Breaking: Chukueni tahadhari dhidi ya uwepo wa COVID 19Afyaclass Forum •
Breaking: Chukueni tahadhari dhidi ya uwepo wa COVID 19
Wizara ya Afya imesema imeendelea kufanya ufuatiliaji wa karibu na kutoa taarifa za kila siku kuhusu magonjwa ya mlipuko pamoja na tetesi za uwepo wa magonjwa hayo nchini ambapo imesema tangu February hadi April 2025, ufuatiliaji wa virusi vya Covid 19 umeonesha ongezeko la maambukizi kutoka 1.4% (Wagonjwa wawili kati ya Watu 139 waliopimwa) mwezi February hadi 16.3% (Wagonjwa 31 kati ya 190 waliopimwa) mwezi March, na kisha 16.8% (Wagonjwa 31 kati ya Watu 185 waliopimwa) mwezi Aprili 2025.
Taarifa iliyotolewa leo May 20,2025 na Mganga Mkuu wa Serikali, Dkt. Grace Magembe imesema “Ugonjwa wa UVIKO-19, ambao ulitangazwa kwa mara ya kwanza nchini March 2020, umeendelea kuwepo kwa kiwango cha chini kama yalivyo magonjwa mengine ya mfumo wa njia ya hewa, hali ya kuongezeka na kupungua kwa ugonjwa huu imekuwepo kila mwaka tangu kutangazwa kwa ugonjwa huu mwaka 2020, kwa kipindi hiki ongezeko hili linaonekana zaidi katika Mkoa wa Dar es salaam, Wizara ya Afya inaendelea kufuatilia kwa karibu mwenendo wa magonjwa ya mfumo wa njia ya hewa nchini na kutoa taarifa”
“Katika kipindi cha kuanzia mwezi Januari hadi Aprili 2025, tumeshuhudia ongezeko la tetesi zinazohusiana na magonjwa ya mfumo wa njia ya hewa katika jamii hapa nchini, hasa katika mkoa wa Dar es salaam, kwa kutumia mifumo ya ufuatiliaji wa magonjwa ya mfumo wa njia ya hewa, ambayo imekuwepo tangu mwaka 2008, tumekuwa tukifuatilia mwenendo wa magonjwa haya ili kubaini aina za vimelea vinavyosababisha maambukizi, ongezeko la visa, pamoja na uwezekano wa kujitokeza kwa kirusi kipya chenye uwezo wa kusambaa kwa haraka”
“Vipimo vya maabara vimebaini kuongezeka na kupungua kwa virusi vya influenza hali ambayo imekuwa ikionekana pia katika miaka iliyopita na ndiyo maana hujulikana kama ‘Seasonal influenza”, vipimo vimeonesha kuwa hakuna kirusi kipya kinachoweza kusambaa kwa haraka na kusababisha mlipuko wa aina ya Pandemiki” Cc:MillardAyoUPDATES
Breaking News;Papa mpya apatikanaAfyaclass Forum •
Breaking News;Papa mpya apatikana
Moshi mweupe umeonekana ukifuka kutoka kwenye bomba la moshi katika Kanisa la Sistine Chapel, ni wazi mchakato wa upigaji kura umekamilika na makadinali wamemchagua mrithi wa Papa Francis.
Bado hatujui ni nani amechaguliwa, lakini itaonekana wazi watakapotokea kwenye roshani ya Kanisa la Sistine, ndani ya kama saa moja.
Roshani inayokodolewa macho
"Viva Papa"
Umati wa watu unaimba "Viva papa", ambayo ina maana ya "maisha marefu Papa" kwa Kiitaliano.
Muziki unaendelea kuchezwa kutoka kwa bendi ambayo sasa iko chini ya roshani katika uwanja wa St Peter's Square.
Nini kinatokea sasa?
Makadinali wateule sasa wamemchagua Papa mpya na mambo yatakwenda kwa haraka sana kuanzia sasa.
Kwa vile moshi mweupe umetokea, kawaida, Papa mpya ataonekana kwenye roshani upande wa moja kwa moja na uwanja wa St Peter's Square ndani ya saa moja ijayo.
Papa mpya sasa anaongozwa hadi kwenye chumba kidogo karibu na Kanisa la Sistine ambapo atavaa mavazi meupe ya papa.
Kardinali mkuu hivi karibuni atathibitisha uamuzi huo kwa maneno "Habemus Papam" - Kilatini ikimaanisha "tuna Papa" - na kumtambulisha Papa mpya kwa jina lake alilochagua la papa.
Umati wajawa na furaha na kuomba wakisherehekea Papa mpya
Shangwe isiyo na kifani yashuhudiwa upande wa waumini huku moshi mweupe ukifuka, kila mtu akiwa anakimbilia kuuona.
Watu wanaruka juu na chini kwa furaha, wengine wanaomba huku wakiwa wanatazama angani. Wanandoa kutoka Ugiriki wanasema "ni tukio ambalo ni nadra sana kutokea maishani", na kuongeza kuwa watasubiri kuona Papa mpya akitokea kwenye roshani.
