Afyaclass Mwanaume achanjwa mara 217 dhidi ya Uviko ndani ya miezi 29

Mwanaume achanjwa mara 217 dhidi ya Uviko ndani ya miezi 29.

Mwanaume mmoja mwenye umri wa miaka 62 kutoka Magdeburg, Ujerumani, “kwa makusudi na kwa sababu za kibinafsi“ alichanjwa mara 217 dhidi ya Uviko ndani ya miezi 29.

Ushahidi ulikusanywa na mwendesha mashitaka wa Magdeburg, aliyeanzisha uchunguzi wa madai ya ulaghai lakini hakufungua mashitaka ya jinai.

Watafiti kutoka Chuo Kikuu cha Erlangen-Nuremberg wamemfanyia vipimo mbalimbali mwanamume huyo kuchunguza madhara ya kinga ya mwili.

Mwanamume huyo “hakuripoti madhara yoyote yanayohusiana na chanjo,” waliandika katika jarida la sanyansi la Lancet.

Hakukuwa na dalili kwamba amewahi kuambukizwa Covid, hata hivyo.

>>Soma Zaidi kuhusu; Ugonjwa wa COVID-19

You, Mehreen and others

WEKA MAONI HAPA(Reply)

Notification
Karibu Afyaclass Forum Jukwaa linalojadili mambo mbali mbali ikiwemo afya,Magonjwa na Updates Zote,Tembelea hapa kila Siku,Pia Share Maoni yako kwenye jukwaa hili Afyaclass Forum ASANTE.
UNDERSTOOD