Afyaclass Bongo Social Tanzania haina Uhaba wa dawa za ARVs

Tanzania haina Uhaba wa dawa za ARVs

 Serikali kupitia Bohari ya Dawa (MSD) imesema imejipanga kukabiliana na changamoto zozote zitakazojitokeza kutokana na uamuzi wa Rais wa sasa wa Marekani, Donald Trump kusitisha misaada ya kwa nchi za Afrika ikiwemo ARVs ambapo Watanzania wametolewa hofu kwamba ARVs zipo za kutosha Tanzania.

Akiongea kuhusu mafanikio ya miaka minne ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan leo Jumatano March 19, 2025 Jijini Dodoma, Mkurugenzi wa MSD, Mavere Tukai amesema kutokana na maelekezo ya Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa MSD, hakuna cha kusubiri “Tumeshafanya maandalizi ya kutosha kwa kuzingatia athari zake kwa Wananchi”

“Tumehakikisha tunayo mikataba ya kutosha katika ununuzi wa dawa zote za miradi msonge (ikiwemo ARVs, vyandarua, chanjo n.k) ambayo inatokana na misaada na ufadhili wa USAD ili Marekani ikisitisha misaada Watanzania wasiathirike na chochote”

You, Mehreen and others
Hashtag:

WEKA MAONI HAPA(Reply)

Notification
Karibu Afyaclass Bongo Social Jukwaa linalojadili mambo mbali mbali ikiwemo afya,Magonjwa na Updates Zote,Tembelea hapa kila Siku,Pia Share Maoni yako kwenye jukwaa hili Afyaclass Bongo Social ASANTE.
UNDERSTOOD