Katina eneo lote la Kanisa la Sistine, kengele zinalia kwa nguvu sana na zinasikika kila mahali huku watu wakishangilia na kupiga mayowe kwa furaha.
Sauti hapa ni nzuri sana, kengele zinalia kwa nguvu sana na zinasikika kila mahali huku watu wakishangilia na kupiga mayowe kwa furaha.
Bendera zinapeperushwa huku watu wakikumbatiana wakati mchakato wa kumtafuta kiongozi wa kanisa katoliki ukifikia tamati.
Bendi inacheza muziki
Bendi maalum iliyovalia nguo za rangi ya buluu na samawati inaonekana ikicheza muziki huku ikipita katikati ya umati wa watu huko Vatikani.
Wanaotembea kando yao ni Walinzi wa Uswizi, wakiwa wamevalia sare zao za mistari ya bluu na njano.
Umati wanapiga makofi na kuinua simu ili kunasa picha hiyo.
Nini Faida ya kutumia Gari kali Siku ya Harusi?Afyaclass Forum •
Nini Faida ya kutumia Gari kali Siku ya Harusi?
Bila shaka ushahudhuria vikao vya sherehe mbalimbali iwe sendoff, harusi na nyingine zenye kufanana na hizo, ukaona namna kamati za maandalizi zinavyohaha kuhakikisha maharusi wanatumia magari mazuri siku ya tukio.
Si ajabu ukaona watu wanafikia hata hatua ya kugombana kuhusu gari la maharusi, huyu akisema aina fulani ya gari ndo nzuri lakini gharama kubwa, mwingine akisema tusijali gharama tuichukue tu kama bajeti ipo.
Sasa kuna mdau anasema ushawahi kujiuliza faida ya kutumia gari kali ni ipi? Yaani usiku mtu anatumia gari kali kwenye harusi anapelekwa ukumbini kisha hotelini, halafu asubuhi anaondoka na Bajaji kuelekea nyumbani kwake, mbwembwe zote zimeisha! Je tumsaidie mdau mawazo au asubiri kwenye shughuli yake aone?
Nimefanyiwa upasuaji mara 100 na siachi' Nini Ushauri wako hapaAfyaclass Forum •
Nimefanyiwa upasuaji mara 100 na siachi' Nini Ushauri wako hapa
Abby Wu alikuwa na umri wa miaka 14 tu alipofanyiwa upasuaji wa urembo bandia kwa mara ya kwanza.
Baada ya kupata matibabu ya homoni, uzito wa mwili wa Abby uliongezeka kutoka kilo 42 hadi kilo 62 ndani ya miezi miwili.
Mwalimu wake wa michezo ya kuigiza aligundua mabadiliko hayo ya mwili.
Mwalimu wangu aliniambia, ''ulikuwa nyota lakini sasa umekuwa mnene kupita kiasi. Chagua moja uondoke kwa tasnia hii au upunguze kilo,'' anakumbuka alichoambiwa kipindi hicho akisubiri kufanya mtihani wake wa tamthilia.
Mama yake Abby aliingilia kati na kuamua kumpeleka kufanyiwa upasuaji wa kuondoa mafuta tumboni na miguuni.
Abby anavuta kumbukumbu jinsi mamake alivyompa motisha akisubiri kufanyiwa operesheni hiyo.
''Kuwa mkakamavu na uingie ufanyiwe. Ukitoka hapo utakuwa mrembo zaidi.''
Upasuaji huo ulimuacha na makovu. Abby alipatiwa dawa za kupunguza uchungu lakini alikuwa macho akifanyiwa operesheni hiyo.
''Ningeona kiasi cha mafuta kilichotolewa mwilini mwangu na damu iliyokuwa ikinivuja,'' anasema.
"Upasuaji ulifanya kazi. Nilijiamini na kuwa na furaha zaidi, siku baada ya siku. Nadhani mama yangu alifanya chaguo sahihi."
Sasa Abby ana umri wa miaka 35 na amefanyiwa upasuaji wa urembo mara mia moja ikimgharimu dola nusu milioni.
Anamiliki kliniki ya ulimbwende katikati mwa mji wa Beijing na amekuwa mtu tajika katika tasnia ya upasuaji wa plastiki nchini China.
Lakini upasuaji huo pia unaathari zake kwa mwili.
Akiwa amekaa mbele ya kioo anajipodoa ili kuficha makovu ya sindano za kupunguza unene usoni, utaratibu anaoufanya kila mwezi ili kuhakikisha uchanga usoni mwake nakuhakikisha hana ngozi zilizolegea baada ya upasuaji wa kupunguza taya uliondoa mifupa mingi.
Lakini anasisitiza kuwa hajutii upasuaji wa urembo aliyofanya kufikia sasa akiamini kuwa mamake hakukosea kumuanzisha katika ulimbwende huu.
Mwanamke achapisha bango na kuita jamii yake baada ya kuwa wa Kwanza kupanda Ndege kwenye jamii nzimaAfyaclass Forum •
Mwanamke achapisha bango na kuita jamii yake baada ya kuwa wa Kwanza kupanda Ndege kwenye jamii nzima
Mwanamke mmoja amechapisha bango na kuita jamii yake kusherehekea naye kwa kuwa "mwanamke wa kwanza kuingia kwenye ndege" katika jamii yake.
