Showing posts with label Elon Musk. Show all posts
Showing posts with label Elon Musk. Show all posts

Elon Musk afikia Utajiri wa dola za Marekani bilioni 600 sawa na Quadrilion 1.4Afyaclass Forum •

Mjasiriamali na bilionea wa teknolojia Elon Musk ameandika historia mpya baada ya kuwa mtu wa kwanza duniani kufikia utajiri wa dola za Marekani bilioni 600 sawa na Quadrilion 1.4, kulingana na takwimu za Forbes.

Hatua hiyo imechangiwa kwa kiasi kikubwa na kampuni yake ya anga, SpaceX, ambayo imezindua mpango wa kuuza hisa unaothamini kampuni hiyo kufikia dola bilioni 800  ongezeko kubwa kutoka dola bilioni 400 zilizokuwepo mwezi Agosti.

Musk, ambaye anamiliki takriban asilimia 42 ya SpaceX, amenufaika moja kwa moja na ongezeko hilo la thamani. Utajiri wake umeongezeka kwa dola bilioni 168, na kufikia takriban dola bilioni 677 kufikia siku ya jana Jumatatu.

Kwa mafanikio haya, Musk anakuwa mtu wa kwanza katika historia ya dunia kufikia kiwango hicho cha utajiri. Kulingana na rekodi za Forbes, hakuna mtu mwingine aliyewahi kufikia hata dola bilioni 500 hapo awali.

0 Comment

Elon Musk anaweza kuwa trillionaire wa kwanza duniani Afyaclass Forum •

Elon Musk anaweza kuwa trillionaire wa kwanza duniani huku wanahisa wa Tesla wakiidhinisha kifurushi chake cha malipo cha dola trilioni 1 ili kuboresha chapa hiyo.


Mkurugenzi Mtendaji wa Tesla na mtu tajiri zaidi duniani alishinda kura ya wanahisa Alhamisi, na kumhakikishia hisa zenye thamani ya dola trilioni 1 ikiwa atafikia malengo fulani ya utendaji katika muongo mmoja ujao, kulingana na Mail Online.

Kura hiyo ilifuatia wiki kadhaa za mjadala kuhusu rekodi yake ya usimamizi katika kampuni ya kutengeneza magari ya umeme na kama kuna mtu yeyote aliyestahili malipo hayo ambayo hayajawahi kutokea.

Mwishowe, zaidi ya asilimia 75 ya wanahisa waliokuwepo katika makao makuu ya kampuni hiyo huko Austin, Texas walipiga kura kuunga mkono mpango huo.

0 Comment

Elon Musk kujiuzulu Ukurugenzi wa Tesla ikiwa kifurushi cha dola trilioni 1 hakitaidhinishwaAfyaclass Forum •

Elon Musk anaweza kujiuzulu kama Mkurugenzi Mtendaji wa Tesla ikiwa kifurushi chake cha malipo cha dola trilioni 1 hakitaidhinishwa, kulingana na onyo la hivi karibuni kutoka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Tesla Robyn Denholm.


Rufaa ya dharura ilitumwa katika barua kwa wanahisa wa kampuni kubwa ya magari ya umeme Jumatatu, Oktoba 27, kabla ya mkutano wa kila mwaka wa Novemba 6 ambapo wawekezaji wamepangwa kupiga kura kuhusu pendekezo kubwa la malipo ambalo halijawahi kutokea.

Onyo hilo linakuja huku kampuni mbili kuu za ushauri wa wakala, Glass Lewis na Institutional Shareholder Services, zikiwahimiza sana wanahisa kupiga kura dhidi ya fidia iliyopendekezwa.

Washauri wa wakala wana ushawishi mkubwa, haswa kwa wawekezaji wakubwa wa taasisi na wa mfuko ambao wanamiliki hisa kubwa katika Tesla.

