WEWE NI SHUJAA,TUMIA UWEZO HUO HUO ULIOKUWA NAO

WEWE NI SHUJAA,TUMIA UWEZO HUO HUO ULIOKUWA NAO

#1

WEWE NI SHUJAA,TUMIA UWEZO HUO HUO ULIOKUWA NAO



Mstari wa Kusimamia ni Waamuzi 6:11-16

Waamuzi 6:11 Malaika wa Bwana akaenda akaketi chini ya mwaloni uliokuwa katika Ofra, uliokuwa mali yake Yoashi, Mwabiezeri; na mwanawe Gideoni alikuwa akipepeta ngano ndani ya shinikizo, ili kuificha machoni pa Wamidiani.

Mstari 12 Malaika wa Bwana akamtokea, akamwambia, Bwana yu pamoja nawe, Ee shujaa.

Mstari 13 Gideoni akamwambia, Ee Bwana wangu, ikiwa Bwana yu pamoja nasi, mbona mambo haya yote yametupata? Yako wapi matendo yake ya ajabu, waliyotuhadithia baba zetu, wakisema, Je! Siye Bwana, aliyetuleta huku kutoka Misri? Ila sasa ametutupa, naye ametutia katika mikono ya Midiani.

Mstari 14 Bwana akamtazama, akasema, Enenda kwa uwezo wako huu, ukawaokoe Israeli na mkono wa Midiani. Je! Si mimi ninayekutuma?

Mstari 15 Akamwambia, Ee Bwana, nitawaokoa Israeli kwa jinsi gani? Tazama, jamaa zangu ndio walio maskini sana katika Manase, na mimi ndimi niliye mdogo katika nyumba ya baba yangu.

Mstari 16 Bwana akamwambia, Hakika nitakuwa pamoja nawe, nawe utawapiga Wamidiani kama mtu mmoja.

Usijidharau wewe ni Shujaa, Kipo kitu ambacho Mungu kaweka ndani yako, kwa uwezo huo huo inuka wewe ni Shujaa ukatende mambo makubwa,

Haijalishi kwenu ni Maskini Sana,Haijalishi wewe ni mdogo kuliko wote, wala haijalishi upo ndani ya mapango umejificha saa hii Kama Gideoni,uwezo wako hauonekani na Mtu yeyote. Bwana yu Pamoja nawe,Ee shujaa,Enenda kwa uwezo wako huu,utafanya mambo makubwa.

Changia Mada hapa(Reply)


image quote pre code