CHANZO CHA KUCHA KUWA NGUMU KAMA BATI

CHANZO CHA KUCHA KUWA NGUMU KAMA BATI

#1

 KUCHA

• • • • • 

CHANZO CHA KUCHA KUWA NGUMU KAMA BATI


Tatizo hili huhusisha kucha kuwa nene na ngumu kupita kawaida, je chanzo chake ni nini?


CHANZO CHA KUCHA KUWA NGUMU KAMA BATI


- Moja ya sababu ya tatizo hili la kucha kuwa ngumu kupita kawaida ni pamoja na;

✓ Maambukizi ya Fangasi ambayo hujulikana kwa kitaalam kama ONYCHOMYCOSIS,


Maambukizi ya YEAST n.k


✓ Kuumia kwenye kucha mara kwa mara, tatizo ambalo huwapata sana watu wa michezo kama vile; Wachezaji wa mpira wa Miguu n.k


✓ Yellow nail syndrome, tatizo ambalo husababisha kucha kubadilika rangi na kuwa manjano na hatimaye kucha kuanza kujikunja na kuwa nene


✓ Matatizo kwenye mfumo wa kinga ya mwili yaani Autoimmune disorder kama vile PSORIASIS,

huweza kusababisha kucha kuwa na mikunjo pamoja na kuwa ngumu


✓ Tatizo la kwenye ngozi kama vile Paronychia ambalo husababisha wekundu kuzunguka kucha pamoja na Kuvimba


✓ Pia tatizo hili la kucha kuwa Ngumu huwapata sana watu ambao wana Umri mkubwa


MATIBABU YA TATIZO LA KUCHA KUWA NGUMU

- tiba ya tatizo hili hutegemea na chanzo chake,Mfano kama chanzo ni maambukizi ya fangasi,basi mgonjwa hupewa dawa za fangasi N.k



KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.




Consultation ya Afya Moja kwa Moja

Mimi ni Dr. Ombeni Mkumbwa. Nakupa ushauri wa kitaalamu kuhusu tatizo lolote la kiafya kwa siri, haraka na uhakika.

WhatsApp

Changia Mada hapa(Reply)


image quote pre code