Daktari atupwa jela kwa kuwabaka mamia ya watoto

Daktari atupwa jela kwa kuwabaka mamia ya watoto

#1

Daktari atupwa jela kwa kuwabaka mamia ya watoto



Mahakama ya Ufaransa imetoa kifungo cha juu cha miaka 20 jela kwa daktari bingwa wa upasuaji ambaye alikiri kuwadhulumu kingono mamia ya wagonjwa, wengi wao wakiwa watoto, kwa zaidi ya miongo miwili.

Kesi hiyo iliyodumu kwa miezi mitatu ya Joel Le Scouarnec, mwenye umri wa miaka 74, imefichua ukubwa wa uhalifu wake na mateso ya waathiriwa lakini pia imezusha maswali kwa nini juhudi zaidi hazikufanywa mapema ili kumzuia. Amepatikana na hatia ya kuwadhulumu kingono na kuwabaka wagonjwa 229 katika kliniki yake mjini Vannes. 

Le Scouarnec, mmoja wa wanyanyasaji wakubwa wa kingono waliopatikana na hatia katika historia ya Ufaransa, alikuwa tayari gerezani baada ya kuhukumiwa mwaka 2020 adhabu ya miaka 15 kwa kuwabaka na kuwadhalilisha kingono watoto wanne, wakiwemo wapwa zake wawili.

Hukumu ya miaka 20 jela kwa uhalifu mkubwa wa ubakaji iliyotolewa na hakimu mfawidhi Aude Buresi ndiyo ya juu zaidi ambayo inaweza kutolewa nchini Ufaransa kwa shtaka la ubakaji uliokithiri, ambapo hukumu hazijumuishwi pamoja kwa kila kosa alilofanya. Le Scouarnec hatakuwa na haki ya kuomba kuondoka jela kabla ya kifungo chake kukamilika, hadi atakapotumikia theluthi mbili ya hukumu yake ambayo ni sawa na miaka 13.

Reply


image quote pre code