SABABU ZA MICHIRIZI YA NGOZI NA MATIBABU YAKEAfyaclass Bongo Social •

MICHIRIZI YA NGOZI

• • • • • •

SABABU ZA MICHIRIZI YA NGOZI NA MATIBABU YAKE

Kwa asilimia kubwa Wanawake wajawazito hupatwa na hii hali ya Mpasuko wa Ngozi au Michirizi katika Ngozi hasa hasa maeneo ya Tumboni. Lakini Yapo maeneo mbali mbali ya mwili ambayo huweza kuathiriwa kwa kiasi kikubwa na tatizo hili la michirizi ya Ngozi kama vile;

- Maeneo ya Makalioni

- Maeneo ya kwenye mapaja

- Maeneo ya kwenye matiti

- Maeneo ya Hips

- Pamoja na kwenye tumbo

SABABU ZA KUTOKEA KWA MICHIRIZI YA NGOZI

  1. Kuwepo kwa vinasaba vya tatizo hilo katika koo husika
  2. Ngozi ya mwili kutanuka kwa sababu mbali mbali, kama unene au Ujauzito
  3. Tatizo la michiri huweza kutokana na Unene
  4. Michirizi kutokana na Hali ya Ujauzito
  5. Tatizo la kwenye vichocheo vya mwili Maarafu kama CORTISONE ambavyo huhusika moja kwa moja na kudhoofisha nyuzi nyuzi ambazo huvuta Ngozi pamoja,hivo kupelekea Ngozi kutanuka na kuachana kisha kutengeneza michirizi

WATU WALIO KATIKA HATARI YA KUPATA MICHIRIZI YA NGOZI NI PAMOJA NA;

- Wanawake

- Wajawazito

- Wanene

- Koo yenye shida hii

- Wanaotumia dawa kama prednisone

- Waliofanyiwa upasuaji unaohusisha kukuza maeneo kama hips,makalio au matiti

NINI CHA KUFANYA KUONDOA MICHIRIZI YA NGOZI?

• Paka mafuta yenye mchanganyiko ufuatao mara moja kwa siku;

1. Tumia Nusu kikombe chenye mafuta aina ya zaituni

2. Nusu kikombe chenye ute wa aloe vera

3. Capsules 6 za vitamin E na Capsules 4 za Vitamin A. Pasua capsules hizo ungaunga wake uchanganye pamoja na olive oil na aloevera kisha upake. Kama utatengeneza mchanganyiko zaidi unaweza Kutunza katika jokofu. Mchanganyiko huu ni salama tofauti na cream nyingi zinazouzwa ambazo hazijathibitishwa na mamlaka husika

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

0 Comment

KANSA YA TUMBO,DALILI ZAKE PAMOJA NA MATIBABU YAKEAfyaclass Bongo Social •

  KANSA YA TUMBO

.........

KANSA YA TUMBO,DALILI ZAKE PAMOJA NA MATIBABU YAKE


Katika mwili wa Binadamu kuna aina nyingi za Kansa Ikiwemo hii ya tumbo ambayo tunaizungumzia hivi Leo. Kansa hizo ni pamoja na;


  1. Kansa ya Damu
  2. Kansa ya Ngozi
  3. Kansa ya Mapafu
  4. Kansa ya Koo
  5. Kansa ya utumbo
  6. Kansa ya shingo ya Kizazi
  7. Kansa ya matiti
  8. Kansa ya kizazi
  9. Kansa ya Ini
  10. Kansa ya Ubongo
  11. Kansa ya Tumbo
  12. N.K

Hivi leo tutazungumzia kuhusu aina hii ya kansa ya tumbo,Je dalili zake ni zipi? na matibabu yake ni yapi?


Kama lilivyo neno lenyewe,Kansa hii hutokea kwenye tumbo, na endapo itatokea Mgonjwa atapata Dalili zifuatazo;

  1. Kupatwa na Maumivu makali ya tumbo
  2. Kujisaidia kinyesi kilichochanganyika pamoja na Damu
  3. Kujisikia kichefuchefu na kutapika pia
  4. Mwili kuchoka kuliko kawaida
  5. Kupatwa na homa za mara kwa mara
  6. Kushuka kwa kasi kwa Uzito wa mwili
  7. Kupoteza kabsa hamu ya kula
  8. Wagonjwa hawa wapo pia katika hatari ya kupatwa na Shida ya utapiamlo
  9. Kupatwa na shida ya mvurugiko wa tumbo mara kwa mara ikiwa ni pamoja na Kuharisha,tumbo kujaa gesi n.k

MATIBABU

Kama zilivyo kansa zingine,urahisi wa matibabu ni pale ambapo ugonjwa huu umegundulika mapema kabla ya kufikia stage mbaya,Kwani ikifikia stage mbaya hata kutibu pia ni vigumu. Hivo pale ukijihisi tofauti pamoja na kuona dalili nilizozitaja hapo juu wahi hospital kwa ajili ya uchunguzi zaidi.


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584






0 Comment

KANSA YA MAPAFU,DALILI ZAKE PAMOJA NA MATIBABU YAKEAfyaclass Bongo Social •

  KANSA YA MAPAFU

.........

KANSA YA MAPAFU,DALILI ZAKE PAMOJA NA MATIBABU YAKE


Katika mwili wa Binadamu kuna aina nyingi za Kansa Ikiwemo hii ya mapafu ambayo tunaizungumzia hivi Leo. Kansa hizo ni pamoja na;


  1. Kansa ya Damu
  2. Kansa ya Ngozi
  3. Kansa ya Mapafu
  4. Kansa ya Koo
  5. Kansa ya utumbo
  6. Kansa ya shingo ya Kizazi
  7. Kansa ya matiti
  8. Kansa ya kizazi
  9. Kansa ya Ini
  10. Kansa ya Ubongo
  11. N.K

Hivi leo tutazungumzia kuhusu aina hii ya kansa ya mapafu,Je dalili zake ni zipi? na matibabu yake ni yapi?


Kama lilivyo neno lenyewe,Kansa hii hutokea kwenye mapafu, na endapo itatokea Mgonjwa atapata Dalili zifuatazo;

  1. Mgonjwa sauti kubadilika na kutoka na mikwaruzo
  2. Kutoa sauti kama filimbi wakati wa kuvuta na kutoa hewa kwenye mapafu
  3. Mgonjwa kupatwa na shida wakati wa upumuaji
  4. Kupatwa na hali ya kuchoka kupita kiasi
  5. Maumivu ya viungo pamoja na Kifua hasa wakati wa kuvuta na kutoa hewa
  6. Kupatwa na shida ya kukuhoa mara kwa mara
  7. kukosa hamu ya kula
  8. Mgonjwa kuchoka kupita kiasi

MATIBABU

Kama zilivyo kansa zingine,urahisi wa matibabu ni pale ambapo ugonjwa huu umegundulika mapema kabla ya kufikia stage mbaya,Kwani ikifikia stage mbaya hata kutibu pia ni vigumu. Hivo pale ukijihisi tofauti pamoja na kuona dalili nilizozitaja hapo juu wahi hospital kwa ajili ya uchunguzi zaidi.


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584





0 Comment

KANSA YA INI,DALILI ZAKE PAMOJA NA MATIBABU YAKEAfyaclass Bongo Social •

  KANSA YA INI

.........

KANSA YA INI,DALILI ZAKE PAMOJA NA MATIBABU YAKE


Katika mwili wa Binadamu kuna aina nyingi za Kansa Ikiwemo hii ya ini ambayo tunaizungumzia hivi Leo. Kansa hizo ni pamoja na;


  1. Kansa ya Damu
  2. Kansa ya Ngozi
  3. Kansa ya Mapafu
  4. Kansa ya Koo
  5. Kansa ya utumbo
  6. Kansa ya shingo ya Kizazi
  7. Kansa ya matiti
  8. Kansa ya kizazi
  9. Kansa ya Ini
  10. Kansa ya Ubongo
  11. N.K

Hivi leo tutazungumzia kuhusu aina hii ya kansa ya ini,Je dalili zake ni zipi? na matibabu yake ni yapi?


