Showing posts with label Vita vya Israel na Hamas. Show all posts
Showing posts with label Vita vya Israel na Hamas. Show all posts

Madaktari kote Gaza wanafanya upasuaji kwa wagonjwa bila ganziAfyaclass Forum •

#PICHA:Mwanaume aliyejeruhiwa amelazwa kwenye kitanda katika hospitali ya Gaza European hospital toka mwishoni mwa Disemba.

Madaktari kote Gaza wanafanya upasuaji kwa wagonjwa bila ganzi,

Madaktari wa Gaza wanasema: ‘Tunawaacha wagonjwa wakipiga kelele masaa kwa masaa’.

Madaktari wa Gaza wameelezea jinsi unavyofanyika upasuaji kwa wagonjwa bila ganzi, ili kuwaondoa watu wenye hali sugu, na kutibu majeraha yanayooza kwa vifaa vichache vya matibabu vilivyopo.

“Kwa sababu ya uhaba wa dawa za kutuliza maumivu tunawaacha wagonjwa wakipiga kelele kwa saa na saa,” mmoja aliambia BBC.

Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) limeelezea hali ya huduma za afya huko Gaza kuwa ni mbaya sana “wametumia maneno haya(beyond words)”.

WHO; Ilisema hospitali 23 huko Gaza hazifanyi kazi hata kidogo hadi Jumapili – 12 zilikuwa zikifanya kazi kwa kiasi na moja kwa kiwango cha chini sana.

Shirika la afya lilisema mgomo wa anga na ukosefu wa vifaa “umemaliza mfumo ambao tayari hauna rasilimali”.

WHO inasema hospitali ya Nasser, iliyovamiwa na IDF, haifanyi kazi

Jeshi la Ulinzi la Israel (IDF) linasema Hamas “kwa chinichini hutumia hospitali na vituo vya matibabu kwa shughuli zake za kigaidi”.

Katika taarifa yake kwa BBC, ilisema IDF “haikushambulia” hospitali, lakini badala yake waliingia katika maeneo maalum… [ili] kuharibu miundo mbinu na vifaa vya Hamas, na kuwakamata magaidi wa Hamas, huku wakifanya kazi kwa tahadhari kubwa”.

IDF Ilisema ilikuwa ikiruhusu misaada ya kibinadamu kuingia Gaza, pamoja na vifaa vya matibabu.

Mashirika ya misaada, ikiwa ni pamoja na WHO, yanasema kumekuwa na “vizuizi vya mara kwa mara vya ufikiaji na kunyimwa kwa huduma”.

Onyo: Makala haya yana maelezo ambayo baadhi ya wasomaji wanaweza kukasirika lakini lengo ni ili kupata Taarifa na kujua hali ya kiafya ilivyo kwa sasa GAZA.

Hii ni kwa mujibu wa Taarifa kutoka WHO, BBC pamoja na mashirika mengine..!!!

Madaktari kote Gaza wanafanya upasuaji kwa wagonjwa bila ganzi
0 Comment

Vita vya Isreal-Hamas: Mtangazaji wa habari wa Israeli amebeba bunduki akiwa hewani kwenye studio (Picha)Afyaclass Forum •

Vita vya Isreal-Hamas: Mtangazaji wa habari wa Israeli amebeba bunduki akiwa hewani kwenye studio (Picha).

Mtangazaji wa habari wa Israel alionekana akiwa na bunduki moja kwa moja hewani alipokuwa akiwasilisha habari kutoka studio huku kukiwa na hofu ya shambulio jingine la Hamas.

Lital Shemesh, mtangazaji wa kituo cha utangazaji cha mrengo wa kulia cha Israel Channel 14, alipigwa picha siku ya Jumanne, Januari 2, akiwa ameketi nyuma ya meza yake huku bunduki ikiwa imewekwa kiunoni mwa suruali yake.

Bunduki ya Shemesh iko karibu kabisa na vipokezi vya maikrofoni yake huku akiwa amekaa kwenye ukingo wa kiti chake cha utangazaji.

Chapisho lake la hivi majuzi kwenye mtandao wa kijamii lilimuonyesha akifanya mazoezi ya ustadi wake wa kufyatua risasi kwenye safu ya bunduki huku akitoa wito kwa watu ‘kutoa bunduki zao’.

