Showing posts with label jamii. Show all posts
Showing posts with label jamii. Show all posts

Ndoa Za Utotoni Na Madhara YakeAfyaclass Forum •

 NDOA ZA UTOTONI NA MADHARA YAKE

Kama nilivyokwisha kuelezea kwenye utangulizi wangu ndani ya baadhi ya makala zinazohusu Mimba za utotoni,

Mojawapo ya matokeo ya Ndoa za utotoni ni Mimba za utotoni,

Bado katika jamii zetu vitendo hivi vipo,watoto wanaolewa wakiwa wadogo kabsa na kupata mimba wakiwa watoto.

MADHARA YA NDOA ZA UTOTONI

-Moja ya hasara kubwa ambayo wengi wao wanapata ni kukatishwa masomo yao na kushindwa kuzifikia Ndoto zao

- Kuanza majukumu makubwa ya kutunza Familia ukiwa bado mtoto

- Kuendelea kuwa na hali mbaya kiuchumi

- Kuendelea kuwa na hali mbaya ya kiafya

- Kuwa kwenye hatari ya kupata magonjwa mbali mbali ya Zinaa katika umri mdogo kama vile;kaswende,kisonono,pangusa(chlamydia) n.k

- Kuwa kwenye hatari ya kupata Maambukizi ya virusi vya UKIMWI

- Kuwa kwenye hatari ya kupatwa na Saratani ya mlango wa kizazi yaani Cervical Cancer

- Kubeba Mimba kwenye umri mdogo na kupata madhara makubwa kama vile;

• Kujifungua kwa upasuaji

• Kuchanika Njia ya kujifungulia

• Kuchanika tumbo la uzazi

• Kuvuja damu nyingi wakati wa kujifungua

• Kupatwa na magonjwa kama Fistula n.k

• Kupoteza maisha n.k



0 Comment

Mtindo mbaya wa Maisha janga kwa Magonjwa yasioambukizaAfyaclass Forum •

Mtindo mbaya wa Maisha janga kwa Magonjwa yasioambukiza.

Jamii imetakiwa kuzingatia mtindo bora wa maisha na kufuata ulaji sahihi kama wanavyoshauriwa na wataalam wa afya ili kujikinga na magonjwa yasiyoambukiza ikiwemo magonjwa ya figo.

Hayo yamesema jana na Dkt.Gunini Kamba, akizungumza kwa niaba ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam ambaye alikua mgeni rasmi katika hafla fupi ya kukabidhi tuzo na medali kwa baadhi ya watumishi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili na taasisi nyingine zilizotolewa na Taasisi ya Profesa Jay ikiwa ni kutambua mchango wao katika kutoa huduma za afya.

Dr. Kamba amesema magonjwa yasiyoambukiza ikiwemo magonjwa ya figo yanazidi kuongezeka na gharama za matibabu kwa magonjwa hayo ni kubwa na si kila mwananchi anayeweza kumudu gharama hizo hivyo ni vyema jamii ikatambua hilo ili iweze kujikingwa kwa kuwa king ani bora kuliko tiba.

Awali akimkaribisha mgeni rasmi, Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dkt. Ellen Senkoro ameipongeza Taasisi ya Professor Jay kwa kutambua mchango mkubwa unaofanywa na Hospitali ya Muhimbili na kuwapongeza baadhi ya watumishi ambao wamechaguliwa kupata tuzo hizo na kusema kuwa Muhimbili itaendelea kutoa mchango kwa tasisi hiyo ili indelee kutoa hamasa kwa jamii kuhusu afya.

Kwa Upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Prof. Mohamed Janabi amesema kuwa kwa siku MNH-Upanga inatoa huduma ya kusafisha damu kwa wagonjwa wa figo 120 hadi 130 ambapo asilimia 90 ya magonjwa wa hayo yanasababishwa ya shinikizo la juu la damu pamoja na kisukari ambapo chanzo chake nikutozingatia lishe sahihi hivyo ni vyema watu wakazingatia swala la lishe bora.

Awali akizungumza baada ya kukabidhi tuzo hizo, Mkurugenzi wa Taasisi ya Professor Jay Florian Rutabingwa amesema taasisi hiyo itaendelea kutoa elimu ya afya kwa jamii ili kusaidia jamii kujikinga na magonjwa hayo ambayo yamekuwa yakiongezeka siku hadi siku.

Mtindo mbaya wa Maisha janga kwa Magonjwa yasioambukiza
0 Comment
Notification
Karibu Afyaclass Forum Jukwaa linalojadili mambo mbali mbali ikiwemo afya,Magonjwa na Updates Zote,Tembelea hapa kila Siku,Pia Share Maoni yako kwenye jukwaa hili Afyaclass Forum ASANTE.
UNDERSTOOD