Mwanamke huyo amekuwa gumzo sana kwenye mitandao baada ya kusherehekea kuwa "mwanamke wa kwanza katika jamii yake kusafiri kupitia ndege."
Gold Ike aliingia kwenye ukurasa wa Facebook siku nne zilizopita ili kushiriki video yake akipiga picha mbele ya ndege.
Kisha, Jumapili, Aprili 6, alifanya Sherehe na kuwaalika watu wa jamii yake kusherehekea pamoja naye.
Pia alichapisha bango ambalo lilikuwa limeandikwa: "Mwanamke wa kwanza kuingia kwenye ndege katika jamii yangu".
Wageni waliohudhuria sherehe yake walipiga picha na bango hilo.
JE,WEWE UNAIONAJE HII? NI SAHIHI AU KAKOSEA?
Hatimaye majibu ya vinasaba (DNA) yaliyokuwa yanasubiriwa yametolewaAfyaclass Forum •
Hatimaye majibu ya vinasaba (DNA) yaliyokuwa yanasubiriwa yametolewa
Hatimaye majibu ya vinasaba (DNA) ya watoto watatu waliozaliwa Machi 24, 2025 katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Arusha (Mount Meru) yametolewa, huku Neema Kilugala, mkazi wa mtaa wa Ndaravoi, Kata ya Daraja Mbili jijini Arusha, akiangua kilio baada ya kutoridhishwa na matokeo hayo.
Neema ambaye alijifungua kwa upasuaji katika hospitali hiyo, alidai kuwa alibadilishiwa mtoto na hakuwahi kuridhika na mtoto aliyekabidhiwa, akisema mtoto wake alizaliwa akiwa mzima wa afya na mwenye uzito wa zaidi ya kilo tatu.
Akizungumza kwa uchungu nje ya Kituo Kikuu cha Polisi mkoani Arusha Aprili 3, 2025, Neema alisema anaamini kuwa mtoto wake yupo hai na kuna mwanamke mwingine aliyepewa mtoto wake kwa bahati mbaya au makusudi.
Mama mzazi wa Neema naye alilia kwa uchungu, akiitaka serikali irejee upya vipimo vya DNA kwa watoto wote watatu, kwa kuwa mtoto ambaye inadaiwa ni wa binti yake (Neema) na tayari ameshafariki, si wake kwa mujibu wa maumbile na hisia zao za kizazi.
Kutokana na utata huo, serikali iliamuru kufanyika kwa vipimo vya DNA kwa wanawake wote waliowajifungua watoto siku hiyo pamoja na watoto wao, ili kupata ukweli wa jambo hilo.
Kwa mujibu wa Afisa Sheria kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Bw. George Daniel, ambaye yupo jijini Arusha kupitia kampeni ya "Samia Legal Aid", alisema walipokea wito kutoka Polisi kwa ajili ya kushiriki katika kusikiliza majibu ya vinasaba hivyo.
“Katika matokeo haya, ambapo wazazi wote watatu walikuwepo, vipimo vimeonyesha kwa asilimia zaidi ya 99 kuwa mtoto anayelalamikiwa na Neema kuwa si wake, ndiye mtoto wake halisi kwa mujibu wa vinasaba,” alisema Bw. Daniel.
Aliongeza kuwa, iwapo Neema bado anahitaji msaada wa kisheria, ofisi yao iko tayari kumsaidia kupitia kampeni ya Samia Legal Aid ambayo inalenga kuwasaidia wananchi wanyonge kupata haki zao.
Diwani wa Kata ya Daraja Mbili aliyefika kituoni hapo pamoja na familia ya Neema alisema kuwa wataitisha kikao cha pamoja kujadiliana hatua za kuchukua kufuatia matokeo hayo.
Kwa upande wake, Makamu wa Rais wa Chama cha Wauguzi Tanzania (TANNA) alitoa wito kwa wauguzi nchini kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi, akibainisha kuwa chama hicho kitaendelea kufuatilia kwa karibu utendaji kazi wa wauguzi kuhakikisha haki na uadilifu vinaendelea kutawala katika huduma za afya.
Watalii walio katika hedhi wazuiwa kuingia kwenye Mahekalu Afyaclass Forum •
Watalii walio katika hedhi wazuiwa kuingia kwenye Mahekalu
Mamlaka huko Bali, Indonesia imezindua sera mpya ya kupiga marufuku "watalii walio katika hedhi" kuingia mahekaluni kwa wasiwasi kwamba damu ya kipindi cha Hedhi ni "chafu" itachafua maeneo yao matakatifu.
Sheria hii "Unorthodox law" imejumuishwa katika orodha ya sera ambazo gavana wa kisiwa cha tropiki, Wayan Koster, aliziweka mnamo Machi 24 ili kuwabana "watalii wanaoenda kinyume",Hii ni kulingana na ripoti kutoka Metro.
"Ninatekeleza waraka huu kama hatua ya haraka ya kudhibiti watalii wa kigeni wanapokuwa Bali," honcho ilitangaza.
