Head

✍️Author: Dr. Ombeni
🛡️Review: AfyaClass

Ukimeza chakula vibaya na ukapaliwa (choking), zifuatazo ni hatua za haraka za kujiokoa:

Ikiwa UMEPALIA WEWE MWENYEWE:

JARIBU KUKOHOA KWA NGUVU

Kohoa kwa nguvu mara kadhaa ili kujaribu kusukuma chakula kilichokwama kutoka kwenye koo.

JIPIGE MGONGONI

Tumia mkono mmoja jipige mgongoni kwa nguvu.

TUMIA "ABDOMINAL THRUST" (Heimlich Maneuver):

Simama na jiweke mikono katikati ya tumbo, chini ya mbavu.

bana kwa nguvu ndani na juu (kama unataka kutoa kitu).

Rudia mara kadhaa (5 au zaidi) hadi chakula kitoke.

KUMBUKA:

Ukiona mtu hawezi kuongea,kashindwa kabsa kupumua,au kapoteza fahamu, hiyo ni dharura ya haraka.

Chukua hatua mara moja – ya kuwahi hospitalini.

#afyaclass #chakula #kupaliwa #huduma

#Reply

#5Replies
🔥 CHAT NASI
Dr. Ombeni Dr. Ombeni
Je, una changamoto yoyote ya Kiafya? Kwa Ushauri & Tiba tuwasiliane. Call (Kawaida) au SMS (WhatsApp): +255 758 286 584