Kama lilivyo neno lenyewe,Kansa hii hutokea kwenye ini, na endapo itatokea Mgonjwa atapata Dalili zifuatazo;

  1. Mgonjwa kuanza kutoa Damu puani
  2. Mgonjwa kujisaidia kinyesi chenye rangi nyeusi
  3. Mgonjwa kukojoa Mkojo wenye rangi nyeusi
  4. Mgonjwa kuanza kupata maumivu ya viungo mbali mbali ikiwemo na mabega
  5. Mgonjwa kushindwa kushiriki vizuri tendo la Ndoa
  6. Mgonjwa kuanza taratibu kupoteza kumbukumbu zake
  7. Mgonjwa kuingiwa na hali ya kukosa usingizi mara kwa mara
  8. Mapigo ya moyo ya mgonjwa kwenda mbio
  9. Kupatwa na hali ya kubadilika rangi kwenye macho pamoja na Ngozi ya mwili kuwa MANJANO kitaalam hujulikana kama JAUNDICE
  10. Kupatwa na maumivu makali ya Tumbo juu kidogo ya kitovu
  11. Mgonjwa kukosa hamu ya kula kabsa
  12. Mwili kuchoka kupita kiasi pamoja na kuhisi kichefuchefu

MATIBABU

Kama zilivyo kansa zingine,urahisi wa matibabu ni pale ambapo ugonjwa huu umegundulika mapema kabla ya kufikia stage mbaya,Kwani ikifikia stage mbaya hata kutibu pia ni vigumu. Hivo pale ukijihisi tofauti pamoja na kuona dalili nilizozitaja hapo juu wahi hospital kwa ajili ya uchunguzi zaidi.


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584






0 Comment

KANSA YA NGOZI,DALILI ZAKE PAMOJA NA MATIBABU YAKEAfyaclass Bongo Social •

 KANSA YA NGOZI

.........

KANSA YA NGOZI,DALILI ZAKE PAMOJA NA MATIBABU YAKE

Katika mwili wa Binadamu kuna aina nyingi za Kansa Ikiwemo hii ya ngozi ambayo tunaizungumzia hivi Leo. Kansa hizo ni pamoja na;

  1. Kansa ya Damu
  2. Kansa ya Ngozi
  3. Kansa ya Mapafu
  4. Kansa ya Koo
  5. Kansa ya utumbo
  6. Kansa ya shingo ya Kizazi
  7. Kansa ya matiti
  8. Kansa ya kizazi
  9. Kansa ya Ini
  10. Kansa ya Ubongo
  11. N.K
Hivi leo tutazungumzia kuhusu aina hii ya kansa ya Ngozi,Je dalili zake ni zipi? na matibabu yake ni yapi?

Kama lilivyo neno lenyewe,Kansa hii hutokea kwenye ngozi, na endapo itatokea Mgonjwa atapata Dalili zifuatazo;
  1. Kupata vidonda kwenye ngozi ambavyo haviponi kwa haraka
  2. Kupata maumivu kuzunguka eneo la kidonda
  3. Ngozi kubadilika rangi na kuwa nyekundu
  4. Rangi ya vidonda kuwa ya brown au nyeupe wakati mwingine
  5. Kupata hali ya homa mara kwa mara
MATIBABU

Kama zilivyo kansa zingine,urahisi wa matibabu ni pale ambapo ugonjwa huu umegundulika mapema kabla ya kufikia stage mbaya,Kwani ikifikia stage mbaya hata kutibu pia ni vigumu. Hivo pale ukijihisi tofauti pamoja na kuona dalili nilizozitaja hapo juu wahi hospital kwa ajili ya uchunguzi zaidi.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584
0 Comment

KANSA YA DAMU,DALILI ZAKE PAMOJA NA MATIBABU YAKEAfyaclass Bongo Social •

 KANSA YA DAMU

••••••••••••


KANSA YA DAMU,DALILI ZAKE PAMOJA NA MATIBABU YAKE


Katika mwili wa Binadamu kuna aina nyingi za Kansa Ikiwemo hii ya Damu ambayo tunaizungumzia hivi Leo. Kansa hizo ni pamoja na;


  1. Kansa ya Damu
  2. Kansa ya Ngozi
  3. Kansa ya Mapafu
  4. Kansa ya Koo
  5. Kansa ya utumbo
  6. Kansa ya shingo ya Kizazi
  7. Kansa ya matiti
  8. Kansa ya kizazi
  9. Kansa ya Ini
  10. Kansa ya Ubongo
  11. N.K

Hivi leo tutazungumzia kuhusu aina hii ya kansa ya Damu,Je dalili zake ni zipi? na matibabu yake ni yapi?


Kama lilivyo neno lenyewe,Kansa hii hutokea kwenye Damu, na endapo itatokea Mgonjwa atapata Dalili zifuatazo;

  • Kuanza kubadilika rangi ya Ngozi na kuwa Nyekundu sana
  • Kupatwa na maumivu mbalimbali yakiwemo ya Mifupa pamoja,joint pamoja na Viungo mbalimbali vya Mwili
  • Mgonjwa kutokwa na jasho sana wakati wa Usku
  • Kupatwa na matatizo ya tumbo mara kwa mara pamoja na kushambuliwa na magonjwa mengine kwa urahisi zaidi
  • Mwili kuchoka kupita kiasi
  • Kupatwa na homa za mara kwa mara

MATIBABU

Kama zilivyo kansa zingine,urahisi wa matibabu ni pale ambapo ugonjwa huu umegundulika mapema kabla ya kufikia stage mbaya,Kwani ikifikia stage mbaya hata kutibu pia ni vigumu. Hivo pale ukijihisi tofauti pamoja na kuona dalili nilizozitaja hapo juu wahi hospital kwa ajili ya uchunguzi zaidi.


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584








0 Comment

DALILI ZA UTI SUGU KWA MWANAMKE NA MWANAUME NI ZIPI?Afyaclass Bongo Social •

DALILI ZA UTI SUGU KWA MWANAMKE NA MWANAUME NI ZIPI?

UTI Sugu ni nini?

UTI sugu kwa kitaalam hujulikana kama Chronic Urinary Tract Infections (UTIs)

UTI Sugu ni Maambukizi ya muda mrefu ya mfumo wa mkojo au ni maambukizi ya mfumo wa mkojo ambayo hayajibu Dawa,hayaponi licha ya kutumia dawa au yanaendelea kujirudia mara kwa mara.

Maambukizi haya Yanaweza kuendelea kuathiri mfumo wako wa mkojo licha ya kupata matibabu sahihi, au yanaweza kujirudia baada ya matibabu.


Mfumo wa mkojo unaundwa na Vitu gani?

Mfumo wa mkojo hujumuisha vitu hivi;

  • Figo; ambazo huchuja damu yako na kutoa uchafu wa mwili kwa njia ya mkojo
  • Ureters; ni mirija inayosafirisha mkojo kutoka kwenye figo hadi kwenye kibofu
  • kibofu; hukusanya na kuhifadhi mkojo
  • Urethra; ni mrija unaosafirisha mkojo kutoka kwenye kibofu hadi nje ya mwili wako

UTI inaweza kuathiri sehemu yoyote ya mfumo wako wa mkojo.  Maambukizi yanapoathiri tu kibofu chako, kawaida ni ugonjwa mdogo ambao unaweza kutibu kwa urahisi.  Hata hivyo, ikiwa inaenea kwenye figo zako, unaweza kukabiliana na madhara makubwa ya Kiafya au kuhitaji kulazwa hospitalini.