Mpango wa malipo wenye utata umeundwa ili kumhifadhi na kumtia moyo Musk, ukimtia moyo kuongoza Tesla kwa angalau miaka mingine saba na nusu, Denholm alisema katika barua yake. Alisisitiza kwamba uongozi wa Musk ni "muhimu" kwa mafanikio ya kampuni, akionya kwamba bila motisha zinazofaa,
0 Comment

Utajiri wa Elon Musk Washuka kwa kiasi cha dolla billion 15Afyaclass Forum •

Utajiri wa Mkurugenzi Mtendaji wa Tesla na SpaceX, Elon Musk, umepungua kwa kiasi cha dola bilioni 15 kwa siku ya leo pekee baada ya hisa za kampuni ya Tesla kuporomoka kwa karibu asilimia 7 na kushuka kwa takriban dola 21.



Kulingana na Bloomberg Billionaires Index, imesema licha ya kupungua kwa kiwango hicho cha fedha Musk bado anaongoza kwa utajiri duniani.

Tukio hili linajiri baada ya Musk kuzindua chama chake kipya cha kisiasa hatua ambayo inaongeza moto kwenye mgogoro wake wa hadharani na Rais wa Marekani, Donald Trump, ambaye Musk alimuunga mkono kwa kiasi kisichopungua dola milioni 277 katika kampeni za uchaguzi wa urais wa mwaka 2024.

Hali ya hisa za Tesla imekuwa mbaya tangu kuapishwa kwa Trump Januari 2025, ambapo thamani ya kampuni hiyo imeshuka kwa asilimia 31, wakati S&P 500 ikiongezeka kwa karibu asilimia 4 katika kipindi hicho hicho.

Kwa mujibu wa taarifa za hivi karibuni, Tesla pia imekumbwa na kushuka kwa mfululizo kwa utoaji wa magari katika robo mbili za mwanzo wa mwaka 2025, hali ambayo haijawahi kushuhudiwa tangu mwaka 2022.

0 Comment

Elon Musk atangaza kuanzisha chama chake kipya cha Kisiasa,America PartyAfyaclass Forum •

Bilionea na mkurugenzi wa kampuni ya Tesla na X (zamani Twitter), Elon Musk, ametangaza kuanzisha chama kipya cha siasa kinachoitwa America Party  akisema lengo lake ni kurudisha uhuru kwa wananchi wa Marekani ambapo hatua hii ikiwa ni ya kujibu hali ya kisiasa ambayo kwa maoni yake inafanya kazi kama mfumo wa chama kimoja.



Tangazo hilo limekuja baada ya kufanya kura mtandaoni kupitia jukwaa lake la X ambapo zaidi ya Watu milioni moja walipiga kura na asilimia 65 wakaunga mkono kuanzishwa kwa chama hicho na Musk ameeleza kuwa chama hicho hakitalenga kugombea urais bali kitawania viti vichache katika Bunge la Marekani ili kuleta ushawishi wa kweli kwenye mchakato wa kutunga sheria.

Elon Musk pia amedokeza kuwa chama hicho kitaweka mkazo katika kupunguza matumizi ya serikali, kupambana na urasimu na kulinda uhuru wa Raia, ingawa hajaeleza kwa undani sera rasmi za chama hicho kwa sasa ila Watu wengi wameona hatua hii kama muendelezo wa tofauti zake za wazi na Rais wa Marekani, Donald Trump.

Hata hivyo inaonekana chama kipya kitaingia kwenye changamoto kubwa hasa kutokana na mfumo wa Marekani wa vyama viwili vikuu (Democrat na Republican) ambapo ni vigumu kwa chama kipya kupata nafasi ya kujiimarisha kitaifa na hadi sasa haijajulikana ni wanasiasa gani au Watu mashuhuri watakaojiunga naye.

0 Comment

Trump amuonya Musk kuwa atarudi kwao Afrika KusiniAfyaclass Forum •

Rais wa Marekani Donald Trump ametishia kusitisha mabilioni ya dola ya ruzuku zinazotolewa kwa kampuni za Tesla na SpaceX zinazomilikiwa na bilionea Elon Musk kufuatia mvutano unaoendelea kati yao ambapo hii ni baada ya Musk kukosoa vikali mswada mpya wa kodi na matumizi ya Serikali unaolenga kufuta ruzuku za ununuzi wa magari ya umeme hatua inayotajwa kuathiri moja kwa moja kampuni ya Tesla.



