Showing posts with label Ajali. Show all posts
Showing posts with label Ajali. Show all posts

Breaking; Lori la Mafuta Laua Watu Zaidi ya 90Afyaclass Forum •

Breaking; Lori la Mafuta Laua Watu Zaidi ya 90

Zaidi ya Watu 90 Wafariki Dunia Wakijaribu Kuchota Mafuta kwenye Ajali ya Lori

Jeshi la Polisi Nchini Nigeria Limesema Zaidi ya watu 90 wameuawa na wengine 50 kujeruhiwa baada ya lori la mafuta kulipuka kaskazini magharibi mwa nchi hiyo.

Msemaji wa Polisi Katika Jimbo la jigawa DSP Lawan Shiisu Adam alisema mlipuko huo ulitokea kwenye barabara kuu ya Taura, huku makumi ya watu wakikimbilia kwenye gari kuchukua mafuta kwenye Lori hilo.

Wakazi walikuwa wakichota mafuta katika lori lililopinduka wakati mlipuko ulipotokea, na kusababisha moto mkubwa ulioua watu 94 papo hapo,” alisema

0 Comment

Zaidi ya Watu 50 Wafariki kufuatia Boti Kuzama Ziwa Kivu, Mashariki Mwa CongoAfyaclass Forum •

Zaidi ya Watu 50 Wafariki kufuatia Boti Kuzama Ziwa Kivu, Mashariki Mwa Congo

Watu zaidi ya 50 wamefariki dunia huku wengine wengi wakiwa hawafahamiki walipo baada ya boti waliyokuwa wakisafiria kuzama katika Ziwa Kivu, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Taarifa za awali zinaeleza kuwa ajali hiyo imetokea leo, Alhamisi, Oktoba 3, 2024 ambapo chanzo kinatajwa kuwa ni boti hiyo kuelemewa na mizigo pamoja na abiria waliokuwa wengi kuliko uwezo wake.

Picha zinasambaa kwa kasi kwenye mitandao ya kijamii, zikionesha vikosi vya uokoaji vikijaribu kuokoa maisha ya watu wengi walioopolewa kwenye mto huo, huku video nyingine ikidaiwa kuwa ndivo jinsi boti hiyo ilivyozama.

Taarifa zaidi zinaeleza kuwa takribani watu 10 wameokolewa wakiwa hai na kukimbizwa hospitali.

0 Comment

Watu saba wamefariki dunia kwa ajali mkoani MorogoroAfyaclass Forum •

Watu saba wamefariki dunia na wengine sita kujeruhiwa mkoani Morogoro baada ya magari mawili kugongana uso kwa uso katika eneo la Dakawa wilayani Mvomero.

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo Kamanda wa Polisi mkoani Morogoro SACP Alex Mkama amesema tukio hilo limehusisha gari aina ya Noah yenye namba za usajili T 101 DKB iliyokuwa inatokea Dumila kwenda Morogoro mjini kugongana na lori lenye namba za usajili RS 980 ambalo lilikuwa linatokea Morogoro kwenda Dodoma.

“Tukio hilo limetokea baada ya Lori kuacha njia yake baada ya kuover take na kukutana uso kwa uso na gari ya abiria Noah na kusababisha vifo na majeruhi kama nilivyosema”amesema Kamanda wa polisi Alex Mkama

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya wilaya ya Mvomero Dkt. Frances Mogel amesema wamepokea majeruhi saba na miili ya watu waliofariki dunia ilikuwa sita

“Leo asubuhi tulikuwa tunatokea Dumila tumepanda Noah kufika bwawa la Hatari ndio Lori likatupush uso kwa uso,tulibahatika kutoka ndio kama unavyotuona ila wenzetu wengine wamefariki akiwemo na dereva wetu,amesema Maimuna Salum manusura wa aajali

Watu saba wamefariki dunia kwa ajali mkoani Morogoro
0 Comment

Raia wa Togo ni miongoni mwa watu waliokuwemo katika ajali ARUSHAAfyaclass Forum •

Raia wa Togo ni miongoni mwa watu waliokuwemo katika ajali iliyotokea Februari 25. 2024 katika eneo la Ngaramtoni mkoani Arusha
na kusababisha vifo vya watu 25 na wengine zaidi ya 20 kujeruhiwa.