Chini ya sheria hizo mpya, wanawake hawataruhusiwa kuingia kwenye mahekalu ya Balinese wakiwa kwenye hedhi kwa kuhofia kwamba Damu ya hedhi ni "chafu" na "itafanya hekalu kuwa najisi," Visit Bali iliripoti.
Kulingana na Stories zilizokuwa zinasimuliwa kutoka "kizazi hadi kizazi, kuna athari mbaya ikiwa umeamua kuingia hekaluni wakati wa hedhi," tovuti hiyo ilionya.
"Wanawake wengi hupata maumivu na kuzimia wakiwa hekaluni. Na Inaripotiwa kwamba kuna matukio mengine mengi ya ajabu ambayo yanaweza kuwapata wanawake walio kwenye hedhi wakiwa kwenye mahekalu hayo."
Na sio tu wanawake wenye hedhi walioathiriwa, kulingana na tovuti hiyo ilitangaza kwamba "wakazi karibu na hekalu wanaweza kuathiriwa na majanga ya asili na magonjwa" yaliyosababishwa na wanawake kuingia hekaluni wakiwa kwenye kipindi cha Hedhi.
Ripoti Mpya: Madaktari wa Kike hatarini KujiuaAfyaclass Forum •
Ripoti Mpya: Madaktari wa Kike hatarini Kujiua
Dar es Salaam. Leo Machi 30 dunia ikiadhimisha siku ya madaktari duniani, Ripoti mpya inaonyesha madaktari wa kike wana uwezekano wa asilimia 76 zaidi ya kufariki dunia kwa kujiua ikilinganishwa na wanawake wengine.
Madaktari hutumia zaidi ya miaka saba kupata maarifa chuoni na hutumia sehemu kubwa au yote ya maisha yao kutoa huduma za afya usiku na mchana.
Taarifa iliyotolewa leo Jumapili, Machi 30, 2025 na Shirika la Afya Duniani (WHO), imeeleza mzigo mkubwa wa kazi, mishahara midogo, mazingira hatarishi na unyanyapaa huwafanya wengi kuteseka kimyakimya.
Imeeleza WHO inaheshimu kujitolea kwa madaktari kote duniani, huku ikitambua janga tulivu linalowakumba.
Amesema madaktari duniani wanakabiliwa na viwango vya juu vya kuchoka kazini, msongo wa mawazo, wasiwasi na hata kujiua. Wanajitolea maisha yao kuponya wengine, lakini afya yao ya akili mara nyingi haizingatiwi.
"Ripoti inaonyesha madaktari wa kike wana uwezekano wa asilimia 76 zaidi wa kufariki kwa kujiua ikilinganishwa na wanawake wengine.
"Mpaka sasa ni asilimia 35 pekee ya nchi zinazoendesha mipango ya kitaifa ya kusaidia afya ya akili inayohusiana na kazi. Tuitumie siku hii kuongeza uelewa na kusherehekea madaktari kote duniani kwa huduma na kujitolea kwao kila siku," imeeleza taarifa hiyo iliyotolewa na Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Dk Tedros Adhanom Ghebreyesus.
Kutokana na ongezeko la watu duniani na kada hiyo kutopewa umuhimu, WHO inaonya juu ya upungufu wa wahudumu wa afya milioni 11 ifikapo mwaka 2030.
Uhalisia nchini
Licha ya changamoto kadhaa zinazoikabili kada hiyo nchini, bado kutotosheleza kwao, huwalazimu kufanya kazi kupita kiasi na hivyo kutumia muda mwingi kazini.
Madaktari wa upasuaji huathirika zaidi hasa kada nyeti, kwa mujibu wa Rais wa chama cha madaktari wa upasuaji Tanzania, Dk Amani Malima kuna idadi ya wataalamu hao 600 pekee nchini.
Kwa mujibu wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), nchini kuna madaktari waliosajiliwa 14,000 na Baraza la Madaktari Tanganyika (MCT).
"Nchini Tanzania Madaktari wanafanya kazi usiku na mchana kuokoa maisha ya watu katika vituo vya kutolea huduma, wanatimiza wajibu huu mkubwa na adhimu kwa kujitoa mno," amesema Rais wa MAT, Dk Mugisha Nkoronko katika taarifa yake.
Amesema madaktari wanatumia muda mrefu kupata maarifa wakati wakisoma, na wanatumia sehemu kubwa au yote ya maisha yao kutoa huduma stahiki za afya kwa wote wanaozihitaji.
Amesema madaktari wametoa maisha yao kuwa sadaka kwa wananchi wanaopokea huduma zao. Na kwamba wito wao haupimiki.
"Madaktari ni askari wa mstari wa mbele katika vita ya kupambana na adui maradhi, ni viongozi katika maendeleo muhimu ya sekta ya afya na ustawi wa Taifa letu.
"Ninawatakia afya njema na maisha marefu madaktari wote nchini. Ninawakumbusha kutimiza majukumu yao kwa weledi na maadili ya hali ya juu," amesema Dk Nkoronko.
