Showing posts with label usikate tamaa. Show all posts
Showing posts with label usikate tamaa. Show all posts

Usikate Tamaa,Kufika Mahali Ambapo Mungu kakupangia inahitaji uwe hodari na moyo wa UshujaaAfyaclass Forum •

Katika Safari ya kuelekea Kanani yako(Mahali ambapo Mungu kakupangia) lazima uwe Hodari na Moyo wa Ushujaa,Hii ina maana lazima Upinzani,Vikwanzo,Majaribu,Kutishwa,kukatishwa tamaa n.k. Vitakuwepo.



Haimaanishi kwa Vile Mungu kakupa,hutapata kikwazo chochote,na haimaanishi Mungu kuwa Upande wako hataibuka Mjaribu.

Kitakachotokea ni kwamba; Mungu akiwa upande wako,atapigana na kila Adui anayesimama mbele yako,atawaondoa mhiti,Mperizi,Myebusi, na kila aina ya kikwazo mbele yako. Wewe unachotakiwa ni kuimarisha Imani yako kwake.

Yoshua wakati Mungu anampa jukumu la kupeleka Wana wa Israel Kanani, Ingawa Mungu alikuwa Pamoja naye, anamwambia;Uwe Hodari na Moyo wa Ushujaa.

Soma:Yoshua 1:6 "Uwe hodari na moyo wa ushujaa, maana ni wewe utakayewarithisha watu hawa nchi hii niliyowaapia baba zao ya kwamba nitawapa".

Hata kama kuna kanani yako Mungu amekupa,Adui watainuka tu. Unachotakiwa ni kuwa hodari na Moyo wa Ushujaa,Utafika Kanani yako.

0 Comment
Notification
My blog is in the process of editing and perfecting the new template, so there are still some functions to click but not yet used. Note which blogs associated with your side please read this lesson to update the blog logo.
UNDERSTOOD