Ugonjwa wa fizi,chanzo,Dalili na Tiba

Ugonjwa wa fizi,chanzo,Dalili na Tiba

#1

Ugonjwa wa fizi,chanzo,Dalili na Tiba

Hapa tunazungumzia matatizo ambayo huathiri Tishu zinazozunguka Meno yako.

Huu ni ugonjwa ambao huathiri sehemu ya fizi na huhusisha matokeo mbali mbali kama vile kuvimba kwa fizi, Fizi kutoa damu, Fizi kuuma N.K

CHANZO CHA UGONJWA WA FIZI

Zipo Sababu mbali mbali zinazopelekea Mtu kupata shida ya Fizi ikiwemo;

- Mtu kushambuliwa na magonjwa mbali mbali ambayo huathiri tisu za meno maarufu kama Periodontal diseases

- Mashambulizi ya vimelea mbali mbali vya magonjwa kama vile; Bacteria,fangasi,virusi N.K

- Kuumia kwa tisu za meno au fizi kutokana na sababu mbali mbali kama vile; Kuchomwa na kitu cha ncha kali N.K

- Mtu mwenye ugonjwa wa kisukari ambao ni ngumu kuudhibiti yupo kwenye hatari pia ya kupatwa na magonjwa ya Fizi

Dalili za Ugonjwa wa Fizi

DALILI ZA UGONJWA WA FIZI NI PAMOJA NA;

1. Mgonjwa kupata maumivu makali ya kwenye fizi hasa wakati wa kula kitu chochote.

2. Fizi za mgonjwa kutoa damu.

3. Fizi za mgonjwa kubadilika rangi na kuwa nyekundu sana kuliko kawaida.

4. Mgonjwa kupatwa na shida ya Fizi kuvimba.

5. Kuwa na vidonda au michubuko kwenye ngozi ya fizi. n.k

MATIBABU YA UGONJWA WA FIZI

- Zipo dawa mbali mbali ambazo hutumika kutibu ugonjwa huu japo hutegemea chanzo husika cha ugonjwa huu.

Hivo ni vizuri mgonjwa kupata uchunguzi kwa kina pamoja na kupata matibabu sahihi kulingana na Shida yake.

KUMBUKA; Usafi wa kinywa ni muhimu sana ili kusaidia kuondoa uchafu wa chakula au mabaki ya chakula, kusaidia kuondoa harufu mbaya mdomoni pamoja na kukukinga na magonjwa mbali mbali ya Fizi.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

REPLY


image quote pre code