Pamoja na hayo amewahakikishia MAT itaendelea kulinda taaluma ya udaktari kwa wivu mkubwa.
Amesema licha ya changamoto zilizopo kada hiyo itaendelea kutimiza wajibu wake kikamilifu, kila wakati usiku na mchana wakati wote.
Wito
Dk Nkoronko ameziomba mamlaka zote zinazohusika ikiwemo Serikali, kuendelea kuweka mazingira wezeshi kwa madaktari kutimiza wajibu wao na kuwafanya wananchi kote nchini kupata huduma bora za afya.
"Waendelee kuboresha maslahi yao, ikiwemo vitendea kazi na mambo mengine yanayoboresha ustawi wao, kama watu muhimu katika jamii.
"Ninawakumbusha kuendelea kujali afya zao pia maana kazi hii inatuweka kazini masaa mengi, tunakosa muda wa kujihudumia binafsi na kupata msongo, na matatizo ya afya ya akili.
"Nasi pia tunaugua wakati mwingine tunaambukizwa magonjwa na tunaowahudumia. Ni muhimu nasi tuendelee kujikinga kwa magonjwa yote ya tabia bwete na ya kuambukizwa," amesema Dk Nkoronko.
Wizara ya Afya yaingilia kati Sakata la Mama kubadilishiwa mtoto baada ya kujifunguaAfyaclass Forum •
Wizara ya Afya yatoa Ufafanuzi kuhusu Sakata la Mama kubadilishiwa mtoto baada ya kujifungua
Wizara ya Afya imetoa ufafanuzi kuhusu taarifa inayosambaa mitandaoni inayodai kuwa Neema Kilugala, mkazi wa Daraja Mbili mkoani Arusha, alibadilishiwa mtoto baada ya kujifungua kwa njia ya upasuaji katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Arusha, Mount Meru, mnamo Machi 24, 2025.
Kwa mujibu wa Neema, baada ya kujifungua, alioneshwa mtoto wake akiwa mzima na muuguzi aliyemhudumia. Hata hivyo, alipomletewa mtoto wake baadaye, alibaini kuwa alikuwa amefungwa vitenge visivyo vyake, hali iliyozua wasiwasi.
Muuguzi aliyekuwa akihudumu hospitalini hapo alidai kuwa kulikuwa na mkanganyiko wa vitenge, na kwa kutambua hali hiyo, alijaribu kurekebisha tatizo hilo. Wizara ya Afya, kwa kushirikiana na uongozi wa hospitali, Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha na Jeshi la Polisi, imechukua hatua za haraka kuchunguza suala hilo, ikiwemo:
(1) Kuchukua sampuli za vinasaba (DNA) kwa wazazi waliojifungua wakati huo pamoja na za watoto wao ili kubaini ukweli katika ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali.
(2) Kumsimamisha kazi muuguzi husika ili kupisha uchunguzi.
Wizara ya Afya imesisitiza kuwa uchunguzi wa kina utafanyika, na mara utakapokamilika, taarifa rasmi itatolewa na hatua stahiki kuchukuliwa.
Kusitishwa kwa ufadhili wa Marekani na Athari kwa Ugonjwa wa Ukimwi;UNAIDSAfyaclass Forum •
Kusitishwa kwa ufadhili wa Marekani na Athari kwa Ugonjwa wa Ukimwi;UNAIDS
Shirika la Umoja wa Mataifa la kupambana na ukimwi UNAIDS leo limeonya kwamba kusitishwa kwa ufadhili wa Marekani sio tu janga kwa vita dhidi ya gonjwa hilo bali ni chachu ya vifo na ongezeko la maambukizi mapya. Flora Nducha amefuatilia onyo hilo lililotolewa leo mjini Geneva Uswisi na Mkurugenzi mtendaji wa UNAUDS Winnie Byanyima alipozungumza na waandishi wa habari.
Bi. Byanyima amewaambia waandishi wa habari kwamba serikali ya Marekani imekuwa mfadhili mkubwa wa mipango ya kukabiliana na UKIMWI, hasa kupitia Mpango wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kupambana na UKIMWI (PEPFAR).
Hata hivyo, kukatwa kwa msaada wa kifedha sasa kunahatarisha programu muhimu zinazotoa matibabu ya kuokoa maisha, huduma za kuzuia maambukizi, na utafiti wa kisayansi hasa kwa nchi ambazo msaada huo ni tegemeo kubwa mathalani amesema.
UNAIDS inatahadharisha kuwa bila msaada wa kifedha wa kutosha, mamilioni ya watu, hasa katika nchi zenye kipato cha chini, wanaweza kukosa huduma muhimu za UKIMWI na hasa wale wanaotegemea dawa za kupunguza makali ya ugonjwa huo ili kuendelea kuishi akisema “Hata kufurugwa kwa muda mfupi kwa matibabu kuna athari kubwa kwa watu wanaoishi na HIV. Endapo mtu ataruka kunywa dozi kutamsababishia usugu wa dawa , hii itaongeza idadi ya virusi, na hii itaongeza maambukizi.”
