Fahamu kuhusu Magonjwa hatari zaidi ya zinaa kwa Sasa
Kulingana na Shirika la Afya Duniani (WHO), Maambukizi ya Zinaa (STIs) ni tatizo kubwa la afya duniani, huku zaidi ya kesi milioni moja za magonjwa ya zinaa yanayotibika zikipatikana kila siku.
Maambukizi haya ambayo huenezwa kwa njia ya kujamiiana; kupitia uke, sehemu ya nyuma, na ngono ya mdomo yanaweza kusababisha matatizo makubwa ya kiafya.
Ifuatayo ni orodha ya magonjwa matano ya zinaa hatari zaidi:
1. HIV/AIDS
UKIMWI ni ugonjwa sugu wa mfumo wa kinga unaosababishwa na virusi vya ukimwi (VVU).
Kulingana na WHO, VVU huharibu mfumo wa kinga na huingilia uwezo wa mwili wa kupambana na maambukizi na magonjwa.
VVU vinaweza kuambukizwa kwa kugusa damu iliyoambukizwa, shahawa, au maji maji ya ukeni. Hakuna tiba ya VVU/UKIMWI, lakini dawa zinaweza kudhibiti maambukizi na kuzuia kuendelea kwa maradhi.
Baadhi ya watu wenye VVU hupata dalili kama za mafua wiki 2 hadi 4 baada ya kupata virusi. Watu wanaotumia dawa za VVU wanaweza wasiwe na dalili nyingine kwa miaka.
Virusi huongezeka na kuharibu seli za kinga, dalili zinaweza kutokea kama vile homa, uchovu, na nodi za lymph kuvimba.
Bila kutibiwa, VVU kwa kawaida hubadilika na kuwa UKIMWI katika takriban miaka 8 hadi 10, na hivyo kuufanya mwili kuwa katika hatari ya kuambukizwa magonjwa yanayonyemelea.
2. Homa ya Ini (Hepatitis B na C)
Hepatitis B na C ni magonjwa ya virusi ambayo husababisha kuvimba kwa ini. Yote husambazwa kupitia damu, lakini hepatitis B pia inaweza kuenea kupitia majimaji mengine ya mwili kama shahawa.
Magonjwa yote mawili yanaweza kusababisha maambukizo ya papo hapo (ya muda mfupi) au sugu (ya muda mrefu). Hepatitis B na C sugu zinaweza kusababisha shida kubwa za ini kama kile maradhi ya cirrhosis na saratani ya ini.
Maradhi hayo pia yanaweza kuenezwa kutoka kwa mama hadi kwa mtoto wakati wa kuzaliwa, kwa njia ya kujamiiana, na kwa kutumia sindano moja au vifaa vingine vya kudunga dawa za kulevya kwa zaidi ya mtu mmoja.
3. Herpes {Malengelenge}
Virusi vya Herpes simplex (HSV) ni maambukizi ya virusi ambayo husababisha vidonda kwenye sehemu za siri au mdomo.
Ni maambukizi ya kawaida ambayo yanaweza kusababisha malengelenge yenye uchungu au vidonda. Kimsingi huenea kwa kugusa ngozi hadi ngozi.
Kuna aina mbili za virusi vya herpes simplex.
Aina ya 1 (HSV-1) mara nyingi huenea kwa mguso wa mdomo na kusababisha maambukizo ndani au karibu na mdomo (malengelenge ya mdomo au vidonda vya baridi).
Inaweza pia kusababisha malengelenge ya sehemu za siri. Watu wazima wengi wameambukizwa na HSV-1.
Aina ya 2 (HSV-2) huenea kwa kujamiiana na husababisha malengelenge sehemu za siri.
4. Kaswende
Kaswende ni maambukizo ya bakteria ambayo yanaweza kusababisha vidonda kwenye sehemu za siri, au mdomo, na pia yanaweza kuenea katika sehemu nyingine za mwili ikiwa haitatibiwa.
Ugonjwa huu ni ugonjwa unaozuilika na unaotibika wa magonjwa ya zinaa (STI). Ikiwa haijatibiwa, inaweza kusababisha shida kubwa za kiafya.
Watu wengi wenye kaswende hawana dalili au hawazitambui.
Kaswende wakati wa ujauzito inaweza kusababisha kuzaliwa mfu, vifo vya watoto wachanga na watoto kuzaliwa na kaswende (ya mazazi).
Matumizi sahihi na ya mara kwa mara ya kondomu wakati wa kujamiiana yanaweza kuzuia kaswende.
Vipimo vya haraka vinaweza kutoa matokeo kwa dakika chache, ambayo inaruhusu kuanza kwa matibabu mtu anapotembelea kituo cha afya.
5. Clamydia
Klamidia ni maradhi ya zinaa (STI) yanayosababishwa na bakteria Chlamydia trachomatis.
Ni maambukizi ya kawaida ambayo yanaweza kutibiwa kwa dawa za antibiotics, lakini yakiachwa bila kutibiwa, yanaweza kusababisha matatizo makubwa ya afya, hasa kwa wanawake.
Ugonjwa huu husambazwa kupitia majimaji ya mwili kama maji ya ukeni na shahawa. Chlamydia mara nyingi haina dalili, hivyo ni vigumu kutambua. Hata hivyo, dalili zinapoonekana, zinaweza kujumuisha kutokwa na majimaji yasiyo ya kawaida katika uke au urethra, maumivu wakati wa kukojoa, na katika baadhi ya matukio, maumivu chini ya tumbo au korodani.
KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU NA TIBA JUU YA TATIZO LOLOTE TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.
Source Used:WHO,BBC
Reply
image quote pre code