Wachezaji kandanda Diogo Jota na André Silva Wapewa heshima zao za mwisho

Wachezaji kandanda Diogo Jota na André Silva Wapewa heshima zao za mwisho

#1

Wachezaji kandanda Diogo Jota na André Silva wamepewa heshima zao za mwisho na familia zao, marafiki na wachezaji wenzao kwenye mazishi ya pamoja nchini Ureno.



Jota, 28, alizikwa pamoja na kaka yake, Silva, 25, baada ya kufariki kwenye ajali ya gari siku ya Alhamisi.

Maafisa wanasema gari lao lilitoka nje ya barabara kutokana na tairi kupasuka huku likipita gari jingine.

Habari hizo ziliuacha ulimwengu wa soka katika mshtuko huku wengi wakiacha risala zao za rambirambi katika vilabu ambavyo alikuwa amecheza.

Jota alikuwa njiani kurejea Liverpool kwa ajili ya mazoezi ya kabla ya msimu mpya, akisafiri kwa gari na feri kwa sababu alikuwa amefanyiwa upasuaji mdogo hivyo madaktari walimshauri asisafiri kwa ndege.

Alikuwa ameoa mpenzi wake wa muda mrefu Rute Cardoso, ambaye alizaa naye watoto watatu, siku 11 tu zilizopita.

Related Discussions

REPLY HAPA


image quote pre code