Showing posts with label TMA yatoa tahadhari. Show all posts
Showing posts with label TMA yatoa tahadhari. Show all posts

TMA yatoa tahadhari mvua kubwa mikoa 19 LeoAfyaclass Forum •

Mvua hizo zinatarajiwa kunyesha Leo Jumapili, Desemba 28, 2025.

Zinaweza kusababisha mafuriko, maporomoko ya udongo na usumbufu wa shughuli za kiuchumi na kijamii. 

Dar es Salaam. Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imewataka wananchi kuchukua tahadhari ya kujikinga na madhara ya mvua kubwa inayotarajia kunyesha katika mikoa 19 nchini ikiwemo Dar es Salaam. 

TMA imesema mvua hizo zinatarajiwa kunyesha kesho Jumapili, Desemba 28, 2025, na huenda zikasababisha madhara mbalimbali ikiwamo mafuriko, maporomoko ya udongo na usumbufu wa shughuli za kiuchumi na kijamii. 

Taarifa ya TMA iliyotolewa leo Desemba 27, 2025 imeeleza kuwa mvua hiyo itanyesha katika mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Manyara, Kigoma, Katavi, Singida, Dodoma, Rukwa, Songwe, Mbeya na Iringa.

Mikoa mingine ni Njombe, Morogoro, Ruvuma, Tanga, Dar es Salaam, Lindi, Mtwara na Pwani ikijumuisha visiwa vya Mafia.

Wananchi wanaoishi katika maeneo tajwa, hususan walioko mabondeni na maeneo hatarishi, kuchukua tahadhari za mapema ili kuepuka athari zinazoweza kujitokeza kutokana na mvua hizo.

TMA imewasisitiza wananchi kuendelea kufuatilia taarifa na utabiri wa hali ya hewa unaotolewa mara kwa mara ili kupata taarifa sahihi na za wakati.

0 Comment

Tahadhari ya Mvua kubwa kwa Siku Tano Mfululizo-TMA Afyaclass Forum •

Tahadhari ya Mvua kubwa kwa Siku Tano Mfululizo-TMA 

Kama unaishi mikoa ya Morogoro, Lindi, Iringa, Mtwara, Mbeya, Songwe, Njombe na Ruvuma, basi kaa mguu sawa kwani Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa angalizo kuhusu uwepo wa hali mbaya ya hewa kwa siku tano.

Utabiri huo unakuja siku chache tangu baadhi ya mikoa kama Dar es Salaam na Morogoro kushuhudia mvua kubwa iliyoathiri miundombinu na kusababisha vifo.

Utabiri huo wa TMA uliotolewa leo Januari 29,2024 utaanza kesho Januari 30 na utadumu hadi Februari 2 mwaka huu.

“Angalizo la mvua kubwa limetolewa katika maeneo machache ya mikoa ya Morogoro, Lindi, Mtwara, Iringa, Mbeya, Songwe, Njombe na Ruvuma,”imeandikwa kwenye taarifa hiyo.

Wakazi katika mikoa hiyo watashuhudia athari ya makazi yao kuzungukwa na maji, pamoja na kuathirika kwa baadhi ya shughuli za kiuchumi.

Mkoani Morogoro hivi karibuni waliripotiwa watu watano kufariki dunia na wengine 246 kuokolewa kutokana na mvua kubwa iliyonyesha mjini Morogoro na kusababisha mafuriko yaliyoharibu makazi na barabara.

Kwa Mkoa wa Dar es Salaam mvua hizo zilisababisha barabara kutopitika, nyumba kuzingirwa maji na wananchi kupita  adha ya usafiri.

Mara kadhaa Serikali imekuwa ikisisitiza wananchi wote waliojenga bondeni kuhama mara moja kuepuka athari za mvua.

Tahadhari ya Mvua kubwa kwa Siku Tano Mfululizo-TMA
0 Comment
Notification
My blog is in the process of editing and perfecting the new template, so there are still some functions to click but not yet used. Note which blogs associated with your side please read this lesson to update the blog logo.
UNDERSTOOD