Showing posts with label Elimu na Ushauri. Show all posts
Showing posts with label Elimu na Ushauri. Show all posts

Kitandani kuna mamilioni ya bakteria, fangasi, wadudu na virusiAfyaclass Forum •

Kitandani kuna mamilioni ya bakteria, fangasi, wadudu na virusi

Fahamu kwamba kitanda chako kinaweza kuwa na mamilioni ya bakteria, fangasi, wadudu na virusi. Ingawa Kila mmoja wetu anadhani kitanda chake ni mahali pazuri sana pa kukaa, ndyo ni Sahihi lakini je unajua pia unaweza kupata vimelea wengi wa magonjwa kitandani?

 Kitandani kuna joto ambalo linaweza kutengeneza mazingira mazuri kwa Vimelea wa magonjwa kukua, pamejaa jasho, mate, chembechembe za ngozi zilizokufa na ndio chakula kwa ajili ya vimelea hao.

Mfano, vijidudu vidogo sana vinavyoishi kwenye vumbi. Tunamwaga seli za ngozi milioni 500 kwa siku, vijidudu hivyo hula seli hizo. Kwa bahati mbaya, vidudu hivyo na mabaki yake (kinyesi) vinaweza kusababisha mzio, pumu pamoja na tatizo la ukurutu.

Mashuka ya kitanda ni kimbilio la bakteria pia. Mwaka 2013, watafiti katika Taasisi ya Pasteur de Lille huko Ufaransa walichunguza mashuka ya kitanda cha hospitali na kugundua yamejaa bakteria wa Staphylococcus, ambao hupatikana zaidi kwenye ngozi ya binadamu.

Ingawa spishi nyingi za staphylococcus hazina madhara, lakini baadhi, kama vile S. aureus, wanaweza kusababisha maambukizi ya ngozi, chunusi na hata nimonia kwa wagonjwa walio na kinga dhaifu.

"Watu hubeba bakteria wengi katika ngozi zao," anasema Manal Mohammed, mwanabiolojia wa Chuo Kikuu cha Westminster nchini Uingereza.

"Ingawa bakteria hawa kwa kawaida hawana madhara, ila wanaweza kusababisha ugonjwa mbaya ikiwa wataingia mwilini kupitia majeraha ya wazi, ambayo ni ya kawaida hospitalini," anasema Manal.

Vitanda vya hospitali

Mwaka 2018, wanasayansi katika Chuo Kikuu cha Ibadan nchini Nigeria walipata bakteria wa E. koli katika mashuka ya kitanda cha hospitali ambayo hayajafuliwa, pamoja na bakteria wengine wa pathogenic wanaojulikana kusababisha maambukizi ya njia ya mkojo, nimonia, kuhara, homa ya uti wa mgongo na sumu katika damu.

Mwaka 2022, watafiti walikusanya sampuli kutoka kwenye vyumba vya wagonjwa waliolazwa hospitalini kwa ugonjwa wa mpox. Waligundua kuwa kitendo cha kubadilisha shuka la kitanda hutoa chembe za virusi kwenye hewa.

Mwaka 2018, mfanyakazi wa afya wa Uingereza inaaminika alipata ugonjwa huo baada ya kuambukizwa virusi wakati akibadilisha mashuka ya kitanda cha mgonjwa.

"Mashuka ya hospitalini huoshwa kwenye maji makali ya moto, ambayo huua bakteria wengi," anasema David Denning, profesa wa magonjwa ya kuambukiza katika Chuo Kikuu cha Manchester nchini Uingereza.

Isipokuwa bakteria wa C. difficile, ambaye husababisha kuhara, hasa kwa watu wazee. Kuosha kunaweza kuharibu nusu ya bakteria C. difficile, lakini seli za bakteria hao ni vigumu kufa. Hata hivyo, viwango vya maambukizi ya C. difficile vimepungua nchini Uingereza.

Bila shaka, kuna uwezekano mkubwa wa kupata bakteria wa pathogenic katika kitanda cha hospitali ambapo mgonjwa amelala kuliko katika kitanda cha mtu mwenye afya.

Vitanda vya Nyumbani

Mwaka 2013, kampuni ya vitanda ya Marekani ya Amerisleep ilichukua sampuli kutoka katika foronya ambayo haikuwa imeoshwa kwa wiki moja. IIikuwa na takribani bakteria milioni tatu kwa kila nchi ya mraba - takribani mara 17,000 zaidi ya bakteria waliopo kwenye sinki la choo.

Mwaka 2006, Denning na wenzake walikusanya mito sita kutoka kwa marafiki na familia. Mito hiyo ilikuwa ikitumika mara kwa mara na ilikuwa na umri wa kati ya miezi 18 na miaka 20. Mito yote ilikuwa na fangasi, hasa aina ya Aspergillus fumigatus - ambao hupatikana kwa wingi kwenye udongo.

"Unazungumza mabilioni au matrilioni ya chembe za fangasi kwenye kila mto," anasema Denning.

"Chanzo cha kupatikana fangasi wengi ni kwa sababu wengi wetu tunatokwa na jasho usiku. Pia sote tuna wadudu wa vumbi vitandani mwetu, na kinyesi cha wadudu hao hutoa chakula kwa fangasi. Na kisha jioni mto hupata joto kwa sababu kichwa chako hulala hapo, kwa hivyo kuna unyevu, kuna chakula, na kuna joto.”

Kwa kuwa wengi wetu huwa hatuoshi mito yetu, fangasi huishi katika hali ya utulivu na wanaweza kuishi kwa miaka. Hata kama utaosha foronya, fangasi wanaweza kuishi katika halijoto ya hadi nyuzi joto 50C (122F), na kwa vyovyote vile kuosha mito au foronya kunaweza kuifanya iwe na unyevu zaidi, na hivyo kuruhusu kukua zaidi.

0 Comment

Usipime presha baada ya kunywa vinywaji kama vile Pombe, vinywaji venye Caffeine, KahawaAfyaclass Forum •

Usifanye Mambo haya wakati wa Upimaji presha;

1. Usipime presha baada ya kunywa vinywaji kama vile Pombe, vinywaji venye Caffeine, Kahawa n.k

2. Usipime presha kama umevuta sigara dakika 30 zilizopita

3. Usipime presha kama ndyo umetoka kufanya mazoezi,kukimbia,kutembea n.k, pumzika kidogo kabla ya kuanza kupima presha

4. Wataalam wa afya hushauri hata kama ulikuwa hufanyi kazi yoyote,unashauriwa kutulia angalau kwa dakika 5-10 kabla ya kuanza kupima presha yako

5. Hakikisha unakaa vizuri kwenye kiti,huku miguu hujaikunja(maarufu kama kukunja Nne),kaa kawaida tu,huku ukinyoosha mkono wako ambao upo upande wa Moyo kwa ajili ya kuanza vipimo

8. Hakikisha miguu yako miwili imegusa chini au imekanyaga chini ya Floor wakati unapima presha

9. Usijifunge cuff ya kupimia presha juu ya shati,hakikisha mkono unakuwa wazi na kipimo kinagusa ngozi ya mwili wako

10. Pia hakikisha unafunga cuff kwenye Msuli wa mkono na sio chini ya kiwiko cha mkono au karibia na viganja vya mkono

11. Hakikisha mpira wa kipimo chako unaangalia kwa juu na sio nyuma ya mkono wako

12. Pia unashauriwa Usiongee wakati wa kupima presha yako

Usipime presha baada ya kunywa vinywaji kama vile Pombe, vinywaji venye
Caffeine, Kahawa
0 Comment

Kwa Mujibu wa Shirika la Afya Duniani(WHO); Afya yako inategemea Vitu hiviAfyaclass Forum •

 

Kwa Mujibu wa Shirika la Afya Duniani(WHO); Afya yako inategemea Vitu hivi;

–  Mazingira Mazuri ya kufanya kazi

– Kuwa Huru na Ubaguzi

– Elimu

– Mazingira Salama na yenye afya

– Kula Vizuri au kula chakula chenye afya(Healthly diet)

– Makazi mazuri au yenye Ubora

– Kupata huduma bora za Afya

– Kuwa na maji Safi na Salama ya kunywa

– Kuwa na hewa Safi n.k

WHO inasema; Afya imejumuishwa kama haki ya binadamu katika katiba za nchi 140, lakini bado mabilioni ya watu wananyimwa haki hii ya kimsingi kiutendaji. Ni wakati wa kuchukua hatua ili kuziba pengo hili.

#AfyaKwaWote #AfyaYanguHakiYangu

Credits; WHO

Photos Source: WHO

Editor,Reviewer: @afyaclass

Kwa Mujibu wa Shirika la Afya Duniani(WHO); Afya yako inategemea Vitu
hivi
0 Comment

Watu wenye ugonjwa wa moyo wanapaswa kupunguza ulaji wa sodiamuAfyaclass Forum •

Watu wenye ugonjwa wa moyo wanapaswa kupunguza ulaji wa sodiamu.

Taasisi ya Moyo ya nchini Marekani “The American Heart Association (AHA)” inapendekeza watu wazima ambao hawana au hawajulikani kuwa wako katika hatari ya kupata ugonjwa wa moyo wasitumie zaidi ya 2,300 mg ya sodiamu kwa siku. Hii ni sawa na kijiko kimoja cha chumvi.

Mtu wa kawaida aliye na ugonjwa wa moyo katika utafiti huu alizidi matumizi ya kiwango hicho kwa karibu miligramu 1,000.

Utafiti ulitumia data kutoka kwa washiriki 3,170 katika utafiti wa NHANEST  wa Kituo cha Kudhibiti Magonjwa. Sampuli hizi zilijumuisha wanaume na wanawake walio na umri wa zaidi ya miaka 20 na utambuzi wa ugonjwa wa moyo na mishipa ya damu yaani cardiovascular disease diagnosis.

Kati ya kundi hili, wengi walikuwa na umri wa miaka 65 au zaidi, walikuwa wazungu, na walikuwa na kiwango cha elimu cha chini ya wahitimu wa shule ya upili. Walikuwa Wanaume, ambao walichukua zaidi ya nusu ya masomo (56.4%), walikuwa na shida ya Uzito Mkubwa(overweight) na wastani wa ulaji wa kalori 1,862 kwa siku.

Ingawa ulaji mwingi wa sodiamu mara nyingi Watu wengi huchukulia  kama matokeo ya kutokula mlo wa kutosha au Mlo kamili swala ambalo hutokea Zaidi kwa watu wenye kipato cha Chini, utafiti huu hubadilisha nadharia hiyo,

Kundi lililokuwa na ulaji mkubwa wa sodiamu walikuwa watu wenye kipato cha Juu na wenye shahada ya chuo kikuu au zaidi.

Waandishi wa utafiti wanapendekeza kwamba watu walio na viwango vya juu vya elimu na mapato wangeweza kuwa bora katika kuripoti na kudhibiti ulaji wao wa sodiamu kila Siku kuliko wengine, ila haikuwa hivo,hii imechangia matokeo kuwa ya kushangaza Zaidi.

Nini kinatokea kwenye moyo ikiwa unatumia sodiamu nyingi?

Jina la kemikali kwenye chumvi ya mezani ni Sodium chloride(Nacl). Sodiamu ni madini ya asili, ambayo ni muhimu kwa afya ya binadamu kwa kiasi kidogo.

“Sodiamu husaidia kusawazisha maji katika mwili wako,” alielezea daktari wa magonjwa ya moyo Jayne Morgan, MD, mkurugenzi wa kimatibabu katika Shirika la Afya la Piedmont huko Atlanta, GA. “Inasaidia hata utendakazi mzuri wa misuli na mishipa.” (Dk. Morgan hakuhusika katika utafiti huo.)

“Kuna msemo Unasema, ‘Mahali sodiamu huenda, maji hufuata,'” aliiambia Medical News Today.

