Showing posts with label Habari za michezo. Show all posts
Showing posts with label Habari za michezo. Show all posts

Mshambuliaji wa Real Madrid Gonzalo Garcia ameshinda tuzo ya mfungaji boraAfyaclass Forum •

Mshambuliaji wa Real Madrid Gonzalo Garcia ameshinda tuzo ya mfungaji bora wa mashindano ya kombe la dunia la vilabu 2025.

Kinda huyo ameibuka mfungaji bora baada ya kufunga jumla ya mabao manne katika michuano hiyo mikubwa iliyotamatika siku ya leo kwa klabu ya Chelsea ya nchini Uingereza kutawazwa kuwa mabingwa.




0 Comment

Cr7 Avunja Ukimya Kuhusu Kutohudhuria Mazishi Ya Diogo JotaAfyaclass Forum •

kumeibuka mjadala mkubwa kuhusu kutokuwepo kwa Cristiano Ronaldo kwenye mazishi ya Mchezaji mwenzake wa Timu ya Taifa ya Ureno, Diogo Jota, aliyefariki Dunia pamoja na kaka yake, André Silva, katika ajali ya Gari huko Zamora, Hispania, Julai 3, 2025.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka Gazeti la Record la Ureno, Ronaldo aliamua kutohudhuria mazishi hayo kutokana na maumivu ya kihisia aliyoyapata baada ya kumpoteza Baba yake, José Dinis Aveiro, mwaka 2005. Tukio hilo lilimuathiri sana, na tangu wakati huo amekuwa akiepuka kuhudhuria hafla za mazishi za Watu wa karibu ili kuepuka kurejea katika hali hiyo ya huzuni.

Gazeti la Mirror Football liliripoti kuwa CR7 alihofia uwepo wake ungeweza kuvuruga utaratibu wa mazishi hayo kutokana na mvuto wake mkubwa kwa vyombo vya habari na Mashabiki. Aliona kuwa ni vyema kutoa nafasi kwa familia ya Jota kuomboleza kwa utulivu na faragha. Ingawa hakuwepo kimwili, Ronaldo alitoa pole zake kwa familia ya Jota kupitia mitandao ya kijamii, akieleza:

"Haieleweki. Tulikuwa pamoja hivi karibuni katika Timu ya Taifa, na ulikuwa umeoa tu. Kwa familia yako, Mkeo na Watoto wako, natuma rambirambi zangu na kuwatakia nguvu zote za Dunia. Najua utakuwa nao daima. Pumzikeni kwa amani, Diogo na André. Tutawakumbuka daima."

Pia, Ronaldo aliahidi kuwa karibu na familia ya Jota na kuwasaidia kadri watakavyohitaji katika kipindi hiki kigumu.

Kutokuwepo kwa Ronaldo kwenye mazishi hayo kuliibua hisia mseto miongoni mwa Mashabiki na vyombo vya habari. Baadhi walielewa uamuzi wake, wakizingatia sababu alizotoa, huku wengine wakieleza masikitiko yao kwa kutomwona Nahodha wa Timu ya Taifa akitoa heshima za mwisho kwa Mchezaji mwenzake.

Uamuzi wa Cristiano Ronaldo kutohudhuria mazishi ya Diogo Jota ulitokana na sababu za kihisia na nia ya kutoa nafasi kwa familia ya Marehemu kuomboleza kwa utulivu. Licha ya kutokuwepo kimwili, Ronaldo alionesha mshikamano na familia ya Jota kwa njia nyingine, ikiwa ni pamoja na kutoa pole zake na kuahidi msaada kwa familia hiyo.

0 Comment

Wachezaji kandanda Diogo Jota na André Silva Wapewa heshima zao za mwishoAfyaclass Forum •

Wachezaji kandanda Diogo Jota na André Silva wamepewa heshima zao za mwisho na familia zao, marafiki na wachezaji wenzao kwenye mazishi ya pamoja nchini Ureno.



Jota, 28, alizikwa pamoja na kaka yake, Silva, 25, baada ya kufariki kwenye ajali ya gari siku ya Alhamisi.

Maafisa wanasema gari lao lilitoka nje ya barabara kutokana na tairi kupasuka huku likipita gari jingine.

Habari hizo ziliuacha ulimwengu wa soka katika mshtuko huku wengi wakiacha risala zao za rambirambi katika vilabu ambavyo alikuwa amecheza.

Jota alikuwa njiani kurejea Liverpool kwa ajili ya mazoezi ya kabla ya msimu mpya, akisafiri kwa gari na feri kwa sababu alikuwa amefanyiwa upasuaji mdogo hivyo madaktari walimshauri asisafiri kwa ndege.

Alikuwa ameoa mpenzi wake wa muda mrefu Rute Cardoso, ambaye alizaa naye watoto watatu, siku 11 tu zilizopita.

0 Comment

Rais wa Marekani Donald Trump ametangaza kuandaa pambano la ngumi WhitehouseAfyaclass Forum •

Rais wa Marekani Donald Trump ametangaza mpango wa kuandaa pambano la UFC katika viwanja vya Ikulu ya White House kama sehemu ya maadhimisho ya miaka 250 ya uhuru wa Marekani mwaka ujao.



