Afyaclass MATATIZO YATOKANAYO NA UNYWAJI WA POMBE KIPINDI CHA UJAUZITO

 MATATIZO YATOKANAYO NA UNYWAJI WA POMBE KIPINDI CHA UJAUZITO

Baadhi ya madhara yanayoweza kumpata kiumbe aliye tumboni kwa mama kutokana na unywaji wa pombe kipindi cha ujauzito ni pamoja na


Kutoka/kuharibika kwa mimba

Mtoto kuzaliwa akiwa na uzito mdogo

Mtoto kuzaliwa akiwa na ulemavu wa mbavu na kidari (sternum)

Mtoto kuzaliwa akiwa na matatizo ya mgongo uliopinda (kibiongo) na vidole vilivyoundana

Mtoto kuzaliwa akiwa na kichwa kidogo kuliko kawaida (microcephaly)

Mtoto kuzaliwa akiwa na matatizo ya pua

Kuzaliwa na matatizo ya taya

Mtoto kuwa na matatizo ya kutokuona mbali

Matatizo ya moyo kama vile moyo kuwa na tundu

Matatizo ya figo

Mtoto kuwa na ubongo mdogo na pia matatizo ya akili

Mtoto kuzaliwa akiwa na mdomo sungura (lip palate na cleft palate)

Matatizo ya kimaumbile ya masikio na ulemavu kwenye sehemu za uzazi (genital malformations).

Aina mojawapo ya kansa ya chembe nyeupe za damu (Acute Myeloid Leukemia). Hii ni kwa mujibu wa utafiti uliochapishwa katika jarida moja la utafiti wa kansa la Marekani lijulikanalo kama Journal of the American Association for Cancer Research.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Karibu Sana..!!!





You, Mehreen and others

WEKA MAONI HAPA(Reply)

Notification
My blog is in the process of editing and perfecting the new template, so there are still some functions to click but not yet used. Note which blogs associated with your side please read this lesson to update the blog logo.
UNDERSTOOD