Trump amenukuliwa akisema kuwa bila ruzuku hizo, Musk atahitaji kufunga biashara na kurudi nyumbani Afrika Kusini, kauli iliyozua mjadala mpana nchini humo na kwa upande wake, Musk hakusita kujibu kwa maneno makali akisema, “Zuia kila kitu sasa.”

Aidha mabishano haya yameibuka wakati ambapo Seneti ya Marekani imepitisha mswada huo kwa kura chache tu huku soko la hisa la Tesla likiripotiwa kushuka kwa asilimia kubwa ambayo ni ishara ya wasiwasi kwa wawekezaji kuhusu mustakabali wa kampuni hiyo.

@dw_kiswahili

0 Comment

Madhara ya kupachika chipu kwenye ubongo wa binadamuAfyaclass Forum •

Telepathy: Chipu ya ubongo ambayo Elon Musk anadai aliiweka ndani ya mwanadamu inaleta mashaka gani?

Kampuni ya Musk haiko peke yake katika kinyang’anyiro cha chipu za ubongo zisizotumia waya.

Je, siku inakaribia ambapo wanadamu wataweza kudhibiti kompyuta kwa kutumia akili zao?

Mjasiriamali Elon Musk alichochea mjadala huo kwa kutangaza siku ya Jumatatu kwamba kampuni yake ya Neuralink ilifanikiwa kupachika moja ya chipu zake za ubongo ndani ya binadamu.

Katika chapisho kwenye X, Elon Musk alisema kuwa shughuli za “kuleta matumaini” za ubongo ziligunduliwa baada ya kuwekewa chipu hizo na kwamba mgonjwa “amepona vizuri.”

Lengo la kampuni ni kuifanya teknolojia iwe yenye kufaa kwa ajili ya kutibu magonjwa magumu ya neva.

“Kwa kampuni yoyote inayotengeneza vifaa vya matibabu, jaribio la kwanza la mwanadamu ni hatua muhimu,” anasema Profesa Anne Vanhoestenberghe kutoka taasisi ya King’s London.

Kwa mujibu wa mtaalamu huyo, makampuni kadhaa yanafanyia kazi bidhaa zinazotia matumaini , lakini ni machache tu ambayo yamefanikiwa kuingiza vifaa vyao kwa binadamu.

Vanhoestenberghe anaonya, hata hivyo, kwamba “mafanikio ya kweli” yanaweza kupimwa kwa muda mrefu tu na kwamba “Elon Musk ni mzuri sana katika kuchochea hisia kuhusu kampuni yake.”

Hadi sasa, hakuna uthibitisho wa kujitegemea wa madai ya Musk. Neuralink pia haikutoa taarifa kuhusu utaratibu huo.

BBC imewasiliana na kampuni hiyo na mdhibiti wa matibabu wa Marekani, Mamlaka ya Chakula na Dawa (FDA), kwa maoni.

Jinsi Telepathy inavyofanya kazi?

Katika chapisho lingine kwenye X, Musk alionyesha kuwa bidhaa ya kwanza ya Neuralink itaitwa Telepathy.

“Watumiaji wa kwanza watakuwa wale ambao wamepoteza udhibiti wa viungo vyao,” aliongeza Bw. Musk.

Kisha akamtaja Stephen Hawking, mwanasayansi maarufu wa Uingereza ambaye aliugua ugonjwa mbaya wa ubongo.

“Fikiria kama mchuuzi angeweza kuwasiliana haraka kuliko dalali. Hilo ndilo lengo.”

Utaratibu huo unahusisha kupandikiza chipu ndogo, iliyofungwa kwa kifaa hermetically moja kwa moja kwenye ubongo wa mgonjwa.

Chipu hii imeunganishwa kwa vifaa vidogo vya kielekroniki 1,024, vyenye ukubwa ulio sawa na ywele za binadamu, na kinaendeshwa na betri inayoweza kuchajiwa bila waya.

Kifaa hiki kinawasiliana na kompyuta ya nje, ikiruhusu kutuma na kupokea ishara.

Je, lenzi ya Neuralink iko salama?

Kampuni kadhaa zimeingia katika matumizi ya matibabu ya vipandikizi vya chip za ubongo.

