Je,Vijana waendelee kupiga Supu ya PWEZA au waache?
Akizungumzia kuhusu faida za pweza, daktari wa tiba ya chakula kutoka hospitali ya KCMC, Japhari Mwijae amesema pweza ni moja ya viumbe wa baharini ambavyo vina protini nyingi inayoitwa ‘arginine.’
Amesema protini hiyo huwa ina kichocheo mwilini na huwa inatoa kemikali inayoitwa ‘nitric oxide’ inayosaidia kupanua mishipa ya damu, kuboresha mtiririko wa damu na kuimarisha nguvu za kiume kupitia mzunguko wa damu.
Dk Mwijae amesema unywaji wa supu ya pweza mara kwa mara, pia unasaidia mzunguko wa damu kuwa mzuri na kwenda kwenye ubungo na sehemu nyingine za moyo.
“Pweza ana madini ya zinki yanayoingia kwenye mwili na inachochea utengenezwaji wa homoni ya ‘testosterone’ ambayo ndio inamfanya mwanamume kuwa na nguvu na hamu ya tendo la ndoa,” amesema Dk Mwijae.
Pia, amesema madini ya zinki yanasaidia kulinda mbegu za mwanamume na kuimarisha nguvu za kiume kwa hali ya ubora, kiasi cha ujazo wake hadi kulifikia yai la kike.
Dk Mwijae amesema pweza anaweza kuwa na mchango mzuri katika afya ya mwanamume kwa jumla kutokana na virutubisho alivyonavyo, lakini si tiba ya moja kwa moja ya kuongeza nguvu za kiume.
REPLY HAPA
image quote pre code