Bi Winnie amesema waathirika wakubwa katika zahma hii ya ukataji ufadhili ni jamii zilizo hatarini, zikiwemo wanawake, watoto, na makundi yaliyotengwa ambayo tayari yanakumbwa na changamoto za kupata huduma za afya hususan Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, ambako kiwango cha maambukizi ya UKIMWI bado ni cha juu, na hivyo kupungua kwa msaada wa kifedha kunaweza kufuta mafanikio yaliyopatikana katika kupunguza maambukizi na kuboresha upatikanaji wa matibabu.
Ametoa wito wa kuchukuliwa hatua za haraka ili kuzuia kurudi nyuma kwa maendeleo katika juhudi za kimataifa za kumaliza janga la UKIMWI ifikapo 2030.
UNAIDS na mashirika mengine ya afya duniani yameitaka serikali ya Marekani kufikiria upya uamuzi wake wa kupunguza ufadhili, yakisisitiza kuwa uwekezaji endelevu ni muhimu ili kuendelea kupiga hatua katika mapambano dhidi ya UKIMWI.
Tathimini ya bara la Afrika
Akizungumzia Afrika ambako Mashariki na Kusini mwa bara hilo kunabeba asilimia 53 ya mzigo wa VVU duniani Bi. Byanyima ameonya kwamba kufunga ghafla vituo vya msaada kwa wasichana na wanawake vijana kutakuwa na madhara makubwa, kwa sababu zaidi ya asilimia 60 ya maambukizi mapya ya VVU barani humo yanawaathiri wasichana na wanawake vijana.
Akizungumza na UN News mapema mwezi huu, mkuu wa ofisi ya UNAIDS nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, Susan Kasedde, alisema bado kuna maswali makubwa kuhusu kiwango na upeo wa kupunguzwa kwa ufadhili wa mpango wa PEPFAR wa Marekani.
Mpango huu, ulioanzishwa mwaka 2003, unalenga kuzuia na kudhibiti maambukizi ya VVU ukiwa ni mpango wa dharura wa urais wa Marekani ambao unakadiriwa kuwa umeokoa maisha ya takriban watu milioni 26.
Kwa sasa, kuna takriban watu 520,000 wanaoishi na VVU nchini DRC, wakiwemo wanawake 300,000 na watoto 50,000. Janga hili linaendelea kukua, kwani idadi ya maambukizi mapya karibu inazidi mara mbili idadi ya vifo vinavyohusiana na ugonjwa huo.
Kwa mujibu wa UNAIDS Mchango wa PEPFAR uliotarajiwa kwa mwaka wa kifedha wa 2025 ulikuwa ni dola milioni 105, na unalenga kutoa matibabu kwa nusu ya watu wanaoishi na VVU nchini DRCambao ni takriban watu 209,000.
"Hii inamaanisha kuwa kwa sasa tuna watu 440,000 wanaoishi na VVU ambao wanapata matibabu. Kupitia matibabu haya, wanaendelea kuishi," alisema Bi. Kasedde.
Aliongeza kuwa "Na matibabu haya hayawezi kufanikiwa bila uwezo wa kiutendaji. Matibabu hayawezi kutolewa ikiwa hakuna mnyororo wa ugavi unaofanya kazi ipasavyo," alisisitiza, akionyesha kuwa hatua dhidi ya VVU nchini DRC zinategemea kwa kiasi kikubwa programu zinazoingiliana na kusaidiana.
Nilikuwa Chanzo cha makovu ya ngozi kwa wananguAfyaclass Forum •
Nilikuwa Chanzo cha makovu ya ngozi kwa wanangu
Maelezo ya picha,Mmoja wa binti za Fatima ana mabaka kwenye midomo yake
Fatima, Mwanamke mwenye umri wa miaka 32 alitumia vipodozi vya kung'arisha ngozi kwa watoto wake wote sita, chini ya shinikizo kutoka kwa familia yake, na sasa matokeo yake anayajutia sana.
Binti mmoja hufunika uso wake kila anapotoka nje, ili kuficha kuungua kwa ngozi yake.
Mwingine aliachwa na ngozi nyeusi kuliko hapo awali, na mduara wa rangi karibu na macho yake, Fatima anasema, wakati wa tatu akiwa na makovu meupe kwenye midomo na magoti yake. Mtoto wa miaka miwili bado ana majeraha - ngozi yake imechukua muda mrefu kupona.
"Dada yangu alizaa watoto wenye ngozi nyeupe lakini watoto wangu wana ngozi nyeusi. Niligundua kuwa mama yangu anawapendelea watoto wa dada yangu kuliko wangu kwasababu ya rangi yao ya ngozi na iliniumiza sana hisia zangu," Fatima anasema.
Anasema alitumia krimu alizonunua kwenye duka la karibu, bila agizo la daktari.
Maelezo ya picha,Majeraha ya mtoto mdogo yanapona polepole sana
Mwanzoni ilionekana kufanya kazi. Bibi yao aliwakumbatia watoto wa Fatima, ambao walikuwa na umri wa kati ya miaka miwili na 16 wakati huo. Lakini baadaye wakaanza kuungua na makovu yalianza kujitokeza wazi.
