Kwanini Watu hujitolea kuambukizwa magonjwa

Kwanini Watu hujitolea kuambukizwa magonjwa

#1

Kujaribu matibabu mapya au chanjo mpya kunaweza kuchukua miaka mingi, ikiwa sio miongo kukusanya taarifa za kutosha, kwa hivyo wanasayansi wanageukia njia yenye utata ambayo inahusisha kuwaambukiza makusudi virusi hatari, vimelea na bakteria watu waliojitolea.



Mwaka 2017 kulikuwa na kundi la vijana waliokuwa wakisubiri kushambuliwa na mbu waliobeba vimelea vinavyoua zaidi ya watu 600,000 kila mwaka.

Kundi hilo lilikubali kushiriki majaribio ya matibabu katika Taasisi ya Jenner ya Chuo Kikuu cha Oxford, ili kupima chanjo mpya dhidi ya malaria. Chanjo hiyo - inajulikana kama "R21."

Taasisi hiyo imekuwa ikifanya majaribio ya chanjo ya mbu tangu 2001. Kila mtu aliyejitolea aliingizwa katika maabara. Juu ya meza ndani ya maabara, kulikuwa na bakuli dogo, kama umbo la kikombe cha kahawa, na kifuniko cha kitambaa chembamba juu.

Ndani yake kuna mbu watano waliokuwa wakipiga kelele, kutoka Amerika Kaskazini, ambao walikuwa wameambukizwa vimelea vya malaria. Mtu aliyejitolea anaweka mkono wake juu ya kibakuli ili mbu waweze kumtafuna, wakiuma kupitia kitambaa chembamba na kuingia kwenye ngozi ya mtu aliyejitolea.

REPLY HAPA


image quote pre code