Aliyekuwa Mbunge wa viti maalum Ester Bulaya amechukua fomu ya kuwania Ubunge wa jimbo la Bunda mkoani Mara kupitia Chama cha Mapinduzi CCM.
Ester Bulaya amechukua fomu hiyo leo June 30 2025, akilenga kuchuana na watia nia wengine akiwemo Mbunge wa jimbo hilo anayemaliza muda wake Robert Maboto.
Ester Bulaya kabla kurejea CCM amewahi kuwa Mbunge wa Vijana kupitia CCM Mwaka 2010, na baadae kwenda Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA na kuwa Mbunge wa kuchaguliwa Mwaka 2010 -2015 jimbo hilo kupitia CHADEMA, Mwaka 2010 - 2020 Mbunge wa Viti Maalum.
Leo Bulaya amekabidhiwa fomu ya kutia nia ya Ubunge ndani ya chama hicho na Katibu wa CCM Wilaya ya Bunda, Evodia Zumba.
REPLY HAPA
image quote pre code