“Hii ndiyo sababu chumvi huongeza kiasi cha damu katika miili yenu. Madhara ya hili ni kuongezeka kwa shinikizo la damu(presha). Kuongezeka kwa shinikizo la damu basi hulazimisha moyo wako kufanya kazi kwa bidii zaidi, ambayo hatimaye inakuweka katika hatari ya kupata ugonjwa wa moyo,” Dk. Morgan alisema.

Dk. Morgan alibainisha kuwa sodiamu iliyozidi kwa muda mrefu imekuwa ikihusishwa na Tatizo la ugumu wa mishipa ya damu au kwa kitaalam atherossteosis.

SOURCES:Rejea Link;

– Taasisi ya Moyo ya nchini Marekani “The American Heart Association (AHA)”

Medical News Today Cited articles from“The American Heart Association (AHA)”

– Utafiti wa NHANEST

– Daktari wa magonjwa ya moyo Jayne Morgan, MD, mkurugenzi wa kimatibabu katika Shirika la Afya la Piedmont huko Atlanta, GA.

– Creator,Editor,Reviewer; Dr.Ombeni Mkumbwa, @afyaclass

Watu wenye ugonjwa wa moyo wanapaswa kupunguza ulaji wa sodiamu
0 Comment

Jinsi tunavyoweza kupambana na ugonjwa wa ukimwiAfyaclass Forum •

Jinsi tunavyoweza kupambana na ugonjwa wa ukimwi

Kupambana na ugonjwa wa UKIMWI ni juhudi inayohitaji ushirikiano wa jamii nzima, kutoka kwa watu binafsi hadi serikali za kitaifa na mashirika ya kimataifa.

Kujikinga na maambukizi ya UKIMWI (HIV) ni muhimu kwa afya ya mtu binafsi na jamii kwa ujumla. Hapa kuna njia za msingi za kujikinga na HIV:

1. Tumia Kondomu kwa Usahihi

Kutumia Kondomu za latex wakati wa tendo zinaweza kupunguza sana hatari ya maambukizi ya HIV na magonjwa mengine ya zinaa.

Hakikisha pia unajua Matumizi sahihi ya kondomu, hii huweza kusaidia kupunguza maambukizi ya VVU.

>>Hizi hapa ni njia Sahihi za Matumizi ya kondomu

2. Punguza Idadi ya wapenzi,kuwa na Mpenzi mmoja

Kuwa na mpenzi mmoja hupunguza hatari ya kuambukizwa HIV. Kuwa katika uhusiano wa kipekee na mtu ambaye hajaambukizwa HIV pia ni njia nzuri ya kujikinga.

3. Pima afya yako na ya mwenzako kabla ya Tendo

Kupima HIV na Mpenzi wako kabla ya kujihusisha na ngono ni hatua muhimu. Kujua hali yako na ya mwenzako kunaweza kusaidia katika kuchukua hatua za tahadhari.

4. Tumia PrEP na PEP

PrEP (Prophylaxis Kabla ya kuwa kwenye mazngira hatarishi): Ni dawa inayochukuliwa kila siku na watu ambao hawana HIV lakini wako kwenye hatari kubwa ya kuambukizwa. Inaweza kupunguza hatari ya maambukizi ya HIV kwa njia ya ngono kwa zaidi ya 90%.

PEP (Prophylaxis Baada ya Kuwa kwenye hatari): Ni dawa inayoweza kuchukuliwa ndani ya masaa 72 baada ya kuwa kwenye mazingira ya kuambukizwa virusi vya HIV kuzuia maambukizi. Ni muhimu kuanza PEP haraka iwezekanavyo baada ya kufichuliwa kuwa kwenye mazingira ya kupata HIV.

>>Soma Zaidi hapa kuhusu

5. Epuka Kushiriki au kushare vitu vya ncha kali kama Sindano na mtu mwingine

Kwa watumiaji wa dawa za kulevya na wengine pia, ushiriki wa sindano, syringes, au vifaa vingine vya ncha kali kama nyembe,pin, n.k huongeza hatari ya kupata maambukizi ya VVU kwa kiwango kikubwa.

6. Matibabu kwa Wajawazito

Wanawake wajawazito wenye HIV wanaweza kupunguza hatari ya kuambukiza virusi kwa watoto wao kwa kuchukua na kutumia dawa za antiretroviral (ARVs) wakati wa ujauzito kwa Usahihi.

7. Jitunze Afya Yako kwa Ujumla

Kuwa na magonjwa mengine ya zinaa kunaweza kuongeza hatari ya kupata HIV. Kupata matibabu kwa magonjwa yoyote ya zinaa na kujitunza afya yako ya kinga ni muhimu.

8. Fahamu Vizuri Dalili za Ukimwi kwa Mtu

>>Soma hapa kwa kina Dalili za Ukimwi kwa Ujumla

>> Fahamu hapa dalili za Ukimwi kwa ngozi

Kwa kuchukua tahadhari hizi, mtu anaweza kupunguza sana hatari ya kuambukizwa HIV. Ni muhimu kukumbuka kwamba kujilinda na kulinda wengine ni jukumu la kila mtu katika jamii.

Hapa kuna njia kadhaa za msingi za kupambana na ugonjwa huu:

1. Elimu na Uelewa

Kutoa elimu sahihi na kamili kuhusu jinsi UKIMWI unavyoenea na jinsi ya kujikinga.

Kubomoa imani potofu na stigmatization inayohusiana na HIV/AIDS. Hivi vinaweza kusaidia kupunguza maambukizi.

2. Kupunguza Maambukizi

Kutumia kondomu kila wakati na kwa usahihi wakati wa kujihusisha na ngono ili kupunguza maambukizi ya HIV.

Kuhimiza uaminifu na kupunguza idadi ya washirika wa kimapenzi.

Kuhimiza na kurahisisha upimaji wa HIV na kushiriki hali ya HIV kwa uwazi na washirika wa kimapenzi. Hivi pia husaidia kupunguza maambukizi na kuongeza watu kuchukua tahadhari Zaidi.

3. Matibabu

Kutoa dawa za kurefusha maisha (ARVs) kwa watu wanaoishi na HIV/AIDS.

Kutumia dawa za kuzuia maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto (PMTCT) wakati wa ujauzito na kujifungua. n.k

4. Utafiti na Ubunifu

Kuendelea kufanya utafiti wa chanjo za HIV na tiba mpya.

Kukuza njia mpya za kuzuia maambukizi, kama vile dawa za kuzuia kabla ya kufichua (PrEP) na baada ya kufichua (PEP).

5. Sera na Ufadhili

Kuunda sera zinazounga mkono upatikanaji wa huduma za afya na matibabu kwa wote, bila ubaguzi.

Kuongeza ufadhili wa kitaifa na kimataifa kwa programu za kuzuia, matibabu, na utafiti wa HIV/AIDS.

6. Kujenga Jamii bora

Kusaidia na kuimarisha jamii za watu wanaoishi na HIV/AIDS.

Kuhimiza ushiriki wa jamii katika kupanga na kutekeleza mikakati ya kuzuia na matibabu ya HIV.

Kwa kuchukua hatua hizi, tunaweza kupunguza maambukizi mapya ya HIV, kutoa msaada kwa wale walioathirika, na hatimaye kumaliza janga la UKIMWI.

Jinsi tunavyoweza kupambana na ugonjwa wa ukimwi
0 Comment

Fahamu hatari ya kutumia mafuta yaliyotumikaAfyaclass Forum •

Fahamu hatari ya kutumia mafuta yaliyotumika

Wataalamu wa afya wameonya kuwa kutumia mafuta zaidi ya mara moja kukaangia chipsi, samaki, maandazi, kuku na vyakula vingine kumetajwa kuwa chanzo cha magonjwa yasiyoambukiza na saratani.

Ununuaji wa vyakula, hasa vilivyokaangwa tayari imeelezwa kuwa hatari zaidi ikiwa hufahamu mafuta yaliyotumika.

Kwa mujibu wa wataalamu wa afya, mafuta yakichemka yanafika nyuzi joto ya juu, yanaungua na kupoteza ufanisi kazi wake na hivyo hutengeneza sumu, inayozalisha kemikali inayoenda kukaa katika leya ya ndani ya utumbo ambayo matokeo yake hutengeneza uvimbe unaogeuka kuwa saratani.

Ofisa muuguzi muelimishaji, Elizabeth Likoko anasema mafuta yanapochemshwa kwa muda mrefu yanatengeneza sumu ambayo inaingia kwenye chakula kinachopikwa wakati huo na mtu akila zile kemikali zinaingia kwenye leya ya utumbo kila siku, zikizidi zinatengeneza uvimbe unaogeuka kuwa saratani.

Anataja ulaji wa mafuta mengi kuwa na athari kubwa. “Kwenye familia ya watu wanne ile chupa ndogo ya mafuta ya kula ya mililis 500 tuitumie kwa mwezi mmoja na katika kukaanga kwa mfano unakaanga kuku au samaki inatakiwa ukadirie kwa kadiri samaki unaokaanga, usiweke mengi ili yale mafuta baada tu ya kukaanga uyamwage. Hayafai kutumika tena.”

Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kutoka Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Tatizo Waane anasema mafuta yanapotumika zaidi ya mara moja husababisha kuzalishwa kwa kemikali hatari mwilini ambazo ni chanzo cha magonjwa mengine yasiyoambukiza, ikiwemo saratani ya utumbo mpana.

Sayansi ya mapishi

Kutokana na ulaji usiofaa wa vyakula vyenye mafuta mengi, wengi wamejikuta wakiwa na vitambi na uzito usiokuwa sawia na urefu wao ‘BMI’ na hivyo kujiweka hatarini kupata maradhi hayo yanayokua kwa kasi nchini.

Daktari kutoka Taasisi inayoshughulika na masuala ya chakula na lishe ya Nsambo Healthcare Polyclinic, Boaz Nkumbo anasema katika sayansi ya mapishi zipo familia zinazozalisha vyakula vinavyokwenda kuwa janga kwa walaji.

Dk Nkumbo anataja makosa madogo madogo ambayo hufanywa na mpishi wakati wa kuandaa chakula jikoni, yanayoleta matokeo hasi katika afya ya binadamu.

“Ninaiona jamii ina uwezo wa kupika chakula kizuri chenye madoido mengi, kitamu, pilau likipikwa pale na samaki nazi huyo ndiyo unamla vizuri. Lakini huyu samaki akiwa amekaangwa pale na mafuta ya mbegu yaliyokaangiwa maandazi jana, wali umepikiwa mafuta ya mbegu yaliyokaangiwa samaki jana,” anasema.

Dk Nkumbo anasema wengi wamekuwa wakikosa kuwa na ufahamu wa sayansi ya mapishi, hivyo kujikuta wakipika vyakula vyao kimakosa.

Anasema ni makosa makubwa kupikia mafuta ambayo tayari yalishapikiwa chakula kingine, kwani huwa yamechemka kufikia kiwango cha juu cha joto na hayatakiwi kupikiwa kwa mara nyingine, kwani yana athari.

“Mkeo anaweza akawa anajua kupika, lakini hajui sayansi ya kile anachokipika, anaweza kuwa anakupikia chakula kitamu lakini chakula kile kinakuletea kisukari, kinakunenepesha, kinakutolea nguvu za kiume, chakula hicho kinakuletea saratani na magonjwa mengine,” anasisitiza.

Dk Nkumbo anasema kuna umuhimu mkubwa wa kujua kile kinachoendelea kwenye mwili wako na msukumo wa kujitathmini na kuona nini unapaswa kufanya ili kuboresha afya yako.

“Kitambi kinatokana na wewe kukosa elimu jinsi ya kuishi na fedha ulizo nazo, chakula ulichonacho, kukosa elimu ya jinsi ya kujaza chakula chako kwenye sahani yako, unapokosa elimu ya hayo mambo ndipo unapopata uzito mkubwa na kitambi,” anasema.

Changamoto hiyo imekuwa ikitiliwa mkazo zaidi na maofisa lishe mbalimbali nchini, ambao wamekuwa wakitoa elimu ya namna ya kukiandaa na kuchanganya chakula ili kupata matokeo bora.

Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Afya, Dk Grace Magembe anasema sayansi ya kupika ni jinsi unavyokiandaa chakula chako, kwani kuna baadhi ya vyakula ambavyo virutubisho vyake vinapotea haraka sana kwenye joto kubwa.

Anataja mboga za majani kwamba wengine huziunga na nazi, mchicha kupikwa kwa saa zima kuna virutubisho hupotea, huku akisema vipo vyakula vinavyoshauriwa kupikwa kwa muda mrefu ili vilainike, yakiwemo makande.

“Unapika chakula unajaza mafuta mengi sana au chumvi nyingi kinakuwa si chakula na badala yake kinaleta madhara, lakini wakati mwingine unatengeneza chakula hukipiki kikaiva vizuri kinabaki na wadudu, minyoo, kwa hiyo anavyokula anapata minyoo, wakati mwingine nyama zinapikwa haziivi vizuri, kunakuwa na wadudu kama minyoo, baadaye wanahamia kwenye mwili wa binadamu,” anasema.

Anasema wakati mwingine chakula kinapikwa cha aina moja, huku akielezea umuhimu wa kuchanganya na kitu kingine. “Kande watoto wanakula siku nzima na ni mahindi ya kuchemsha pekee, weka maharage mule ndani, njugu mawe, unaweza ukaweka njegere, carrot, hoho, kitunguu, wengine wanaweka mpaka nyama kwenye makande, hayo yanakuwa mlo kamili, mtoto akila anapata afya njema.”

Dk Magembe anasema wengine wanawapikia watoto uji wa dona peke yake bila kuchanganya na vitu vingine kama soya, karanga na kwa wafugaji hawaongezi maziwa au mayai ili watoto wapate afya.

Anasema changamoto kubwa nchini watu wanaweza kuwa na chakula lakini namna ya kukichanganya ili kiweze kutoa virutubisho vyote vinavyohitajika ikawa ni changamoto, lakini elimu inaendelea kutolewa.

“Tumewaagiza maofisa lishe waweze kutoa elimu. Wakati mwingine ni ukosefu wa chakula, wakati mwingine tuna chakula hatujui namna ya kukipika, namna ya kukichanganya. Chakula bora ni kilekile kilichopo kwenye mazingira yako, ni vizuri tu ukivichanganya, kwa mfano Wahaya wanapika ndizi wanaweka na kitunguu, hoho, nyanya chungu, maharage, mchicha kinakuwa chakula bora,” anasema Dk Magembe.

Athari za mafuta mwilini

Miongoni mwa athari ni pamoja na kuongeza uzito wa mwili, kuziba mishipa ya damu na baadaye mtu kupata presha na huchangia unene kupita kiasi.

Dk Waane anasema mtu mmoja anatakiwa kutumia mafuta ujazo wa nusu dolegumba kwa siku na asizidishe zaidi ya hapo, hivyo mtu anapokula mafuta mengi, uwezekano wa kupata shinikizo la damu ni mkubwa.

“Ni muhimu katika chakula, usile chukuchuku, umuhimu wa mafuta mwilini upo na yaliwe kiasi kwa kuwa vitamin aina nne A, B, C na E zinaingia mwilini iwapo chakula kina mafuta lakini yasiwe mengi,” anasema.

Mkurugenzi wa Kinga kutoka Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI) Dk Crispin Kahesa, anasema ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi ni chanzo cha magonjwa ya saratani.

“Mafuta na sukari vyote kwa ujumla wake vinachangia kwa kiasi kikubwa kusababisha unene kupita kiasi na hivyo ndivyo visababishi vya saratani zilizo nyingi,” anasema Dk Kahesa.

Mwenyekiti wa chama cha wagonjwa wa kisukari nchini, Profesa Andrew Swai anasema ni mafuta kiasi kidogo yanayohitajika mwilini, kwani yakivunjwavunjwa kilocarolies zinazohitajika ni kiasi kidogo kutoka kwenye hicho kiini lishe, kwani mwili unahitaji kilocaloris 9 ambazo ni nyingi na unapozidisha unaupa mwili calori nyingi na masalia mengi yanabaki mwilini.

Licha ya mafuta yaliyorudiwa, virutubisho vya mafuta ‘transfat’ ambavyo mara nyingi hupatikana katika vyakula vya vitafunio, bidhaa zilizookwa na baadhi ya mafuta ya kupikia, navyo vimethibitishwa kuwa huziba mishipa ya damu, kusababisha mshtuko wa moyo na kifo.

Daktari bingwa wa magonjwa ya fiziolojia ya homoni na mazoezi na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Muhas, Dk Fredrick Mashili ambaye amefanya tafiti kadhaa katika eneo hilo, anasema takwimu zinaonyesha kila mwaka, wastani wa watu 10,000 barani Afrika hufa mapema kutokana na ugonjwa wa moyo unaosababishwa na matumizi ya virutubisho vya mafuta.

Kwa mujibu wa Dk Mashili, katika uchunguzi walioufanya walipima kiwango cha mafuta kwenye vyakula vilivyokaangwa sana kwa kuchemshwa kwa nyuzi joto kubwa, hali ambayo husababisha asidi hiyo kujizalisha na kugundua baadhi ya mafuta yana viwango vikubwa vinavyozidi asilimia 2.

“Tulibaini baadhi ya vyakula vina mpaka viwango vya asilimia 8 vya asidi hiyo ambayo inaleta athari kubwa kwa kusababisha magonjwa ya moyo na mishipa ya damu kuziba,” anasema.

Anasema walibaini kiwango kikubwa cha asidi hiyo kwenye mafuta yaliyochakatwa kiwandani katika aina 10 maarufu ya mimea kwa matumizi Dar na Zanzibar baada ya kuyachunguza.

Chanzo: mwanachidigital

Fahamu hatari ya kutumia mafuta yaliyotumika
0 Comment

Njia bora za Kupiga Mswaki na kulinda meno yako na kinywaAfyaclass Forum •

Njia bora za Kupiga Mswaki na kulinda meno yako na kinywa

Wengi wetu hatutumii njia bora zaidi za kupiga mswaki, licha ya hatari za kiafya za kushindwa kufanya hivyo.

Kusafisha meno yako kwa ufanisi hupunguza uwezekano wa kupata magonjwa mengi sugu, pamoja na kuweka meno na fizi zako kwenye afya nzuri. Lakini wengi wetu tunafanya vibaya. Hapa kuna njia za jinsi ya kupiga mswaki meno yako vizuri, kulingana na wataalam.

Kwa kawaida wengi wetu tumekuwa tukipiga mswaki kwa mazoea tu pasipo kujua zipi ni njia sahihi za kupiga mswaki,

Nchini Sweden, utafiti mmoja uligundua kuwa Mtu mmoja kati ya 10 ndye anayetumia mbinu bora zaidi ya kupiga mswaki. Bima ya afya ya Uingereza, Bupa iligundua kuwa takriban nusu ya watu waliojibu hawakujua jinsi ya kupiga mswaki ipasavyo katika uchunguzi wa watu 2,000 nchini Uingereza.

“Kuna uwezekano mkubwa kwamba mtu yeyote ambaye hajapata maelekezo rasmi kutoka kwa daktari wake wa meno au mtaalamu wa usafi anapiga mswaki kimakosa,” anasema Josefine Hirschfeld, profesa mshiriki na mtaalamu wa urejeshaji wa meno katika Chuo Kikuu cha Birmingham nchini Uingereza. “Kutokana na uzoefu wangu, hii itakuwa idadi kubwa ya watu katika nchi yoyote ile.”

Labda hiyo haishangazi, kwa kuzingatia aina mbalimbali za maudhui zinazopatikana kuhusu jinsi unapaswa kupiga mswaki. Utafiti mmoja ulipata angalau ushauri 66 tofauti, wakati mwingine unaokinzana.

“Nadhani inachanganya sana kwa watumiaji,” anasema Nigel Carter, mtendaji mkuu wa Wakfu wa Afya ya Kinywa nchini Uingereza. Mkanganyiko huu huimarishwa na safu ya bidhaa za meno zinazopatikana kununua, ili mtu atumie kwa ajili ya meno yake.

Ni ipi njia bora ya kupiga mswaki meno yako?

“Wagonjwa wengi wanaelewa kuwa wanachohitaji kufanya ni kuondoa mabaki ya chakula,”. “Hiyo ni kweli kwa kiasi. Ni muhimu zaidi kuondoa bakteria kwenye meno.”

Bakteria hawa na vijidudu vingine hukua ndani ya kinywa cha kila mtu, na kuunda Utando usio na kifani unaojulikana kama “Teeth plaque”.

Inajumuisha takriban spishi 700 tofauti za bakteria, anuwai ya pili kwa ukubwa katika mwili wa binadamu baada ya utumbo, pamoja na kundi la fangasi na virusi. ” Bacteria hawa Wanaishi kwenye utando wa kunata uliokwama kwenye meno na pia kwenye tishu laini,”. “Utando huu wa kunata hauwezi kuoshwa kwa urahisi – inahitaji kusafishwa kwa mikono.”

Sehemu muhimu zaidi ya kuiondoa au kudeal nayo sio kwa kweli meno tu, lakini inaitwa gumline. Hapa ndipo vijidudu vinaweza kupenya vyema kwenye tishu za ufizi na kusababisha uvimbe, na hatimaye hali kama vile periodontitis.

GUMLINE; ni nini?

” Gumline ni ile ncha ya fizi ambapo hukutana na meno “the edge of the gums, where they meet the teeth”. ANGALIA HAPA KWENYE PICHA

Kwa kweli, “kupiga mswaki” ni jambo linalohitaji ujue nini unafanya na sio mazoea tu. “Fikiria kusugua zaidi gumline yako, badala ya meno yenyewe tu, ” Na Meno yatapigika mswaki yenyewe.”

Mbinu za Kupiga Mswaki Vizuri

Hizi hapa ni baadhi ya mbinu za kutumia ili upige mswaki vizuri na kusafisha meno na kinywa kama inavyotakiwa;

1. Bass technique

Mbinu hii inahusisha kuweka brashi ya Mswaki kwa pembe ya digrii 45 kwenye uso wa jino (lililoinamishwa chini kwenye taya ya chini na ya juu, kana kwamba unajaribu kukaribia ukingo chini ya ufizi).

Kisha unafanya harakati ndogo, za mtetemo na kurudi kwenye gumline.

2. Stillman technique

Mbinu hii hufanya kazi nzuri ya kuondoa biofilm. Hapa unakuwa kama unafagia mara kwa mara meno kutoka kwenye gumline, wakati ambapo unaendelea kuangalia maeneo yenye Utando Zaidi uliobaki.

Nguvu,mgandamizo au Shinikizo linalotumika linapaswa kutokuwa zaidi ya 150-400g, Kupiga mswaki kwa nguvu sana, hasa kwa kutumia brashi yenye bristled, kunaweza kusababisha majeraha kwenye ufizi.

Majeraha madogo kwenye tishu laini yanayosababishwa na upigaji mswaki kwa nguvu ni fursa kwa bakteria kuingia kwenye damu.

3. Fones technique

Mbinu hii ni nzuri zaidi kwa watoto na watu wanaoanza kujifunza kupiga mswaki,

Mbinu ya Fones inahusisha kushikilia brashi ya mswaki kwa digrii 90 na kufanya usogezaji wa mviringo juu ya meno, kuruka gumline.

Je,Unatakiwa kusafisha Meno kwa Muda gani?

Kupiga mswaki inatakiwa iwe si chini ya dakika mbili kwa wakati mmoja, mara mbili kwa siku ni pendekezo kutoka Shirika la Madaktari wa Meno la Marekani, NHS, Shirika la Madaktari wa Kihindi, Shirika la Madaktari wa Meno la Australia na mashirika mengine mengi ya kitaifa ya afya.

Shida ni kwamba, wengi wetu ni hawapo vizuri katika kukadiria muda wa dakika mbili kweli. Wastani wa muda ambao tunapiga mswaki hutofautiana kwa kiasi kikubwa, kutoka sekunde 33, sekunde 45 sekunde 46 hadi sekunde 97  kulingana na tafiti mbalimbali.