Wasiwasi kuhusu teknolojia hii ni pamoja na hatari za kimwili za muda mfupi, athari za muda mrefu za matibabu na maswali ya kimaadili.

Uendeshaji wowote wa ubongo hubeba hatari.

Mnamo Disemba 2022, ripoti ya Reuters ilionyesha kuwa Neuralink ilishiriki katika majaribio ambayo yalisababisha vifo vya takriban wanyama 1,500, wakiwemo kondoo, nyani na nguruwe.

Mnamo Julai 2023, Idara ya Kilimo ya Marekani, ambayo ina jukumu la kuchunguza masuala ya ustawi wa wanyama, ilisema haikukubaini ukiukwaji wowote wa sheria za utafiti wa wanyama katika kampuni ya Musk, ingawa uchunguzi tofauti unaendelea.

Ukweli kwamba FDA iliidhinisha majaribio ya kibinadamu, hata hivyo, ina maana kwamba kampuni ya Musk imeshinda baadhi ya vikwazo vyake.

Labda wasiwasi mkubwa zaidi ni matokeo ya muda mrefu ya kutumia kifaa kama hicho kwenye ubongo, chombo kigumu ambayo bado hayajajulikana.

Kwa vile hii ni tasnia changa, hakuna data za kutosha kuhusu madhara yanayoweza kutokea. Hii itabadilika na majaribio ya kibinadamu na itakuwa muhimu kwa maendeleo ya bidhaa zinazofanana.

Maswali ya kimaadili ni ya kibinafsi zaidi. Teknolojia hizi huibua wasiwasi kuhusu ulinzi wa data, matumizi yanayowezekana na uwezekano wa kuimarisha uwezo wa utambuzi wa binadamu.

Miradi mingine

Nchini Uchina, kituo kimejitolea pekee kwa utafiti na uvumbuzi katika uwanja wa ujumuishaji wa ubongo na kompyuta.

Wakati teknolojia ya Musk ikijadiliwa kufuatia tangazo lake, baadhi ya wapinzani wake wamekuwa na teknolojia hii miongo miwili.

Kampuni ya Marekani ya Blackrock Neurotech, yenye makao yake makuu katika jimbo la Utah, ilitekeleza njia ya kwanza kati ya nyingi za kompyuta za ubongo mwaka wa 2004.

Precision Neuroscience, iliyoundwa na mmoja wa waanzilishi-wenza wa Neuralink, pia inalenga kusaidia watu waliopooza.

Kipandikizi chake kinaonekana kama kipande chembamba cha mkanda ambacho huwekwa kwenye uso wa ubongo na kinaweza kupandikizwa kupitia “cranial microslit,” ambayo kampuni inasema ni utaratibu rahisi zaidi.

Vifaa vingine vilivyopo pia vimetoa matokeo.

Katika tafiti mbili tofauti za kisayansi zilizofanywa hivi karibuni nchini Marekani, vipandikizi vilitumiwa kufuatilia shughuli za ubongo wakati mtu alipojaribu kuongea, shughuli ambayo inaweza kuamuliwa ili kuwasaidia binadamu katika mawasiliano.

Makampuni mengine yamefanya maendeleo sawa katika eneo hili, ikiwa ni pamoja na École Polytechnique Fédérale de Lausanne (EPFL) ya nchini Uswisi, ambayo iliweza kumwezesha mtu aliyepooza kutembea kwa kufikiri tu.

Ili kufanya hivyo, vipandikizi vya kielektroniki viliwekwa kwenye ubongo na uti wa mgongo wa mwanamume huyo ili kuwasilisha mawazo yake bila waya kwenye miguu yake.

Maelezo ya awali ya maendeleo ya utafiti huu yalichapishwa katika jarida lililopitiwa na jarida la tathimini ya uvumbuzi wa kisayansi – Nature, mnamo mwezi Mei 2023.

Madhara ya kupachika chipu kwenye ubongo wa binadamu
0 Comment
Notification
Karibu Afyaclass Forum Jukwaa linalojadili mambo mbali mbali ikiwemo afya,Magonjwa na Updates Zote,Tembelea hapa kila Siku,Pia Share Maoni yako kwenye jukwaa hili Afyaclass Forum ASANTE.
UNDERSTOOD