Akizungumza katika tamasha la “America 250” lililofanyika kwenye viwanja vya maonyesho ya jimbo la Iowa, Trump alisema:

“Kila moja ya maeneo yetu ya kitaifa ya kihistoria na vita vitakuwa na matukio maalum kuadhimisha America 250. Na tutakuwa na pambano la UFC — fikiria hilo — katika viwanja vya White House.”

Msemaji wa Ikulu, Karoline Leavitt, alithibitisha mpango huo na kusema kuwa rais “yuko makini kabisa” kuhusu wazo hilo. Msemaji wa UFC pia aliambia CNN kuwa wako kwenye majadiliano na Ikulu kuhusiana na tukio hilo, lakini hawakuwa na maelezo zaidi kwa sasa.

Trump ana uhusiano wa muda mrefu na shirika la UFC pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wake, Dana White. Uhusiano wao ulianza tangu 2001, wakati White alipokuwa na changamoto za kupata ukumbi wa kuandaa pambano la UFC na Trump akaamua kulifanyia kwenye Trump Taj Mahal, Atlantic City.

0 Comment

Ukimya wa Dakika 1 kwenye Mechi kumuenzi Diogo JotaAfyaclass Forum •

#MICHEZO: UEFA imeidhinisha ombi lililotolewa na FA ya Ureno kuhusu kuwepo na dakika 1 ya ukimya kwenye mechi ya timu ya Taifa ya Ureno dhidi ya Uhispania katika mchezo wa Euro 2025 kwa Wanawake utakaopigwa hii leo Alhamis Saa 4.00 Usiku kufuatia kifo cha kushtua cha Diogo Jota.



Mshambuliaji huyo wa Liverpool ameaga dunia alfajiri ya leo baada ya kupata ajali ya gari akiwa barabarani kaskazini-magharibi mwa Uhispania pamoja na mdogo wake Andre ambaye naye pia amepoteza maisha.

Wakati ulimwengu wa soka ukiendelea kuomboleza vifo vya nyota hao wote wawili, imeripotiwa kuwa sasa kutakuwa na salamu za heshima kwa dakika moja ya ukimya kabla ya mechi hiyo ya EURO 2025 usiku wa leo kama ishara ya kuwaenzi nyota hao wawili.

Mechi gani hutaisahau ambayo amewahi kucheza Diogo Jota?

#DiogoJota

0 Comment

Diogo Jota amefariki dunia kwa AjaliAfyaclass Forum •

MADRID, Hispania: MSHAMBULIAJI wa mabingwa wa Ligi Kuu England, Diogo Jota amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika ajali ya gari akiwa na umri wa miaka 28.



Idara ya Ulinzi wa Kiraia ya Hispania imesema pia ndugu wa Jota, Andre Silva amefariki katika ajali hiyo iliyotokea katika Valladolid uliopo Jimbo la Zamora.

Mshambuliaji wa Liverpool, Diogo Jota, amefariki dunia katika ajali ya gari akiwa na umri wa miaka 28.

Jota alifunga ndoa na mchumba wake wa muda mrefu, Rute Cardoso, ambaye wana watoto watatu pamoja, mwezi uliopita tu.

Ndugu yake, Andre Silva, ambaye ni mshambuliaji wa timu ya taifa ya Ureno, pia alifariki katika ajali hiyo ambayo ilitokea katika jimbo la Zamora, nchini Hispania.

Silva, mwenye umri wa miaka 26, alikuwa pia mchezaji wa kandanda wa kulipwa katika klabu ya daraja la pili ya Ureno, Penafiel.

0 Comment

Aliyekuwa kocha mkuu wa Klabu ya Yanga,Miloud Hamdi ameteuliwa kuwa kocha mkuu wa Klabu ya Ismaily SC ya MisriAfyaclass Forum •

Aliyekuwa kocha mkuu wa Klabu ya Yanga  ya Tanzania, Miloud Hamdi (54), raia wa Algeria, ameteuliwa rasmi kuwa kocha mkuu wa Klabu ya Ismaily SC ya Misri kwa mkataba wa mwaka mmoja, ukiwa na kipengele cha kuongeza mwaka mmoja zaidi endapo pande zote zitakubaliana.



Hamdi anajiunga na Ismaily akitokea Yanga , ambako aliandika historia ya kipekee kwa kuiwezesha klabu hiyo kutwaa mataji matatu makubwa katika msimu wa 2024/2025. Chini ya uongozi wake, Yanga ilinyakua ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Kombe la Shirikisho la CRDB (FA Cup), na Kombe la Muungano.

Kuteuliwa kwa Hamdi kunakuja wakati Ismaily SC ikisaka kurejesha heshima yake katika soka la Misri, ikiwa ni mojawapo ya vilabu vyenye historia ndefu na mafanikio ya muda mrefu katika bara la Afrika.

Hatua hiyo pia inaashiria mwanzo mpya kwa Yanga , ambayo sasa italazimika kusaka kocha mpya atakayeendeleza mafanikio na ramani ya ushindani kimataifa ambayo Hamdi ameijenga.

Kocha huyo mwenye uzoefu, ambaye amewahi pia kuzinoa klabu kadhaa barani Afrika na Asia, anatarajiwa kuanza kazi mara moja akiungana na kikosi cha Ismaily kujiandaa kwa msimu mpya wa Ligi Kuu ya Misri.

0 Comment
Notification
My blog is in the process of editing and perfecting the new template, so there are still some functions to click but not yet used. Note which blogs associated with your side please read this lesson to update the blog logo.
UNDERSTOOD