Pia alichapisha picha kadhaa akiripoti kutoka mstari wa mbele na pia akiwa amevalia sare za askari wake.

Mwandishi huyo wa habari na askari wa akiba wa Jeshi la Ulinzi la Israel (IDF) amezungumza hapo awali kuhusu kupambana na Hamas.

“Nchi nzima inaajiriwa kupigana vita hivi dhidi ya ugaidi, kupigana vita hivi dhidi ya Hamas,” Shemesh aliiambia Fox News muda mfupi baada ya shambulio la Oktoba 7.

‘Hatujaona mauaji kama haya katika Israeli katika miaka 75 ya kuwepo kwa Israeli. Haya ni maangamizi makubwa ya pili kwetu.’

Haya yanajiri huku hofu ya kutokea mashambulizi mengine ya Hamas ikizidi kuongezeka baada ya kundi hilo la kigaidi kuwaua watu 1,140 wengi wao wakiwa raia wakati wa shambulio lao la Oktoba 7, kulingana na hesabu iliyotokana na takwimu rasmi za Israel.

Vita vya Isreal-Hamas: Mtangazaji wa habari wa Israeli amebeba bunduki
akiwa hewani kwenye studio (Picha)
0 Comment

WHO:Hatari kubwa ya Magonjwa ya mlipuko Kusambaa GazaAfyaclass Forum •

WHO:Hatari kubwa ya Magonjwa ya mlipuko Kusambaa Gaza.

Shirika la Afya Duniani WHO linaangaza athari mbaya za mzozo unaoendelea likisema kuna hatari kubwa ya magonjwa ya milipuko kusambaa.

Tangu Oktoba 7, 2023 mapigano yalipoanza, kumekuweko na wagonjwa 179,000 wa magonjwa ya njia ya hewa, wagonjwa 136,000 wa kuhara miongoni mwa watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano, na wagonjwa 55,400 wa vidonda na chawa.

Tangu shambulio la Hamas dhidi ya Israel tarehe 7 Oktoba 2023, lililosababisha vifo vya watu 1,200 na wengine 240 watekwe nyara, mapigano kwenye ukanda wa Gaza, na mashambulizi kutoka angan ina ardhini  na vile vile baharini yanayofanywa na jeshi la Israel (IDF) yamesababisha vifo vya zaidi ya watu 22,000 wengi wao wakiwa ni wanawake na watoto, kwa mujibu wa maafisa wa afya wa Palestina.

Takwimu za IDF zilizotolewa Desemba 30, 2023 zinadokeza kuwa askari 168 wa Israel wameuawa tangu kuanza kwa operesheni za kijeshi za ardhini huko Gaza na wengine 955 wamejeruhiwa.

Wizara ya afya Gaza nayo inaripoti kuwa zaidi ya wapalestina 200 wameripotiwa kuuawa tangu jana jumatatu pekee hadi leo, huku wengine 338 wamejeruhiwa.

Maelfu wahofiwa kufa

Wakati huo huo, WHO katika taarifa yake mpya inasema watu wengine 7,000 kwa sasa hawajulkani waliko au wamefukiwa kwenye vifusi.

Ripoti hiyo pia inasema watu 600 wameuawa kufuatia mashambulizi 300 kwenye hospitali tangu Oktoba 7, mashambulizi ambayo yameharibu hospitali 26 na magari ya wagonjwa 38.

Kati ya watu milioni 1.93 waliofurushwa makwao Gaza, 52,000 ni wajawazito ambao wanajifungua watoto 180 kila siku, kwa mujibu wa WHO. Imeelezwa pia wagonjwa 1,100 wanahitaji huduma ya kusafisha figo kila siku, 71,000 ni wagonjwa wa kisukari na 225,000 wanahitaji tiba dhidi ya shinikizo la damu.

WHO:Hatari kubwa ya Magonjwa ya mlipuko Kusambaa Gaza
0 Comment

Damu imetapakaa kila mahali kwenye hizi hospitali:CaseyAfyaclass Forum •

PICHA: Mvulana mwenye umri wa miaka 3, ambaye nyumba yake ilishambuliwa kwa bomu, anapata nafuu katika hospitali ya Nasser baada ya kukatwa sehemu ya mguu wake wa kulia.