Takriban 25% tu ya watu hupiga mswaki kwa muda wa kutosha, kwa shinikizo na mwendo sahihi, kulingana na utafiti mmoja ulioongozwa na Carolina Ganss, profesa katika idara ya meno ya kihafidhina na ya kuzuia katika Chuo Kikuu cha Justus-Liebig Giessen nchini Ujerumani.

Njia bora za Kupiga Mswaki na kulinda meno yako na kinywa
0 Comment

Kwa nini chakula cha makopo ni hatari kwa afya yako?Afyaclass Forum •

Kwa nini chakula cha makopo ni hatari kwa afya yako?

Chakula cha makopo kimehusishwa na zaidi ya matatizo 30 ya moyo, saratani na kukosa usingizi.

Vyakula hivi vinachangia zaidi ya asilimia 50 ya matumizi ya wastani nchini Marekani na Uingereza na vinapata umaarufu katika sehemu nyingine za dunia.

Chakula cha makopo ni nini?

Hakuna njia moja ya kuelezea vyakula vya makopo lakini vina viungo ambavyo havitumiwi nyumbani.

Vingi vyao ni kemikali na vitu vinavyobadilisha rangi ya chakula na ladha ya chakula ambayo hutumiwa kuongeza ubora na ladha ya chakula.

Mifano ni malimau ya makopo na pipi na kuku wa kukaanga. Hata hivyo, vinaweza kuhusisha vyakula kama mkate, maziwa na vyakula vinavyochanganywa na nafaka.

Chakula cha makopo kinatofautiana na chakula kilichosindikwa

Ili kuwasaidia watu kutambua aina tofauti za chakula, mfumo wa ngazi nne hutumiwa mara nyingi.

Ni vyakula vibichi na vilivyochakatwa pamoja na vyakula vya makopo na vilivyotiwa rangi.

Vyakula vinavyobadilisha rangi au ladha ni mchanganyiko wa vyakula kama vile matunda na mboga mboga, karanga, mayai na vionjo vilivyochakatwa.

Kwa mfano, mkate uliotengenezwa kwa ngano, maji, chumvi na kiungo kinachofanya chakula kiinuke, yaani ‘chachu’, ni chakula kilichosindikwa.

Hata hivyo, ikiwa utabadilishwa rangi au vihifadhi hutumiwa, mkate utakuwa umesindikwa.

Unawezaje kutambua vyakula vilivyosindikwa?

Vyakula ambavyo vina zaidi ya viungo vitano vinaweza kuwa vimesindikwa, kwa mujibu wa mtaalam wa afya ya umma, Profesa Maira Bes-Rastrollo wa Chuo Kikuu cha Navarra nchini Uhispania.

Mara nyingi vyakula vya kusindika huwa na chumvi nyingi, sukari na mafuta. Nchini Uingereza na nchi nyingine, hii imeandikwa kwenye kopo.

Huenda kikawa chakula kibichi ambacho hakijaharibika, lakini kinaweza kuchukua muda kabla ya kuharibika kwa sababu ya ufungaji utakaokizuia kuharibika. Angalia mwili wa kopo kwa kemikali kama vile sodium benzoate, nitrate, sulphite, BHA na BHT.

Chakula cha makopo kimeeneaje duniani?

Watu nchini Uingereza na Marekani hula chakula kilichosindikwa zaidi.

Kufikia 2023, chakula hiki kinachukua asilimia 58 ya wastani wa watu wazima nchini Marekani ambao hutumia viungo vya kuongeza nishati na asilimia 66 ya watoto.

Idadi ya watu ni chini ya asilimia moja ya watu wazima na watoto wa Uingereza.

Katika nchi za Asia kama vile Korea Kusini na Japan na nchi za Amerika Kusini kama vile Brazil na Chile, chakula cha makopo kinachukua asilimia 20 hadi 30 ya ulaji wa nishati ya watu. Nchini Afrika Kusini, idadi hiyo ni asilimia 39.

Je, kuna athari yoyote inayotokana na ulaji chakula cha makopo?

Hakuna ushahidi wa kuaminika kuhusu madhara ya kiafya ya kula chakula cha makopo.

Lakini utafiti wa hivi majuzi uliochapishwa katika Jarida la Matibabu la Uingereza – kuhusu data kutoka kwa watu milioni 9.9 kote ulimwenguni – umehusishwa na:

Hatari ya kifo kutokana na magonjwa ya moyo na mishipa kama vile mshtuko wa moyo na kiharusi

Aina ya 2 ya kisukari

Matatizo ya usingizi

Wasiwasi

Hata hivyo, haiwezekani kuamua ikiwa ni chakula cha kusindika kilichosababisha ugonjwa huo au kwamba vingi vyao vina mafuta mengi, sukari na chumvi.

Hivi ndivyo vyanzo vya unene, aina ya 2 ya kisukari, magonjwa ya moyo na aina fulani za saratani.

Unene uliokithiri

Kuongezeka uzito ni athari ya kwanza inayoonekana ya kula chakula cha makopo, “anasema Chris van Tulleken, mtaalamu wa kinga katika Chuo Kikuu cha London, ambaye pia ameandika juu ya lishe.

“Vyakula hivi vina mafuta mengi, chumvi na sukari nyingi. Lakini pia vimeundwa – kwa rangi na ladha yao – kuliwa kupita kiasi.”

Utafiti kutoka Chuo cha Imperial unaonyesha kuwa zaidi ya watu bilioni moja duniani – mmoja kati ya watu wanane – wanaishi na unene uliokithiri.

Na utafiti wa hivi karibuni wa Shirika la Afya Duniani, WHO na Global Health Observatory kutoka 2016, ulisema kuwa zaidi ya asilimia 28 ya watu wazima nchini Marekani wanakabiliwa na unene uliokithiri wakati kuna asilimia 26 Ulaya, asilimia 19 katika Mashariki ya Mediterania na asilimia 9 barani Afrika.

WHO inasema watu bilioni 2.8 hufa kila mwaka kutokana na unene uliokithiri.

Ugonjwa wa kisukari

Watu zaidi ulimwenguni sasa wana kisukari cha aina ya 2, kulingana na Chama cha Kisukari.

“Chumvi, sukari na mafuta katika vyakula vya makopo vyote vina hatari ya kusababisha kisukari cha aina ya 2 – pamoja na vyakula vyenye kalori nyingi na virutubishi vidogo,” alisema Jaakko Toumilehto, profesa wa afya katika jumuiya ya Al’ katika Chuo Kikuu cha Helsinki.

Ukanda wa Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini umekumbwa na ongezeko la watu wenye kisukari cha aina ya 2.

“Nchi nyingi kati ya hizi hazizalishi chakula chao,” alisema Profesa Toumilenhto. “Chakula cha makopo ni rahisi kuhifadhi na kusafirisha. Ni kile ambacho makampuni ya usindikaji wa chakula husafirisha zaidi.”

Utapiamlo

Chakula cha makopo kinasababisha utapiamlo katika nchi nyingi za Kusini mwa Jangwa la Sahara, alisema Dk Johnson.

Alisema “Wanakosa virutubishi vinavyopatikana kwenye vyakula vya asili kama vile madini ya chuma, madini na vitamini,”.

Lakini wanasayansi katika Chuo Kikuu cha Purdue nchini Marekani wanasema kwamba chakula cha makopo kinaweza kuwa na manufaa, kama vile:

• Kutoa virutubisho kama vile vitamini E na kalsiamu

• Kutoa chaguzi za bei nafuu zaidi kwa chakula kisicho na ladha kwa watu ambao hawawezi kumudu

• Kupunguza upotevu wa chakula na uwezekano wa kula chakula kilichochafuliwa

Wakfu wa Lishe wa Uingereza, ambao unafanya kazi kwa ufadhili kutoka kwa makampuni ya chakula, unaeleza kuwa si vyakula vyote vya makopo vinavyofanana.

“Aina za vyakula vinavyoingia kwenye kundi la chakula cha makopo, kama vile vyakula vinavyotengenezwa na nafaka, mkate, chumvi na sukari.” Alisema Sara Stanner, mkurugenzi wa sayansi wa msingi huo.

“Vyote hivi ni vyanzo muhimu vya virutubisho.”

Ni hatua gani zimechukuliwa dhidi ya chakula cha makopo?

Serikali ya Uingereza ilitoza ushuru kwa ndimu za chupa mnamo 2018 na kampuni nyingi zimepunguza kiwango cha sukari katika kujibu.

Mnamo 2023, Colombia ilitoza ushuru wa asilimia 10 – ambayo itaongezeka katika siku zijazo – kwa ndimu za chupa na vyakula vya makopo.

Mnamo mwaka wa 2016, Chile – ambayo ina watoto wanene zaidi duniani – inachapisha onyo juu ya vyakula vilivyo na sukari nyingi, mafuta na nyongeza.

Pia ilidhibiti matangazo ya vyakula vyenye sukari nyingi na chumvi na viambato vya kuongeza nguvu kwa watoto.

Lakini katika miaka minne baada ya hatua hizo kuanzishwa, kulikuwa na ongezeko la kuendelea kwa watoto wenye uzito mkubwa.

Via:Bbc

Kwa nini chakula cha makopo ni hatari kwa afya yako?
0 Comment

Kila siku, zaidi ya watoto 1000 chini ya miaka 5 hufa kutokana na magonjwa yanayohusishwa na maji yasiyo salamaAfyaclass Forum •

Kila siku, zaidi ya watoto 1000 chini ya miaka 5 hufa kutokana na magonjwa yanayohusishwa na maji yasiyo salama-UNICEF

Mambo 10 kuhusu maji,Jinsi maji yasiyo salama yanavyoweka watoto katika hatari.

Watu wengi wanajua kuwa huwezi kuishi bila maji. Lakini ukweli,Unahitaji zaidi ya maji tu – unahitaji maji SALAMA

Pia unahitaji vyoo salama ili kuweka mazingira safi, na pia sabuni na maji ili kuzuia kuenea kwa magonjwa.

Kwa mujibu wa UNICEF;

Jua zaidi kuhusu kwa nini maji salama, usafi wa mazingira na usafi binafsi ni muhimu sana:

1. Kuna shida ya maji na inatokea sasa.

Watu bilioni 2.2 bado hawana maji ya kunywa yaliyosimamiwa kwa usalama.

2. Maji yanahitaji kuwa zaidi ya safi, lazima “yadhibitiwe kwa usalama”.

Maji yanayosimamiwa kwa usalama inamaanisha kuwa na maji nyumbani (kwenye majengo), wakati wowote inapohitajika, na bila uchafuzi.

3. Bila usafi wa mazingira unaosimamiwa kwa usalama, magonjwa yanaenea kwa kasi.

Watu bilioni 3.6 – karibu nusu ya dunia – hawana huduma ya vyoo iliyosimamiwa kwa usalama, kumaanisha choo kinachotenganisha kinyesi cha binadamu na mguso, na mfumo wa kuhakikisha kuwa uchafu huo unatupwa kwa usalama.

4. Kujisaidia wazi ni mojawapo ya dalili za wazi za kutofautiana.

Watu milioni 494 wanajisaidia haja kubwa wazi, ikimaanisha wanajisaidia kando ya barabara, mashambani au vichakani.

5. Watoto wako hatarini zaidi.

Kila siku, zaidi ya watoto 1000 chini ya miaka 5 hufa kutokana na magonjwa yanayohusishwa na maji yasiyo salama, usafi wa mazingira na usafi, ambayo pia huua watu milioni 1.4 kila mwaka.

6. Watoto wanazaliwa katika mazingira machafu.

Katika nchi zenye maendeleo duni zaidi, wanawake milioni 16.6 hujifungua katika vituo vya afya visivyo na maji ya kutosha, vyoo na usafi wa mazingira – na kuwaweka katika hatari ya kuambukizwa, magonjwa na kifo.

