Mtoto Azaliwa ndani ya Ndege na kupewa tiketi ya bure ya Kusafiri ndani ya ndege Maisha yake yote

Mtoto Azaliwa ndani ya Ndege na kupewa tiketi ya bure ya Kusafiri ndani ya ndege Maisha yake yote

#1

Mwaka 2022 Mwanamke mmoja raia wa Yemen, Hiyam Nasr Naji Daaban, alijifungua akiwa ndani ya ndege ya EgyptAir iliyokuwa ikisafiri kutoka London kuelekea Cairo mnamo Septemba 16. Akiwa angani katika anga la Ujerumani, Daaban alianza uchungu wa uzazi na rubani akaomba kibali cha kutua kwa dharura mjini Munich, lakini mama huyo alijifungua kabla ya ndege kutua. 



Baada ya tukio hilo, kampuni ya EgyptAir ilitangaza kumpa mtoto huyo tiketi ya kusafiri bure maisha yake yote kwa ndege zao kama zawadi maalum. Picha ya mtoto huyo pamoja na salamu za pongezi kwa mama Daaban na mwenyekiti wa EgyptAir, Rushdi Zakaria, zilitumwa kupitia Twitter ya kampuni hiyo. 

Tukio hili linafuatia matukio mengine ya watoto kuzaliwa angani, ikiwemo mtoto aliyezaliwa ndani ya ndege ya Jet Airways mwaka 2017 na kupewa tiketi ya maisha, huku baadhi ya mashirika mengine kama Emirates yakiwa hayajatoa zawadi kama hiyo kwa watoto waliozaliwa katika ndege zao.

Related Discussions

REPLY HAPA


image quote pre code