Wahudumu wa afya huko Ukanda wa Gaza Jana jumanne wameendelea na kazi ya kuokoa maisha ya manusura wa mashambulio ya makambora yakiwemo mashambulio karibu na kambi ya wakimbizi kwenye eneo hilo lililozingirwa na Israel, mashambulio ambayo yameripotiwa kuua zaidi ya watu 100, limesema shirika la afya, WHO.

Mratibu wa Timu ya Matabibu wa Dharura Sean Casey amesema wagonjwa zaidi ya 100 walifikishwa Jumatatu kwenye hospitali ya Al-Aqsa ndani ya muda wa dakika 30, kufuatia milipuko karibu na kambi ya wakimbizi ya Al-Maghazi.

Wagonjwa wote hao walikuwa wanahitaji matibabu ya dharura wakiwa na majeraha makubwa,  amesema Afisa huyo wa WHO akizungumza na Idhaa ya Umoja wa Mataifa.

Amesema huku wagonjwa hao wakiletwa hospitali, takribani maiti wengine 100 walifikishwa muda huo huo.

Wamenasa chini  ya vifusi

Nayo Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya haki za binadamu, OHCHR, imeelezea wasiwasi wake mkubwa juu ya mashambulizi makubwa ya mabomu yanayoendelea kufanywa na jeshi la Israel katikati ya Gaza, ambapo zaidi ya mashambulizi 50 kutoka angani yameripotiwa kufanyika tangu tarehe 24 mwezi huu wa Desemba.

Mashambulio hayo yameripotiwa kuua zaidi ya wapalestina 100 tangu siku hiyo ambapo OHCHR inasema, “hii inatia zaidi wasiwasi kwa ripoti ya kwamba jeshi la Israel limeagiza wakazi walioko kusini mwa eneo la Wadi Gaza, wahamie eneo la kati la Gaza na Tal a-Sultan.”

Kambi tatu za wakimbizi zilipigwa kwa makombora, amesema msemaji wa OHCHR, Seif Magango kwenye taarifa iliyotolewa leo, akitaja kambi hizo kuwa ni Al Bureij, Al-Nuseirat na Al-Maghazi.

“Makombora mawili yalipiga makazi sav ana kuua tarkibani wapalestina 86 na kujeruhi wengine wengi,” amesema Magango huku akiongeza kuwa, “idadi isiyojulikana ya watu yaaminika wamefukiwa kwenye vifusi.”

Tedros achukizwa

Kupitia ukurasa wake kwenye mtandao wa X (zamani ukijulikana kama Twitter) Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Dkt. Tedros Ghebreyesus amelaani mauaji yanayosababishwa na mashambulizi ya kutoka angani yanayofanywa na jeshi la Israel dhidi ya Gaza ikiwa ni kisasi cha mashambulizi yaliyofanywa na Hamas tarehe 7 mwezi Oktoba mwaka huu. Takribani watu 1,200 waliuawa na wengine 240 walitekwa nyara siku hiyo.

“WHO ina wasiwasi mkubwa juu ya mzigo mkubwa kwa hospitali chache zinazoendelea kutoa huduma kwenye eneo hilo kutokana na kuendelezwa kwa chuki kati ya pande mbili hizo. Hospitali zilizosalia wazi ni chache ambapo nyingi zao uwezo wa kutoa huduma uko taabani,” alisema Dkt. Tedros siku ya Jumatatu.

Kupitia ukurasa wake wa X, Bwana Casey ameelezea hali katika hospitali ya Al-Aqsa kuwa ni dimbwi la damu. Alionesha Ahmed, mvulana mwenye umri wa miaka tisa ambaye alikuwa amalala kwenye sakafu ya hospitali hiyo baada ya kujeruhiwa kwa kiasi kikubwa na mlipuko wakati akivuka mtaa mmoja karibu na Nuseirat.

“Tumeona watoto, wanawake, vijana wa kiume, wazee wakivuja damu,” amesema Bwana Casey, huku akiongeza kuwa wagonjwa hawawezi kuhamishiwa eneo lingine kwa ajili ya matibabu ya kuokoa maisha yao.

“Damu imetapakaa kila mahali kwenye hizi hospitali. Tunaona wagonjwa wako na viwewe, damu kila mahali, tulishasema, ni mauaji.”