7. Kuzuia magonjwa si rahisi kama inavyopaswa kuwa.

Kunawa mikono kwa sabuni na maji ni mojawapo ya njia rahisi na nzuri za kuzuia kuenea kwa magonjwa,

Lakini watu bilioni 2.3 bado hawana vifaa vya msingi vya kunawa mikono na sabuni na maji nyumbani. Hiyo ni karibu theluthi moja ya idadi ya watu duniani.

8. Mabadiliko ya hali ya hewa yanaifanya Hali hii kuwa mbaya zaidi.

Mabadiliko ya hali ya hewa yanaharibu, kukauka na kuchafua vyanzo vya maji,

Mnamo 2022, watoto milioni 436 walikuwa wakiishi katika maeneo yenye hatari kubwa ya maji au ya juu sana, ambayo inachangiwa na mabadiliko ya hali ya hewa.

9. Watu wa vijijini ndio wenye hali duni zaidi.

Watu 8 kati ya 10 ambao wanakosa hata maji ya kimsingi ya kunywa wanaishi vijijini. Theluthi mbili ya watu ambao hawana hata vyoo vya msingi wanaishi vijijini. Watu 9 kati ya 10 wanaojisaidia haja kubwa wanaishi vijijini.

10. Lazima tufanye zaidi.

Ulimwengu upo kwenye hatari kubwa,upatikanaji wa maji salama, usafi wa mazingira na usafi kwa wote bado ni changamoto.

Afyaclass inatoa wito wa kupewa kipaumbele zaidi kisiasa na kuongeza ufadhili ili kuboresha upatikanaji wa maji, usafi wa mazingira na usafi wa kaya, ikilenga jamii zilizo hatarini zaidi.

Kila siku, zaidi ya watoto 1000 chini ya miaka 5 hufa kutokana na
magonjwa yanayohusishwa na maji yasiyo salama
0 Comment

Insha kuhusu ugonjwa wa kipindupinduAfyaclass Forum •

Insha kuhusu ugonjwa wa kipindupindu

Kama unahitaji kuandika Insha kuhusu Ugonjwa wa Kipindupindu,Makala hii itakusaidia vitu vya muhimu kuzingatia;

Ugonjwa wa kipindupindu, au kwa jina la kitaalamu hujulikana kama cholera, ni ugonjwa wa kuambukiza unaosababishwa na bakteria aina ya Vibrio cholerae. Ugonjwa huu husambazwa hasa kupitia maji na chakula kilichochafuliwa na bakteria hao.

Insha kuhusu ugonjwa wa kipindupindu inaweza kuandikwa kwa kuzingatia mambo kadhaa yanayohusiana na ugonjwa huu, ikiwa ni pamoja na:

1. Historia na Asili:

Insha inaweza kuanza kwa kuelezea historia ya ugonjwa wa kipindupindu, pamoja na jinsi ulivyogunduliwa na kusambaa katika maeneo mbalimbali duniani. Pia, inaweza kuzungumzia asili ya bakteria ya Vibrio cholerae na jinsi inavyoathiri binadamu.

2. Dalili na Matokeo:

Insha inaweza kuelezea dalili za ugonjwa wa kipindupindu, kama vile kuharisha sana pamoja na kutapika, na jinsi dalili hizi zinavyoweza kusababisha upungufu mkubwa wa maji mwilini (dehydration) na hata kifo ikiwa haishughulikiwi haraka.

3. Mbinu za Kuzuia:

Insha inaweza kuzungumzia mbinu mbalimbali za kuzuia maambukizi ya ugonjwa wa kipindupindu, kama vile kusafisha maji kabla ya kunywa, kuhakikisha usafi wa chakula, na kufuata mbinu bora za usafi wa mazingira.

4. Matibabu na Madhara:

Insha inaweza kuelezea mbinu za matibabu ya ugonjwa wa kipindupindu, kama vile kutoa matibabu ya rehydration therapy kwa wagonjwa ili kurejesha maji mwilini. Pia, inaweza kuzungumzia madhara ya muda mrefu ya ugonjwa huu kwa jamii na uchumi.

5. Muktadha wa Ugonjwa kwa Sasa:

Insha inaweza kuzungumzia hali ya sasa ya ugonjwa wa kipindupindu katika dunia ya leo, ikiwa ni pamoja na mikakati ya kimataifa ya kudhibiti na kuzuia maambukizi, na jinsi teknolojia mpya inavyoweza kusaidia katika kukabiliana na ugonjwa huu.

Kila sehemu ya insha inaweza kusaidia kuelimisha wasomaji kuhusu ugonjwa wa kipindupindu, umuhimu wa kuzuia maambukizi, na njia za kutibu na kudhibiti ugonjwa huu.

>> Soma Zaidi hapa kuhusu Ugonjwa wa kipindupindu na chanzo chake

Insha kuhusu ugonjwa wa kipindupindu
0 Comment

Jinsi ambavyo IBADA husaidia kuboresha afya ya AkiliAfyaclass Forum •

Jinsi ambavyo IBADA husaidia kuboresha afya ya Akili

Kwa mujibu wa Tafiti nyingi,inaonyesha kwamba Ibada ina Sehemu kubwa sana kwenye kuboresha afya ya akili,

Dawa nyingi za Kimagharibi hazijajishughulisha sana na ustawi wa kiroho. Lakini hiyo inaweza kubadilika kwa hivi sasa, kwani ushahidi unaoongezeka unaonyesha mazoezi ya kiroho na ya kidini yanaweza kuwa na matokeo chanya kiafya, haswa kuhusiana na afya ya akili.

Ubongo wako na Swala la Kiroho na KiDini(IBADA):

Viwango vya juu vya hali ya kiroho na kidini kwa Mtu vinahusishwa na kupunguza kwa kiwango kikubwa matatizo kama vile Msongo wa mawazo, kujiua, na matumizi mabaya ya dawa katika idadi yoyote ya Tafiti zilizofanyika.

Mazoezi endelevu ya kiroho (kwenda kanisani, kusali, kutafakari, kusaidia wengine) yanaweza pia kusaidia Mtu kujilinda dhidi ya ugonjwa wa mfadhaiko na hali ya Msongo wa mawazo inayotokana na kuumizwa“posttraumatic stress” na kuongeza ukuaji wa kisaikolojia baada ya hali ya kufadhaisha, utafiti unaonyesha.

Mazoea haya yanaweza kukusaidia kuhisi “kupendwa na kushikiliwa” wakati wa kukata tamaa, anasema Lisa Miller, PhD, mwanzilishi wa Taasisi ya Kiroho, Mwili na Akili katika Chuo cha Ualimu, Chuo Kikuu cha Columbia.

Hii inatuonyesha dhahiri ni jinsi gani IBADA husaidia kwenye kuboresha afya ya akili, na Kumfanya Mtu kuishi kwa kujiamini na matumaini makubwa.

Watu ambao hupata maana na kusudi la kupitia hali yao ya kiroho mara nyingi huibuka kutoka kwenye nyakati ngumu, na kujisikia tayari kushughulikia jambo linalofuata la kutisha ambalo linaweza kutokea.

Na sio afya ya akili tu. Watu wanaohudhuria ibada za kidini mara kwa mara wana uwezekano mdogo wa kuishia hospitalini kwa sababu yoyote.

Na wanapofanya hivyo, hulazwa hospitalini kwa muda mfupi, tafiti zinaonyesha. Hata walio wagonjwa zaidi kati yetu wanaweza kufaidika. Miongoni mwa watu walio na saratani, haijalishi ni kali vipi, wale walio na mazoezi ya kiroho huripoti hali bora ya maisha.

Jinsi ambavyo IBADA husaidia kuboresha afya ya Akili
0 Comment

Chanzo cha rangi nyeusi kwapani na jinsi ya kuondoaAfyaclass Forum •

Chanzo cha rangi nyeusi kwapani na jinsi ya kuondoa

Wataalamu wa afya wasema fangasi na uchafu ndio visababishi vikubwa vya weusi kwapani.

Usafi na kuepuka matumizi ya vifaa vya kunyolea visivyo sahihi ni mbinu ya kuepukana na tatizo hilo.

Weusi kwapani? Ndio.  Ni jambo la aibu  kwa baadhi ya watu na hawapendi kulizungumzia suala hili hadharani.

Baadhi yao hulazimika kuvaa nguo zenye mikono mirefu kwa kuepuka sehemu hizo kuonekana.

“Kwa sisi wanawake weusi kwapani unatutesa, unashindwa hata kuvaa nguo za kuogelea kwa amani ukihofia kuaibika endapo watu wakikuona,” anasema Anaheri Richard mkufunzi wa kuogelea (swim coach) jijini Dar Es Salaam.

Ikiwa wewe ni mmoja wa wahanga wa tatizo hili makala hii ni kwa ajili yako ambapo tutaangazia chanzo na jinsi ya kuondoa weusi kwapani.

Fangasi ndio chanzo cha weusi makwapani

Daktari Zabron Mbatiya kutoka Hospitali ya Kairuki ya jijini Dar es Salaam anasema chanzo kikubwa cha weusi kwapani ni maambukizi ya fangasi wa ngozi wanaopendelea kukaa sehemu zenye joto na unyevu unyevu.

“Tatizo hili husababishwa na fangasi aina ya ‘candida’ ambao huota kwenye makwapa, chini ya matiti, sehemu ya ndani ya mapaja na ndani ya  mashavu ya uke,” amesema Dk Mbatiya.

Fangasi hao hujishikiza kwenye vitundu vya vinyweleo na kusababisha miwasho ambapo kadri mtu anavyojikuna ndivyo weusi unavyoongezeka katika sehemu hizo.

Mbali na uwepo wa fangasi, Meshack Mhalila, mtaalamu wa afya wa kujitegemea kutoka mkoani Mbeya anasema kunyoa kwa vifaa visivyo sahihi kama viwembe butu pamoja na uchafu huchangia makwapa kuwa meusi.

Mtaalamu huyo amesema baadhi ya watu hawajisafishi ipasavyo na kusababisha mlundikano wa uchafu sugu ambao mwisho hutengeneza rangi nyeusi.

“Wengine hawajisafishi vizuri, hayo maeneo hayasuguliwi kabisa hapo lazima kuwe na rangi nyeusi… pia wale wanaovaa nguo za kubana kwa muda mrefu wanaweza kupata tatizo hilo,” anasema Mhalila.

Sambamba na hayo wataalamu hao wa afya wamesema matumizi yaliyokithiri ya vidhibiti harufu (vipodozi) makwapani na sehemu nyingine za mwili yanachangia sehemu hizo kuwa nyeusi kutokana na wingi wa kemikali zilizopo.

Fanya haya kuepukana na weusi kwapani

Licha ya kwamba tatizo hilo linatibika ikiwa utatembelea vituo vya afya na kutumia dawa, zipo mbinu zitakazokusaidia kuepukana nalo.

Wataalamu wa afya wanasema ili kuepukana na weusi kwapani njia ya kwanza ni kuhakikisha usafi wa sehemu hizo mara kwa mara.

“Sehemu ambazo zina uchafu ndipo fangasi wanapenda kukaa hivyo ukijisafisha na kujiweka safi unapunguza uwezekano wa fangasi kuzaliana na kusababisha weusi,” amesema Dk Mbatiya.

Kunyoa kwapani kwa vifaa sahihi ni miongoni mwa njia itakayokusaidia kupunguza weusi kwapani. Picha | Popsugar.

Kunyoa kwapani kwa vifaa sahihi

Baadhi ya vifaa vinavyotumika kunyolea huwa ndio kisababishi cha weusi kwapani. Wataalamu hao wa afya wanasema kutumia vifaa bora vya kunyolea kunaweza kusaidia.

“Watu wananyoa kwa kiwembe, hali lazima iwapate hususani akiwa amenyoa kwa muda mrefu,” amesema Mhalila.

Epuka matumizi yaliyokithiri ya vidhibiti harufu (vipodozi)

Matumizi yaliyokithiri ya vipodozi vinavyodhibiti harufu maarufu kama ‘deodorant na spray’ yanayoweza kusababisha ngozi ya kwapa kuwa nyeusi.