 Ingawa UTI inaweza kutokea kwa mtu yeyote katika umri wowote, maambukizi Haya ni makubwa zaidi kwa wanawake

DALILI ZA UTI SUGU KWA MWANAMKE NA MWANAUME NI ZIPI

Je, ni Zipi dalili za maambukizi ya muda mrefu ya njia ya mkojo au Dalili za UTI SUGU?

DALILI ZA UTI KWA WOTE(MWANAMKE NA MWANAUME) NI PAMOJA NA;

  1. Kupata maumivu makali ya nyonga,mgongo,joint pamoja na viungo mbali mbali vya mwili
  2. Kupata maumivu ya tumbo hasa hasa upande wa kushoto
  3. Kuhisi kukojoa mara kwa mara ila ukikojoa mkojo haushi
  4. Kuhisi hali ya kuchoma wakati wa kukojoa
  5. Kukojoa mkojo wenye rangi kama pink au nyekundu,hii ni baada ya UTI kuwa ya mda mrefu na kuanza kuleta madhara makubwa

Dalili za UTI  sugu zinazoathiri kibofu chako ni pamoja na:

 1. kukojoa mara kwa mara

 2. Kukojoa damu au mkojo mweusi

 3. Hisia ya kuwaka moto wakati wa kukojoa

 4. Kupata maumivu katika figo, ambayo ina maana utahisi maumivu haya kwenye mgongo wako wa chini,Kiuno au chini ya mbavu zako

 5. Kupata maumivu katika eneo la kibofu chako

 Ikiwa UTI Sugu itaenea kwenye figo zako, inaweza kusababisha:

- kichefuchefu

- kutapika

 - Kuhisi baridi

 - Kupata homa kali, zaidi ya 101°F (38°C)

- Kupata uchovu wa mwili

 - Dalili za kuchanganyikiwa akili

Watu wanaoishi na UTI sugu wanaweza pia kupata matatizo.  Maambukizi ya mara kwa mara ya mfumo wa mkojo yanaweza kusababisha:

• Magonjwa ya figo, maambukizi ya figo, na uharibifu mwingine wa kudumu wa figo, hasa kwa watoto wadogo

 • Tatizo la sepsis, ambayo ni matatizo ya kutishia maisha kutokana na maambukizi kwenye damu,

septicemia ni hali ambayo bakteria wameingia kwenye mkondo wa damu

• kuongezeka kwa hatari ya kuzaa kabla ya wakati au kupata watoto wenye uzito mdogo n.k.

CHANZO CHA UTI SUGU KWA MWANAMKE NA MWANAUME

UTI ni matokeo ya maambukizi ya bakteria, Mara nyingi, bakteria huingia kwenye mfumo wa mkojo kupitia urethra na kisha kuzidi kuzaliana kwenye kibofu.

Kugawanya UTI kuwa maambukizi ya kibofu na urethra Itasaidia kuelewa vizuri jinsi yanavyokua. Soma Zaidi hapa..

Maambukizi ya kibofu(Bladder infections):

Bakteria Escherichia coli (E. coli) ni chanzo cha kawaida cha maambukizi kwenye kibofu au cystitis.  E. koli kawaida huishi ndani ya matumbo ya watu na wanyama wasio wagonjwa(wenye afya).Katika hali yake ya kawaida, E.coli hawasababishi matatizo yoyote,Lakini ikiwa E.coli hupata njia na kutoka nje ya matumbo na kwenda kwenye njia ya mkojo, Wanaweza kusababisha maambukizi.

 Hii kwa kawaida hutokea kwa njia mbali mbali kama vile;

  • Wakati vipande vidogo sana au vikubwa vya kinyesi vinapoingia kwenye njia ya mkojo. Hii inaweza kusababisha vimelea hawa kupenya kwenye njia ya Mkojo
  • Kutokea wakati wa kufanya Mapenzi.  Kwa mfano, hii inaweza kutokea ikiwa utabadilisha na kufanya tendo kwenye njia ya haja kubwa na ya uke.

 Mapenzi kinyume na maumbile huongeza hatari ya kupata UTI kwa kiasi kikubwa.  Maambukizi ya kibofu pia yanaweza kutokea kutokana na maji ya chooni au kupangusa kusikofaa.  Mkojo wenye povu pia unaweza kuashiria tatizo.

Maambukizi ya urethra(Urethral infections)

Pia inajulikana kama urethritis, maambukizi ya urethra yanaweza kutokana na bakteria kama vile E. coli.  Ugonjwa wa urethra unaweza pia kuwa matokeo ya maambukizi ya magonjwa ya Zinaa (STI).  Hata hivyo, hii ni nadra.  Magonjwa ya zinaa ni pamoja na:

  • Herpes
  • kisonono
  • klamidia

Ni nini huongeza hatari ya kupata maambukizi Sugu ya njia ya mkojo au UTI SUGU?

 • Kuwa mwanamke

 UTI sugu huwapata zaidi wanawake.  Hii ni kutokana na vipengele viwili tofauti vya maumbile(anatomy) yao;

(i) Kwanza, urethra iko karibu na rectum kwa wanawake.  Kwa hivyo, ni rahisi kwa bakteria kutoka kwenye rektamu kufikia urethra, hasa ikiwa unafuta nyuma kwenda mbele badala ya mbele kwenda nyuma wakati wa kujisaidia haja kubwa.  Hii ndiyo sababu wasichana wadogo mara nyingi hupata UTI.  Hawajajifunza jinsi ya kufuta vizuri.

(ii) Pili, urethra ya Mwanamke ni fupi.  Hii ina maana kwamba bakteria wana umbali mfupi wa kusafiri ili kufika kwenye kibofu cha mkojo, ambapo wanaweza kuzaliana na kusababisha maambukizi kwa urahisi zaidi.

 • Mtindo wa maisha

Baadhi ya mtindo wa maisha unaweza kukuweka katika hatari zaidi ya kupata UTI sugu, kama vile;

  1.  kutumia Vifaa vya kutengeneza wakati wa tendo la ndoa.
  2. Kutokufanya Usafi vizuri wa Vyoo,vyombo vya kutumia Toilet,Maji machafu n.k
  3. Tabia ya kuongeza maji juu ya maji yaliyokaa kwa muda mrefu chooni, hapa kuna uwezekano mkubwa wa kukuza bakteria.
  4. Kutumia vyoo vichafu, hasa public toilets, kama za Stend,masokoni,hotelini,shuleni n.k mara kwa mara

 • Mfano mwingine ni kubadilisha kila mara mazingira Asilia ya bakteria wa ukeni

 Hii inaweza kuongeza hatari kwako ya kupata UTI sugu.  Ikiwa unatumia mara kwa mara mojawapo ya bidhaa zifuatazo, basi unabadilisha mazingira asilia ya bakteria wa ukeni:

  1. Kutumia dochi za uke 
  2. Kutumia dawa za kuua manii
  3. Baadhi ya dawa,antibiotics

Kukoma hedhi

 Kukoma hedhi kunaweza kusababisha matatizo sawa kwa baadhi ya wanawake.  Kukoma hedhi husababisha mabadiliko ya homoni ambayo yanaweza kusababisha mabadiliko katika bakteria wa uke wako.  Hii inaweza kuongeza hatari ya kupata UTI ya muda mrefu au UTI Sugu.

