali wakati wa kufanya mapenzi
  2. Mwanamke kutokwa na maji maji ukeni ambayo yana harufu sana
  3.  Mwanamke kutokwa na ute ute ambayo umechanganyika na usaha ukeni
  4. Kutokwa na damu baada ya kufanya tendo la ndoa
  5. Kupatwa na shida ya blid mara mbili ndani ya mwezi mmoja
  6. Kupatwa na maumivu makali ya tumbo
  7. Joto la mwili kupanda au kuwa na homa
  8. Kuvimba kwenye eneo la mashavu ya uke

DALILI ZA UGONJWA WA KISONONO KWA MWANAUME NI PAMOJA NA;

– Kutokwa na usaha sehemu za Siri

– Kuwashwa kwenye kitundu ambacho mkojo hupita

– Kupatwa na hali ya kuchomwa wakati wa kukojoa ambayo tunasema kwa kitaalam burning sensation

– Mwanaume kupatwa na tatizo la kushindwa kukojoa kabsa au mkojo kugoma kutoka, kitu ambacho huweza kumsababishia maumivu makali pamoja na mahangaiko

– Kukojoa mkojo ambao umechanganyika na Damu

– Joto la mwili kupanda au kuwa na homa

MATIBABU YA UGONJWA WA KISONONO

Ni vizuri kwenda hospital kufanyiwa vipimo kwanza kabla ya dawa, Na baada ya hapo kama utagundulika una tatizo hili basi utapata matibabu sahihi kulingana na ugonjwa wako pamoja na hatua ulipofikia.

TIBA YA KISONONO(Ugonjwa wa zinaa)

Kwa asilimia kubwa Mgonjwa wa kisonono hupewa Dawa ya Cefriaxone 500mg Single dose ambapo ni sindano anachomwa matakoni au sehemu yoyote yenye msuli Kwa kitaalam tunaita Intramuscular Injection(IM).

Epuka matumizi ya dawa hovio pasipo maelekezo na vipimo kutoka kwa wataalam wa afya. Kwani ni hatari kwa afya yako,badala ya kukutibu inaweza kuwa sumu ya kukuua.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Dawa ya gono kwa mwanaume
0 Comment
Notification
My blog is in the process of editing and perfecting the new template, so there are still some functions to click but not yet used. Note which blogs associated with your side please read this lesson to update the blog logo.
UNDERSTOOD