Mhalila anasema vipodozi hivyo huzuia mchakato wa utoaji taka mwili kwa njia ya jasho na kusabisha maeneo hayo kuwa meusi.

“Vipodozi vyenye viambata vya ‘aluminium salt’ husababisha seli za ngozi kufa ndio maana unakuta maeneo hayo ni meusi ikimaanisha kuwa maeneo hayo hakuna uhai,” ameongeza Mhalila.

Chanzo cha rangi nyeusi kwapani na jinsi ya kuondoa
0 Comment

Je, Visigino Vyako Vina shida? unapata maumivu au tatizo lolote?Afyaclass Forum •

Je, Visigino Vyako Vina shida? unapata maumivu au tatizo lolote?

Matatizo ya kisigino ni ya kawaida na yanaweza kusababisha maumivu. Hii hutokana na mkazo mwingi kwenye mfupa wa kisigino chako na tishu zinazozunguka.

Zipo sababu mbali mbali za kupata tatizo la kisigino ambalo huleta maumivu. Hali hii Inaweza kusababishwa na:

• Majeraha
• Michubuko kutokana na kukimbia au kuruka
• Kuvaa viatu ambavyo havilingani na miguu yako
• Kuwa na uzito kupita kiasi.n.k

Hizi zinaweza kusababisha tendinitis, bursitis, na fasciitis, ambayo ni aina zote za kuvimba kwa tishu zinazozunguka kisigino chako.

Baada ya muda mkazo unaweza kusababisha tatizo la mfupa na ulemavu. Magonjwa fulani, kama vile rheumatoid arthritis, na gout, yanaweza pia kusababisha matatizo ya kisigino.
Matibabu ya matatizo ya kisigino yanaweza kujumuisha:

• Kupumzika
• Dawa
• Mazoezi
• Kuvaa viatu maalum
• Upasuaji hauhitajiki sana.

Kwa Maelezo zaidi:endelea kufuatilia hapa hapa Instagram au, Link google: afyaclass….!!!!!

Je, Visigino Vyako Vina shida? unapata maumivu au tatizo lolote?
0 Comment

Jinsi ya kukabiliana na magonjwa yasiyoambukizaAfyaclass Forum •

Jinsi ya kukabiliana na magonjwa yasiyoambukiza

Wataalamu wa afya washauri kuzingatia ulaji sahihi wa vyakula ikiwa ni pamoja na kupunguza matumizi ya sukari, chumvi na mafuta.

Wakati dunia ikiendelea kushuhudia wimbi la ongezeko la magonjwa yasiyoambukiza Mratibu wa Magonjwa Yasiyoambukiza kutoka Hospitali ya Nyamagana, Dk.Sarah Mwendi anasema kubadili mtindo wa maisha ni miongoni mwa njia za kuu za kukabiliana na magonjwa hayo.

Shirika la Afya Duniani (WHO) linaainisha magonjwa yasiyoambukiza kuwa ni saratani, magonjwa ya moyo, kisukari pamoja na magonjwa ya mfumo wa upumuaji ambayo huwaathiri sana watu wenye vipato vya chini na vya kati.

Magonjwa hayo husababisha vifo vya watu takribani milioni 41 kila mwaka sawa na asilimia 76 ya vifo vyote vinavyotokea duniani.

Dk. Mwendi ameiambia Nukta habari kuwa miongoni mwa sababu kubwa zinazochangia magonjwa hayo ni pamoja na mfumo usiofaa wa maisha ambao unahusisha tabia bwete na ulaji usiofaa.

“Ninavyoongelea ulaji mbovu, ninaongelea ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi kama chips, piza…ni muhimu watu wakazingatia ulaji wa mlo kamili ambao umekusanya virutubisho vyote,” amesema Dk. Mwendi.

Sababu nyingine ambazo husababisha magonjwa hayo ni uvutaji wa sigara na tumbaku, matumizi ya vilevi, pamoja na athari za uchafuzi wa hewa.

Jinsi ya kuepuka magonjwa yasiyoambukiza

Ili kukabiliana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza, Dtk. Mwendi amewashauri wananchi  kuzingatia ulaji sahihi wa vyakula ikiwa ni pamoja na kupunguza matumizi ya sukari, chumvi na mafuta hali ambayo itasaidia kupunguza magonjwa hayo.

Pia wametakiwa kuzingatia ufanyaji wa mazoezi kwa wingi ili kupunguza magonjwa hayo ikiwemo kisukari na shinikizo la juu la damu kwa kuwa maradhi hayo yanatumia gharama kubwa katika kuyatibu.

Kwa upande wa kituo anachofanyia kazi Dk. Mwendi amebainisha kuwa asilimia kubwa ya wagonjwa wanaoripoti katika hospitali hiyo hubainika kuwa na magonjwa hayo hususani presha na sukari huku kundi linaloathirika zaidi ni wanawake.

“Wanawake kwa maana ya kwamba ndio watu wanaojitokeza kwa wingi kwenda kuchunguza afya zao tofauti na wanaume ambao hata kama anashida hiyo huchukulia kawaida au wakati mwingine kupata mawazo yasiyo sahihi kutoka kwa marafiki,” amesema Dk.Mwendi

Kwa mujibu wa Dk. Mwendi  asilimia 15 ya wagonjwa wanaofika hospitalini hapo husumbuliwa na magonjwa yasiyoambukiza, huku wengi wakisumbuliwa na presha na kisukari.

Baadhi ya wagonjwa waliofika katika hospitali hiyo kupata matibabu ya magonjwa hayo yasiyoambukiza wamesema pamoja na kupatiwa huduma zote mhimu lakini wanakumbana na changamoto ya gharama kubwa za matibabu na kuiomba Serikali ingalie namna ya kuwapunguzia.

“Tunahudumiwa vizuri, lakini changamoto tunayokumbana nayo ni gharama za matibabu kuwa kubwa, na unaweza kupatiwa dawa aina moja nyingine unaelekezwa kwenda kununua sehemu nyingine hivyo tunaomba Serikali itusaidie dawa ziweze kupatikana hospitali,” amesema Mary Minga mkazi wa Mahina.

Jinsi ya kukabiliana na magonjwa yasiyoambukiza
0 Comment

Mamilioni ya watu wako hatarini kuugua kipindupindu kutokana na ukosefu wa maji safiAfyaclass Forum •

Mamilioni ya watu wako hatarini kuugua kipindupindu kutokana na ukosefu wa maji safi, sabuni na vyoo, pamoja na uhaba wa chanjo ya kipindupindu.(WHO)

Hatua za haraka zinahitajika ili kukomesha ongezeko la wagonjwa wa kipindupindu duniani kote, hii ni kulingana na Kundi la Kimataifa la Kuratibu kuhusu Utoaji Chanjo “the International Coordinating Group (ICG)”

Hatua hizo ni pamoja na kuwekeza katika upatikanaji wa maji salama, usafi wa mazingira na usafi, kupima na kugundua milipuko haraka, kuboresha ubora na upatikanaji wa huduma za afya, na kufuatilia kwa haraka uzalishaji wa ziada wa dozi za bei nafuu za chanjo ya kipindupindu kwa njia ya mdomo (OCV) ili kuzuia visa zaidi.

ICG inasimamia hifadhi ya kimataifa ya chanjo ya kipindupindu. Kundi hilo linajumuisha Shirikisho la Kimataifa la Mashirika ya Msalaba Mwekundu na Hilali Nyekundu, Médecins Sans Frontières, UNICEF na WHO. Gavi, Muungano wa Chanjo, hufadhili hifadhi ya chanjo na utoaji wa OCV.

Wanachama wa ICG wanatoa wito kwa serikali, wafadhili, watengenezaji chanjo, washirika na jumuiya kuungana katika juhudi za haraka za kukomesha na kubadili ongezeko la kipindupindu.

Kipindupindu kimekuwa kikiongezeka duniani kote tangu 2021, huku visa 473 000 vilivyoripotiwa kwa WHO mwaka wa 2022, zaidi ya mara mbili ya wale walioripotiwa mwaka wa 2021.

Takwimu za awali za 2023 zinaonyesha ongezeko zaidi, huku zaidi ya kesi 700 000 zikiripotiwa. Milipuko mingi ina viwango vya juu vya vifo, vinavyozidi kiwango cha 1% kinachotumika kama kiashirio cha matibabu ya mapema na ya kutosha ya wagonjwa wa kipindupindu.

Mitindo hii ni ya kusikitisha ikizingatiwa kuwa kipindupindu ni ugonjwa unaoweza kuzuilika na unaoweza kutibika na kwamba kesi zimekuwa zikipungua miaka ya nyuma.

Kipindupindu ni maambukizi makali ya matumbo ambayo huenea kupitia chakula na maji yaliyochafuliwa na kinyesi kilicho na bakteria ya Vibrio cholerae.

Kuongezeka kwa ugonjwa wa kipindupindu kunachangiwa na mapungufu yanayoendelea katika upatikanaji wa maji salama na usafi wa mazingira.

Ingawa jitihada zinafanywa ili kuziba mapengo haya katika maeneo haya, katika maeneo mengine mengi mapengo hayo yanaongezeka, yakichochewa na mambo yanayohusiana na hali ya hewa, ukosefu wa usalama wa kiuchumi, migogoro, na kuhama kwa watu. Maji yanayosimamiwa kwa usalama na usafi wa mazingira ni sharti la kukomesha maambukizi ya kipindupindu.

Hivi sasa, nchi zilizoathirika zaidi ni pamoja na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Ethiopia, Haiti, Somalia, Sudan, Syria, Zambia, na Zimbabwe.

Sasa zaidi ya hapo awali, nchi lazima zichukue mwitikio wa sekta nyingi kupambana na kipindupindu.

Wanachama wa ICG wanatoa wito kwa nchi zinazoweza kuathirika kwa sasa na zinazoweza kuathiriwa kuchukua hatua za haraka ili kuhakikisha kuwa wakazi wao wanapata maji safi, huduma za usafi na usafi wa mazingira, na taarifa muhimu ili kuzuia kuenea kwa kipindupindu.

Uanzishwaji wa huduma hizi unahitaji utashi wa kisiasa na uwekezaji katika ngazi ya nchi. Hii ni pamoja na kuunda uwezo wa kutambua na kuitikia mapema, ugunduzi bora wa magonjwa, ufikiaji wa haraka wa matibabu na utunzaji, na kufanya kazi kwa karibu na jamii, ikijumuisha mawasiliano ya hatari na ushiriki wa jamii.

Mamilioni ya watu wako hatarini kuugua kipindupindu kutokana na ukosefu
wa maji safi
0 Comment

Jinsi ya Kunyoa sehemu za siri bila kupata vipele na muwashoAfyaclass Forum •

Jinsi ya Kunyoa sehemu za siri bila kupata vipele na muwasho

Kunyoa nywele sehemu za siri ni jambo linalofanyika kwa sababu ya usafi wa mwili. Muwasho na vipele baada ya kunyoa sehemu za siri huleta hali ambayo humfanya mtu kujihisi vibaya na wakati mwingine kupata maambukizi katika mashina ya nywele. Hali hii huwapata sana wale wanaotumia kiwembe.

Jinsi ya kunyoa sehemu za siri

Zifuatazo ni hatua muhimu za kufuata wakati wa kunyoa nywele za sehemu za siri;

1. Anza kwa kupunguza nywele na mkasi, pia unaweza kuishia katika hatua hii ikiwa hauhitaji kuziondoa kabisa kuacha upara

2. Mwagia maji ya uvuguvugu eneo husika kisha paka sabuni au jeli, au krimu maalumu ya kunyolea

3. Nyoa kwa kufuata uelekeo wa nywele zinavyoota

4. Usirudie rudie kupitisha kinyoleo eneo moja

5. Nyoa taratibu bila kuweka mgandamizo mkubwa

6. Safisha vizuri na maji ya uvuguvugu kuondoa mabaki ya nywele ulizonyoa

7. Paka mafuta ya maji kulainisha ngozi ya eneo hilo

Mambo ya kuzingatia

✓ Usitumie kiwembe kitupu kunyoa sehemu za siri kwani huleta marejaha madogo sana yanayoweza leta muwasho na kukuweka katika hatari ya kupata magonjwa ya ngono

✓ Usinyoe mara kwa mara kuzuia mkereketo katika ngozi ya sehemu za siri

✓ Safisha vifaa vyako kila unapomaliza kunyoa

✓ Badili kinyoleo baada ya kutumia walau mara 5

✓ Usitumie kinyoleo chenye kiwembe butu

✓ Usinyoe kila siku

Tunakushauri siku zote uwasiliane na daktari wako kabla ya kuchukua hatua yoyote ile kiafya baada ya kusoma vidokezo hivi.

