Showing posts with label mvua za El Nino. Show all posts
Showing posts with label mvua za El Nino. Show all posts

Jikinge na Radi wakati wa Mvua kwa kufanya hayaAfyaclass Forum •

Mambo ya kuzingatia ili kujikinga na Radi wakati wa mvua.

Radi ni umeme unaotoka katika mawingu na hasa Wingu linaloitwa Wingu Anga ambalo lina barafu ndani yake, inapotokea Wingu na Wingu yanagongana ndipo umeme unapotokea, hali hiyo pia inaweza kuchangia barafu kushuka kwenye ardhi na kuwa mvua inayoitwa ‘Mvua ya Mawe’

Mtaalam na Mchambuzi wa Hali ya Hewa kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa (#TMA), Rose Senyagwa anaeleza Umeme wa Radi unaweza kuishia kwenye mawingu kwa maana ya kutoka ulipo kwenda juu au kwenda wingu lingine au kushuka ardhini

Anasema Umeme unaposhuka ardhini unaweza kusababisha madhara kwa viumbe na vitu vingine kwa kuwa mara nyingi Radi huwa inaanza kushambulia vitu virefu vya eneo husika.

Mambo ya kuzingatia ili kujikinga na Radi wakati wa mvua

1. Si Salama kujificha au kujikinga chini ya miti mirefu;

Kwa kawaida uelekeo wa Radi unachagua vitu virefu kuliko vyote katika eneo husika, miti ina uwezo wa kusafirisha umeme,

Hivo epuka kujificha au kujikinga chini ya miti mirefu.

2. Si Salama kujificha chini ya Minara au kwenye kitu chochote kirefu katika eneo husika ikiwemo chini ya nguzo za umeme au Transfoma.

3. Hauruhusiswi kutembea katika maji yanayotiririka au yaliyotuama

Mfano; kwenye dimbwi au maji yanayotembea barabarani,mtoni,Ziwani au katika bwawa,

Kwani maji yanaweza kupigwa na Umeme wa Radi.

4. Haishauriwi kutumia vifaa vya Umeme au vinavyotumia mionzi

Mfano; Simu, Kompyuta, au Laptop, TV, Radio, au Friji kwa kuwa mionzi yake inaweza kuingiliana na Radi.

Hayo ni baadhi ya mambo ya kuzingatia ili kujikinga na Radi wakati wa Mvua.

Chukua Tahadhari…!!!!

Jikinge na Radi wakati wa Mvua kwa kufanya haya
0 Comment

Mvua kubwa,mvua za el nino mpaka Aprili: TMA TanzaniaAfyaclass Forum •

Mvua kubwa,mvua za el nino mpaka Aprili: TMA Tanzania

TMA imesema kuna viashiria vya El-Nino kuendelea hadi Aprili, 2024.

Dar es Salaam. Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imesema bado kuna viashiria vya uwepo wa El-Nino hadi Aprili mwaka huu.

El-nino ni mfumo wa hali ya hewa unaosababishwa na ongezeko la joto la bahari katika eneo la kati la Kitropiki kwenye Bahari ya Pasifiki.

Mwaka jana, TMA ilieleza kuwepo kwa El-Nino katika kipindi cha mvua za msimu wa vuli zilizotarajiwa kuanza Oktoba hadi Desemba.

Mvua zimeendelea kunyesha kwenye maeneo mbalimbali nchini hadi sasa, TMA ikizitaja kuwa ni za nje ya msimu ambazo zimechangiwa na unyevunyevu kutoka magharibi ya misitu ya Congo, pia kuendelea kwa viashiria vya El-Nino.

Akizungumza na Mwananchi Digital, leo Januari 30, 2024  Meneja wa Utabiri wa TMA, Dk Mafuru Kantamla amesema viashiria vya El-Nino bado vipo hadi Aprili.

“Viashiria vyake bado vipo, ingawa nguvu yake si kubwa kama ilivyokuwa awali, mwanzo ilionyesha kilele chake ni Desemba au Januari, lakini viashiria bado vipo hadi Aprili,” amesema.

Akizungumzia wingi wa mvua katika maeneo mbalimbali nchini, amesema unasababishwa na migandamizo midogo ya hewa iliyoko mashariki mwa Kisiwa cha Madagascar.

“Hii migandamizo imekuwa na mchango mkubwa kwenye kuvuta upepo wenye unyevunyevu kutoka magharibi ya misitu ya Congo kuja maeneo mengi ya nchi.

“Kuwepo kwa migandamizo hii kwa takribani wiki tatu na kuimarika kwa ukanda wa mvua kumesababisha uwepo wa mvua hizi, ingawa inaonyesha Februari mosi na pili, 2024 migandamizo hii itakwenda kusini mwa ncha ya Bara la Afrika, hivyo hata mvua zitaanza kupungua,” amesema.

Akizungumzia athari kwa wakulima, amesema maeneo ambayo mvua inanyesha kwa wingi, kiwango cha unyevunyevu kwenye udongo huongezeka.

“Unyevunyevu ukipitiliza unaweza kuathiri mazao ambayo hayaendani na maji mengi, ni vema wakulima wachukue ushauri kutoka kwa maofisa ugani,” amesema.

Amesema katikati ya Februari, 2024 watatoa utabiri wa mvua za masika zinazotarajiwa kuanza Machi hadi Mei na kutoa mwelekeo wake.

Jana Januari 29, 2024, TMA ilitoa angalizo la uwepo wa hali mbaya ya hewa kwenye mikoa ya Morogoro, Lindi, Iringa, Mtwara, Mbeya, Songwe, Njombe na Ruvuma kwa siku tano kuanzia leo Januari 30, 2024, ikiwataka watu wachukue tahadhari.

Angalizo hilo limetolewa tayari, baadhi ya mikoa kama vile Dar es Salaam na Morogoro ikishuhudia madhara makubwa ya miundombinu ya barabara, madaraja na nyumba yaliyotokana na mvua.

Mvua kubwa,mvua za el nino mpaka Aprili: TMA Tanzania
0 Comment

Zaidi ya Watu 30 wamefariki kutokana na mafuriko makubwaAfyaclass Forum •

Waziri wa Habari wa Somalia, Daud Aweis amesema Mvua kubwa zinazoendelea kunyesha nchini humo zimesababisha mafuriko makubwa yaliyowaua watu zaidi ya 30.

Aweis amesema watu takribani laki 500,000 wameyahama makazi yao kutokana mafuriko na kuonya kwamba wengine zaidi ya milioni moja huenda wakaathirika.

Uharibifu mkubwa umeshuhudiwa katika mkoa wa Gedo, ulioko kusini mwa Somalia pamoja na Mkoa wa kati wa Hiran ambako kingo za Mto Shabelle zimevunjika na barabara kusombwa na maji katika mji wa Beledweyne.

Taifa hilo la pembe ya afrika limekumbwa na mvua kubwa isiyoisha tangu mwanzoni mwa mwezi Novemba, kutokana na hali ya hewa na ujio wa mvua za El Nino.

Zaidi ya Watu 30 wamefariki kutokana na mafuriko makubwa
0 Comment
Notification
My blog is in the process of editing and perfecting the new template, so there are still some functions to click but not yet used. Note which blogs associated with your side please read this lesson to update the blog logo.
UNDERSTOOD