MATIBABU YA UTI SUGU KWA MWANAMKE NA MWANAUME

Matibabu ya Hospitali;

Kozi ya antibiotics inayotolewa kwa wiki 1 ndiyo matibabu ya msingi ya UTI yanayoweza kutumika,Hata hivyo, ikiwa una UTI ya muda mrefu au UTI SUGU, daktari wako anaweza kuagiza antibiotics ya muda mrefu kwa zaidi ya wiki 1 baada ya dalili za awali kupungua.  Katika hali nyingi, hii husaidia kuzuia dalili kutokea mara kwa mara.

 Daktari wako anaweza pia kupendekeza kozi ya matibabu ambayo unatumia antibiotics baada ya kila wakati unapojamiiana.

 Mbali na antibiotics, daktari wako atataka ufuatilie mfumo wako wa mkojo kwa karibu zaidi.  Kwa mfano, wanaweza kukuuliza ufanye vipimo vya kawaida vya mkojo ili kuangalia maambukizi.

 Ikiwa UTI yako ya muda mrefu itatokea wakati wa kukoma kwa hedhi, unaweza kutaka kuzingatia matibabu ya estrojeni ya uke.  Hii inaweza kupunguza hatari ya kupata UTIs siku zijazo, ingawa ina mabadiliko kadhaa.  Hakikisha njia hii unaijadili na daktari wako.

 Ikiwa una maambukizi na unapata hali ya kuungua wakati wa kukojoa, Daktari wako anaweza kuagiza dawa za maumivu ili kupunguza hali ya kuungua na kuumia kwenye kibofu cha mkojo na njia ya mkojo(urethra).  Hii itasaidia wewe kujisikia vizuri hata kama upo kwenye tiba zingine.

 Daktari wako pia anaweza kukuandikia dawa zingine kwa ​​matibabu ya hali ambazo hazitibiwi kwa kutumia antibiotic.

Matibabu ya Asili;

Kulingana na Tafiti za Mwaka 2023 kutoka kwenye Chanzo Kilichoaminiwa, unywaji wa juisi ya cranberry kila siku unaweza kusaidia kupunguza kujirudia kwa UTI kwa wale walio na UTI sugu.

 Dawa nyingine ya asili ya kutibu UTI ni kunywa maji mengi.  Maji yanaweza kusaidia kupunguza mkojo na kuondoa bakteria kwenye njia ya mkojo.

Baadhi ya Tafiti pia,Zinaonyesha unywaji wa maji kuanzia Lita 2.5 kwa siku husaidia kupunguza maambukizi ya UTI za mara kwa mara kwa Zaidi ya asilimia 50%

 Ikiwa unapata maumivu, kuweka padi ya kupasha joto au chupa ya maji moto kwenye kibofu chako kunaweza kukusaidia.

JINSI YA KUZUIA UTI SUGU KWA MWANAMKE NA MWANAUME

Ikiwa una uwezekano wa kupata UTI mara kwa mara, hakikisha:

✓ Unakojoa mara nyingi zaidi (haswa baada ya kujamiiana)

✓ Futa mbele kwenda nyuma baada ya kukojoa au kujisaidia haja kubwa

 ✓ kunywa maji mengi ili kuondoa bakteria kwenye mfumo wako

✓ kunywa juisi ya cranberry kila siku

✓ Jenga Tabia ya Kuvaa chupi za pamba

✓ epuka suruali za kubana

✓  Epuka kutumia diaphragms na dawa za kuua manii, spermicides kwa njia za kudhibiti Ujauzito

✓ Epuka kunywa vinywaji ambavyo vinaweza kukera kibofu chako (kama vile kahawa, vinywaji vya matunda ya machungwa, soda, pombe n.k) 

✓ Tumia lubrication wakati wa tendo, ikiwa ni lazima

 ✓ Osha govi lako mara kwa mara ikiwa hujatahiriwa n.k

JINSI YA KUGUNDUA UTI SUGU KWA MWANAMKE NA MWANAUME,Diagnosis

Njia ya kawaida ambayo madaktari hutumia kugundua UTI ni kufanya uchunguzi wa kimaabara kwenye sampuli ya mkojo, kwa Kitaalam Urinary Analysis, Mtaalamu wa matibabu huchunguza sampuli chini ya darubini, akitafuta uwepo wa bakteria.

 Katika tendo la kutayarisha mkojo, Mtaalam huweka sampuli ya mkojo kwenye mrija ili kusaidia bakteria kukua.  Baada ya siku 1 hadi 3, wanaangalia bakteria ili kuamua matibabu bora.

 Ikiwa daktari wako anashuku uharibifu wa figo, anaweza kuagiza uchunguzi wa X-ray na figo.  Vifaa hivi vya kupiga picha huchukua picha za sehemu za ndani ya mwili wako.

 Ikiwa una UTI inayojirudia,UTI SUGU, huenda daktari wako akataka kukufanyia cystoscopy.  Katika utaratibu huu, watatumia cystoscope, Hii Ni mirija mirefu na myembamba yenye lenzi mwishoni inayotumika kutazama ndani ya urethra na kibofu chako.

Daktari wako atatafuta upungufu wowote au masuala ambayo yanaweza kusababisha UTI kuendelea kurudi.

KUMBUKA;

Je, Mtazamo wa muda mrefu ni upi?

 Maambukizi ya njia ya mkojo hayafurahishi na yanaumiza.  UTI nyingi sugu zitatatuliwa kwa kozi ya muda mrefu ya Antibiotics, lakini ufuatiliaji wa dalili zaidi ni muhimu kwa kuwa kwa kawaida hujirudia.

 Watu wenye UTI wanapaswa kufuatilia miili yao na kutafuta matibabu mara moja mwanzo wa maambukizi mapya.  Matibabu ya mapema hupunguza hatari Kwako ya kupata matatizo makubwa zaidi ya muda mrefu.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

HITIMISHO:

UTI SUGU

_______________

DALILI ZA UTI SUGU KWA MWANAMKE NA MWANAUME NI ZIPI?

Kwanza tujue tukisema UTI tuna maana gani na tukisema UTI Sugu tuna Maana gani. Pamoja na tofauti zake ni zipi

• Kwa ufupi UTI kirefu chake ni Urinary track Infection na maana yake ni maambukizi katika mfumo mzima wa Mkojo ukijumuisha maeneo mbali mbali kama vile; kibofu cha Mkojo(urinary bladder), Njia ya mkojo(urethra), Figo, pamoja na tezi mbali mbali kama Prostate gland.

Maambukizi haya kwa asilimia kubwa huwa ya Bacteria,ambapo yanaweza kuwa ya mda mfupi,ya mda mrefu,au ya kujirudia rudia mara kwa mara.

• UTI SUGU maana yake; ni maambukizi katika mfumo mzima wa mkojo ambayo yamekuwa ya kujirudia rudia kila mara na ya mda mrefu hata baaada ya kutumia dawa nyingi na matibabu mbali mbali.

DALILI ZA UTI KWA WOTE(MWANAMKE NA MWANAUME) NI PAMOJA NA;

  1. Kupata maumivu makali ya nyonga,mgongo,joint pamoja na viungo mbali mbali vya mwili
  2. Kupata maumivu ya tumbo hasa hasa upande wa kushoto
  3. Kuhisi kukojoa mara kwa mara ila ukikojoa mkojo haushi
  4. Kuhisi hali ya kuchoma wakati wa kukojoa
  5. Kukojoa mkojo wenye rangi kama pink au nyekundu,hii ni baada ya UTI kuwa ya mda mrefu na kuanza kuleta madhara makubwa

MADHARA YA UTI SUGU

Uti ikishakuwa ya mda mrefu huweza kuleta madhara makubwa kama;

- Matatizo ya Figo

- Kwa mwanamke kuwa hali ya Uke Mkavu kupita kawaida

- Shida kwenye kibofu cha Mkojo

- N.K

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584

0 Comment

UGONJWA WA UKOMA PAMOJA NA DALILI ZAKEAfyaclass Bongo Social •

 UKOMA

...............

