Familia imefikia makubaliano na serikali juu ya mazishi ya Raisi Edgar Lungu

Familia imefikia makubaliano na serikali juu ya mazishi ya Raisi Edgar Lungu

#1

Familia imefikia makubaliano na serikali juu ya mazishi ya Raisi Edgar Lungu 



Baada ya tamko la Familia ya aliyekuwa Rais wa Zambia Edgar Lungu ambalo yalikuwa ni maagizo yake ya kwamba mpinzani wake wa kisiasa na Rais wa sasa Hakainde Hichilema hapaswi kufika popote karibu na mwili wake familia imefikia makubaliano na serikali juu ya mazishi ya Kiongozi Huyo na mpango wa mazishi umekamilika.

Baada ya Mazungumzo ya muda mrefu baina ya familia ya Lungu wamekubaliana kwamba Mwili wa Rais huyo wa zamani utasafirishwa kutoka Afrika Kusini kwenda mji mkuu wa Zambia, Lusaka siku ya Jumatano wiki hiii kwa ndege binafsi ya kukodi, na baada ya kuwasili utapokelewa na familia na kisha kutakuwa na heshima kamili ya Kijeshi na baada ya hapo utasafirishwa kwenda kwenye makzi yake mjini Lusaka. 

Aidha wananchi wa Zambia watapata nafasi ya kutoa heshima zao za mwisho kwanzia alhamis na zoezi hilo litakamilika siku ya jumamosi ambapo Mazishi ya Kitaifa yatafanyika jumapili Juni 22, 2025 na maombolezo yatakamilika jumatatu ambapo mapaka sasa bado haijajulikana endapo atazikwa katika eneo rasmi la mazishi ya Rais au katika makazi yake binafsi.

Hata hivyo msemaji wa familia Makebi Zulu katika mazungumzo yake na vyombo vya habari akiwa pamoja na Katibu wa Baraza la Mawaziri la Zambia Patrick Kangwa amesema familia hiyo imeomba radhi kwa usumbufu na maumivu ambayo mazungumzo ya muda mrefu yamesababisha ambapo amesema wamefanya kila linalowezekana kuhakikisha wanaheshimu matakwa ya kibinafsi ya Rais wa zamani.

Sambamba na hilo kwa upande wa serikali Katibu Mkuu wa serikali Patrick Kangwa amewashukuru wananchi wa Zambia kwa uvumilivu wao wakati huu mgumu ambapo kwa upande wa familia umesisitiza kuwa wanaamini kuwa Serikali haitakwenda kinyume na makubaliano yao.

REPLY HAPA


image quote pre code