AU KWA ushauri Zaidi,Elimu na Tiba wasiliana na Wataalam ndani ya Afyaclass

Rejea za mada hii:

1. How to treat and prevent razor bumps in the pubic area. Medical Newa Today. https://www.medicalnewstoday.com/articles/how-can-people-treat-razor-bumps-in-the-genital-area#vs-st-is. Imechukuliwa 20.01.2024

2. How to Get Rid of or Prevent Razor Burn and Ingrown Hairs. Healthline. https://www.healthline.com/health/how-to-get-rid-of-razor-burn#takeaway. Imechukuliwa 20.01.2024

3. Razor Burn Treatment: Effective Remedies and Solutions. WebMd. https://www.webmd.com/skin-problems-and-treatments/remedies-relieve-razor-burn. Imechukuliwa 20.01.2024

Jinsi ya Kunyoa sehemu za siri bila kupata vipele na muwasho
0 Comment

Hizi ndizo chanjo ambazo watoto na watu wazima wanapaswa kupataAfyaclass Forum •

Hizi ndizo chanjo ambazo watoto na watu wazima wanapaswa kupata

Je! watoto wako wamechanjwa? Usisahau kupata chanjo. Mara kwa mara huwa tunasikia maneno kama haya. Lakini siku zote huwa tunafikiria chanjo kwa watoto, ila je, unajua kwamba watu wazima pia wanapaswa kupewa chanjo?

Hizi ni pamoja na chanjo ambazo wasichana wanapaswa kupewa kabla ya ndoa.

Hata wazee zaidi ya miaka 60 wanapaswa kupata chanjo ili kupata kinga dhidi ya magonjwa mengi.

Dk. Vemuri Priyanka kutoka Visakhapatnam alitoa maelezo ya chanjo.

Je! ni chanjo gani zinapaswa kutolewa kwa watoto?

Kwa ujumla, Ratiba ya Kitaifa ya Chanjo na ratiba ya IAP (Indian Academy of Paediatrics) hufuatwa kwa ajili ya chanjo ya watoto kuanzia kuzaliwa hadi umri wa miaka kumi.

Kulingana na hilo, daktari wa watoto Dk. Vemuri Priyanka alielezea ni chanjo gani inapaswa kutolewa kwa watoto katika umri gani.

Kuna chanjo zinazotolewa ndani ya saa 24 baada ya kuzaliwa kwa chanjo zinazotolewa kabla ya umri wa miaka 10.

Kiwango cha sifuri ya matone ya polio hutolewa kwa watoto wachanga waliozaliwa siku yao ya kuzaliwa. Wanapewa chanjo ya ECG. Chanjo ya hepatitis B itatolewa. Hizi ni chanjo ambazo hutolewa kwa watoto wote katika nchi zote duniani. Matone ya polio hutolewa kuzuia ugonjwa wa polio.

Chanjo ya BCG hutolewa kuzuia Kifua Kikuu (TB). Kila mtu hupata TB wakati fulani maishani. Chanjo hii itaizuia kuwa mbaya zaidi wakati hilo litatokea. Ndiyo maana wengi wetu hata hatujui kwamba tulipata TB na kwamba tumeshapata.

Chanjo ya tetekuwanga

Chanjo ya Varicella hutumiwa kuzuia tetekuwanga. Mtu yeyote wa umri wowote anaweza kupata chanjo ya tetekuwanga. Watoto wanapaswa kuchukua dozi mbili. Dozi ya 1 katika miezi 15 na dozi ya 2 katika miezi 18 hadi 21.

Kwa diphtheria, pepopunda na kifaduro inayosababishwa na bakteria, dozi tano za chanjo ya DTAP zinafaa kutolewa. Dozi ya kwanza hutolewa kwa miezi miwili na ya pili baada ya miezi minne. Kisha dozi moja hutolewa katika umri wa miezi 6, nyingine katika miezi 15 hadi 18, na dozi nyingine katika umri wa miaka 4 hadi 6.

Dozi tatu au nne za chanjo ya ‘Haemophilus influenzae aina B’ hutolewa ili kuzuia maambukizi ya VVU. Dozi ya kwanza hutolewa katika umri wa miezi miwili, dozi ya pili katika umri wa miezi minne na dozi ya tatu katika umri wa miezi sita ikiwa inahitajika. Dozi ya mwisho hutolewa kati ya umri wa miezi 12-15.

Dozi mbili za chanjo ya hepatitis A hutolewa. Dozi ya kwanza katika umri wa mwaka mmoja na dozi ya pili hutolewa kati ya umri wa miezi 6 na 18.

Chanjo ya hepatitis B hutolewa kwa dozi tatu au nne. Dozi ya kwanza hutolewa wakati mtoto anazaliwa, na dozi ya pili hutolewa kati ya mwezi 1 na 2. Dozi ya tatu hutolewa katika umri wa miezi minne na dozi ya mwisho hutolewa kati ya umri wa miezi 6 na 18.

Kwa Surua na Rubela

Chanjo ya (mafua) inahitajika kwa watoto wenye umri wa miezi sita hadi wazee wenye umri wa miaka 60.

Watoto chini ya umri wa miaka tisa wanapaswa kupewa dozi mbili. Lakini mtoto anapaswa kumuuliza daktari ikiwa dozi ya pili ni muhimu.

Chanjo za IPV huzuia polio. Watoto hupewa dozi nne za chanjo hii ya polio. Dozi ya kwanza hutolewa kwa miezi miwili, ya pili kwa miezi minne, ya tatu kati ya miezi 6-18, na ya nne kati ya miaka 4-6.

Dozi mbili za chanjo ya MMR ya surua, mabusha na rubela (MMR) inahitajika chini ya Ratiba ya Kitaifa ya Chanjo. Dozi ya kwanza hutolewa kati ya miezi 12-15. Dozi ya pili hutolewa kati ya umri wa miaka 4-6.

Chanjo ya encephalitis ya Kijapani pia inatolewa katika majimbo ambayo ugonjwa wa encephalitis umeenea. Encephalitis ya Kijapani husababisha homa ya ubongo. Ili kuzuia hili, dozi moja ya chanjo hutolewa katika umri wa miezi 9-12 na dozi ya pili katika umri wa miezi 16-24.

Chanjo ambayo unapewa kama ulikosa kupewa kwa wakati

Pata chanjo Kulingana na Ratiba ya Kitaifa ya Chanjo, kila chanjo inapaswa kutekelezwa kwa wakati maalum.

Lakini Dk. Priyanka alisema kama hawataweza kupata chanjo kwa wakati, kutakuwa na chanjo ambazo mtu anaweza kupata ikiwa pengine alikosa kupewa kwa wakati stahiki.

Wahusika hutakiwa kuwasiliana na madaktari wao kwanza na kupewa chanjo hizi kulingana na maagizo.

Sio tu kwa watoto, bali pia kwa watu wazima: Sravanti

Tunapozeeka, mfumo wetu wa kinga hupungua, na kutufanya tuwe na magonjwa mbalimbali.

Kwa hiyo watu wazima pia wanahitaji kupata chanjo.

Mganga Mkuu Dk. T. alisema pamoja na kwamba baadhi ni lazima, nyingine zinapaswa kutolewa kulingana na hali ya afya ya mhusika.

Dr. Sravanti anasema nini kuhusu chanjo kwa wazee…

Chanjo ya mafua: Dozi moja ya chanjo ya mafua ambayo haijaamilishwa inapaswa kuchukuliwa kila mwaka ili kujikinga na virusi vya mafua, ambayo ina maana ni kuzuia mafua ya mara kwa mara na kikohozi.

Lakini kila mwaka inabadilika. Lazima upate iliyotolewa mwaka huo. Watu wenye magonjwa sugu pamoja na wahudumu wa afya, walimu na wanafunzi wanaosafiri kwa vikundi wanapaswa kupata chanjo hii.

Chanjo ya Human Papilloma virus (HPV): Wasichana na wavulana walio na umri wa zaidi ya miaka 10 wanapaswa pia kupata ili kujikinga na saratani ya mlango wa kizazi. Chanjo hii inapaswa kuchukuliwa kabla ya kujamiiana au ndoa. Vinginevyo haitakuwa na faida nyingi wakati mwingine. Kawaida chanjo hutolewa kwa dozi 3 kwa muda wa miezi 6. Virusi vya papilloma ya binadamu husababisha saratani ya shingo ya kizazi kwa wanawake. Kuna aina mbili za chanjo hii, Cervarical na Gardasil.

Tdap (Tdap), Td (Td): Chanjo hii inapaswa kutolewa ili kuzuia pepopunda, diphtheria, (kifaduro). Kwa kawaida tunaita sindano hii ya TT. TeaDop inatolewa kwa kila mtu. Dozi moja inaweza kuchukuliwa hata baada ya miaka 18 ikiwa haijatolewa. Watu wazima wenye umri wa miaka 18 hadi 64 ambao wamekamilisha ratiba ya msingi ya chanjo wanapaswa kupokea dozi ya nyongeza ya TD kila baada ya miaka 10.

Chanjo ya homa ya ini: Chanjo ya homa ya ini hulinda dhidi ya virusi vya homa ya ini vinavyosababisha ugonjwa wa ini. Tunachosikia zaidi ni chanjo ya Hepatitis B. Maambukizi ya virusi vya Hepatitis B inaweza kusababisha ugonjwa wa cirrhosis na saratani ya ini. Inatolewa kwanza kabla ya kuambukizwa na virusi hivi.

Baadhi ya chanjo zaidi: Chanjo ya MMR inaweza kuchukuliwa na watoto pamoja na watu wenye umri wa kati ya miaka 19 na 60 ili kujikinga na magonjwa ya surua, mabusha na rubela. Chanjo ya pneumococcal inapaswa kutolewa ili kujikinga dhidi ya nimonia. Inachukuliwa kwa njia mbili.

Wale ambao ni zaidi ya umri wa miaka 65 hawawezi kuvumilia pneumonia. Ndiyo maana wanapaswa kupata chanjo hii kwa ajili ya ulinzi. Pia, watu walio chini ya umri wa miaka 65 ambao wana matatizo ya kisukari, ini na moyo wanapaswa pia kupata chanjo hii ili kuzuia nimonia.

Dk Sravanti alisema kuwa kuna chanjo nyingi ambazo hata wazee wanapaswa kupata.

Je, watu wazima wanaweza kupata chanjo ambazo hawakupata wakiwa watoto?

Wengine hukosa chanjo wakiwa watoto. Watu wengi pia wana shaka ikiwa chanjo hizo zinaweza kutolewa wakiwa watu wazima. Dk Priyanka alisema hivi kuhusiana na hili …. Chanjo ambazo hazikutolewa utotoni hazihitajiki kwa kila mtu katika utu uzima.

Wale ambao hawajapata chanjo ya tetekuwanga wakiwa na umri wa miaka miwili wanapewa chanjo ya tetekuwanga hadi umri wa miaka 12.

Via:Bbc

Hizi ndizo chanjo ambazo watoto na watu wazima wanapaswa kupata
0 Comment

Punguza matumizi ya sukari, chumvi na mafuta pamoja na kufanya mazoeziAfyaclass Forum •

Punguza matumizi ya sukari, chumvi na mafuta pamoja na kufanya mazoezi.

Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu ametoa wito Kwa Watanzania kuzingatia mtindo bora wa maisha ili kuepuka magonjwa Yasisyoambukiza ikiwemo Kisukari na Shinikizo la Juu la Damu (Presha) kwa kupunguza matumizi ya sukari, chumvi na mafuta pamoja na kufanya mazoezi.

Waziri Ummy ametoa wito huo leo Machi 17, 2024 akimuwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika fainali ya Mashindano ya Ishirini na Tatu ya Kuhifadhi Qur’an Tukufu Kitaifa yaliyoandaliwa na Taasisi ya Aisha Sururu yaliyofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee Jijini Dar Es Salaam.

“Tukizingatia hayo mambo makubwa Matatu, kupumguza matumizi ya sukari, chumvi pamoja na mafuta tutajiepusha na magonjwa mbalimbali Yasiyoambukiza kwa maana magonjwa haya yanaongeza kila siku na yanagharama kubwa sana kuyatibu.” Amesema Waziri Ummy

Punguza matumizi ya sukari, chumvi na mafuta pamoja na kufanya mazoezi
0 Comment

Haya ni Madhara ya Energy Drink kwa Afya ya BinadamuAfyaclass Forum •

Madhara ya Energy Drink kwa Afya ya Binadamu: Je, Unayajua?

Kwa miaka mingi, energy drink zimekuwa maarufu sana kati ya vijana na watu wazima. Wengi huchukulia energy drink kama njia ya kuongeza nguvu na kuboresha utendaji wao wa kila siku.

Lakini, wachache tu wanajua kuwa matumizi ya mara kwa mara ya energy drink yanaweza kusababisha madhara makubwa kwa afya ya binadamu.

Katika makala hii, tutajadili Madhara ya Energy Drink kwa Afya ya Binadamu, ikiwa ni pamoja na jinsi ya kuzuia athari mbaya za matumizi ya energy drink.

Madhara ya Energy Drink kwa Afya ya Binadamu

Hapa chini, tutaangalia baadhi ya madhara ambayo yanaweza kutokea kwa afya ya binadamu kutokana na matumizi ya energy drink:

1. Kupungua kwa usingizi: Kiungo kikuu cha energy drink ni kafeini, ambayo ni stimulant.

Matumizi ya kafeini yanaweza kusababisha kupungua kwa usingizi na hii inaweza kusababisha matatizo ya afya.

2. Kuongezeka kwa presha ya damu: Baadhi ya energy drink pia zina sukari nyingi, ambayo inaweza kusababisha kuongezeka kwa presha ya damu.

3. Matatizo ya moyo: Matumizi ya mara kwa mara ya energy drink yanaweza kusababisha matatizo ya moyo,

ikiwa ni pamoja na kuziba kwa mishipa ya damu na kusababisha magonjwa kama vile shinikizo la damu na moyo kushindwa kufanya kazi.

4. Kupungua kwa uwezo wa akili: Matumizi ya energy drink yanaweza kusababisha kupungua kwa uwezo wa akili,

ikiwa ni pamoja na kushindwa kuzingatia na kupungua kwa uwezo wa kumbukumbu.

5. Matatizo ya kiafya kwenye viungo vya ndani: Baadhi ya energy drink zina viungo vya ziada ambavyo vinaweza kusababisha matatizo ya kiafya ya ndani, ikiwa ni pamoja na uharibifu wa figo na ini.

Jinsi ya Kuzuia Madhara ya Energy Drink kwa Afya ya Binadamu

Ingawa energy drink ina madhara, bado inaweza kufurahisha kama inavyopaswa kuwa. Hapa kuna baadhi ya njia za kuzuia athari mbaya za matumizi ya energy drink:

1. Kunywa maji mengi: Wakati wa kunywa energy drink, ni muhimu kunywa maji mengi pia ili kuondoa sumu mwilini.

2. Kunywa kwa kiasi kidogo: Kwa sababu energy drink ina kafeini nyingi, unapaswa kunywa kwa kiasi kidogo na usitumie mara kwa mara.

Watu wengi hupata matokeo mazuri baada ya kunywa chupa moja ya energy drink kwa siku.

3. Kula vyakula vyenye afya: Ni muhimu kula vyakula vyenye afya kama matunda, mboga mboga za majani, na vyakula vyenye protini ili kuweka afya yako sawa.

4. Pata usingizi wa kutosha: Usingizi wa kutosha ni muhimu sana ili kuboresha afya yako na kuzuia madhara ya energy drink kwa afya yako.

FQs

Maswali Yanayoulizwa Mara kwa Mara Kuhusu Energy Drink

Hitimisho

Energy drink ni chanzo cha haraka cha nishati, lakini inaweza kuwa na madhara kwa afya ya binadamu.

Ni muhimu kutumia energy drink kwa kiasi kidogo na usitumie mara kwa mara ili kuzuia athari mbaya kwa afya yako.

Kumbuka pia kunywa maji mengi, kula vyakula vyenye afya, na kupata usingizi wa kutosha ili kuboresha afya yako.

Kama kawaida, unapaswa kuwasiliana na daktari wako ikiwa una wasiwasi wowote juu ya athari za energy drink.


Madhara ya energy drink,Soma hapa Kufahamu

Baada ya kukutana na maswali mengi,Wasomaji wengi wa afyaclass wamependekeza kupata elimu juu ya energy drinks,

kuhusu madhara ya Energy drinks ni yapi?,Je energy inatoa Mimba? n.k Leo tumechambua kidogo kuhusu vinywaji hivi-Energy drinks

Energy Drink ni nini?

Hapa tunazungumzia vinywaji vyote ambavyo lengo lake kubwa ni kuupa Mwili nguvu zaidi na kukuchangamsha,

vinywaji hivi vina kiwango kikubwa cha caffeine, Sukari nyingi, pamoja na vionjo vingine(additives au stimulants) ili vilete matokeo yaliyokusudiwa,

Mchanganyiko wa vitu hivi unaweza kuleta matokeo mbali mbali ikiwemo;

  • Kuongeza hamasa,
  • Kuleta attention zaidi,
  • Kusisimua mwili,
  •  Kukupa Nguvu-energy,
  • Kupandisha Presha,
  • Kuongeza mapigo ya moyo,
  •  pamoja na kuongeza kasi ya Upumuaji,

Pia vinywaji hizi hutumiwa zaidi na wanafunzi ili kuwapa nguvu zaidi na kuwafanya wachangamke,

Ingawa Vionjo(stimulants) ndani ya vinjwaji hivi huweza kuleta madhara kwenye mfumo wa fahamu- nervous system.Hii ni kwa mujibu wa vituo vya Udhibiti na Kupambana na magonjwa yaani Centers for diseases control and prevention(CDC)

Kama wewe ni mtumiaji Mzuri wa Energy drinks, utakuwa shahidi Pia,

Kwamba kila chupa ya Energy inamaelezo pale kuhusu baadhi ya tahadhari kwenye matumizi yake,

Mfano;

  1. Kwa Watoto
  2. Na Kwa Wajawazito

Kama bado hujafwatilia,Nakupa kazi,Hakikisha unasoma Maelezo kwenye CHUPA za Energy kuhusu matumizi ya energy drinks na tahadhari zake kabla ya Matumizi.

MADHARA YA ENERGY DRINK

Haya hapa ni baadhi madhara kutokana na matumizi ya Energy drinks;

1. Kusababisha tatizo la mwili kukosa Maji ya kutosha yaani Dehydration,

2. Kusababisha matatizo mbali mbali ya Moyo-Heart complications kama vile;

  • Mapigo ya Moyo kubadilika- irregular heartbeat
  •  Pamoja na tatizo la Moyo kushindwa kufanya kazi-heart failure.

3. Kusababisha tatizo la Wasiwasi-Anxiety

4. Kusababisha tatizo la Kukosa Usingizi-Insomnia

5. Kusababisha kiwango kikubwa zaidi cha Caffeine(Caffeine overdose) mwilini

6. Kusababisha tatizo la Kuongezeka kwa Uzito zaidi(Weight gain/Overweight)

7. Kusababisha matatizo ya Meno,kama meno kuharibika/Kuoza/au kushambuliwa na bacteria kwa urahisi zaidi kutokana na Sukari nyingi ndani ya vinywaji

8. Kupata addictions n.k

TAHADHARI

Kinga ni bora kuliko tiba,Tumia Vinywaji hivi kwa kiasi na epuka matumizi kupita kiasi.

Soma maelekezo kwa kila chupa ya Energy,utaona limitations zake na hata Idadi ya chupa ambazo unatakiwa kutumia na usizidishe kwa siku umeandikiwa.

Haya ni Madhara ya Energy Drink kwa Afya ya Binadamu
0 Comment

Ugonjwa wa vifaranga kushusha mabawaAfyaclass Forum •

Ugonjwa wa vifaranga kushusha mabawa

Ugonjwa wa vifaranga kushusha mabawa, unaojulikana pia kama “Marek’s disease” au “ugonjwa wa kudhoofika kwa misuli,” ni tatizo linaloweza kuathiri vifaranga na kusababisha dalili kama vile kushusha mabawa, matatizo ya kutembea, kupoteza uzito, na hata kifo.

Ugonjwa huu unasababishwa na virusi vya Marek’s disease virus (MDV), ambavyo ni aina ya herpesvirus. Hapa chini kuna muhtasari wa ugonjwa huu na jinsi ya kukabiliana nao:

Dalili za Ugonjwa wa vifaranga kushusha mabawa

– Kushusha mabawa kwa vifaranga.

– Ugumu wa kutembea au paralizi.

– Mabadiliko katika rangi ya iris au upofu.

– Kuongezeka kwa saizi ya viungo vya ndani.

– Kupoteza uzito licha ya kula kawaida.

Uenezaji wa Ugonjwa wa vifaranga kushusha mabawa

Virusi vya Marek’s huenezwa kwa njia ya hewa kupitia vumbi lililo na ngozi iliyokufa na manyoya ya kuku walioambukizwa. Mara baada ya kuku kuingiwa na virusi, huwa na uwezekano mkubwa wa kubeba virusi kwa maisha yao yote, hata kama hawaoneshi dalili.

Kuzuia Ugonjwa wa vifaranga kushusha mabawa

Chanjo: Njia bora zaidi ya kuzuia ugonjwa wa Marek’s ni kwa chanjo.

Vifaranga huchanjwa siku moja baada ya kuzaliwa. Ingawa chanjo haina uwezo wa kuzuia maambukizi, inaweza kusaidia kupunguza uwezekano wa vifaranga kuonesha dalili za ugonjwa huo.

Usafi na Udhibiti wa Mazingira: Kudumisha usafi katika mazingira ya kuku na kuzuia msongamano ni muhimu. Hii inajumuisha kusafisha mara kwa mara na kuondoa vumbi na manyoya ambayo yanaweza kuwa yamebeba virusi.

Quarantine na Udhibiti wa Magonjwa: Kuzuia kuingizwa kwa kuku wapya katika kundi bila kuwaweka karantini kwanza na kuhakikisha hawana ugonjwa ni muhimu ili kudhibiti kuenea kwa ugonjwa.

Matibabu ya Ugonjwa wa vifaranga kushusha mabawa

Hakuna matibabu maalum ya kuondoa virusi vya Marek’s kutoka kwa kuku walioambukizwa. Mara vifaranga wanapoonesha dalili, lengo la matibabu huwa ni kupunguza mateso na kudhibiti dalili, lakini mara nyingi matokeo siyo mazuri.

Kumbuka, kuzuia ni muhimu zaidi kuliko matibabu linapokuja suala la magonjwa mengi ya kuku, na chanjo dhidi ya ugonjwa wa Marek’s ni sehemu muhimu ya programu ya afya ya kundi la kuku. Kwa ushauri maalum na miongozo inayohusiana na hali yako, ni muhimu kuwasiliana na mtaalamu wa afya ya mifugo.

Ugonjwa wa vifaranga kushusha mabawa
0 Comment
Notification
My blog is in the process of editing and perfecting the new template, so there are still some functions to click but not yet used. Note which blogs associated with your side please read this lesson to update the blog logo.
UNDERSTOOD