UGONJWA WA UKOMA PAMOJA NA DALILI ZAKE


Kwa kawaida Ugonjwa wa Ukoma ni ugonjwa ambao huathiri viungo mbali mbali vya mwili wa binadamu kama  Vile Mikono,miguu,Macho,Uso pamoja na Ngozi pia.



BAADHI YA DALILI ZA UGONJWA WA UKOMA NI PAMOJA NA;


- Kukatika baadhi ya Viungo vya Mwili kama vile Vidole vya Miguu au mikono


- Ugonjwa wa ukoma huweza kusababisha Ganzi miguuni au mikononi pia


- Kuhisi hali ya kuchomwa eneo lote la Vidole vya miguuni au mikononi


- Vidole vya miguu pamoja na mikono kupooza


- Ugonjwa huu wa ukoma unaweza kusababisha matatizo ya macho ikiwa ni pamoja na upofu wa macho


- Ugonjwa huu wa ukoma huweza kuwa chanzo kikubwa cha uharibifu wa shape ya Pua pamoja na Uso kwa Ujumla.


- Ugonjwa wa ukoma huweza kubadilisha rangi ya ngozi na kuifanya kuwa nyeusi na kuwa na vitu mithili ya ukurutu Hasa mikononi na miguuni.


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.



0 Comment

AINA YA MAUMIVU YA KICHWA AMBAYO NI HATARI KWA AFYA YAKOAfyaclass Bongo Social •

KICHWA KUUMA

• • • • • •

AINA YA MAUMIVU YA KICHWA AMBAYO NI HATARI KWA AFYA YAKO


Sio kila Maumivu ya kichwa ni yakawaida na yakupuuzia kama watu wengi wanavyodhani. Ipo aina ya maumivu ya kichwa ambayo huhitaji msaada wa haraka wa kiafya kwani Ishara yake ni mbaya.


Kuumwa na kichwa ni swala la kawaida kwa kila binadamu,lakini leo nakufundisha ujue kutofautisha kati ya maumivu ya kawaida ya kichwa na maumivu ambayo ni hatari sana kwa afya yako.


AINA YA MAUMIVU YA KICHWA AMBAYO NI HATARI KWAKO


  • Kuumwa na kichwa sana kunakoenda sambamba na uwepo wa homa kali kwa wakati Mmoja
  • Kuumwa na kichwa sana kunakoenda sambamba na kuwepo kwa hali ya kupoteza fahamu au kumbukumbu
  • Kuumwa na kichwa sana kunakoenda sambamba na hali ya kutingishwa kwa Mwili
  • Kuumwa na kichwa sana kinachogonga mithili ya Mtu anagonga na Nyundo
  • Kuumwa na kichwa sana kunakoenda sambamba na shida ya shingo Mfano kukakamaa kwa shingo n.k
  • Kuumwa na kichwa sana kunakoenda sambamba na hali ya kuchanganyikiwa kabsa


Ukihis aina hii ya Maumivu ya kichwa, Fanya haraka sana kuonana na wataalam wa afya kwa Ajili ya matibabu sahihi ya Shida yako.


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584





0 Comment

KUSAFISHA DAMU(DIALYSIS) KWA WAGONJWA WENYE TATIZO LA FIGO KUFELIAfyaclass Bongo Social •

KUSAFISHA DAMU(DIALYSIS)

• • • • • •

KUSAFISHA DAMU(DIALYSIS) KWA WAGONJWA WENYE TATIZO LA FIGO KUFELI


Zipo njia mbalimbali hutumika katika kusafisha Damu yaani kwa kitaalam Dialysis kwa Mgonjwa mwenye matatizo ya Figo kufeli, ikiwemo mgonjwa mwenye matatizo ya Figo kufeli kuwekewa aina ya Mrija maalumu Unaojulikana kama PERM-SO CATH,ambapo mrija huu huweza kuwekwa katika maeneo tofauti ya mwili kama vile Kifuani,Shingoni,Au kwenye paja.(Tazama picha hapo Chini kama Mfano)


MAMBO YAKUFANYA KWA AJILI YA KULETA AFYA YA FIGO ZAKO


1. Epuka kabsa matumizi ya pombe kupita kiasi, kwani huleta madhara makubwa na huathiri sana figo zako.


2. Kunywa maji ya kutosha,ni bora sio tu kwa afya ya mwili kwa Ujumla,ila ni pamoja na Figo.


3. Thibiti matumizi ya Dawa kwani huharibu figo zako


4. Hakikisha unadhibiti magonjwa kama Shinikizo la damu au presha pamoja na kisukari endapo unavyo.


5.  Dhibiti uzito wako wa mwili kwani uzito kupita kiasi pia ni hatari kwa Figo zako


6. Kama unapata dalili kama Mkojo kuchoma, kukojoa mara kwa mara, au maumivu upande wa kushoto, zaweza kuwa dalili za UTI,tibu uti iishe kabsa,Kwani UTI sugu huathiri mfumo mzima wa mkojo ikiwemo kibofu cha Mkojo pamoja na Figo.





0 Comment

YAJUE MADHARA YA KUVAA VIATU VIREFU (HIGH HEELS)Afyaclass Bongo Social •

VIATU VIREFU

• • • • • •

YAJUE MADHARA YA KUVAA VIATU VIREFU (HIGH HEELS)


Mbali na kwamba uvaaji wa Viatu virefu maarufu kama high heels siku hizi umepamba moto,na imeonekana kama Fashion na inaongeza sana Mvuto wa kipekee kwa Mwanamke.Kiafya uvaaji huo sio salama kabsa.


Madhara huweza kuonekana katika maeneo mbali mbali ya Mwili kama vile kwenye KIUNO,MGONGO au UTI WA MGONGO KWA UJUMLA WAKE,KISIGINO CHA MGUU,VIDOLE VYA MGUU pamoja na MAGOTI.


Tafiti zinaonyesha kwamba, wanawake wanaovaa viatu hivi virefu(high heels) husumbuliwa na Maumivu makali katika maeneo niliyoyataja hapo juu(kiuno,Mgongo,kisigino,vidole vya mguuni n.k), ikiwemo kuathirika kwa Uti wa mgongo pamoja na pingili zake kusagika kwani hufanya kazi kubwa sana ya kujipinda na kuleta balance ya mwili


KUMBUKA; Hakuna mda maalum wa kuanza kuona athari za Uvaaji wa viatu virefu,pengine athari zake huweza kuchukua mda kidogo kutokea, hata siku zikija utashindwa kugundua chanzo ni nini.


Kinga ni Bora kuliko Tiba,Chukua hatua.


Kwa Ushauri Zaidi,Elimu au Tiba tuwasiliane kwa namba +255758286584.






0 Comment

SABABU YA KUVIMBA MIGUU UKIWA SAFARINI NA MATIBABU YAKEAfyaclass Bongo Social •

MIGUU KUVIMBA

• • • • • •

SABABU YA KUVIMBA MIGUU UKIWA SAFARINI NA MATIBABU YAKE


Kuna watu wengi hupatwa na hii hali ya kuvimba miguu pale wanaposafiri hususani umbali Mrefu. Safari ambayo huhusisha kukaa kwa Mda mrefu kwenye kiti cha Gari. Ingawaje sio lazima ukiwa tu unasafiri, ila kuna wengine hata akikaa mda mrefu akiwa nyumbani Miguu huvimba.


JE NINI KINASABABISHA HALI HII?


