Amuua mwenza wake kwa kumshutumu kumuambukiza UKIMWI

Amuua mwenza wake kwa kumshutumu kumuambukiza UKIMWI

#1

Amuua mwenza wake kwa kumshutumu kumuambukiza UKIMWI







Jeshi la Polisi Mkoa wa Mara, linamshikilia Samwel Emmanuel maarufu Nzaliya (20) mkazi wa kijiji cha Nata Wilaya ya Serengeti kwa tuhuma za mauaji ya Josephina Magani( 52).

Kwa mujibu wa Taarifa ya Kamanda wa Polisi mkoani humo,  Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Pius Lutumo, amesema tukio limetokea Mei 7, 2025 majira  ya saa saba usiku  katika kitongoji cha Mamaswe Kijiji cha Nata, ambapo  Emmanuel   alimchoma Josephina kwa kutumia kitu chenye ncha kali  maeneo ya tumboni  na kusababisha  kumwaga damu nyingi na kupelekea kufariki dunia.

“ Mtuhumiwa mara baada ya Kutenda kosa hilo aliuburuza mwili wa marehemu kutoka nyumbani kwake na kuutumbukiza  kwenye shimo ambalo lilikuwa linatumika kwa ajili ya shughuli  za uchimbaji madini ya dhahabu” amesema Kamanda Lutumo.

Ameongeza kuwa  uchunguzi wa awali umebaini chanzo cha tukio ni ugomvi baina ya marehemu na mtuhumiwa kwa kile  kilichodaiwa kuwa ni mtuhumiwa  alikuwa anamshtumu marehemu kumuambukiza maradhi ya ugonjwa wa ukimwi  kwani walikuwa wakiishi kama mume na mke.

 Kutokana na tukio hilo, Jeshi la Polisi linatoa wito kwa wananchi kuacha tabia ya kujichukulia sheria mkononi na badala yake watoe taarifa  kwa vyombo husika ili malalamiko yaweze kushughulikiwa kisheria.

Reply


image quote pre code