Showing posts with label Kenya. Show all posts
Showing posts with label Kenya. Show all posts

Wagonjwa wateseka Kenya,Kisa mgomo wa madaktariAfyaclass Forum •

Wagonjwa wateseka Kenya,Kisa mgomo wa madaktari

Huduma za matibabu maeneo mbali mbali nchini Kenya zimevurugika kufuatia mgomo wa kitaifa wa madaktari wagonjwa wanaotafuta huduma na kutoa wito kwa serikali kupata suluhu la haraka kuutatua mgomo huo.

Mgomo huu ambao umeathiri hospitali za umma kote nchini Kenya umeibua hali ya mahangaiko miongoni mwa wagonjwa ambao wengi wamelalamikia kukosa huduma hasaa zinazohitaji utaalamu wa madaktari kama vile upasuaji.

Alvester Goldmea na Billy Aoko ni miongoni mwa wagonjwa waliotafuta huduma za matibabu katika hospitali ya rufaa na mafunzo ya Jaramogi Oginga Odinga inayotegemewa sana na wakaazi Magharibi mwa Kenya, wanasema kuna utofauti katika utoaji huduma za matibabu kipini hiki cha mgomo wa madaktari.

Katika hospitali kuu ya Kisumu, Goldmea anasema, “Vyenye nilikuja nikiiangalia na hii ya jana iko tofauti wanakuja kidogo naye Aoko anasema hospitali kuu ya rufaa na mafunzo ya Jaramogii Oginga Odinga,” daktari hajakuja hospitalini hatujahudumiwa bado.”

Mgomo huu unaendelea huku muungano wa kitaifa wa madaktari KMPDU ukishikilia kuwa wanachama wake wataendelea na mgomo huo hadi pale mahitaji yao yatakapoangaziwa mazungomzo kati ya muungano huo na wizara ya afya yakigonga mwamba licha ya kukutana na waziri Susan Nakhumicha.

Baadhi ya yanayoshinikiza ni kuangaziwa upya marupurupu ya madaktari walio kwenye mafunzo ya nyanjani, utekelezwaji na jumla makubaliano ya mwaka 2017 yaliyolenga kuimarisha maslahi ya madaktari ikiwemo mishahara yao anavyoelezea katibu mkuu muungano wa madaktari KMPDU Dkt. Davji Atellah, “Mgomo ungalipo, tutaishia kuchosha kurudia maana tutakuwa katika hali hii kwa muda mrefu sana, tunalenga huu kuwa mgomo wetu wa mwisho wa mwongo huu.

Wizara ya afya hata hivyo imeratibu kuwasilisha madaktari wa nyanjani katika hospitali za umma nchini kuanzia tarehe mosi mwezi Aprili ili kutimiza mojawapo ya hitaji linaloshinikizwa na muungano wa KMPDU ambao unashikilia kuwa, ahadi hii itazingatiwa tu baada ya utekelezwaji wake.

Wizara ya afya ya kitaifa imeahidi kuangaziwa tatizo la mgomo wa madaktari kupitia kushirikishwa kwa washikadau muhimu kwenye asasi za serikali kauli ambayo imetolewa na waziri wa afya ya kitaifa Susan Nakhumicha, “Ni mambo ambayo yanashirikisha wizara ya elimi, Baraza la magavana, huduma ya uma, tume ya uratibu mishahara ya ummaa SRC, wizara ya afya, mkuu wa huduma za umma na  tunafurahi kuyapelekwa huko.”

Miongoni mwa asasi zilizochukua hatua kwa mgomo wa madaktari ni baadhi ya serikali za kaunti mfano jimbo la Kisii ambalo liliwasilisha hoja ya kupigwa marufuku madaktari jimbo hilo kushiriki mgomo mahakama ya leba ikiidhinisha ombi hilo,  serikali jimbo la Kisumu pia limetaja mgomo huo kuwa kinyume cha Sheria.

Credits; Source Info|

Dw_Swahili

Wagonjwa wateseka Kenya,Kisa mgomo wa madaktari
0 Comment

Kenya;Bingwa Marathon Kelvin Kiptum afariki kwa kujeruhiwa kichwaniAfyaclass Forum •

Kenya;Bingwa Marathon Kelvin Kiptum afariki kwa kujeruhiwa kichwani

Uchunguzi wa maiti umebaini kuwa bingwa wa rekodi ya dunia ya mbio za marathon nchini Kenya Kelvin Kiptum alifariki kutokana na majeraha mabaya kichwani katika ajali ya barabarani mapema mwezi huu.

Mwanapatholojia mkuu wa serikali ya Kenya Johanssen Odor aliambia vyombo vya habari kuwa majeraha hayo yalikuwa sawa na yale wanayopata watu katika ajali za barabarani.

Nyota huyo mwenye umri wa miaka 24 na kocha wake Mnyarwanda Gervais Hakizimana walifariki katika ajali iliyotokea usiku wa kuamkia tarehe 11 Februari karibu na nyumbani kwake kaskazini-magharibi mwa Kenya.

Mazishi ya Hakizimana yamefanyika nchini Rwanda.

Kiptum atazikwa Ijumaa katika kijiji cha nyumbani kwake, Chepkorio katika Kaunti ya Elgeyo-Marakwet, kwenye hafla inayotarajiwa kuwa ya kiserikali.

Kiptum alipata umaarufu mwaka jana aliposhinda mbio za marathon za Chicago na kuweka rekodi mpya ya dunia ya saa 2:00:35.

Alishinda rekodi ya awali iliyokuwa ikishikiliwa na Eliud Kipchoge kwa sekunde 34 – na kumfanya Kiptum kuwa mpinzani mkuu wa Kipchoge msimu wa 2024.

Wawili hao walikuwa wametajwa katika timu ya Kenya ya mbio za marathon kwa ajili ya Michezo ya Olimpiki ya Paris baadaye mwaka huu.

Timu yake ilikuwa imetangaza kwamba Kiptum angejaribu kukimbia umbali wa kilomita 42 chini ya saa mbili katika mbio za Rotterdam marathon – hatua ambayo haijawahi kufikiwa katika mashindano ya wazi.

Kenya;Bingwa Marathon Kelvin Kiptum afariki kwa kujeruhiwa kichwani
0 Comment

Mkenya avunja rekodi kwa kufundisha somo la Sayansi kwa saa 62Afyaclass Forum •

Mkenya avunja rekodi kwa kufundisha somo la Sayansi kwa saa 62.
• • • • • •
Mwalimu kutoka Kenya Rose Tata Wekesa ameweka jina lake katika vitabu vya historia kwa kufundisha darasa refu zaidi la sayansi kuwahi kutokea, akitumia saa 62 dakika 33 na sekunde 34.

“Nina timu nyuma yangu ambayo imesaidia katika kuandaa somo. Siku tatu zilizopita, nilikesha kwa saa 44 ili kuuzoesha mwili wangu kukesha,” alisema.

Rose Tata Wakesa mwalimu katika shule ya St Austin’s Lavington amefanya jaribio hilo ikiwa ni katika hatua za kuvunja rekodi ya dunia ya Guiness kama somo lililofundishwa kwa muda mrefu zaidi.


Guinness World Record, bado haijaidhinisha mafanikio ya Wekesa.

Mkenya avunja rekodi kwa kufundisha somo la Sayansi kwa saa 62
0 Comment
Notification
Karibu Afyaclass Forum Jukwaa linalojadili mambo mbali mbali ikiwemo afya,Magonjwa na Updates Zote,Tembelea hapa kila Siku,Pia Share Maoni yako kwenye jukwaa hili Afyaclass Forum ASANTE.
UNDERSTOOD