Shule ya Nuseirat iliyoko Gaza Kati inayoendeshwa na UNRWA sasa ni makazi ya maelfu ya watu waliofurushwa makwao kutokana na mashambulizi yanayoendelea Gaza.

Mapigano usiku kucha

“Hakuna mahali salama Gaza,” amesema Bwana Casey. “Hivi sasa hapa Rafah nje ya mlango wa jengo hili niliko, meta 50 hivi, kuna kambi ya maelfu ya watu ambao wamesaka hifadhi hapa. …wanaishi kwenye makazi yaliyofunikwa kwa karatasi za nailoni. Jana usiku tulisikia mashambulizi usiku kucha huku kukiwa na ripoti za kuweko kwa majeruhi wengi, wakipelekwa hospitali zilizoko hapa kusini.”

Uwezo wa hospitali Gaza hivi sasa ni takribani asilimia 20 ya kabla ya tarehe 7 Oktoba mashambulizi yalipoanza. “Takribani hospitali zote zimeacha kufanya kazi.”

Wanasubiri kufa

Bwana Casey amezungumzia pia wagonjwa walioko mahututi huko Gaza Kaskazini ambao kwa sasa wanasubiria kufa tu kwani hospitali ya mwisho iliyokuwa inatoa huduma imefungwa na sasa wako kwenye viwanja vya kanisa wakilala kwenye viti.

“Kiwango cha uharibifu ni kikubwa, barabara zimesheheni vifusi hivyo ni vigumu kufikia wahitaji.”

“Bado tunahitaji kuchukua hatua zaidi kusafirisha hawa wagonjwa, lakini fursa ya kufanya hivyo inazidi kuwa fingu kila uchao kwani ufikiaji wa hospitali ni mgumu,” amesema Bwana Casey.

Kwa mujibu wa Wizara ya Afya Gaza, takribani watu 20,000 yaaminika wameuawa tangu kuanza kwa mapigano Oktoba 7, mwaka huu.

Damu imetapakaa kila mahali kwenye hizi hospitali:Casey
0 Comment

Israel Yaomboleza Vifo Vya Mateka Wa Israel Waliouawa Kimakosa Na Jeshi LakeAfyaclass Forum •

Israel Yaomboleza Vifo Vya Mateka Wa Israel Waliouawa Kimakosa Na Jeshi Lake

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu, ameyataja mauaji ya mateka hao kuwa ni “janga lisilovumilika” na kuahidi kuendelea “kwa juhudi kubwa za kuwarejesha mateka wote nyumbani wakiwa salama”.

Israel inaomboleza vifo vya mateka watatu wa Israel waliouawa kimakosa na wanajeshi wa Israel wakati wa operesheni yake ya ardhini katika Ukanda wa Gaza.

Msemaji mkuu wa jeshi hilo, Admirali Daniel Hagari, amesema vikosi vya Israel viliwatambua kimakosa mateka hao kama tishio, na kuwafyatulia risasi Ijumaa. Alisema kuwa haijafahamika iwapo mateka hao waliwatoroka watekaji wao, au walikuwa wametelekezwa.

Vifo vyao vilitokea katika eneo la Shijaiyah huko Gaza City, eneo la mapigano ya umwagaji damu kati ya jeshi la Israel na wanamgambo wa Hamas. Alisema jeshi limeelezea masikitiko makubwa na linafanya uchunguzi.

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu, ameyataja mauaji ya mateka hao kuwa ni “janga lisilovumilika” na kuahidi kuendelea “kwa juhudi kubwa za kuwarejesha mateka wote nyumbani wakiwa salama”.

Israel Yaomboleza Vifo Vya Mateka Wa Israel Waliouawa Kimakosa Na Jeshi
Lake
0 Comment

Serikali ya Israel yaijulisha Tanzania kuwa Mtanzania Joshua Mollel aliuawa na Hamas Afyaclass Forum •

Serikali ya Israel yaijulisha Tanzania kuwa Mtanzania Joshua Mollel aliuawa na Hamas.

Serikali ya Israel imeijulisha Tanzania kuwa Mtanzania Joshua Mollel aliyekuwa anasoma nchini Israel aliuawa mara tu baada ya kutekwa na kundi la Hamas 7 Oktoba 2023.