Kwa sasa Apelo anapatiwa matibabu katika hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Arusha, Mount Meru ambapo ameishukuru Serikali kwa huduma nzuri za matibabu anazopatiwa hospitalini hapo.

Amesema kwa namna ajali hiyo ilivyokuwa na huduma alizopatiwa kama asingekuwa Tanzania angekuwa amekwishafariki dunia na kwamba ukarimu wa Watanzania ndio uliookoa maisha yake.

“Kwa ajali hii ningekuwa nchini kwetu tayari ningekuwa nimepoteza maisha, kwani kule bila kulipia huduma za matibabu hupatiwi huduma, lakini kwa Tanzania walivyo wakarimu na weledi wameweza kuokoa maisha yangu mpaka sasa naendelea vizuri na naweza kuongea,” Amesema raia huyo wa Togo

Apelo alikuja Tanzania kushiriki kwenye semina iliyokuwa ikifanyika mkoani Arusha, ambapo pia walikwenda kufanya utalii na walipokuwa wakirejea ndipo wakapata ajali.

Raia wa Togo ni miongoni mwa watu waliokuwemo katika ajali ARUSHA
0 Comment

Idadi waliofariki dunia kwenye Ajali Arusha yafika 25Afyaclass Forum •

Idadi waliofariki dunia kwenye Ajali Arusha yafika 25

Gari la Shule ya Mchepuo wa Kiingereza ya New Vision, likinyanyuliwa baada ya kugongwa na lori katika eneo la Kibaoni (Ngaramtoni), wilayani Arumeru leo Jumamosi Februari 24, 2024 katika Barabara Kuu ya Arusha-Namanga

Ajali ilitokea Februari 24, 2024 eneo la Kibaoni (Ngaramtoni), wilayani Arumeru ikihusisha magari manne.

Arusha. Idadi ya vifo vilivyotokana na ajali iliyohusisha magari manne eneo la Kibaoni (Ngaramtoni), Barabara Kuu ya Arusha-Namanga imeongezeka na kufikia 25, majeruhi wakiwa 21.

Ajali ilitokea Jumamosi Februari 24, 2024 ikihusisha lori na magari mengine madogo matatu.

Akitoa taarifa jana usiku katika Hospitali ya Rufaa ya Mount Meru, Kamishna wa Polisi Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi, Awadhi Juma Haji amesema miongoni mwa waliofariki  wanawake ni 11, akiwamo mtoto mdogo wa kike na raia wa kigeni saba.

Ajali ilihusisha lori lenye namba za usajili KAC 943 H aina ya Mack lenye tela namba ZF 6778 mali ya kampuni ya KAY Construction ya Nairobi nchini Kenya.

“Idadi ya majeruhi ni 21 kati yao wanaume ni 14 na wanawake ni saba,” amesema.

Magari mengine yaliyopata ajali katika tukio hilo ni T 623 CQF aina ya Nissan Caravan, T 879 DBY aina ya Mercedes Benz Saloon na T 673 DEW aina ya Toyota Coaster mali ya shule ya mchepuo wa Kingereza ya New Vision.

Kuhusu chanzo cha ajali, amesema uchunguzi wa awali umeonyesha kuwa ni kufeli mfumo wa breki wa lori, hivyo kusababisha liyagonge magari mengine yaliyokuwa mbele yake.

Amesema Jeshi hilo linaendelea kumsaka dereva wa lori hilo anayedaiwa kutoroka baada ya ajali.

Awali, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Justine Masejo alitaja idadi ya waliofariki kuwa ni 15 na kati yao raia wa kigeni walikuwa watatu.

Credits:Mwananchi.

Idadi waliofariki dunia kwenye Ajali Arusha yafika 25
0 Comment
Notification
My blog is in the process of editing and perfecting the new template, so there are still some functions to click but not yet used. Note which blogs associated with your side please read this lesson to update the blog logo.
UNDERSTOOD