Kwa kitaalam hali hii hutokana na kukosekana kwa Mzunguko wa Damu mzuri katika mishipa ya miguu kutokana na kukaaa kwa mda mrefu, hivo kupelekea damu kutuwama sehemu moja na kupelekea Maji yaliyopo ndani ya mishipa Ya damu kutoka na kujikusanya kwa Nje hivo kutengeneza hali ya Uvimbe kwenye miguu



MATIBABU


Kuvimba miguu ukiwa safarini sio tatizo, hali hii huweza kuisha yenyewe ndani ya mda mfupi baada ya wewe kutoka ulipo kaa na kuanza kutembea,Ila endapo kuvimba huko kumekaa kwa mda mrefu hata baada ya kutembea, huku ukiendelea kupata maumivu makali basi huenda kuna shida nyingine kama Damu kuganda N.K hivo ni vizuri kuongea na wataalam wa afya kujua nini shida


MAMBO YA KUFANYA;


1. Anza kutembea baada ya kuona shida hii ya kuvimba miguu


2. Epuka kuvaa viatu vinavyobana miguu


3. Endapo maumivu na uvimbe bado upo,waone wataalam wa afya


Kwa Ushauri zaidi,Elimu au Tiba tuwasiliane kwa namba +255758286584.





0 Comment

FAHAMU SABABU KUBWA ZA MAZIWA YA MWANAMKE KULALAAfyaclass Bongo Social •

MAZIWA KULALA

• • • • • •

FAHAMU SABABU KUBWA ZA MAZIWA YA MWANAMKE KULALA


Vipo vitu vingi ambavyo huchangia mabadiliko ya  umbo la titi la Mwanamke,ambapo baadhi ya sababu ni za mda mfupi na zingine ni za mda mrefu.


SABABU ZA MAZIWA YA MWANAMKE KULALA


✓ Kwa asilimia kubwa Mama akishabeba ujauzito tu,umbo la titi huanza kubadilika na kuwa kubwa na wakati mwingine kushuka


✓ Kujifungua Mara nyingi pamoja na kuwa na watoto wengi


✓ Uvutaji wa sigara kwa mwanamke,nayo pia ni miongoni mwa sababu zinazochangia maziwa ya mwanamke kulala


✓ Kadri umri unavyosogea ndivo na umbo au shape ya Maziwa hubadilika na kushuka


✓ Kuwa Mnene kupita kiasi kunaweza kusababisha matiti yako kushuka


✓  Lakini pia kwa wengine,hii hali hutokana na kuwepo kwa vinasaba vya hali hii katika ukoo wao hivo ni kama tatizo la Kurithi.


✓ Upungufu mkubwa wa baadhi ya Vitamin Mwilini Mfano VITAMIN C.  Hii ni kutokana na Kuwa Vitamin C hutengeneza kitu kinachoitwa COLLAGEN ambacho ni muhimu sana katika kuimarisha ngozi ya Ziwa pamoja na kushikilia ziwa lisishuke. Hivo basi upungu wa Vitamin C ni upungufu wa Collagen na ni matokeo ya Ziwa kushuka.


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.





0 Comment

SABABU ZA MTU KUPATA KITAMBIAfyaclass Bongo Social •

KITAMBI

• • • • • 

SABABU ZA MTU KUPATA KITAMBI


Zipo sababu mbali mbali ambazo huweza kusababisha mtu kupata kitambi, Leo tugusie baadhi ya Sababu hizo;


  • Kukaa Mda mrefu au kufanya kazi za kukaaa kwa Mda mrefu pasipo kufanya Mazoezi yoyote
  • Kula vyakula vyenye Wanga mwingi na kwa kiasi kikubwa
  • Unywaji wa pombe Mara kwa mara kwani pombe ina kiwango kingi cha sukari
  • Kula vyakula Jamii ya mafuta mafuta Kwa wingi


ANGALIZO:

Kitambi sio kuwa na afya Nzuri kama watu wengi wanavyodhani, Kama una kitambi jitahidi;

  1. Kufanya Mazoezi
  2. Kuepuka kula vyakula vywenye wanga mwingi na kwa kiasi kikubwa
  3. Epuka kula vyakula vya mafuta sana
  4. Epuka unywaji wa pombe


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.




0 Comment

ATHARI ZA KUBEBA WALLET MFUKO WA NYUMA WA SURUALIAfyaclass Bongo Social •

WALLET MFUKO WA NYUMA

• • • • • •

ATHARI ZA KUBEBA WALLET MFUKO WA NYUMA WA SURUALI


Watu wengi hawajui kwamba kuna madhara makubwa ya kubeba wallet kwa Mfuko wa nyuma wa Suruali hasa pale ikiwa imejaa na ina uzito.


Athari hizo ni Pamoja na;


- Kupata Ganzi kwenye paja la nyuma pamoja na kalio kama umekaa kwa Mda mrefu


- Kupata pia maumivu makali eneo hilo hilo la paja la Nyuma na kalio ambao umebebea wallet yako


- Hali hii huja baada ya kubonyezwa kwa Neva ya Sciatica kutokana na Wallet uliyobeba


- Athari nyingine ambazo huweza kutokea ni pamoja na kuufanya mgongo wa mhusika kuinamia upande Mmoja


JE WEWE NI MBEBAJI WA WALLET KWA STAILI HII? ACHA MARA MOJA.




0 Comment

KUOTA UPELE KWENYE NGOZI WAKATI WA HEDHIAfyaclass Bongo Social •

HEDHI NA UPELE

• • • • • •

KUOTA UPELE KWENYE NGOZI WAKATI WA HEDHI


Hali hii huwatokea baadhi ya Wanawake kila wakifika karibu na kipindi cha Hedhi kuanza kuota upele kwenye ngozi halafu baada ya kumaliza Hedhi upele huo huisha kabsa, lakini hawafahamu sababu za tatizo hilo.


Sababu za Kuota upele kwenye Ngozi wakati wa Hedhi ni pamoja na;


Uchocheaji wa tezi za sebaceous ambao husababishwa na kushuka kwa kichocheo cha Progesterone na Estrogen mwanamke anapokaribia kuingia Hedhi.


Hali hiyo hupelekea utengenezaji wa mafuta kwenye Ngozi ya mwili maarafu kama SEBUM kwa kitaalam.


Mafuta hayo yanapokuwa mengi kwenye ngozi,hujazana sehemu moja na kutengeneza kitu kama chunusi au kipele



HIVO NDIVYO KIPELE HUTOKEA KWENYE NGOZI HASA USONI WAKATI WA HEDHI KWA BAADHI YA WANAWAKE.


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584




0 Comment

JE UMEKAA MDA MREFU PASIPO KUONA HEDHI YAKO? ZIJUE BAADHI YA SABABU ZA TATIZO HILOAfyaclass Bongo Social •

KUKOSA HEDHI

• • • • • •

JE UMEKAA MDA MREFU PASIPO KUONA HEDHI YAKO? ZIJUE BAADHI YA SABABU ZA TATIZO HILO


Mzunguko wako wa hedhi ulikuwa uko sawa gafla unashangaa mwezi wa kwanza unaisha bila kuona hedhi,mwezi wa pili nakuendelea,wengine mpaka mwaka unaisha,na hawaelewi wana shida gani au tatizo ni nini.


Tatizo hili huwapata wanawake wengi siku hizi,sio wewe peke yako. Twende pamoja katika makala hii,utanielewa taratibu hakuna shida.


ZIPO SABABU ZA KUSABABISHA MWANAMKE KUKOSA HEDHI KAMA VILE;


Kuna sababu ya kawaida kabsa ambayo sio tatizo ni UJAUZITO, Ukipata mimba huwezi ukaona siku zako za hedhi.


