Niliteseka na maumivu ya tumbo – ndipo nikagundua ni Ugonjwa wa amoeba

Niliteseka na maumivu ya tumbo – ndipo nikagundua ni Ugonjwa wa amoeba

#1

Niliteseka na maumivu ya tumbo – ndipo nikagundua ni Ugonjwa wa amoeba

Mimi naitwa Amani kutoka Mkoa wa Dodoma nchini Tanzania,Katika Hali ambayo haikuwa ya kawaida,nilianza kupata maumivu ya Tumbo hali ambayo ilinisumbua kwa muda wa Zaidi ya wiki 2,

Maumivu haya ya tumbo yaliambatana na kuharisha choo kama cha Makamasi,hali ambayo ilishtua sana.

Baada ya kuona hali hii,nilianza kufuatilia ni kitu gani hiki kinaendelea kwenye Mwili wangu? Nikakutana na Mtu mmoja "rafiki yangu",akaniambia tunajaribu kuangalia Mtandaoni hizi ni dalili za Kitu gani? tukiangia mtandao wa Google, ndipo nilipokutana na Makala kutoka Afyaclass ikielezea Dalili hizi kwa Kina, ndipo nikaamua kutafuta Msaada kwao na kupata Ushauri na kupona kabsa tatizo Langu.

Kwa Idhini ya Mgonjwa,aliomba Ujumbe huu uandikwe ili kusaidia wengine kujifunza na kupata msaada wa kupona ikiwa wana tatizo kama lake Amani lililompata.

Maelezo kutoka kwa Dr.Ombeni wa Afyaclass: 

Zipo Cases nyingi za Aina hii ambazo tunazipata kila Siku, Lakini kwa Uzoefu niloupata asilimia 80% ya Wagonjwa wa amoeba ambao nilikutana nao;Wengi wao walikuwa na Dalili hizi;

Maumivu ya tumbo,Kuharisha,Choo kuwa kama chenye Makamasi, Kukosa hamu ya kula,na baadhi yao kupata Kichefuchefu na kutapika. Sasa, Je Ugonjwa wa Ameoba ni Ugonjwa gani?

Ugonjwa wa amoeba au amoebiasis ni ugonjwa unaosababishwa na kimelea(parasite) kinachoitwa Entamoeba histolytica. Entamoeba histolytica  ni kimelea kwenye kundi la anaerobic parasite na kwa mara ya kwanza hupatikana kwenye Utumbo mpana(colon);

Kimelea hiki kinaishi kwenye Utumbo wa binadamu na kinaweza kusababisha ugonjwa wa amoeba kwa mtu yeyote anayekula au kunywa kitu kilichoambukizwa na kimelea hiki.

Dalili Kubwa za Ugonjwa huu wa Amoeba ni pamoja na;

- Mgonjwa kujisaidia kinyesi chenye vitu kama makamasi

- Mgonjwa kuanza kupata maumivu ya tumbo sana mithili ya tumbo kusokota

- Mgonjwa kuanza kujisaidia choo kilaini sana

- Mgonjwa kuharisha au kujisaidia haja kubwa ya maji maji sanaa

- Mgonjwa kujisaidia kinyesi ambacho kimechanganyika na damu

- Mgonjwa kutoa hewa kwa njia ya haja kubwa mara kwa mara(kujamba)

- Mgonjwa kupata maumivu ya tumbo,Kifua na viungo mbali mbali vya mwili

- Joto la mwili la mgonjwa kupanda au mgonjwa kuwa na Homa

- Mgonjwa kupatwa na tatizo la kupungukiwa na damu 

- Kupoteza appetite ya chakula kabsa

- Mgonjwa kupatwa na hali ya kichefu chefu pamoja na kutapika

- Mgonjwa kupungua uzito wa mwili na kukonda

NB:Hizi ni Miongoni mwa Dalili kubwa ambazo tunaziona kwa Wagonjwa wenye Vimelea hivi vya Amoeba, Na Ukifuatilia historia ya Ugonjwa wao(Patient history) ulivyoanza asilimia 88% wanaishi kwenye mazingira ambayo maji sio Salama,wala mazingira ya maandalizi ya Vyakula Sio Masafi Pia.

Ushauri wangu kwako,hakikisha Unakunywa maji Safi,Chakula kiwe Safi,Vyoo Safi utakuwa Salama....

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Changia Mada hapa(Reply)


image quote pre code