Taarifa hiyo imetolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba ambapo ameeleza kuwa

“kwa sasa Serikali inaendelea na mpango wa awali wa kuwapeleka Mzee Mollel na mwanafamilia mwingine pamoja na Afisa wa Serikali nchini Israel, kuungana na Balozi wetu na maafisa waliopo huko,

kukutana na kuzungumza na mamlaka za nchi hiyo ili kupata taarifa za ziada.” Ameandika Waziri katika mitandao ya kijamii.

Serikali ya Israel yaijulisha Tanzania kuwa Mtanzania Joshua Mollel
aliuawa na Hamas
0 Comment

Israel yawatambua Watanzania wanaoshikiliwa mateka na HamasAfyaclass Forum •

Serikali ya Israel imethibitisha utambulisho wa watu wawili kutoka Tanzania wanaoaminika kushikiliwa na Hamas tangu shambulio la Oktoba 7 dhidi ya jamii za kusini mwa Israel, karibu na mpaka na Gaza.

Joshua Loitu Mollel na Clemence Felix Mtenga walikuwa nchini Israel kama sehemu ya programu ya mafunzo ya kilimo, kulingana na taarifa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Israel.

“Walitekwa nyara na magaidi wa Hamas na wanazuiliwa mateka huko Gaza,” ujumbe huo ulisema. “Tafadhali ungana nasi kuwaombea warudi salama na mara moja.”

Mollel na Mtenga walikuwa sehemu ya kundi la wanafunzi waliokuwa wakiishi Kibbutz Nahal Oz. Walikuwa wametoweka tangu mashambulizi hayo, lakini Israel ilikuwa bado haijathibitisha utambulisho wao au kuripoti kilichowapata.

Tanzania ilisema Alhamisi kuwa inafahamu kuhusu wanafunzi wawili waliopotea ambao ni sehemu ya kundi la Watanzania 260 nchini Israel, lakini bado haijathibitisha walipo. Watanzania tisa waliokuwa Israel walirejea nyumbani Oktoba 18.

BBC hapo awali ilizungumza na familia ya mmoja wao, Joshua Mollel, ambaye ni mmoja wa mwanafunzi hao lakini ikasema haikuwa imewasiliana naye tangu wakati wa shambulio hilo.

Habari hizo zinakuja huku kukiwa na majadiliano ya pendekezo la Hamas la kuwaachilia mateka. Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Hossein Amirabdollahian, alisema wiki iliyopita kwamba Hamas iko tayari kuwaachilia mateka lakini “ulimwengu unapaswa kuunga mkono kuachiliwa kwa Wapalestina 6,000” ambao wamekuwa wakishikiliwa katika jela za Israel.

“Viongozi wa vuguvugu la ukombozi la Hamas wametangaza kuwa tayari kuwaachilia wafungwa wasiokuwa wanajeshi na Iran, Uturuki na Qatar ziko tayari kutekeleza jukumu lao katika juhudi hii muhimu,” alisema mwanadiplomasia huyo wa Iran.

Ubalozi wa Israel mjini Pretoria awali uliripoti kuwa raia wawili wa Afrika Kusini, raia wa Eritrea na raia mmoja wa Sudan pia walikuwa miongoni mwa waliofariki au kutoweka.

Source:Bbc

Israel yawatambua Watanzania wanaoshikiliwa mateka na Hamas
0 Comment

TANZIA: Mtanzania alietekwa nchini Israel Afariki duniaAfyaclass Forum •

TANZIA: Mtanzania alietekwa nchini Israel Afariki dunia

Mmoja kati ya wanafunzi wawili wa Tanzania waliotekwa na wapiganaji wa Hamas wakati wa uvamizi wao Israel amefariki.

Mmoja kati ya wanafunzi wawili wa Tanzania waliotekwa na wapiganaji wa Hamas wakati wa uvamizi wao Israel amefariki. Kulingana na taarifa kutoka kwa serikali ya Tanzania iliotumwa katika vyombo vya habari bwana Clemence Felix Mtenga , alikua hajulikani alipo tangu uvamizi wa wapiganaji wa Hamas nchini Israel mnamo tarehe saba mwezi Oktoba 2023.

TANZIA: Mtanzania alietekwa nchini Israel Afariki dunia
0 Comment
Notification
My blog is in the process of editing and perfecting the new template, so there are still some functions to click but not yet used. Note which blogs associated with your side please read this lesson to update the blog logo.
UNDERSTOOD