Lakini sababu zifuatazo Sio za kawaida au ni Tatizo;


- Mvurugiko wa vichocheo vya mwili au kwa kitaalam Hormone imbalance, ambapo shida hii huchangiwa na vitu vingi kama matumizi ya baadhi ya Njia za Uzazi wa mpango kama Sindano N.K


- Kuwa na tatizo la Uzito mdogo sana au kwa kitaalam tunaita Underweight


- Tatizo la Msongo wa mawazo


- Kupatwa na shida katika tezi lako la Thyroid hivo kuathiri mifumo mbali mbali ya mwili hasa katika vichocheo vyako


- Matumizi ya baadhi ya Njia za Uzazi wa Mpango kama nilivyoeleza hapo juu Mfano ni SINDANO.


- Kupatwa na Tatizo la  polycystic ovarian syndrome au PCOS kwa kifupi


- Kutokula chakula bora au Balance diet


- Kufanya Mazoezi kupita Kiasi au kufanya kazi Ngumu sana.


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584






0 Comment

FAHAMU MBINU ZA JINSI YA KUONGEZA UZITO WAKO WA MWILI KWA WEWE UNAYETAKA KUONGEZA UZITOAfyaclass Bongo Social •

MBINU ZA JINSI YA KUONGEZA UZITO KWA WEWE UNAYEHITAJI KUONGEZA UZITO WAKO

• • • • • •

Kama ilivyokupunguza Uzito,sio kila mtu anahitaji kupunguza Uzito, kuna wengine pia huhangaika na Jinsi ya kuongeza Uzito wao. Wametumia mbinu nyingi lakini mafanikio ni kidogo au hakuna kabsa.


Kama ilivyo na madhara pale ambapo ukiwa na uzito kupita kiasi au OVERWEIGHT AU OBESITY,vivyo hivo na kuwa na Uzito Mdogo sana pia kuna madhara yake,Kama vile Vifo N.K


Hivo basi Uzito wa juu una madhara na uzito wa chini una madhara pia, Lakini Unaweza kutumia Njia na mbinu mbali mbali za kiafya ili kuongeza Uzito wako kama ilivyo katika kupunguza.


MAMBO YA KUZINGATIA KATIKA KUONGEZA UZITO


1. Pendelea kula vyakula vyenye virutubisho vingi vya kujenga mwili yaani vyakula vya PROTEIN kama Samaki,Maharage,Nyama n.k


2. Fanya Mazoezi ya kujenga mwili sio ya kupunguza Uzito, Mfano mazoezi kama Jim n.k


3. Usile mlo mmoja kwa siku; kuna,watu wengi sana hujinyima Chakula cha Mchana, wakipendelea kula vitu vidogo vidogo tu, hii sio nzuri sana kwa afya yako, Kwani mbali na kutokuongezeka mwili,pia unaweza pata magonjwa Kama matatizo ya Vidonda Vya Tumbo.

 

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KUPITIA NAMBA +255758286584.






0 Comment

MAMA MJAMZITO KULA UDONGO(PEMBA)Afyaclass Bongo Social •

 JE WAJUA PEMBA SIO NZURI?


SOMA HAPA..!!!


Kuna madhara mengi ambayo huweza kumpata mama mjamzito kwa kula Udongo maarufu kama PEMBA. Hebu tuone kwanza nini kinapatikana kwenye udongo huu ambao mama wengi wakiwa wajawazito hupendelea kula.


Chuo kikuu cha Afya na Sayansi BUGANDO wakishirikiana pamoja na Wenzetu kutoka CANADA na MAREKANI walifanya utafiti katika Mikoa 12 Ya Tanzania ambayo ni;


  1. RUVUMA
  2. TANGA
  3. KILIMANJARO
  4. KIGOMA
  5. MOROGORO
  6. MARA
  7. KUSINI PEMBA
  8. MBEYA
  9. DODOMA
  10. LINDI
  11. RUKWA
  12. SINGIDA

Majibu ya utafiti huo; Waligundua kwamba ndani ya udongo kuna madini mengi ambayo ni hatari kwa afya ya mama na mtoto aliyetumboni, madini hayo ni pamoja na;


  • Aluminium
  • Nickel
  • Cadmium
  • Arsenic
  • Pamoja na madini ya Risasi au Lead


Kumbuka pia; Mbali na utafiti huo,kwa hali ya kawaida ndani ya udongo kuna uchafu wa kila namna unaojua wewe, Kama vile kinyesi,mikojo, n.k


Epuka Tabia Hii kwa afya Bora kwako na Mtoto wako aliyetumboni.

Kinga ni Bora kuliko Tiba

WE CARE, WE SHARE...!!!!



@Kwa Ushauri zaidi,elimu au Tiba usisite pia tuwasiliane kupitia namba +255758286584.






0 Comment

CHANZO CHA MAUMIVU YA TUMBO MARA KWA MARAAfyaclass Bongo Social •

  MAUMIVU YA TUMBO MARA KWA MARA


Maumivu haya ya tumbo huweza kumpata mtu wa jinsia yoyote (mwanamke au mwanaume), mtu wa umri wowote(mtoto au mtu mzima), au mtu wa jamii yoyote, na pia maumivu haya huweza kuhusisha, maumivu ya tumbo chini ya kitovu, maumivu ya tumbo upande wa kushoto,maumivu ya tumbo upande wa kulia,maumivu ya tumbo eneo la nyonga,maumivu ya tumbo juu ya kitovu au maumivu ya tumbo katikati ya kitovu.


CHANZO CHA MAUMIVU YA TUMBO LA MARA KWA MARA


Maumivu ya tumbo katika maeneo yote niliyoyataja hapo juu,huweza kuchangiwa na sababu mbali mbali ikiwemo;


1). Uwepo wa tatizo la Hernia au Ngiri


2). Matatizo ya korodani,ikiwemo korodani kushindwa kushuka hasa kwa mtu ambaye tayari umri ni mkubwa


3). Tatizo la vidonda vya tumbo kwa mhusika na hii hutokea mara kwa mara baada ya kula vyakula vyenye acid kali, kama maharage,pilipili n.k


4). Maaumbikizi katia njia na mfumo mzima wa mkojo,au kwa kitaalam Urinary track infection(UTI), hasa hasa watu wenye UTI hupata maumivu ya tumbo upande wa kushoto


5). Kupatwa na tatizo la Kidole tumbo au kwa kitaalam tunaita APPENDIX


6). Kupata matatizo kwenye utumbo mkubwa


7). Kupatwa na shida ya kukosa choo au kupata choo kigumu sana


8). Tumbo kujaa gesi


9). Kupatwa na tatizo la mawe ya Figo kwa kitaalam hujulikana kama Kidney stones


10). Kifuko cha nyongo kupasukia tumboni


11). Kupata matatizo ya Ini


12). Kupatwa na mchafuko wa tumbo ambao huchangiwa na sababu mbali mbali kama vyakula,Vinywaji, Maji, au kula kitu chenye Sumu


13). Kuziba kwa mirija ya Uzazi( blocked Fallopian tubes)


14). Kupatwa na shida ya uvimbe kwenye kizazi au kwenye vifuko vya mayai.


15). Maumivu ya tumbo chini ya kitovu kwa sababu ya HEDHI


16). Kupatwa na shida ya Mimba kutunga Nje ya Kizazi( Ectopic pregnancy)


17). Kupatwa na shida ya Mimba kuharibika


Ni matumaini yangu kwamba angalau umepata picha juu ya vyanzo mbali mbali vya maumivu ya tumbo, japo kwa ushauri zaidi,elimu au tiba tunaweza kuwasiliana kupitia namba +255758286584.

Karibu sana..!!!




0 Comment

AINA YA MAZOEZI MUHIMU KUFANYA KILA SIKUAfyaclass Bongo Social •

 MAZOEZI YA MWILI


Kuna aina nyingi sana za mazoezi ya mwili pamoja na Viungo. Lakini pia watu wengi hawajui umuhim wa kufanya Mazoezi ya mwili kila siku.