Vipodozi vya Kung'arisha ngozi au kuifanya iwe nyeupe pia hujulikana kama bleaching nchini Nigeria, na hutumiwa katika sehemu mbalimbali za dunia kwasababu za urembo, ingawa tafiti zinaonyesha mara nyingi vipodozi hivyo hutengenezwa majumbani.
Wanawake wa Nigeria hutumia bidhaa za kung'arisha na kuchubua ngozi zaidi kuliko nchi nyingine barani Afrika - 77% kati yao hutumia vipodozi hivi mara kwa mara, kulingana na Shirika la Afya Duniani (WHO).
Nchini Kongo-Brazzaville idadi ni 66%, nchini Senegal 50% na Ghana 39%.
JE,UNAFAHAMU ATHARI ZA VITU HIVI? TUPE MTAZAMO WAKO HAPA CHINI
Credits:BBC,WHO
Mwanaume wa kwanza duniani kupandikiziwa chipu kwenye ubongo Afunguka hayaAfyaclass Forum •
Mwanaume wa kwanza duniani kupandikiziwa chipu kwenye ubongo Afunguka haya!
Mwanaume wa kwanza duniani kupandikiziwa chipu ya kusoma mawazo kwenye ubongo wake kupitia kampuni ya Elon Musk ya Neuralink ameanza kushuhudia matokeo ya teknolojia hiyo ya kisasa ambapo teknolojia hii inadaiwa kuwa hatua kubwa katika utafiti wa muingiliano kati ya Ubongo wa Binadamu na kompyuta ikilenga kusaidia Watu wenye ulemavu wa mwili kuwasiliana na mazingira yao kwa urahisi zaidi.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka Neuralink chipu hiyo imewekwa kwa mafanikio na tayari inatoa ishara kuwa inaweza kuchukua mawazo ya Mtumiaji na kuyatafsiri katika mfumo wa kidijitali, Mwanaume huyo ambaye jina lake halijatajwa ameripotiwa kuwa anaweza kutumia akili yake kuendesha mifumo ya kompyuta bila kugusa kifaa chochote, jambo linaloonekana kama mapinduzi makubwa katika sayansi ya neva na uhandisi wa matibabu.
Elon Musk ambaye ndiye mwanzilishi wa Neuralink ameeleza kuwa chipu hii inalenga kusaidia Wagonjwa walio na matatizo ya mfumo wa neva kama vile wale waliopooza kutokana na ajali au maradhi pia Musk amedokeza kuwa teknolojia hii inaweza kusogea mbele zaidi na hatimaye kuruhusu mawasiliano ya moja kwa moja kati ya akili za Binadamu kupitia mawazo pekee jambo linaloashiria mabadiliko makubwa katika mawasiliano ya Binadamu.
Ingawa hatua hii imeibua matumaini makubwa Wataalamu wa afya na maadili wanaendelea kujadili athari na changamoto zinazoweza kujitokeza, ikiwemo masuala ya faragha ya mawazo na matumizi sahihi ya teknolojia hii katika Jamii vilevile wanatazamua mafanikio haya kuwa yanaweka msingi wa maendeleo mapya katika sayansi na tiba ya mfumo wa fahamu.
UNA MTAZAMO GANI JUU YA HILI,SHARE MAWAZO YAKO CHINI YA COMMENT SECTION,KARIBU DISCUSSION CORNER.
Siku ya hali ya hewa duniani, tarehe 23 MachiAfyaclass Forum •
Siku ya hali ya hewa duniani, tarehe 23 Machi
Jana tarehe 23 Machi ilikuwa siku ya hali ya hewa duniani, Tafiti mbali mbali Zinaonyesha kila mwaka kwa kipindi cha miaka kumi iliyopita kumerikodiwa hali ya joto kali zaidi katika historia ya Dunia,
Pia kuna mifano ya namna mataifa mbali mbali yalivyoathirika kwa majanga kama vile moto wa msituni, mafuriko, vimbunga vikali na dhoruba zisizotarajiwa.
“Katika zama hizi za maafa yasababishwayo na tabianchi, kila mtu duniani anapaswa kulindwa na mfumo wa tahadhari ya mapema kama haki ya msingi. Pamoja, lazima tuchukue hatua sasa.”
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameeleza “bado karibu nusu ya nchi duniani hazina mifumo ya kutabiri majanga na kuwaonya wananchi mapema. Ni jambo la aibu kwamba katika enzi hii ya kidijitali, watu bado wanapoteza maisha na riziki kwa sababu hawana mifumo madhubuti ya tahadhari ya mapema.”
Mpango wa Umoja wa Mataifa wa Tahadhari za Mapema kwa Wote unalenga kuhakikisha kuwa kila mtu, kila mahali, analindwa na mfumo wa onyo ifikapo mwaka 2027. Na ili kuhakikisha hili linafikiwa Guterres amependekeza mambo kadhaa yafanyike.
Tunahitaji msaada wa kisiasa wa kiwango cha juu kwa mpango huu ndani ya nchi, msaada wa kiteknolojia, ushirikiano mkubwa kati ya serikali, wafanyabiashara, na jamii, pamoja na juhudi kubwa za kuongeza fedha.