Aina za baadhi ya Mazoezi ni kama;


  • Kuna mazoezi ya kucheza Mpira,mfano; mpira wa miguu,kikapu n.k
  • Kuna mazoezi ya kuruka kamba
  • kuna mazoezi ya viungo tu
  • Kuna mazoezi ya Jim 
  • N.K

UMUHIMU WA KUFANYA MAZOEZI NI PAMOJA NA;

  1. Kuimarisha kinga ya Mwili na kukukinga na magonjwa mbalimbali
  2. Kuimarisha na kuleta nguvu katika misuli ya mwili
  3. Kuleta uhai katika seli hai za mwili
  4. Kuimarisha mzunguko wa damu hivo kusaidia vidonda kupona haraka,Mfano kwa mama ambaye alijifungua kwa Njia ya upasuaji
  5. Kusaidia kuondoa stress kwa Mtu
  6. Mazoezi huleta furaha
  7. Mazoezi hujenga Urafiki kati ya mtu na mtu
  8. Mazoezi husaidia kupunguza Uzito kwa wale ambao wana Uzito uliozidi.


JE WEWE UNAFANYA MAZOEZI?


@kwa ushauri zaidi,Elimu au Tiba tuwasiliane kwa namba +255758286584.




0 Comment

NGUO ZA NDANI NA UENEZAJI WA FANGASI SEHEMU ZA SIRIAfyaclass Bongo Social •

 Tambua kwamba, Nguo ya Ndani huweza kuwa chanzo kikubwa cha kukusababisha Upate Fangasi Sehemu za Siri.


Je inawezekanaje hii?


Kuvaa Nguo ya Ndani mbichi,au ambayo haijakauka vizuri hutengeneza mazingira mazuri kwa ajili ya Fangasi sehemu za Siri.


Wewe utakuja kuona dalili tu kama vile miwasho sehemu za Siri, au kwa wanawake hata uchafu wenye rangi kama maziwa na wenye harufu mbaya huanza kutoka ukeni


Epuka Tabia hii,Sio salama kwako


Kwa Ushauri zaidi,Elimu au Tiba pia tuwasiliane kwa namba +255758286584.




0 Comment

UGONJWA WA KICHOCHO,VISABABISHI VYAKE,DALILI,VIPIMO,MATIBABU NA MADHARA YAKEAfyaclass Bongo Social •

 UGONJWA WA KICHOCHO HUSABABISHWA NA NINI?


Huu ni ugonjwa ambao husababishwa na vimelea ambao kwa kitaalam hujulikana kama aina ya SCHISTOSOMA.


MTU HUAMBUKIZWAJE?


Ugonjwa huu huambikizwa kupitia maji yenye vimelea hivi vya SCHISTOSOMA vinapopenya kwenye Ngozi ya mtu.


DALILI ZA UGONJWA WA KICHOCHO


  1. Kupata maumivu makali ya Tumbo
  2. Kujisaidia kinyesi chepesi kilichochanganyika na Damu
  3. Kukojoa Damu wakati wa haja ndogo
  4. Kupatwa na hali ya kikihozi
  5. Kupata Homa
  6. Kuanza kuwashwa sana na Ngozi
  7. Pamoja na mwili kuchoka kupita kiasi

VIPIMO VYA KICHOCHO NI PAMOJA NA

  • kipimo cha Damu
  • Kipimo cha Mkojo
  • Kupigwa X-ray ya tumbo
  • Au kupigwa Ultrasound ya Tumbo


MATIBABU YA UGONJWA WA KICHOCHO


Ugonjwa huu hutibika kupitia Dawa aina ya PRAZIQUANTEL ambapo mgonjwa atapewa Dose moja tu,hilo tatizo litaisha.


MADHARA YA UGONJWA WA KICHOCHO


Ni pamoja na kupatwa na Magonjwa ya Figo pamoja na Saratani ya Kibofu cha Mkojo.



KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.




0 Comment

DALILI ZA UGONJWA WA KISUKARIAfyaclass Bongo Social •

 DALILI ZA KISUKARI


Kabla ya kujua dalili za ugonjwa huu wa kisukari, hebu tuangalia kidogo kuhusu vihatarishi vya kupata tatizo hili.

Vihatarishi hivo ni pamoja na;


- Kupendelea kula vyakula vya sukari nyingi


- Unywaji wa Pombe sana


-  Utumiaji wa baadhi ya mafuta ya kula


- Kwa ujumla wake mtindo mzima wa maisha au Lifestyle huweza kuchangia pia mtu kupatwa na ugonjwa kisukari


- Kongosho lenyewe kufeli au kushindwa kufanya kazi


- Unene au kuwa na uzito mkubwa sana


- Ulaji wa vyakula vya mafuta sana


- Kutokuushuhulisha mwili wako


- Kuna swala pia la umri


- Tatizo la presha pia huweza kusababisha mtu kupata ugonjwa wa kisukari


DALILI ZA UGONJWA WA KISUKARI

Dalili za kisukari ni pamoja na;


  • Uzito kupungua sana
  • Kupatwa na shida ya kukojoa kojoa mara kwa mara
  • Kuwa na njaa sana mara kwa mara
  • Kupatwa na shida ya kutokuona vizuri
  • Kupata kiu sana
  • Kupata uchovu sana wa mwili
  • Kupatwa na Ganzi miguuni pamoja na kwenye Mikono
  • Kushindwa kuhimili tendo la Ndoa vizuri

Kama una Dalili hizi, kutana na wataalam wa afya kwa ajili ya Vipimo na Msaada wa kimatibabu



KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.




0 Comment

TATIZO LA CHUPA YA UZAZI KUPASUKA MAPEMA KABLA YA WAKATI(PREMATURE RUPTURE OF MEMBRANE(PROM))Afyaclass Bongo Social •

 CHUPA YA UZAZI KUPASUKA MAPEMA


Hii ni mojawapo ya dalili za hatari kwa mama mjamzito ambapo kwa kitaalam huitwa premature rupture of membrane(PROM), Hivo basi endapo mjamzito kakutana na hali hii ni bora sana kukimbilia hospital kwa ajili ya kupata msaada zaidi.


BAADHI YA SABABU ZA CHUPA YA UZAZI KUPASUKA MAPEMA


- Maambukizi ya magonjwa mbali mbali au Infection kama vile za,UTI, FANGASI,PID, Kaswende(syphilis), N.K


- Kupatwa na shida ya kuanguka au kupigwa wakati wa ujauzito


- Hali ya maji kuwa mengi sana katika tumbo la uzazi hivo kupelekea mgandamizo au presha kubwa ndani ya tumbo la uzazi(polyhdrominous)


- Uwepo wa watoto zaidi ya mmoja tumboni(multiple pregnancy), kama vile mapacha, watoto watatu N.K


KUMBUKA; mama ambaye chupa ya uzazi imeshapasuka yupo katika hatari ya kupata maambukizi mengine ambayo huweza kupenya na kupita moja kwa moja kwenda kwa mtoto aliyetumboni na kumsababishia madhara makubwa.


Inashauriwa mama baada ya kupatwa na shida hii ya chupa kupasuka mapema,azalishwe  mapema ili kumuokoa yeye na mtoto aliyetumboni pia.



Kwa Ushauri zaidi,elimu au tiba tuwasiliane kwa namba +255758286584 tuma ujumbe au piga simu utasikilizwa na kusaidiwa.




0 Comment
Notification
Karibu Afyaclass Bongo Social Jukwaa linalojadili mambo mbali mbali ikiwemo afya,Magonjwa na Updates Zote,Tembelea hapa kila Siku,Pia Share Maoni yako kwenye jukwaa hili Afyaclass Bongo Social ASANTE.
UNDERSTOOD