Kuimarisha uwezo wa kukopesha wa Benki za Maendeleo ya Kimataifa ni hatua muhimu. Mkataba wa Baadaye (Pact for the Future) uliokubaliwa mwaka 2024 ulifanya maendeleo makubwa, lakini lazima utekelezwe kikamilifu. Vivyo hivyo, matokeo ya fedha ya COP29 lazima yahakikishwe.
Na mwisho ameeleza juhudi za kukabiliana na mgogoro wa tabianchi lazima ziongezwe kwa haraka. Inahitajika kupunguza kwa kina na haraka utoaji wa gesi chafuzi ili kuzuia hali kuwa mbaya zaidi. Mwaka huu, nchi zote zinapaswa kutimiza ahadi zao za kuwasilisha mipango mipya ya kitaifa ya kukabiliana na tabianchi, mipango ambayo inazingatia lengo la kuzuia ongezeko la joto la dunia lisizidi nyuzi joto 1.5°C.
WEWE UNAFIKIRI NINI KIFANYIKE ILI KUKABILIANA NA MABADILIKO HAYA MAKUBWA YA HALI YA HEWA?
Kusambaratika kwa programu za kuzuia na kukabiliana na HIVAfyaclass Forum •
Kusambaratika kwa programu za kuzuia na kukabiliana na HIV
Uamuzi wa Serikali ya Trump kusitisha misaada ya kigeni iliyokuwa ikisimamiwa na Shirika la misaada la Marekani USAID imeathiri usambazaji na matibabu ya virusi vya VVU kwa nchi nyingi, ambazo kutakuwa na uhaba wa dawa za kupunguza makali ya virusi hivi, Shirika la Afya duniani WHO laonya.
Kusambaratika kwa programu za kuzuia na kukabiliana na HIV huenda kukalemaza juhudi zilizoafikiwa ndani ya miaka 20 ,'' Mkurugenzi Mtendaji wa WHO Tedros Adhanom Ghebreyesus amesema hayo katika kikao na wanahabari.
Alisema kuwa Shirika hilo lina wasiwasi kwani upungufu wa dawa hizi za VVU utasababisha maambukizi mapya milioni 10 na vifo milioni tatu vilivyochochewa na makali ya VVU.
Juhudi za kukabiliana na magonjwa kama vile VVU, Malaria, Kifua kikuu na Polio zimeathirika pakubwa baada ya Trump kusitisha misaada ya kigeni iliyoelekezwa kwa programu hizo dakika chache baada ya kuingia katika ikulu ya White House.Via Bbc
KARIBU DISCUSSION CORNER,WEKA MTAZAMO WAKO HAPA KWENYE COMMENT SECTION,JUU YA HILI
Mara ya Mwisho kutumia dawa za Minyoo ni Lini?Afyaclass Forum •
WHO yaonya maambukizi mapya ya HIV na Vifo kuongezeka baada ya ARVs kusitishwaAfyaclass Forum •
WHO yaonya maambukizi mapya ya HIV na Vifo kuongezeka baada ya ARVs kusitishwa
Shirika la Afya Duniani (WHO) limeonya maambukizi mapya ya HIV zaidi ya milioni 10 na vifo vya Watu milioni 3 vinavyohusiana na UKIMWI vinaweza kushuhudiwa kufuatia kusitishwa kwa msaada wa kigeni wa Marekani unaosaidia upatikanaji wa dawa za kufubaza makali ya virusi vya UKIMWI, ARVs.
Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Tedros Adhanom Ghebreyesus WHO amesema hatua ya Marekani kujiondoa kusaidia mapambano ya HIV imeathiri usambazaji wa dawa katika nchi saba za Afrika, zikiwemo Kenya, Lesotho, Sudan Kusini, Burkina Faso, Mali, Nigeria, na Haiti, ambazo zinaweza kuishiwa dawa ndani ya miezi michache ijayo.
Dr. Tedros amesema kusitishwa kwa msaada huo wa Marekani kunaweza kufuta mafanikio ya miaka 20 katika kupambana na HIV huku pia akionya kuwa juhudi za kudhibiti magonjwa mengine kama polio, malaria, na kifua kikuu zimeathirika vibaya na ameiomba Marekani kuhakikisha kuwa inatoa muda wa mpito kwa nchi zilizoathirika ili ziweze kupata vyanzo mbadala vya fedha badala ya kusitisha msaada kwa ghafla, hatua ambayo inaweza kusababisha madhara makubwa ya kiafya duniani.
Itakumbukwa Rais wa Marekani, Donald Trump alitangaza mwezi huu kusitisha kutoa fedha za misaada kupitia miradi iliyokuwa chini ya Shirika lake la misaada la USAID, hali iliyoibua taharuki hasa kwa nchi nyingi za Afrika zinazotegemea fedha za ufadhili kushughulika na magonjwa kama Ukimwi.
KARIBU DISCUSSION CORNER,WEKA COMMENT YAKO HAPA CHINI JUU YA MADA HII
#Afya News




















.jpg)



.jpeg)


